Friday, October 31, 2008

No Matter What Else You're Doing, You Can Always Be Praying

You don't have to be down on your hands & knees to be praying. In fact, in everything you're doing you ought to be praying & "looking unto Jesus, the Author & Finisher of our faith." (Heb.12:2)
Prayer is like breathing, just breathing the Holy Spirit all the time. Stay in constant communication with the Lord, constantly thinking about Him, & you will be anointed & Spirit-led in everything you do! If you're praying about what you're doing & asking God for wisdom, He has promised to give it to you! (Jam.1:5)
The Lord can save you a lot of work, a lot of trouble & a lot of time if you'll just pray first before you start a job. Pray about it & ask the Lord to help you & lead you, even if it's just a word--"Jesus, please help me!" You can pray in a split of a second & get the answer back quickly.

God is within all things but not included; outside all things, but not excluded; above all things, but not beyond their reach.

To find God, we must be willing to seek Him.

Stay blessed in Jesus name..

Mr. President (JK) to address the nation today

President Jakaya Kikwete is due to address the nation today amid speculation that he is likely to give a last word regarding the Bank of Tanzania`s External Payment Arrears (EPA) account scandal. A one-page State House statement to press yesterday informed of the head of state`s speech. ``In his speech, he will dwell on various social and economic developmental issues that ensued in the country and abroad,`` read the statement, in part. State House communications director Salvator Rweyemamu, who talked to The Guardian by telephone later in the evening, declined to unveil the President`s agenda. However, with the deadline on the EPA implementation report expiring today, political analysts believe he will definitely touch on the matter. Chairman of the presidential task-force on EPA Johnson Mwanyika told this paper in an exclusive interview last week that Kikwete himself would give ``the final word`` on the matter. The AG urged people to remain calm and stop pre-empting the Head of State because the deadline was just around the corner.
SOURCE: Guardian

Tuesday, October 28, 2008

Although there were so many, the net was not broken

John 21:1-14

1 After these things Jesus showed Himself again to the disciples at the Sea of Tiberias, and in this way He showed Himself: 2 Simon Peter, Thomas called the Twin, Nathanael of Cana in Galilee, the sons of Zebedee, and two others of His disciples were together. 3 Simon Peter said to them, “I am going fishing.”They said to him, “We are going with you also.” They went out and immediately got into the boat, and that night they caught nothing. 4 But when the morning had now come, Jesus stood on the shore; yet the disciples did not know that it was Jesus. 5 Then Jesus said to them, “Children, have you any food?” They answered Him, “No.” 6 And He said to them, “Cast the net on the right side of the boat, and you will find some.” So they cast, and now they were not able to draw it in because of the multitude of fish. 7 Therefore that disciple whom Jesus loved said to Peter, “It is the Lord!” Now when Simon Peter heard that it was the Lord, he put on his outer garment (for he had removed it), and plunged into the sea. 8 But the other disciples came in the little boat (for they were not far from land, but about two hundred cubits), dragging the net with fish. 9 Then, as soon as they had come to land, they saw a fire of coals there, and fish laid on it, and bread. 10 Jesus said to them, “Bring some of the fish which you have just caught.” 11 Simon Peter went up and dragged the net to land, full of large fish, one hundred and fifty-three; and although there were so many, the net was not broken. 12 Jesus said to them, “Come and eat breakfast.” Yet none of the disciples dared ask Him, “Who are You?”—knowing that it was the Lord. 13 Jesus then came and took the bread and gave it to them, and likewise the fish. 14 This is now the third time Jesus showed Himself to His disciples after He was raised from the dead.

..I greet you all in the name of JESUS CHRIST.
Today the LORD has something special for you.I was reading in John 21:11 and the LORD told me to share with you this revelation that ...He is going to bless His people with big tangible blessings in such away that eyes have never seen and ears never heard....The kind of blessing He gonna bless you will not affect your spiritual life...He says in John 21:11 .."and although there were so many, the net was not broken"..I want to tell you that you will not leave him or degrade your spritual standards life because of that awesome blessings that He gonna bless you..net will not break apart...
I have seen many christians ..in the tender times of thier salvation ,they used to love GOD to high extent..they were prayer worriers and leaving holy life..but soon after being blessed ...their net (Salvation) began to break apart..they start loosing coming to church..not praying any more..and living unholy life...Some of you who are reading this message are in that condition right now....your net is broken and you can't help yourself anymore...I want to tell you Jesus is waiting for you on the sea shore..we read that on verse 12 that Jesus has prepared a break fast for you on the sea shore ..here He says ..come and eat..I know that your net in marriage is broken...your net in relationship is broken or is starting to break apart..
some of you the net of your job has started to break apart...I want to tell you that Jesus is calling on the sea shore ..please come and eat...
You know what nets in your life have started to break apart...I want to tell you that...Jesus has a bread and a fish for you in the sea show..

If you are touched with this message and you want us to pray for you...please don't hestitate and write to me thru' the email miwlc@yahoo.com ..

May God richly bless you..

Mtade,
India

Monday, October 27, 2008

Mchungaji kortini kwa kuharibu mali ya kanisa

Mchungaji wa kanisa la Pentekosti, Mackdonard Mwakisambwe (46), mkazi wa Sinza, jijini Dar es Salaam, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu mkazi Kinondoni, kujibu shtaka la kuharibu mali ya kanisa hilo. Inspekta, Bennet Kipasika, alidai mbele ya Hakimu Frednand Kiwonde kuwa mshtakiwa aliharibu kanisa kwa kuezua paa, kuchafua madhabau na kuweka mchanga sehemu ya ibada. Alidai kuwa gharama zote za uharibifu huo ni sh. 600,000, mali ya kanisa hilo. Ilidaiwa Mahakamani hapo kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo, Oktoba 15 mwaka huu, saa 11:00 jioni huko Sinza. Hata hivyo, mshtakiwa alikana shtaka na yupo nje kwa dhamana hadi Novemba 5 mwaka huu, itakapotajwa.

CCM haihusiki na OIC-Msekwa:MAOMBI YA WANASAYUNI :LEO TUPO SIKU YA 6

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeukana mpango wa Tanzania kujiunga na Jumuiya ya Kimataifa ya Kiislamu (OIC) na kusema kwa hilo vyombo vya habari na maaskofu wanakionea. Akizungumza na Nipashe jijini Dar es Salaam jana, Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Pius Msekwa, alisema suala la kujiunga na OIC limo mikononi mwa Serikali na CCM haihusiki. ``Mbona mnanionea jamani, kwa kweli kuniuliza juu ya jambo hili mnatuonea. Suala la kujiunga na OIC sio la CCM na wala aliyesema maneno hayo sio mimi wala kiongozi wa Chama,`` alisema. Pamoja na Msekwa kuukana mpango huo, lakini maamuzi makubwa yanayohusu nchi hayawezi kuamuliwa na serikali bila chama tawala kutoa baraka zake?. Hata hivyo, Msekwa alisema hawezi kuingia kwa undani kujibu kauli iliyotolewa na maaskofu 58 wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) kwamba watauangalia upya uhusiano wao na Serikali pamoja na Chama tawala, iwapo mipango wa kuiingiza nchi katika jumuiya hiyo pamoja na kuruhusu kuundwa kwa Mahakama ya Kadhi itaendelea. Alisema hawezi kuamini kwamba ni kweli maaskofu walitoa kauli hiyo, kwa vile katika mkutano huo yeye hakualikwa na wala hakuhudhuria. Alipoulizwa kwamba Serikali inaweza kuchukua uamuzi mkubwa kama huo (wa kujiunga na OIC) bila kupata baraka ya Chama tawala, Msekwa alizungumza kwa hasira huku akilalamika kwamba maswali hayo yana lengo la kumuonea. Hivi aliyetoa kauli ya OIC ni mtendaji wa Serikali au mtendaji wa CCM? alihoji na kuongeza: Unataka ufafanuzi juu ya uhalali au ubaya wa hicho unachouliza, tafadhali muoneni huyo huyo aliyesema, Chama hakihusiki, mbona mnaendelea kunisakama kwa jambo nisilolijua. Msekwa alisema anaamini Serikali ina majibu mazuri na yenye uhakika kwa vile haiwezi kufanya jambo ambalo halina maslahi. Wiki iliyopita Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Kamillius Membe, aliwaambia waandishi wa habari kuwa suala la kujiunga na OIC halina madhara kwa taifa. Kauli hiyo iliamsha wasikwasi wa maaskofu ambao licha ya kukemea kauli ya Membe na kumtaka ajiuzulu, pia walisema kitendo hicho ni uvunjaji wa Katiba ya nchi na kubomoa misingi ya umoja wa kitaifa. Hata hivyo, Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) lilipinga kauli ya maaskofu kwa kupitia kwa Kaimu Mufti, Sheikh Suleiman Gorogosi, kuwa inalengo la kupotosha. Wakati huo huo, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imeunga mkono mpango wa Serikali ya Muungano wa Tanzania wa kutaka kujiunga na OIC kwa kuwa itasaidia juhudi za kukuza uchumi na ustawi wa wananchi wake. Tamko hilo lilitolewa jana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma, alipokuwa akizungumza mjini Zanzibar baada ya kujitokeza kwa tofauti kati ya taasisi za kidini dhidi ya uamuzi wa Serikali ya Muungano. ``Zanzibar tunaunga mkono uamuzi wa Serikali ya Muungano wa kufikiria Tanzania kujiunga na OIC kwa vile suala hilo halihusiani na mambo ya dini na litanufaisha jamii katika ustawi wa maendeleo, alisema Hamza. Alisema ndio maana Zanzibar imekuwa ikitetea kila mara Tanzania ijiunge na Jumuiya hiyo kwa vile misaada na mikopo inayotolewa na OIC ikiwemo miradi ya elimu na huduma za kijamii itanufaisha Watanzania wote bila ya kujali itikadi zao za imani ya dini. Alisema kuna mataifa mengi yaliyojiunga na Jumuiya hiyo licha ya nchi hizo kuwa na waumini wachache wa dini ya kiislamu na kuzitolea mfano nchi hizo kuwa ni Uganda na Msumbiji ambazo tayari zimeshanufaika na mfuko wa maendeleo wa OIC katika sekta za elimu, afya na viwanda. Akizungumiza suala laMahakama ya kadhi,, Waziri Hamza alisema wananchi waondoe hofu kwa vile mahakama hiyo si jambo geni kutokana na mfumo huo kuwepo visiwani Zanzibar bila ya kuathiri madhehebu mengine ya dini. Mhadhiri wa Sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Sengodo Mvungi, amesema kunahitajika meza ya mazungumzo itakayokutanisha makundi yote ya Watanzania kujadili masuala mazito yanayowakabili kama kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi na la kujiunga na OIC. Akizunguza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Dk. Mvungi alisema malumbano yaliyozuka hivi karibuni, na ambayo bado yanaendelea yanaonyesha dalili mbaya kwa mustakabali wa kitaifa. Alisema matatizo yaliyopo nchini, yanasababishwa na mambo mengine, lakini lililokubwa zaidi ni ile tabia ambayo imejengeka nchini kwamba hakuna anayetaka kumsikiliza mwenzake. ``Hoja kama OIC au Mahakama ya Kadhi zinatakiwa zijadiliwe kwa lugha ya utaifa, pande zote zinazohusika zikutane, zikae pamoja na zijadiliane kwa maslahi ya kitaifa, tuache pembeni dini zetu, kabila zetu na koo zetu,`` alisema na kuongeza ``Katika mambo mazito kama yanayoendelea nchini lazima utaifa utangulizwe mbele, vinginevyo tutaishia kulumbana na kugombana lakini hatutapata jawabu la matatizo yetu, alisema.

Source: ippmedia

WAPENDWA WANA SAYUNI.SISI KAZI YETU NI KUOMBA TU.LEO TUPO SIKU YA SITA YA MAOMBI YETU.NENO LA KUSIMAMA NALO NI LILE LILE LA 2NYAKATI 7:14.KAMA UNAPENDA KUUNGANA NA SISI KUHUSU MAOMBI HAYA TUANDIKIE KWENYE EMAIL HII: MIWLC@YAHOO.COM

if my people, who are called by my name, will humble themselves and pray and seek my face and turn from their wicked ways, then will I hear from heaven and will forgive their sin and will heal their land. Now my eyes will be open and my ears attentive to the prayers offered in this place.

Sunday, October 26, 2008

Askofu Gamanywa na Askofu Kakobe wamjia juu Waziri Membe kuhusu OIC:MAOMBI YA WANASAYUNI :LEO TUPO SIKU YA 5

Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu wa Makanisa ya Kipentekosti Tanzania (PCT), Askofu Sylvester Gamanywa, alisema pingamizi la maaskofu dhidi ya Mahakama ya Kadhi na OIC, siyo chuki dhidi ya Uislamu, OIC na mahakama hiyo, bali linalenga kuzuia mgawanyiko wa kitaifa, ambao alisema hautawanufaisha wanaotaka kutekelezewa maslahi yao. Alisema maaskofu wamelazimika kuweka pingamizi hilo kwa vile hawakushirikishwa katika mambo hayo hata katika mazingira ya kawaida na kwamba wamekuwa wakiulizwa na waumini wao makanisani kuhusu mambo hayo. ``Naomba Rais atumie hekima na busara katika jambo hili,`` alisema Askofu Gamanywa.
Askofu Mkuu Zakaria Kakobe wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship amesema suala la kujiunga na OIC ni la kijinga na hivyo amemtaka Membe na naibu wake wajiuzulu mara moja kwa vile wanataka kuliingiza taifa kwenye machafuko makubwa. Akizungumza na Nipashe jijini Dar es Salaam jana, kiongozi huyo aliyeonekana kuwa na hasira alisema kama Waziri Membe anataka kusilimu na kupokea fedha, basi asilimu mwenyewe, lakini asiwalazimishe Watanzania. ``Hakuna ujinga unaonikera kuzidi huu wa kujiunga na OIC, Mwalimu Nyerere alisema mtu yoyote anayefikiri kwamba Tanzania inaweza kuwa nchi ya Kiislamu au ya Kikristo ni mjinga, anachokifanya Membe hivi sasa ni ujinga mtupu,`` alisema kiongozi huyo kwa ukali. Akijibu hoja za Waziri Membe na Naibu wake Balozi Seif Iddi walizotoa kwa nyakati tofauti, Askofu Kakobe alisema hapahitajiki utafiti wala zoezi la kuthibitisha ubaya wa kujiunga na OIC kwani jina lenyewe la Jumuiya hiyo linajitambulisha kuwa ni chombo cha Kiislam. Tamko la CCT limetolewa siku moja baada ya Waziri Membe, kukaririwa na gazeti hili jana akiwataka Watanzania waondokane na woga wa kuiogopa OIC. Kauli hiyo ilitolewa na Waziri Membe alipozungumza na waandishi wa habari, makao makuu ya wizara hiyo, jijini Dar es Salaam juzi, ikiwa ni siku moja baada ya Naibu wake, Balozi Seif Ali Iddi kukaririwa na gazeti hili akiweka bayana kuhusu azma hiyo. Membe alisema anawashangaa baadhi ya Watanzania kutoa kauli zinazoashiria kuiogopa OIC na baadhi ya nchi za Kiislamu, kama vile Iran, wakati wanasifika kuwa ni watu jeuri na majasiri wanaoweza kumudu kukabiliana na mambo makubwa, mazito na ya kutisha. Membe alitoa kauli hiyo alipokuwa akijibu swali aliloulizwa na mmoja wa wanahabari, ambaye katika maelezo yake, alionyesha wasiwasi kuhusu msimamo wa serikali kuwa na uhusiano na Iran na azma yake ya kutaka kujiunga na OIC. Kutokana na hali hiyo, Membe alisema haoni ubaya mtu kunufaika na fedha za shetani na kwamba, kitendo cha Watanzania kuiogopa jumuiya hiyo na Iran, ni kujivua sifa yao ya ujeuri na ujasiri na pia ni kushindwa kumuenzi Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere ambaye hakuwa anaogopa hata kitu kimoja. ``Kama unakuta shetani mahali ana hela si uchukue. Ujeuri wetu uko wapi? Kwa nini tunaiogopa Iran. Ukiona mchele umewekwa Kur`ani, hiyo Kur`ani si unaitupa tu, halafu unakula mchele?,`` alisema Membe. ``Tuiache Israeli iiogope Iran. Tuna ubalozi wa Iran, hatukuwafukuza. Kwa nini tunaogopa na jeuri zetu. Uamuzi huu utafanywa na Watanzania wote, serikali kazi yake ni kutoa changamoto. Naomba Watanzania tujiamini. Hata Tanzania tunachukiwa kwa kuishambulia Uganda, lakini tulikuwa na sababu. Kama (serikali) tungekuwa na woga tusingejiunga na Marekani kwa sababu hawa (Marekani na Iran) ni maadui,`` alisema Membe.
Waziri Membe alipotakiwa na waandishi wa habari katika viwanja vya Mnazi Mmoja muda mfupi baada ya kuhudhuria sherehe za �Siku ya Umoja wa Mataifa (UN)``, kueleza msimamo wake kuhusu kauli ya maaskofu ya kumtaka ajiuzulu, alisema: ``Sina taarifa, hivyo unavyoniambia ndio ninasikia.`` Alipoelezwa kuwa ndivyo maaskofu walivyosema wakimtaka ajiuzulu, Waziri Membe alisema: �Siwezi kwa sababu siamini.``

Source: Nipashe


WAPENDWA WANA SAYUNI.SISI KAZI YETU NI KUOMBA TU.LEO TUPO SIKU YA TANO YA MAOMBI YETU.NENO LA KUSIMAMA NALO NI LILE LILE LA 2NYAKATI 7:14.KAMA UNAPENDA KUUNGANA NA SISI KUHUSU MAOMBI HAYA TUANDIKIE KWENYE EMAIL HII: MIWLC@YAHOO.COM

if my people, who are called by my name, will humble themselves and pray and seek my face and turn from their wicked ways, then will I hear from heaven and will forgive their sin and will heal their land. Now my eyes will be open and my ears attentive to the prayers offered in this place.

Aliyefufuliwa kutoka wafu baada ya kuombewa kwenye mkutano wa Reinhard Bonke

Mathayo 10:8 "Waponyeni wagonjwa, wafufueni wafu, watakaseni wenye ukoma, wafukuzeni pepo. Mmepokea bure, toeni bure."
Angalia kwa makini video hii utaona jinsi mama huyo wa huko Nigeria aliyoamua kung'ang'ania ahadi za Bwana na hata akamlilia Mungu na kuchukua hatua ya imani kuubeba mwili wa mume wake aliyekuwa amekufa na kuupeleka kwenye mkutano kanisani ambapo Mwingilisti Bonke alikuwa anaombea watu...
Fuatilia series hii utaona jinsi Mungu wetu tunayemuamini alivyo wa rehema na upendo na uwezo mwingi zaidi ya kufufua maiti na kuleta uhai wa mwili lakini anaweza kuleta uhai wa roho yako ili isiangamie milele katika moto wa jehanamu...

angalia ushuhuda huu sehemu ya 1.





Sehemu ya 2





Sehemu ya 3





"Jesus has finished the mansions but the saints are not ready.."

Sehemu ya 4



Sehemu ya 5





Sehemu ya 6





YESU KRISTO anaweza yote.Ushuhuda mkubwa zaidi ya yote ni wewe kumpa YESU maisha yako awe Bwana na Mwokozi wa maisha yako.Biblia inasema itamfaa nini mtu kuupata ulimwengu wote na baadaye kuukosa ufalme wa mbinguni..?
Kama unataka kumpa YESU maisha yako, omba maombi haya mafupi na utaokoka.

"Bwana YESU.
Mimi ni mwenye dhambi.
Natubu dhambi zangu zote nilizozitenda.
Naomba unisamehe na unitakase kwa damu yako iliyomwagika msalabani kwa ajili ya wokovu wangu.
Nakukiri kwa kinywa changu kuwa wewe ni Bwana na mwokozi wa maisha yangu.
Futa jina langu katika kitabu cha hukumu ya milele na moto wa jehenamu.
Andika jina langu katika kitabu cha uzima wa milele.
Nipe roho wako mtakatifu na uniwezeshe kuishinda dhambi.
Kwa jina lako YESU KRISTO mwana wa Mungu aliye hai naomba.
Amen."


Kama umeomba sala hii fupi.Tuandikie kwa email hizi hapa chini ili tuombe pamoja na wewe ili uweze kukua katika wokovu.
miwlc@yahoo.com
savedlema2@yahoo.com

Masheikh kuwajibu Maaskofu kuhusu OIC:MAOMBI MLIMA SAYUNI:TUPO SIKU YA TANO

SUALA la Tanzania kujiunga na Jumuiya ya Nchi za Kiislaam (OIC) limechukua sura mpya baada ya masheikh kutoka tasisi na madhehebu mbambali kufanya kikao cha dharura jana na kujipanga kutoa msimamo wao Ijumaa ijayo.
Masheikh hao ambao ni Maimamu wa misikiti mbalimbali jijini Dar es Salaam pamoja na viongozi wa taasisi mbalimbali za kiislaam nchini baada ya mjadala huo walitoka na msimamo kuwa watatangaza uwanja baadaye na kuwajibu maaskofu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) waliotoa tamko la kupinga Tanzania kujiunga OIC na kumtaka Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe anayelishadadia ajiuzulu.
Katibu wa Kamati ya masheikh hao, Ramdhan Sanze alithibitisha kuwa tamko lao litatolewa Ijumaa.
“Kwa kweli askofu kumwambia waziri apewe kadi nyekundu kwa kukubali jambo lenye maslahi kwa taifa si kauli nzuri na ni kiburi, sasa tunataka kujua kiburi hiki wamekitoa wapi?” alihoji Sheikh Sanze.
Alifafanua kama maaskofu wanatumia kigezo cha katiba ambacho hakina nguvu kwa sababu katiba ipo kwa maslahi ya Watanzania wote wa dini, makabila na rangi zote.
“Kama wao hawataki na hawawezi kukubali Tanzania ijiunge na OIC na sisi pia hatutaki na wala hatuwezi kukubali kukosa manufaa makubwa ya kijamii na kiuchumi kutokana na vikwazo vyao,” alisema Sheikh Sanze.
Sheikh Sanze alisema kuwa kama hali itakuwa hivyo wataona baada ya jahazi kuachana nani atachukua nini.
“Masheikh wamekubaliana kuwa tutoa tamko letu rasmi na zito siku ya Ijumaa ijayo na tena tutalitoa uwanjani, ni uwanja gani na saa ngapi yapo katika mchakato na tutatangaza,” alisema Sheikh Sanze.
Sheikh Sanze alisema watahoji mtazamo na msimamo wa serikali kuhusiana na kiburi cha maaskofu hao wa CCT kujiunga na OIC.
Alisema Tanzania si ya wakristo wala waislaam bali ni ya wote kwa hiyo kila mmoja ana haki ya kupata kile anachostahili kupata bila ya kuwekewa vikwazo na imani nyingine.
Aliongeza kuwa suala la Mahakama ya Kadhi na OIC si mapya kwa Tanzania kwa sababu yalikuwepo na hakuna madhara yoyote waliyoyapata Watanzania kutokana na uwepo wake.
“Hili si jambo jipya lilikuwepo na tulikuwa tunafaidika sana kwa hiyo ni kulirejesha tu na wala si la kuasisiwa upya,” alisema Sheikh Sanze.
Kwa mujibu wa sheikh Sanze OIC ni taasisi inayoongoza kwa kutoa misaada na mikopo yenye riba nafuu duniani kote, hivyo Tanzania ina kila sababu ya kujiunga na Jumuiya hiyo.
“Hapa tatizo si dini tatizo ni kwa kiwango gani Watanzania watafaidika na iwapo nchi yao itakuwa mwanachama wa OIC bila kujali dini,” alisema Sheikh Sanze.
Alisema Tanzania inajiunga na Jumuiya mbalimbali za kimataifa ambazo zinatoa misaada na mikopo kwa nchi yetu yenye masharti magumu na kuhoji kwa nini OIC ipingwe.
Juzi CCT ilitoa tamko la kumwonya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe kuwa kauli zake kuhusu kujiunga na Jumuiya ya Kimataifa ya Nchi za Kiislamu (OIC) zinaweza kusababisha mgawanyiko wa kitaifa na kumtaka aachane nazo au ajiuzulu wadhifa wake.
Tamko hilo la maaskofu wa makanisa ya Kikristo limekuja baada ya Waziri Membe kukaririwa akisema kuwa hakuna athari zozote kwa Tanzania kujiunga na taasisi hiyo, ambayo madhumuni yake ni kutetea binadamu na hasa Waislamu na sehemu takatifu.
Wakitoa tamko lao kwa waandishi wa habari juzi, maaskofu hao kutokana makanisa ya kiprotestanti walisema kauli ya Waziri Membe ina lengo la kutetea maslahi ya watu wachache.
Katika hatua nyingine maaskofu zaidi ya 300 wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania, (KLPT) waliokuwa wanakutana jijini Dar es Salaam, nao wamepinga serikali kudhamiria kujiunga na OIC na kuonya kwamba taifa litasambaratika.
Mwangalizi Mkuu wa Kanisa hilo, Askofu Philemon Tibanenason alisema wao kama kanisa wanalipinga hilo kwa kuwa lipo nje ya katiba. “Nchi inakoelekea si pazuri, mfano kutumika kwa uislamu na ukristo, ni kinyume na katiba.
Tayari vikundi vya waumini na taasisi mbalimbali vimekwishatoa misimamo yao kupinga hatua ya Waziri Membe na msaidizi wake, Seif Alli Iddi juu ya suala hilo.
“Dini ni nje ya serikali ndiyo maana hakuna Waziri wa Uislamu…sisi kama kanisa kwanza tunashangazwa na hii ya kupeleka masuala ya dini bungeni, kuzungumza masuala ya dini bungeni, pia ni kinyume na katiba…sisi hatuna dini sasa iweje leo hii tunaingiza mijadala ya kidini?
“Hatuchukii dini wala Uislamu, lakini tunachopinga ni nchi kuendeshwa katika misingi hiyo. Tunaona Pakistan, Sudan, Lebanon, kila kukicha ni mapigano…,” alisema Tibanenason.
Aliongeza kusema: ”Kanisa linapenda kuitahadharisha serikali na kuitaka kusimamia bila woga katiba yetu kwa kuwa serikali imepewa dhamana hiyo na wanachi kwa kiapo.
”Sisi kama kanisa la Pentekoste Tanzania, tunaungana na wote hao kupinga kwa nguvu kusudio hilo la serikali..kazi ya kutangaza, kueneza na kuamini ni suala la mtu binafsi na uendeshaji wa taasisi ni nje ya shughuli za mamlaka ya nchi.
Akisisitiza, Tibanenason alisema kujiunga na OIC kutaleta mgawanyiko na hofu katika jamii huku akiiunganisha na Mahakama ya Kadhi kuwa haina mashiko kwa jamii nyingine isiyo ya Kiislamu.
Alisema kwa kuwa serikali ina chombo chake cha kutoa haki kwa wananchi, kama mahakama, na kuiingiza Mahakama ya Kadhi ni kuinyang’anya serikali mamlaka yake ya utoaji na usimamizi wa haki sawa kwa wananchi wake. Mahakama hiyo haiwezi kukubalika katika taifa ambalo si la Kiislamu
Akizungumzia suala la ufisadi, alisema ni matokeo ya ubinafsi wa viongozi wengi. ”Wengi wamekosa upendo, ni wapenda pesa kiasi cha kusahau maadili ya uongozi. Watu wanaopewa madaraka si waadilifu tena na ingekuwa inawezekana, wangeenguliwa kutoka madarakani ili tutafutwe waadilifu wa kweli.
”Watu wanafahamika, tunadhani hata Rais anatakiwa kuangalia watu waadilifu, tunataka ateue watu wenye moyo wa kweli wa kuipenda nchi na watu wake,” alisema.
Juu ya mauaji ya maalbino, alisema azimio la mkutano wao ulioanza Alhamisi iliyopita hadi jana, ni kwamba serikali iwanyang’anye waganga wa jadi leseni za kuendesha biashara zao kwa kuwa ni chanzo na wachochezi wa mauaji.
Source:Mwananchi


WAPENDWA WANA SAYUNI.SISI KAZI YETU NI KUOMBA TU.LEO TUPO SIKU YA TANO YA MAOMBI YETU.NENO LA KUSIMAMA NALO NI LILE LILE LA 2NYAKATI 7:14.KAMA UNAPENDA KUUNGANA NA SISI KUHUSU MAOMBI HAYA TUANDIKIE KWENYE EMAIL HII: MIWLC@YAHOO.COM


if my people, who are called by my name, will humble themselves and pray and seek my face and turn from their wicked ways, then will I hear from heaven and will forgive their sin and will heal their land. Now my eyes will be open and my ears attentive to the prayers offered in this place.

Saturday, October 25, 2008

Serikali yatoa tamko kuhusu OIC:MAOMBI MLIMA SAYUNI:TUPO SIKU YA NNE

Serikali imefafanua kwamba haijaamua kujiunga na Jumuiya ya Kimataifa ya Nchi za Kiislamu (OIC). Ofisa Mwandamizi wa Serikali aliiambia HabariLeo jana kwamba uamuzi wowote kuhusu suala hilo utawahusisha Watanzania, lakini bado hakuna uamuzi ambao umechukuliwa. Hatua hiyo imekuja baada ya Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), kumtaka Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, ajiuzulu wadhifa wake wa kisiasa iwapo ataendelea kupigia debe suala la Tanzania kujiunga na Jumuiya ya Kimataifa ya Nchi za Kiislamu (OIC). Membe akizungumza juzi na wanahabari alionyesha kushangazwa na hatua ya baadhi ya Watanzania kuogopa Tanzania kujiunga na OIC. Waziri huyo alifafanua kuwa Tanzania haijajiunga na OIC, bali iko kwenye mchakato wa kufanya hivyo. Alifafanua kuwa hata hivyo suala la Tanzania kujiunga ama kutojiunga na OIC liko mikononi mwa Tanzania. Alisema makundi yote ya wananchi watatoa mawazo yao hivyo kwa sasa hakuna haja ya kuogopa wala kuzusha mijadala isiyokuwa na manufaa kwa nchi. “Waziri anayesukuma suala hili, anatakiwa ajiuzulu aache kuzungumzia suala hilo, kwani wananchi wamewatuma kuzungumzia masuala ya OIC?” Alihoji Askofu Dk. Owdenburg Mdegela baada ya kusomwa kwa tamko la maaskofu wa CCT jana Dar es Salaam. Naye Askofu Dk. Steven Munga alisema wao hawasimamii udini, bali wanasimamia Utanzania na akafafanua kuwa baraza hilo linasubiri suala hilo lipelekwe bungeni ndipo na wao watajua cha kufanya. Dk. Munga alisema kitendo cha Membe kutoa mfano wa Uganda kuwa inanufaika na OIC hakina manufaa kwani Watanzania ambao alisisitiza hawana cha kujifunza kwa taifa hilo ambalo alidai limegubikwa na vita ya wenyewe kwa wenyewe kwa muda mrefu. Askofu Sylvester Gamanywa alidai pingamizi la CCT sio la chuki kwa Uislamu ila ni pingamizi la kuzuia mgawanyiko wa kitaifa iwapo taasisi kama OIC itaingizwa kwenye mamlaka ya nchi. Pingamizi hilo lililosainiwa na Mwenyekiti wa CCT Askofu Mkuu Donald Mtetemelwa, walidai endapo nchi itaingia katika OIC, Katiba itakuwa imevunjwa na Watanzania wataingizwa katika migogoro itakayoua maridhiano, mshikamano, amani, utangamano na umoja wa kitaifa.
Source: Habari Leo

WAPENDWA WANA SAYUNI.SISI KAZI YETU NI KUOMBA TU.LEO TUPO SIKU YA NNE YA MAOMBI YETU.NENO LA KUSIMAMA NALO NI LILE LILE LA 2NYAKATI 7:14.KAMA UNAPENDA KUUNGANA NA SISI KUHUSU MAOMBI HAYA TUANDIKIE KWENYE EMAIL HII: MIWLC@YAHOO.COM

if my people, who are called by my name, will humble themselves and pray and seek my face and turn from their wicked ways, then will I hear from heaven and will forgive their sin and will heal their land. Now my eyes will be open and my ears attentive to the prayers offered in this place.

Maaskofu wamtaka Waziri Membe ajiuzulu: MAOMBI MLIMA SAYUNI:TUPO SIKU YA NNE

JUMUIYA ya Kikristo Tanzania (CCT) imemuonya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe kuwa kauli zake kuhusu kujiunga na Jumuiya ya Kimataifa ya Nchi za Kiislamu (OIC) zinaweza kusababisha mgawanyiko wa kitaifa na kumtaka aachane nazo au ajiuzulu wadhifa wake.
Tamko hilo la maaskofu wa makanisa ya Kikristo imekuja baada ya Waziri Membe kukaririwa akisema kuwa hakuna athari zozote kwa Tanzania kujiunga na taasisi hiyo, ambayo madhumuni yake ni kutetea binadamu na hasa Waislamu na sehemu takatifu.
Membe alisema hakuna haja ya kuwa na woga wa kujiunga na taasisi hiyo wakati katika mchakato wake wakristo na waislamu watanufaika na miradi itakayokuwa ikisimamiwa na OIC, na akashangaa ujasiri wa Watanzania wa kupambana na matatizo umekwenda wapi kiasi cha kuogopa nchi kujiunga na jumuiya hiyo.
Suala hilo liliwahi kuibuka mwishoni mwa utawala wa Rais Ali Hassan Mwinyi wakati vyombo vya habari vilipofichua kuwa serikali ilijiunga kinyemela na jumuiya hiyo. Baadaye viongozi wa serikali walikiri kufanya hivyo kabla ya kujiondoa, lakini safari hii upinzani umekuwa mkubwa zaidi.
Wakitoa tamko lao kwa waandishi wa habari jana, maaskofu hao kutokana makanisa ya kiprotestanti walisema kauli ya Waziri Membe ina lengo la kutetea maslahi ya watu wachache.
Maaskofu hao walisema kwa kuwa katiba ya OIC hiyo inaeleza bayana kuwa italinda mila, desturi na tamaduni za kiislamu, kujiunga na jumuiya hiyo itakuwa ni kukiuka katiba ya nchi inayoeleza kuwa dini ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi, na kwamba shughuli ya uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchini.
"Kama serikali ikikubali, kutakuwa ni mwanzo wa kuruhusu kubomoka na kuvunjika kwa amani ya nchi kwa sababu yanagusa hisia na itikadi za wananchi," alisema Askofu Peter Kitula, ambaye ni makamu mwenyekiti wa kwanza wa CCT.

Askofu Kitula, ambaye alisoma tamko hilo la maaskofu, alisema baada ya kutafakari kwa roho ya kiutume na kinabii wameamua kupinga kuanzishwa kwa mahakama ya kadhi pamoja na mchakato wa kujiunga na OIC.
Alisema katiba ya Tanzania ibara ya 19 kifungu cha 2 inaeleza wazi kuwa kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi, na shughuli ya uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchini.
"Ibara hii ni muhimu sana kwa ajili ya kusimamia na kuhakikisha kwamba mambo ya dini yanatenganishwa kabisa na shughuli za uendeshaji wa nchi," alisema.
Alisema sehemu hiyo ya katiba inapingana na ibara ya 1 kifungu cha 11 ya katiba ya OIC kinachosema kuwa jumuiya hiyo inatetea mila, tamaduni na desturi za kiislamu, kuwalinda na kuwaelimisha wananchi kuhusu uislamu nchini, jambo ambalo askofi huyo alisema linaonyesha wazi kuwa kujiunga na IOC itakuwa ni ukiukwaji wa katiba.
Alisema siku za hivi karibuni Bunge la Jamuhuri ya Muungano limekuwa likijadili miswada ya sheria ya kuanzisha au kujihusisha na vyombo hivyo viwili, lakini akasema kuwa kushinikiza kukubalika kwake ndani ya bunge ni kwenda kinyume na katiba.
Naye Owdernburg Mdegela, askofu wa dayosisi ya Iringa ya Kanisa la Kiinjili la Kilutherani Tanzania (KKKT), alisema kitendo cha Waziri Membe kulizungumza jambo hilo bila kulionea haya ni kutetea maslahi ya watu wachache na kuvunja katiba.
Alisema Tanzania ina rasilimali za kutosha hivyo kujiunga na umoja huo kwa lengo la kutafuta misaada ama kutafuta kula na baadaye kupoteza mwelekao wa taifa, ni kujiingiza katika mtego ambao kujinasua kwake kunahitaji gharama ambayo ni kumwaga damu.
"Sisi tunasimama kama viongozi wa kanisa tukimwambia Membe kuwa hafai wadhifa huo, hivyo ni vema akaacha mara moja kutoa kauli zake zisizo na mantiki. Lakini kama hawezi, basi inampasa ajiuzulu," alisema Askofu Mdegela.
Naye askofu wa kanisa pentekoste, Sylivester Gamanywa alisema Waziri Membe anatoa kauli ambazo zina lengo la kuweka hisia binafsi na mgawanyiko wa kitaifa pamoja na kuvunjika kwa amani.
Alisema kitendo cha waziri huyo kusema kuwa serikali inaruhusu fedha chafu na kwamba kama mtu akikuta fedha za shetani inampasa kuzichukuwa, ni kuwadhalilisha Watanzania na taifa lao kwa ujumla.
Naye askofu wa Anglikana, Dk. Stephen Munga alisema kuwa waziri Membe hafai katika kushughulikia masuala ya kitaifa kwani hakuna mamalaka yoyote iliyomuagiza aende kuzungumzia suala la kuaanzishwa kwa OIC.
"Inampasa Waziri Membe afahamu kuwa sisi ni Tanzania na tutafuata mambo yetu na si kuiga masuala ya nje. Anavyosema tuwaige Waganda si jambo sahihi," alisema Dk. Munga.
Alisema kama kanisa msimamo wao ni kuyakataa mambo hayo mawili na kuitaka Serikali na mamlaka zake zote kuacha kuendelea kukaribisha mijadala ya mambo hayo kwani kufanya hivyo ni kupoteza muda wa wenye dhamana ya mamlaka ya nchi hii na rasilimali zake.
"Tunauhakika kuwa yaliyomo ndani ya OIC ni hatari kabisa, kwani endapo yakikubalika katiba ya nchi itakuwa imevunjwa na Watanzania watakuwa wameingia katika migogoro itakayoua maridhiano, mshikamano, utengemano na umoja wa kitaifa," alisema Askofu Kitula.
"Kwa kuzingatia wajibu wetu wa kinabii na kiutume, tunatoa wito kwa bunge kutoruhusu kamwe uanzishwaji wa mahakama ya kadhi kwa kupitia mchakato wa utendaji wa mamlaka ya nchi, pia kutoridhia uanachama wa Tanzania katika OIC."
Akizungumzia tamko la maaskofu, mwenyekiti wa kamati ya msikiti wa Idrissa, Sheikh Ally Basaleh alisema kuwa awali kabla ya kuanza kwa mchakato wa masuala hayo serikali ilishafanya uchambuzi wa kina na kugundua umuhimu wa kuanzishwa kwa vyombo hivyo.
"Kauli za maaskofu hawa na viongozi wa kanisa zinadhihirisha kuwa wanakataa maamuzi yao ya awali kwamba Rais Jakaya Kikwete ni mteule wa Mungu, kwani ndiye anayesimamia masuala haya yote," alisema Basaleh.
Alisema waislamu ni sehemu ya jamii hivyo wao kama viongozi wa dini wanaandaa mchakato wa kutoa tamko litakalokuwa likitoa mchanganuo kuhusu uhalali wa kuanzishwa kwa vyombo vyote hivyo viwili nchini.
Source: Mwananchi


WAPENDWA WANA SAYUNI.SISI KAZI YETU NI KUOMBA TU.LEO TUPO SIKU YA NNE YA MAOMBI YETU.NENO LA KUSIMAMA NALO NI LILE LILE LA 2NYAKATI 7:14.KAMA UNAPENDA KUUNGANA NA SISI KUHUSU MAOMBI HAYA TUANDIKIE KWENYE EMAIL HII: MIWLC@YAHOO.COM


if my people, who are called by my name, will humble themselves and pray and seek my face and turn from their wicked ways, then will I hear from heaven and will forgive their sin and will heal their land. Now my eyes will be open and my ears attentive to the prayers offered in this place.

Friday, October 24, 2008

Waziri Membe na OIC --MAOMBI MLIMA SAYUNI:TUPO SIKU YA TATU

Azma ya Tanzania kutaka kujiunga na Jumuiya ya Kimataifa ya Nchi za Kiislamu (OIC), imezidi kupata nguvu, baada ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, kuwataka Watanzania waondokane na woga wa kuiogopa jumuiya hiyo. Kauli hiyo ilitolewa na Waziri Membe alipozungumza na waandishi wa habari, makao makuu ya wizara hiyo, jijini Dar es Salaam jana, ikiwa ni siku moja baada ya Naibu wake, Balozi Seif Ali Iddi, kukaririwa na gazeti hili jana akiweka bayana kuhusu azma hiyo. Alisema anawashangaa baadhi ya Watanzania kutoa kauli zinazoashiria kuiogopa OIC na baadhi ya nchi za Kiislamu, kama vile Iran, wakati wanasifika kuwa ni watu jeuri na majasiri wanaoweza kumudu kukabiliana na mambo makubwa, mazito na ya kutisha. Membe alitoa kauli hiyo alipokuwa akijibu swali aliloulizwa na mmoja wa wanahabari, ambaye katika maelezo yake, alionyesha wasiwasi kuhusu msimamo wa serikali kuwa na uhusiano na Iran na azma yake ya kutaka kujiunga na OIC. Mwandishi huyo alikwenda mbali zaidi kwa kudai kuwa wakati wa utawala wa Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi, moja ya nchi za Kiislamu iliwahi kuingiza nchini msaada wa mchele, huku vifurushi vyake vikiwa vimewekwa juu yake misahafu ya Kur�ani Tukufu kwa nia ya kuwasilimisha Watanzania. Leo pia, katika utawala wa Rais Muislamu tunaelezwa kuwa Tanzania inataka kujiunga na OIC, kitu ambacho mimi nitakipinga hadi dakika ya mwisho,� alisema mwanahabari huyo. Wasiwasi wa mwanahabari huyo ulikuja baada ya Membe kueleza hatua nzuri iliyofikiwa katika mazungumzo kati yake na Rais wa Iran, Mahmoud Ahmednejad ambayo yalilenga kuiomba nchi hiyo kufuta madeni inayoyadai Tanzania yapatayo zaidi ya Sh bilioni 200. Membe aliitisha mkutano huo kwa lengo la kuipongeza nchi ya Uganda kwa kuwa mwanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kusema kuwa kuingia kwa nchi hiyo kutasaidia katika utatuzi wa migogoro inayolikumba Bara la Afika. Kauli ya mwandishi huyo, ilimfanya Waziri Membe ambaye awali katika mkutano huo na waandishi wa habari alizungumza kwa upole, umahiri na kwa ufasaha wa hali ya juu, abadilike na kuanza kuzungumza kwa ukali. Kwa nini tunashikwa na uoga? Tukipewa msaada na Marekani tunaambiwa kuna mkono wa mtu, tukipewa na Iran tunaambiwa hivyo. Niambieni mimi kama Waziri wa Mambo ya Nje niende wapi?, alihoji Membe na kumtaka mwandishi huyo amtajie japo nchi mbili duniani ambazo ni takatifu kwa asilimia mia moja ili Tanzania ijenge uhusiano nazo na iachane na nchi nyingine. Alisema kwa mfano Uganda, ambayo ni mwanachama wa OIC, asilimia 66 ya wananchi wake ni Wakristo, asilimia 10 tu ndio Waislamu na asilimia iliyosalia ni ya watu wasio wa dini hizo na pia, mapapa watatu wamewahi kwenda nchini humo. Hata hivyo, Membe alisema pamoja na Uganda kujiunga na OIC, idadi ya Waislamu wala misikiti haijaongezeka nchini humo. Kutokana na hali hiyo, alisema haoni ubaya mtu kunufaika na fedha za shetani na kwamba, kitendo cha Watanzania kuiogopa jumuiya hiyo na Iran, ni kujivua sifa yao ya ujeuri na ujasiri na pia ni kushindwa kumuenzi Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere ambaye hakuwa anaogopa hata kitu kimoja. Kama unakuta shetani mahali ana hela si uchukue. Ujeuri wetu uko wapi? Kwa nini tunaiogopa Iran. Ukiona mchele umewekwa Kur`ani, hiyo Kur`ani si unaitupa tu, halafu unakula mchele?`` alisema Membe. Hata hivyo, Mwalimu Nyerere wakati wa uhai wake katika miaka ya 1990 aliwahi kukemea hatua ya Zanzibar kujiunga na OIC kwa kuwa ilikuwa ni ukiukaji wa katiba, licha ya maelezo kwamba ingevinufaisha visiwa hivyo kiuchumi. Katika makemeo yake, Mwalimu Nyerere alisema hawezi kukaa kimya kuruhusu Zanzibar inufaike kwa kuvunja Katiba ya nchi. Hata hivyo, Waziri Membe jana alisema suala la Tanzania kujiunga na OIC au la, litaamuliwa na wananchi wenyewe na kusisitiza kuwa aliposema bungeni Agosti 22, mwaka huu kwamba, kujiunga na OIC hakuna madhara hakumaanisha kuwa Tanzania imeshajiunga na jumuiya hiyo. ``Tuiache Israeli iiogope Iran. Tuna ubalozi wa Iran, hatukuwafukuza. Kwa nini tunaogopa na jeuri zetu. Uamuzi huu utafanywa na Watanzania wote, serikali kazi yake ni kutoa changamoto. Naomba Watanzania tujiamini. Hata Tanzania tunachukiwa kwa kuishambulia Uganda, lakini tulikuwa na sababu. Kama (serikali) tungekuwa na woga tusingejiunga na Marekani kwa sababu hawa (Marekani na Iran) ni maadui`` alisema Membe. Jana gazeti hili lilimkariri Balozi Iddi akisema kwamba mchakato kwa Tanzania kujiunga na OIC unatarajiwa kuanza wakati wowote na kwamba, hatua ya mwanzo ya mchakato huo. Alisema viongozi wa serikali ya Jamhuri ya Muungano watakutana na wenzao wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kwa ajili ya kupata msimamo wa pamoja kuhusu suala hilo. Naibu Waziri huyo alisema hayo alipoulizwa na Nipashe kama mchakato kwa Tanzania kujiunga na jumuiya hiyo umeshaanza au la tangu Waziri Membe atoe kauli hiyo bungeni, mjini Dodoma, Agosti 22, mwaka huu. Alisema mchakato kwa Tanzania kujiunga na OIC ni mrefu, ambao unatarajiwa pia kulishirikisha Baraza la Mawaziri kufikia maamuzi. Balozi Iddi alisema hatua nyingine ya mchakato, ambayo serikali inatarajia kuichukua, ni kutoa elimu kwa umma ili kuwaondoa uoga wote walioonyesha hofu iwapo Tanzania itajiunga na jumuiya hiyo. Agosti 22, mwaka huu Waziri Membe wakati akifunga mjadala wa hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake, alisema hakuna madhara yoyote kwa Tanzania kujiunga na IOC.
SOURCE: Nipashe

WAPENDWA WANA SAYUNI.SISI KAZI YETU NI KUOMBA TU.LEO TUPO SIKU YA TATU YA MAOMBI YETU.NENO LA KUSIMAMA NALO NI LILE LILE LA 2NYAKATI 7:14.
KAMA UNAPENDA KUUNGANA NA SISI KUHUSU MAOMBI HAYA TUANDIKIE KWENYE EMAIL HII: MIWLC@YAHOO.COM

if my people, who are called by my name, will humble themselves and pray and seek my face and turn from their wicked ways, then will I hear from heaven and will forgive their sin and will heal their land. Now my eyes will be open and my ears attentive to the prayers offered in this place.

Thursday, October 23, 2008

Tanzania kujiunga OIC ni dhahiri: Asema Naibu waziri wa mambo ya nje

Tanzania inatarajia kujiunga na Jumuiya ya Kimataifa ya Nchi za Kiislamu (OIC) wakati wowote katika siku zijazo baada ya serikali kuweka bayana azma hiyo jana. Azma hiyo ya serikali iliwekwa bayana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Seif Ali Iddi, alipozungumza na Nipashe jana, ikiwa ni wiki chache tangu Waziri wa Wizara hiyo, Bernard Membe, aliambie Bunge kwamba, hakuna madhara yoyote kwa Tanzania kujiunga na jumuiya hiyo. Balozi Iddi alisema mchakato kwa Tanzania kujiunga na OIC, unatarajiwa kuanza wakati wowote na kwamba, hatua ya mwanzo ya mchakato huo, viongozi wa serikali ya Jamhuri ya Muungano watakutana na wenzao wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kwa ajili ya kupata msimamo wa pamoja kuhusu suala hilo. Naibu Waziri huyo alisema hayo alipoulizwa na Nipashe kama mchakato kwa Tanzania kujiunga na OIC umeshaanza au la tangu Waziri Membe atoe kauli hiyo bungeni, mjini Dodoma, Agosti 22, mwaka huu. ``Bado hatujaanza mchakato. Kuna kikao tunachotaka kwanza kufanya kwa ajili ya kushauriana na wenzetu wa Zanzibar ili tuwe na msimamo mmoja kuhusu hilo. Ilikuwa tuanze sasa, lakini Mheshimiwa Waziri (Membe) hayupo na Bunge linatarajiwa kuanza,`` alisema Balozi Iddi. Alisema mchakato kwa Tanzania kujiunga na OIC ni mrefu, ambao unatarajiwa pia kulishirikisha Baraza la Mawaziri kufikia maamuzi. Balozi Iddi alisema hatua nyingine ya mchakato, ambayo serikali inatarajia kuichukua, ni kutoa elimu kwa umma ili kuwaondoa uoga wote walioonyesha hofu iwapo Tanzania itajiunga na jumuiya hiyo. ``Hao wanaopinga, ni waoga tu, hawajaeleweshwa kwani haina maana Tanzania itakuwa nchi ya Kiislamu. Zipo nchi kama vile Uganda zimejiunga na OIC, lakini hazijabadilika kuwa nchi za Kiislamu. Tutawaelewesha wakati ukifika, tunavyo vyombo vya kuelimisha hilo,`` alisema Balozi Iddi. Agosti 22, mwaka huu Waziri Membe wakati akifunga mjadala wa hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake, alisema hakuna madhara yoyote kwa Tanzania kujiunga na IOC. Waziri Membe alisema serikali mwaka huu, ilifanya kikao na Baraza la Wawakilishi kuhusu suala hilo na kugundua kuwa nchi 21 zimejiunga na jumuiya hiyo. Alisema kati ya nchi hizo, zimo pia nchi za Wakristo ambazo zimejiunga na hazijapata madhara yoyote. ``Tumeshakusanya takwimu za nje na kuona hakuna madhara yoyote ya kujiunga na IOC, bora tu kufuata taratibu,`` alisisitiza Waziri Membe. Alisema suala hilo lilileta utata awali kwa sababu aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wakati huo, marehemu Ahmed Hassan Diria, alipeleka ombi la Zanzibar kujiunga kwenye jumuiya hiyo bila kuishirikisha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hata hivyo, alisema suala hilo limefanyiwa kazi na serikali na kuona kuwa hakuna madhara kujiunga na IOC. Siku chache baada ya Waziri Membe kutoa kauli hiyo bungeni, viongozi wa makanisa na baadhi ya wasomi, akiwamo Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Dk. Methodius Kilaini, walipinga vikali kauli hiyo ya serikali. Wengine waliopinga suala hilo, ni Askofu Stefano Msangi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Pare, Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT Tanzania, Dk. Alex Malasusa, Mhadhiri Mwandamizi wa Sheria wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Sengodo Mvungi. Hata hivyo, Imamu Mkuu wa Msikiti wa Mnyamani, Buguruni, jijini Dar es Salaam, Sheikh Mohammed Iddi, amekuwa akijitokeza kuwapinga maaskofu kuhusu kauli zao za kupinga suala hilo.
SOURCE: Nipashe

Mauaji ya albino Tanzania

Wachungaji zaidi ya 300 na wazee wa Kanisa la Pentecoste Tanzania (KLPT), wanakutana jijini Dar es Salaam kuzungumzia masuala mbalimbali yanayoitikisa nchi kwa sasa, yakiwemo mauaji ya maalbino na ufisadi. Mambo mengine yatakayojadiliwa katika mkutano huo ulioanza jana na ambao umepangwa kumalizika Jumapili ijayo, ni ugonjwa wa ukimwi, afya ya uzazi na kufanya tathmini ya shughuli za kanisa hilo kwa mwaka uliopita na kupanga mikakati mipya kwa ajili ya mwaka ujao. Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa KLPT, Fanuel Shekihiyo, alisema kuwa mkutano huo ambao unawakutanisha pamoja wachungaji na wazee wa kanisa hilo kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani, utaongozwa na Askofu Mkuu wa kanisa hilo, Philemon Tibanenson. Alisema ajenda za mauji ya maalbino, ufisadi, afya ya uzazi na ugonjwa wa ukimwi zitajadiliwa kwa kina wakati wa mkutano huo kwa sababu mambo hayo kwa sasa yanaitingisha nchi na kuwafanya wananchi waishi kwa hofu. Alisema wao wakiwa kama viongozi wa kiroho wameona wana wajibu wa kuyajadili masuala hayo yanayoenda kinyume cha mafundisho ya Mungu, ili kuwaongoza wanadamu katika mambo mema, baada ya mkutano huo kanisa hilo litatoa tamko juu ya masuala hayo. Kilio cha mauaji dhidi ya watu wa jamii ya albino kilichoelezwa wiki iliyopita jijini Dar es Salaam wakati wa maandamano ya kupinga vitendo hivyo, vimeendelea kutikisa taifa baada ya watu wasiojulikana juzi kumkata miguu akiwa hai mwanafunzi albino na kisha kutokomea nayo. Mwanafunzi huyo wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi ya Shilela, kata ya Segese, Kahama mkoani Shinyanga, Esther Charles (9), alifariki dunia baada kukatwa miguu na kunyofolewa nywele za utosini na kisogoni na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia juzi na kutoweka na viungo hivyo. Tukio hilo la kusikitisha linafanya idadi ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) waliouawa nchini kutokana na imani za kishirikina kufikia 29 na kuibua upya hofu miongoni mwa jamii.
SOURCE: Nipashe

Wednesday, October 22, 2008

MAMBO YA KUTAFAKARI KABLA YA KUFANYAUAMUZI WA KUOA AU KUOLEWA

Bwana Yesu asifiwe!
Ndugu wapenzi wote wa Mlima Sayuni, tunawaletea mafundisho mazuri ya Neno la Mungu yaliyofundishwa na mtumishi wa Mungu, Mwalimu Christopher Mwakasege. Somo hili lenye sehemu 11 linaitwa "MAMBO YA KUTAFAKARI KABLA YA KUFANYAUAMUZI WA KUOA AU KUOLEWA" Tunaamini kuwa hili somo litakuwa ni baraka kubwa kwa wote, na hasa kwa wale ambao hawajoa au kuolewa na wana mpango huo. Mungu akubariki, wataarifu na wengine pia.


Utangulizi

Ukifungua kitabu cha Yoeli.3:14 kinasema, “Makutano makubwa, makutano makubwa, wamo katika bonde la kukata maneno! Kwa maana siku ya Bwana i karibu”. Huyu ndugu, mtumishi wa Mungu, aliyekuwa anaitwa Yoeli, Mungu alimpa nafasi ya kuona mambo ambayo yamekuwa yanafanyika tangu kuumbwa kwa ulimwengu, mpaka hapo Yesu atakaporudi tena. Anasema, ameona makutano makubwa, makutano makubwa, katika bonde la kukata maneno.
Tafsiri nyingine ya bonde la kukata maneno maana yake ni bonde la kufanyia maamuzi. Kukata maneno ni kufanya maamuzi. Sasa, bonde la kukata maneno, kwa tafsiri ya haraka ni dunia hii, wakati huu, mwanadamu anapoishi duniani.
Kwa sababu kabla hujazaliwa huna uwezo wa kuamua. Biblia inasema Mungu alimwambia Yeremia, “Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, kabla hujatoka tumboni nalikutakasa” (Yeremia 1:5). Kabla hajawekwa tumboni mwa mama yake, Mungu alimjua Yeremia, ambayo inamaanisha Yeremia alikuweko, lakini alifananaje sijui! Lakini maandiko yananiambia ya kwamba alikuwepo na Mungu alimjua. Alipokuwa tumboni Mungu alimtakasa, maana yake alimtenga kwa ajili ya utumishi na wito wake.
Lakini Yeremia hakuwa na uwezo wa kuamua. Kabla ya kuzaliwa huwezi kuamua, baada ya kufa huwezi kuamua kitu chochote. Ndio maana tunatamani kila mtu lazima aokoke, aamue anataka kuishi maisha ya namna gani baada ya kufa, maamuzi hayo unayafanya kabla hujafa. Baada ya kufa hakuna mahali pa kufanyia maamuzi hayo tena!
Kwa hiyo kipindi hiki, ambacho mwanadamu anaishi ndicho kipindi cha kukata maneno. Bonde la kukata maneno ni dunia hii. Makutano makubwa; maana yake aliona watu wengi sana wamekaa katika bonde ambalo wanatakiwa kufanya maamuzi.
Katika dunia hii, (Kama ulikuwa hujafahamu afadhali ufahamu), ya kwamba kati ya jambo muhimu sana ambalo utawajibika nalo mwenyewe ni kufanya maamuzi. Na yako maamuzi ambayo unahitaji kuwa mwangalifu sana unapotaka kuyachukua, kwa sababu yatasababisha mabadiliko ya maisha yako kabisa.
Kwa mfano maamuzi ya kuokoka, kwa mfano maamuzi ya kumtumikia Mungu, yanabadilisha kabisa maisha yako, ndio maana Yesu anasema, mtu kabla hajamfuata, akae chini, ahesabu gharama; kuna gharama katika kumfuata Yesu, na kuna gharama katika kumtumikia Yesu. Maisha yako yanabadilika kabisa! Huwa saa nyingine mimi na mke wangu tunatamani kuishi maisha ya kawaida kama watu wengine, lakini haiwezekani, (watumishi wa Mungu wataelewa kitu ninacho elezea hapa), ukiishafanya maamuzi ya kusema unataka kumtumikia Mungu, maisha yako hayawezi kuwa ya kawaida tena, sio maamuzi madogo hayo.
Kuna maamuzi ya masomo, watu wanafanya mchezo wanapotaka kufanya maamuzi ya masomo, usifanye mchezo, ni maamuzi muhimu. Kuna maamuzi ya marafiki, unataka kuwa na marafiki wakina nani. Maamuzi haya yanaweza yakakubadilishia kabisa maisha yako. Lakini pia kuna maamuzi ya unachotaka kufanya maishani mwako ni nini. Mwingine atajitetea na atasema, Mungu anajua, - sawa Mungu anajua, lakini anahitaji maamuzi yako!
Wengine wanasubiri wakiishamaliza sekondari, au wakiishamaliza chuo kikuu, ndipo waamue wanataka kufanya nini. Ukiishafika chuo kikuu ndipo unataka kuamua cha kufanya maishani, utakuwa umechelewa. Kwa sababu, kama unataka kuamua kufanya kitu ambacho hukusomea, mambo yanawezayakawa magumu kwako, labda iwe ni Mungu anakupitisha hapo kwenye eneo hilo jipya.
Lakini pia kuna masuala ya kuamua kuoa au kuolewa, katika somo hili tutaangalia somo linalosema, “Mambo ya kutafakari kabla ya kufanya uamuzi ya kuoa au kuolewa”. Wengine mnaosoma somo hili ni vijana ambao umri wa kufikia kuolewa bado, lakini huu ni muda muafaka wa kukufikirisha jambo hili. Wengine wanaosoma somo hili wana karibia - karibia kuoa au kuolewa; au wameshaingia kwenye ndoa tayari. Halafu wanajikuta ya kwamba, afadhali wangekuwa wamejiuliza na kutafakari yaliyomo humu mapema zaidi.
Kwa muda ambao Mungu ametupa wa kuwahudumia watu mbalimbali katika miaka ya utumishi ambayo Mungu ametupa, kati ya jambo ambalo limesababisha maisha ya watu wengi yakawa mabaya au yakawa mazuri, yakawa magumu au yakawa marahisi, ni suala la kuoa au kuolewa.
Saa nyingine huwa ninawaambia vijana, Kama kijana anataka kuoa au kuolewa na ana haraka sana ya kutaka kuoa au kuolewa, basi asije kwangu kwa ushauri! Kama unataka kuoa au kuolewa, na una haraka sana ya kufanya hivyo tafadhali usije. Kwa sababu mambo niliyoyaona kwenye ndoa mbalimbali yananifanya hata mtu akija kwa ushauri wa kutaka kuoa au kuolewa, nimpitishe kwenye maswali magumu sana yatakayomfanya atafakari sana na kuomba kabla ya kuamua kuoa au kuolewa.
Nia niliyonayo ni ili nijue kama kweli amefikia mahali ambapo anajua kitu anachotaka kufanya. Maana wengi wanafikiri ni jambo rahisi. Mungu wangu aweze kukusaidia kuona ili usilichukuie jambo hili kwamba ni jambo jepesi, maana linabadilisha kabisa maisha yako.


Hii ni sehemu ya utangulizi wa somo hili lililofundishwa na Mwalimu wa Neno la Mungu, ndugu Christopher Mwakasege. Tutaendelea kuwaletea sehemu zinazofuata.
Tunawapenda,
-Sayuni.

A Christian Is Not Perfect, But He Is Forgiven

Some people say you've either got to be black or white & there's no gray in between. But the fact of the matter is, there's no such thing as black or white, we're just about all gray!--Aren't we? Nobody is perfectly clean & white except by the blood of Christ & by faith!Look at some of the greatest men in the Bible!--Men of faith, but all of them made mistakes. They all became shining examples--not of their own greatness, but of their utter dependence on God.Nobody's ever good enough! We're all fallible, we all make mistakes, we all have sins, & it's only the grace of God that we are saved! It's only His Love & mercy & His grace & His sacrifice on Calvary that saves us!--Nothing else!--Nothing! Thank God Salvation doesn't depend on how good we are or even how bad we are! It only depends on our faith in the mercy & grace of Jesus Christ! In spite of all our sins & shortcomings, failures, mistakes & unsaintliness, God can still save us through Jesus! He still loves us & we can still be Christians if we will just receive the Lord & His gift of Eternal Life! Only Jesus is perfect & able to help us!--Which is why He had to come!

God bless you all, We love you all.
Sayuni.

Tuesday, October 21, 2008

KUPANDA MLIMA SAYUNI KWA AJILI YA TANZANIA

BWANA ASIFIWE SANA WAPENDWA.

TULITANGAZA MAOMBI HAPA MLIMA SAYUNI KUHUSU KUIOMBEA NCHI YETU HASA KATIKA MAMBO MAKUU HAYA MATATU.
1.SUALA LA OIC
2.SUALA LA MAHAKAMA YA KADHI
3.SUALA LA AMANI YA NCHI YETU.

MAOMBI NDIO NJIA PEKEE AMBAYO SISI KAMA WATU WA MUNGU TUNAWEZA KUITUMIA KATIKA KUTAKA MUNGU AFANYE YALE TUNAYOYATAKA KUHUSU NCHI YETU NZURI YA TANZANIA.

MAOMBI HAYA YALICHELEWA KUANZA HASA KWA KUWA TULIKUWA TUNASUBIRIA KUJUA TAREHE YA KUANZA BUNGE LETU ILI TUMWOMBE MUNGU AWAPE HEKIMA WABUNGE WETU WAWEZE KUAMUA MAMBO HAYA KWA MUHSTAKABALI MZURI WA TAIFA LETU.
KESHO TAREHE 22NA SISI WANAMLIMA SAYUNI TUNAAMUA KAMA ALIVYOFANYA ESTHER ALIPOINGIA KWA MFALME AHASUERO KUMWOMBA MUNGU KWA AJILI YA MAMBO HAYA.
MAOMBI YETU YATAKUWA NI YA KUFUNGA KWA WALE WATAKAO WEZA KWA MUDA WA SIKU 21 NA KAMA BWANA AKIKUWEZESHA WAWEZA KUFUNGA KWA KADRI ZA NGUVU ZA MWILI WAKO ILA HAKIKISHA KILA SIKU KABLA HUJAFANYA SHUGHULI YEYOTE ILE UNAMWOMBA MUNGU KUHUSU MAMBO HAYA KADRI BWANA ATAKAVYOKUWEZESHA.
KATIKA KITABU CHA ESTHER ,TUNASOMA KUWA MODEKAI ALIMWAMBIA ESTHER KUWA KAMA WEWE USIPOFANYA ZAMU YAKO USIDHANI KAMA MUNGU HATALETA MSAADA KWA ISRAEL KUTOKEA SEHEMU NYINGINE...NATAKA NIWAAMBIE WATU WA MUNGU WA TANZANIA...AMBAO MNASIMAMA KAMA ESTHER MAANA NAJUA WAPO MA ESTHER WENGI WANASOMA HABARI HII NA PENGINE WANASITA SISTA KUMLILIA MUNGU KUHUSU HABARI HII..BWANA ANASEMA KUWA .....ANAWEZA KULETA MSAADA KWA WATANZANIA KWA NJIA NYIGNINE KAMA MSIPOFANYA NA KUSIMAMA KWA ZAMU ZENU...HII HABARI NIMEIPENDA SANA KWANI ILITOKEA HUKU BARA HINDI (INDIA) AMBAKO NIPO KWA SASA.MFALME AHASUERO ALITAWALA SEHEMU KUBWA YA DUNIA KUTOKEA HAPA INDIA NA WANA WA ISRAEL WALITANGAZIWA KUANGAMIZWA KWA KUWA KUNA BAADHI YA WATU WALIMDANGANYA MFALME AHASUERO KUHUSU WANA WA ISRAEL HATA AKATIA SAHIHI WARAKA WA KUWAANGAMIZA WA ISRAEL.
LAKINI IKUMBUKWE KUWA MFALME AHASUERO HAKUWA MTU MBAYA ILA ALIPATA USHAURI MBAYA KUTOKA KWA JAMAA MMOJA ANAITWA HAMANI...UTASOMA ZAIDI KITABU CHOTE CHA ESTHER NA NDICHO KITAKUWA MSINGI MKUU WA MAOMBI YETU.
BIBLIA INASEMA KATIKA 2NYAKATI 7:14..IKIWA WATU WANGU ..WALIOITWA KWA JINA LANGU..WATAJINYENYEKEZA NA KUNITAFUTA NA KUNIOMBA ..NITAIPONYA NCHI YAO.....OOH HALELUYA......!
HUU NI WAKATI WA KUOMBA NA SI KULALAMIKA KAMA WAFANYAVYO WANASIASA..SISEMI KUWA SIASA NI MBAYA HAPANA...ILA NASEMA SISI KAMA WATU TUNAOMJUA MUNGU MAOMBI NDIO NJIA PEKEE YA KUBADIRISHA JAMBO LOLOTE...



KAMA UNAPENDA KUUNGANA NA WANASAYUNI WENGINE KATIKA KUOMBA KWA AJILI YA HILI...HEBU TUMA EMAIL KWENDA MIWLC@YAHOO.COM na ANDIKA SUBJECT YA EMAIL YAKO "HIVI "KUPANDA MLIMA SAYUNI KWA AJILI YA TANZANIA"KWENYE EMAIL YAKO ANDIKA JINA LAKO KAMILI, UMRI, MAHALI UNAPOISHI KWA SASA,UTAIFA WAKO, JINSIA YAKO,NAMBA YAKO YA SIMU UKIPENDA, PIA ANDIKA KWA KIFUPI KUHUSU KUUNGA KWAKO MKONO MAOMBI HAYA YA MNYORORO...TUTAANZA MAOMBI HAYA KUANZIA TAREHE 22/10/2008 .
N.B: EMAIL ZITAKAZOTUMWA HAPA HATUTAZITANGAZA HAPA UBARIKIWE NA BWANA YESU KRISTO WA NAZARETH.
AMEN

if my people, who are called by my name, will humble themselves and pray and seek my face and turn from their wicked ways, then will I hear from heaven and will forgive their sin and will heal their land. Now my eyes will be open and my ears attentive to the prayers offered in this place.

Monday, October 20, 2008

THIS WEEK'S SERMON!


Nehemiah: Lessons In Rebuilding

Is there something broken in your life that you’d like to fix, but don’t know how? A broken marriage, a failing business, a dying relationship? Or is there something that’s fallen apart that you’d like to rebuild: a house, a church, a ministry, a career? If so, then you'll love to learn some lessons in rebuilding from the biblical book of Nehemiah.

Nehemiah took on a rebuilding project that seemed imposing, impractical and nearly impossible. But when he told God what he wanted to do, and God gave him the green light to do it, God walked him through every step of the project. With God’s help, Nehemiah rebuilt a wall around the entire city of Jerusalem--a wall that is still standing and you can still visit today, several thousands of years later!

People told Nehemiah it was impossible; people tried to stop his work; people threatened his life. But Nehemiah pressed on. After many months of planning, praying, fighting and building, the work was finally completed. When all the surrounding countries, including his enemies, saw what Nehemiah had done, they also knew how he got it done. The book of Nehemiah says:

“...they realized that this work had been done with the help of our God” (Nehemiah 6:16).

If you’d like to learn how Nehemiah did it, and how God helped him along the way, I invite you to join me in learning about this great rebuilding project as recorded in the book of Nehemiah. If you’ve got something on your heart that you want to rebuild, I’d like to encourage you in the weeks ahead to do it.

Here’s a simple truth: if it matters to you, it matters to God. God cares about the details of your life. He cares about the things that you care about. That doesn’t mean that He always wants to head out and do whatever you want to do. Our plans are not always His plans. But if He doesn’t want you to do it, He’ll let you know, if you’re willing to listen. God has redirected many people’s good plans so He can do something better through them, (see 2 Samuel 7, for instance).

But if God does want you to go forward with your plans, He’d love to help you succeed. He is undoubtedly for you. He created you, He loves you and He has an incredible plan for your life. You could say He has a “vested” interest in you, because He’s in-vested so many gifts and skills into your life because He has so many things He wants to do through you.

The hardest part of starting a project is often believing that God really wants you to do it; that He really cares, and that He’ll really help you every step of the way. Once you know that, you’re half-way there! After that, it’s just a matter of figuring out the details of how to proceed. I hope this study encourages you on both levels, giving you both the confidence to believe in the project that’s on your heart, and giving you the practical steps to do it.

Nehemiah followed a series of practical steps to rebuild the wall around Jerusalem, steps which you can follow to rebuild the things in your own life that need rebuilding. It involved much prayer, much planning, many people and fair amount of hard work. But He didn’t have to do it alone: God helped him all along the way.

By the end of this study, I hope that you’ll have the confidence and the tools that you need in order to reach the goal that Nehemiah reached as recorded in Nehemiah 6:15:

“So the wall was completed...” (Nehemiah 6:15).

Those words are stated with such simplicity that they could never do justice to the work involved, nor the accomplishment that was achieved. But they are stated in a way that when I hear them, I’m inspired that what Nehemiah was able to accomplish, I just might be able to accomplish, too, with God’s help. My prayer is that they inspire you as well.

As we go through this study, I’ll include Scripture Reading to go with each devotional. I hope you’ll read these passages along with what I write, because I can only touch on one or two thoughts each time, but God has so much He wants to say to you! By the end of the study, when you’re finished reading each of these Scripture Readings, you’ll have also read through the entire book of Nehemiah.

I’ve also included a prayer that you can pray with me at the end of each devotional. I hope this helps you to begin a quiet time of prayer with God in response to what you’ve read. Here’s today’s prayer:

Prayer: Father, open my eyes to see what Nehemiah saw that helped him to accomplish what was on his heart, and help me learn how to do the same. In Jesus’ name, Amen.

Today’s Scripture: Nehemiah 6:15-16
(Read these verses online at: http://www.biblegateway.com )

May the Lord Bless you always. Please welcome your friends to join this Mailing Lists.

Sunday, October 19, 2008

Salamu kutoka India

Bwana asifiwe sana wapendwa,
Kwa sasa nipo India,hapa New Delhi.
Leo nimetafuta mahali pa kuabudu sijapaona...naomba wapendwa na wanasayuni mliopo hapa India mnielekeze sehemu nzuri ya kuabudu..hasa hapa New Delhi na kule Derhadun maana nitakaa muda mwingi huko kwa kipindi nitakachokuwa hapa..
Mbarikiwe sana na nitakuwa nawapatia habari katika mlima sayuni kutokea huku kwa kadri Bwana YESU atakavyokuwa ananijalia..
Mbarikiwe sana..

Mtade,
Sayuni

Friday, October 17, 2008

Billy Graham kusherekea Birthday yake ya 90!

BWANA YESU ASIFIWE!
Ndugu wapenzi wa Mlima Sayuni, sina shaka kuwa wengi mnamfahamu au mmewahi kumsikia sana Mtumishi wa Mungu mzee Billy Graham wa USA, namna ambavyo amekuwa akimtumikia Mungu kwa zaidi ya miaka 60 sasa. Mnamfahamu pia mtoto wake anayeendeleza kazi hii ya Injili, aitwaye Franklin Graham. Familia yake ipo kwenye kipindi cha furaha kuu kwani mtumishi huyu wa Mungu (Billy Graham) anasheherekea sikukuu yake ya kuzaliwa(Birthday) November 7,hii ikiwa ni ya 90!

Mtoto wake na wanatimu wote wa shirika lake la kueneza Injili wamewakaribisha watu wote ambao wamewahi kuguswa na huduma ya mtumishi huyu kushiriki katika sikukuu yake hiyo, kwa njia ya internet. Unaweza kubonyeza (Clicking) hii picha yake na utaletewa mahali utakapoweza kumwandikia Ujumbe mfupi ambao atasomewa katika hiyo sikukuu yake.

Sisi kama watumishi wa Mungu, tunajisikia furaha na amani sana tunapoona Bwana amempa uhai na afya njema hata katika umri huu wa miaka 90! Je, hili nalo siyo moja ya matendo makuu ya Mungu? Hakika! Hii itutue moyo sisi wote tunaomwamini Bwana, Biblia inasema "Tutalala katika umri mwema" ,"tukiwa tumeshiba siku nyingi" tena "Sitakufa bali nitaishi niyatangaze matendo ya Bwana" Tunauona huu kama ushuhuda wa Upendo wa Baba yetu aliye juu.

Je, una lolote la kusema kuhusu hili? tueleze.

Mungu akubariki, nawe "usife bali uishi na kuyatangaza matendo makuu ya Bwana"

Sisi wana-Sayuni wote tunambariki ndugu Billy Graham katika Jina la Yesu na kumwombea miaka mingine MINGI kwa utukufu wa Baba.-Amen.

If You've Been Born Only Once You'll Die Twice, But If You've Been Born Twice You'll Die Only

If You've Been Born Only Once You'll Die Twice, But If You've Been Born Twice You'll Die Only

OnceIf you've been born physically of the flesh, & then born again of the Spirit by receiving Jesus' pardon for your sins, then you die only once--physically. But if you've only been born once, just physically, you're going to die twice! First the natural physical death; second the spiritual death, "the second death"! (Rev.20:14)Christ's death was far worse than mere crucifixion & the physical agony that He was suffering. He was suffering the spiritual agony of the lost sinner dying for his sins, without Salvation, without God! Only in His case He wasn't dying for His Own sins, He was dying for the sins of the World!--Yours & mine! He did that so you won't have to go through that horror of dying a sinner's lonely death!Those who reject Christ's atonement have to suffer for their own sins. But those who receive Jesus now are completely forgiven & completely relieved from the punishment of sin. "For the blood of Jesus Christ cleanses us from all sin!" (1Jn.1:7)So make sure you're born again, & you'll die only once!--Then you go to be with the Lord forever!

God bless you all.
Team at Sayuni.

PRAY FOR OUR FELLOW BROTHERS AND SISTERS

Praise the Lord!
Please we beg you all, let us pray for these our fellow brothers and sisters who are facing persecution because of their faith. PLEASE pray for them, do not ignore them.

UZBEKISTAN
– Christian Released from Prison – VOM Sources/Forum 18 NewsPraise God! Aimurat Khayburahmanov, a Christian arrested and detained on charges of terrorism in the autonomous region of Karakalpakstan, was released on Sept. 30, according to Forum 18 News and VOM sources. The Nukus City Criminal Court ruled that the “religious extremism” charges against Khayburahmanov be dropped and that he receive amnesty for the charges of “teaching religion without official approval.” Praise the Lord for his release. Ask God to protect Aimurat as he continues serving the Lord despite pressure from the government. Pray for other believers in Uzbekistan who are facing prosecution because of their faith.Philippians 4:6-7

IRAQ
- Christians Killed in Mosul – Associated Press/VOM SourcesSeven Christians have been killed in Mosul, Iraq, so far this month, The Associated Press and VOM sources reported. On Oct. 4, an armed group of suspected Islamist extremists assassinated a man named Hazim Thomaso Youssif in front of his clothing shop, and Ivan Nuwya was shot to death in front of his home, located near a mosque in the Christian-majority neighborhood of Tahrir. Meanwhile on Oct. 6, a disabled 25-year-old shopkeeper was shot and killed in the neighborhood of Karama. The Associated Press reported Iraqi police said four other Christians, a pharmacy employee, a disabled man who owns a spare-parts store and two day-laborers have also been killed. Some Christians believe that extremists are targeting shopkeepers in an effort to wipe out the Christian community's economic activity and drive out believers from the area. Pray for those who mourn these lost lives. Ask God to continue to embolden the Christian community in Mosul to proclaim the gospel even while suffering.2 Timothy 4:16-18

INDIA
– More Christians Killed in Anti-Christian Violence in Orissa – VOM SourcesAt least three more Christians have been killed in the widespread violence that began seven weeks ago in Orissa state’s Kandhamal district. On Oct. 1, an elderly Christian, Lalji Nayak, died from axe wounds he received when a mob of Hindu extremists attacked the village of Hrudangia. His wife, also attacked with an axe, was seriously injured in the head, and his brother was hospitalized with multiple gunshot wounds. Meanwhile on Oct. 2, two men were dragged out of their home in Sindhipankha village, shot and then dismembered. The assailants also massacred cattle belonging to believers and burned homes owned by Christians. Approximately 400 homes have been set on fire by extremists in Kandhamal and Boudh districts over the past week. Pray that those who mourn will find peace in the fact that those who have suffered with Christ will be glorified with Him. Pray for healing for those injured. Pray that Christians in India will continue to live as cross-bearing disciples and remain steadfast in faith at all cost.Romans 8:15-17

SOMALIA
– Church Destroyed by Islamic Extremists – VOM SourcesOn Sept. 30, Muslim extremists demolished a Catholic church in Kismayo, a town in southern Somalia, VOM sources reported. The area has been in the control of a militant Islamic organization affiliated with Al-Qaeda since August. The militants have vowed to launch similar attacks on all other local non-Muslim places of worship. They plan to replace the destroyed church with a mosque. Islamists have reportedly imposed Sharia law in Celwaq, another southern town, elevating concern for Christians in the region. Pray that the believers in Somalia will be steadfast in their service for the Lord. Pray that they will rejoice in the opportunity to grow in Christ likeness through their tribulations.James 1:2-4

Please share this with others too and be blessed always.
-Lema for Sayuni.

Wednesday, October 15, 2008

Ni muhimu na lazima kuanza mapema kuuombea uchaguzi mkuu 2010.

BWANA YESU ASIFIWE!
(hili ni somo nililolituma kwa wale waliojiunga na Mailing lists)

KUZIJENGA KUTA ZILIZOBOMOKA NA KUSIMAMA MAHALI PALIPOBOMOKA TANZANIA-2
• Ni muhimu na lazima kuanza kuombea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 Tanzania.

Katika somo nililotuma mara ya mwisho, Roho Mtakatifu alikuwa anatuhizima sote tudumu katika kuomba toba kwa ajili ya taifa letu la Tanzania, Bwana Yesu asifiwe kwa ajili ya watu wote ambao tayari wamechukua hatua kuanza kufanya hivyo, wale walionitaarifu pia na wale ambao hawajanitaarifu, awape nguvu zaidi. Katika somo hili la leo, nataka niweke ndani yako wito (“mzigo”) wa kuanza kuombea uchaguzi mkuu wa viongozi wa Serikali wa Tanzania, utakaofanyika mwishoni mwa mwaka 2010. Katika mazoea yetu, huo mwaka 2010 waonekana kuwa mbali sana kutoka sasa, lakini nafikiri hii ni picha ya kimwili tuu, kwa sisi tumwaminio Bwana, kipindi hicho kii karibu nasi kuliko ionekanavyo katika mwili. Ninaamini unafahamu kuwa, shetani akitaka kuweka watu wake kwenye uchaguzi huo, basi yeye hataanza jitahada zake ikifika hiyo 2010, yeye huanza mapema sana, labda kwa sababu Biblia inasema “Kwa kuwa anajua anao wakati mchache”. Na sisi watu tuliookoka tunatakiwa kuanza kufanya hivyo mapema, mapema kumzidi hata “adui” yetu. Hii ndio sifa ya walinzi bora, wale tuliojifunza katika sehemu ya kwanza ya somo hili. Baba Mungu anapenda aanze kufanya kazi yake mapema, lakini kumbuka siku zote kuwa Baba Mungu mara nyingi anatusubiri tufanye kitu (tuombe) ndio na yeye atusaidie. Tukikaa kimya bila kuomba, tunaweza kupata viongozi wasio-mpango wa Baba Mungu na hasara zake zikatupata wote. Neno la Baba Mungu linatuagiza katika kitabu cha 2 Timotheo 2:1-3: “1Basi, kwanza kabisa, naagiza kwamba dua, sala, maombezi na shukrani zitolewe kwa ajili ya watu wote: 2kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani, tukimcha Baba Mungu na kuwa wenye heshima kwa kila njia. 3Jambo hili ni jema na linampendeza Baba Mungu Mwokozi wetu “ Neno hili ni wakati wake sasa kwa sisi wote kuliweka katika matendo kwa ajili ya nchi yetu ya Tanzania. Kwa wale ambao hupata nafasi ya kufuatilia vikao vya bunge la Tanzania, wanaweza kuelewa ni kitu gain kitatokea kama Baba Mungu asipoweka watu wake kule ndani ya bunge. Vivyo hivyo kwa sehemu nyingine za madaraka katika nchi yetu. Kama wote tujuavyo, Baba Mungu akitaka kufanya kitu mahali, huwatumia watu wake aliowaweka hapo mahali, na shetani vilevile, akitaka kufanya maovu yake mahali, huwatumia watu wake walio mahali hapo. Kwa hiyo ni muhimu na msingi sana tumwombe Bwana Baba Mungu ili awaweke watu wake katika sehemu mbalimbali za uongozi katika nchi hii. Tumwombe atupe rais anayemjua, makamu wake, waziri mkuu, mawaziri wote na manaibu wao, wabunge, madiwani, wenyeviti wa vijiji, lakini pia wakuu wa mikoa, wilaya na maeneo mengine yote. Ni imani yangu kuwa kama Kanisa tukijipanga vizuri na kuanza kuomba, basi Baba Mungu atakaa upande wetu na atatupa viongozi watakatuongoza kwa kufuata Neno la Baba Mungu. Tatizo au kosa ambalo tumekuwa tukilifanya ni kwamba huwa tunasubiri hadi ule mwaka wa uchaguzi ndiyo tunaanza kuombea uchaguzi huo. Sisemi kuwa Baba Mungu hatajibu kabisa, lakini ni vizuri zaidi kuanza kuomba mapema iwezekanavyo. Maana naamini michakato hii ya uchaguzi imeshaanza ‘kimyakimya’ ndani ya wanasiasa na vyama vyao hata sasa. Ninaamini kuwa kila chama kimeshaanza kuweka umakini mkubwa kwenye uchaguzi wa 2010, kulizidi kanisa. Inatupasa mimi na wewe, na vikundi vyetu vya maombi pamoja na waombaji wengine, tuanze kumwomba Baba Mungu ili kuanzia katika ngazi ya chama, aanze kuwainua na kuwaweka watu kwa ajili ya kugombea nafasi katika uchaguzi wa 2010. Tena tumwombe Baba Baba Mungu ili awaondoe/kuwazuia watu wote ambao shetani kwa hila zake atajaribu kuwaingiza katika harakati zote za uongozi wa nchi hii. Ni muhimu sana kuombea jambo hili kwani viongozi wa serikali wana athari kubwa (nzuri au mbaya) katika taifa wanaloongoza. Ikumbukwe pia kuwa, maamuzi ambayo viongozi wanayafanya yanatuhusu sisi kanisa la Mungu pia, yanagusa hata namna kazi ya Mungu Baba inavyofanyika katika nchi hii. Tukipewa viongozi wamjuao Bwana Mungu, basi itakuwa ni rahisi zaidi kwa taifa la Tanzania kupokea Baraka nyingi sana ambazo Mungu ametuahidi (sisi kama Tanzania) Ni wakati muafaka sasa, sote tuamke na kushika zamu zetu kuanza kuomba kwa ajili ya uchaguzi wa 2010, tumwombe Mungu Baba atupe viongozi; wanaomjua yeye sana (Ayubu 22:21), wenye hofu ya Mungu na wacha Mungu, watakoongoza hii nchi kwa kufuata Neno la Mungu, watakapenda kutenda haki n,k kama Roho atakavyokuongoza. Unapokuwa kwenye maombi likumbuke hili, unapokuwa kwenye vikundi vya maombi kanisani au popote usisite kuwashirikisha wengine jukumu hili. Ninaamini kuwa Roho Mtakatifu ataendelea kusema na wewe juu ya jambo hili na Yeye pia atakusaidia kufanya sehemu yako katika kuhakikisha kuwa mapenzi ya Mungu yanatimia katika uchaguzi wa 2010 na katika mambo mengine yote katika nchi hii.

(**Kupokea masomo mengine kupitia email yako, jiunge na mailing lists kwa kutembelea www.lema.or.tz)

Tuendelee kuombeana daima.
Katika Utumishi wa Kristo,
Frank Lema. Arusha.

This Week's Sermon

What It Means To Be “Saved”By Eric Elder


When people say they’re “saved,” what do they mean? And what exactly are they saved from?

To say you’re saved means more than just the fact that you’re a Christian. It means you’ve been saved from something. Specifically, it means you’ve been saved from hell, both the literal hell that Jesus talked about when people are separated from God for all eternity, and the practical hell that you can experience here on this earth when you continue to follow your own sinful ways.

To someone who isn’t “saved,” the word seems to be either offensive or just plain laughable. But to someone who is “saved,” the word is full of life, because they know what would have happened to them had Jesus not come to save them.

I read this week that one of the candidates running for office is being questioned because their pastor “preaches hell for anyone who doesn’t believe in Jesus.” I guess when you put it that way, it does sound rather offensive. But the truth is, it’s the same message that Jesus preached. (Good thing He isn’t running for office--He’d probably get crucified again!)

Some people, unfortunately, think that Jesus is out to get them, that He came to condemn them for what they’ve done. But Jesus didn’t come to condemn you. He came to save you. He even says so in His own words:

“For God did not send His Son into the world to condemn the world, but to save the world through Him. Whoever believes in Him is not condemned, but whoever does not believe stands condemned already because he has not believed in the name of God’s one and only Son” (John 3:17-18).

So, yes, there is hell to pay if you don’t believe in Jesus. But no one’s going to hell because they haven’t believed in Jesus; they’re going to hell because of their sins, which is a completely different reason altogether. Whenever you sin, it separates you from God. And without a savior, you’d be separated from God forever. That’s hell. That’s the fate from which Jesus came to save you.

When the Apostles Peter and John were arrested for preaching that Jesus could save people from their sins, they didn’t back down even when threatened with death. In Acts chapter 4, they spoke boldly about the fact that Jesus alone had the power to save:

“Salvation is found in no one else, for there is no other name under heaven given to men by which we must be saved” (Acts 4:12).

Faith saves. One of my favorite scenes in the Indiana Jones series is when Indy comes to the edge of a cliff and can’t see any way across to the cliff on the other side. With a look of exasperation, he says, “It’s a leap of faith!” With his enemies pressing in from behind and no other way forward, he takes a giant step into what looks like thin air in front of him, only to find that he has stepped onto a solid rock bridge that had been camouflaged from view. Indy’s “leap of faith” had saved him.

Jesus wants to save you from more than just a bad ending to the movie of your life. He wants to save you from hell, both here on earth and on into eternity.

When Jesus died on the cross, He extended an invitation to every person in the world who had strayed from God to come back to Him. The price for our sins had been paid. But reconciliation is a two way street. Just because one party wants to be reconciled with the other doesn’t mean they are reconciled. Both parties have to agree to it.

Jesus has done His part. Now He’s waiting for each person to respond individually. And the way you respond is by faith.

If you’ve never put your faith in Christ to save you from your sins, I pray you’ll do it today. He’d love to say to you what He said to the woman who wiped His feet with her tears:

“Your sins are forgiven. Your faith has saved you; go in peace” (Luke 7:48,50).

Let’s pray...

Father, forgive me for the sins I have committed, too, as I put my faith in Christ. In Jesus’ name, Amen.

-----------------

Friday, October 10, 2008

There Is Great Power In United Prayer Together

There Is Great Power In United Prayer TogetherSome people are a bit shy about praying with others, & sometimes they probably think about what Jesus said, "When thou prayest, enter into thy closet & pray to thy Father which is in secret; & thy Father which seeth in secret shall reward thee openly." (Mat.6:6) Well, there is a time for that, but there is also a time to pray together!Sometimes it's important that you make your request known, not only to the Lord, but to others also, in order that they can join with you in prayer & manifest their faith & confess their dependence upon the Lord along with you. So never be ashamed to ask for prayer when you need it!The Lord loves to give the answers & He has to give the answers when He sees we're united in love & prayer & purpose & mind & heart & spirit. "Where two or three are gathered together in My Name, there am I in the midst of them." And, "if any two of you shall agree on Earth as touching anything that they shall ask, it shall be done for them of My Father which is in Heaven." (Mat.18:20,19) God's dynamics of the Spirit really operate amazingly! The Lord says, "When one can only chase a thousand, two can put ten thousand to flight!" (Deu.32:30)--So pray together!
VOM Prayer Update for October 6, 2008On Tue. Oct 07 2008 at 09:02 AM Moderator wrote: IRAN - Two Iranian Christians released from prison - VOM SourcesUPDATE: Praise God! The Voice of the Martyrs contacts report that on Sept. 25 two Christians, Mahmood Matin Azad and Arash Basirat, were released from prison in Shiraz. "A reliable source reported the two men appeared before a local judge and they have been released. The families are very grateful for your prayer support. Please continue to pray for their recovery and safety," VOM contact said. Azad and Basirat were arrested on May 15 and charged with apostasy. Believers around the world had expressed concern for them because of the impending law in Iran that makes death the only punishment for apostasy. VOM actively supports persecuted believers in Iran and provides resources for them to share the gospel and disciple new converts. Pray for the safety of Azad and Basirat and ask God to use their testimony to bring their persecutors into the knowledge of Jesus Christ.Philippians 4:6-7

KENYA - Muslim Youth Attack Church
- Compass Direct NewsCompass Direct News reported that more than 49 Muslim youth stormed into The Redeemed Gospel Church in Garissa, Kenya, on Sept. 14 and attacked those present. The mob threw stones at the congregation, damaged pews and walls, destroyed the pulpit and burned a church banner. The attack was sparked by tensions between local Muslims and Christians over a mosque that was constructed three meters from the church building in June 2007. When the mosque was constructed Christians complained that it blocked the church's entryway. Local authorities proposed Christians relocate to a new worship site, but the believers refused to do so, arguing that the solution was only temporary. At last report, the Christians were being prevented from returning to the ransacked church building and did not have a new building in which to worship. Pray that believers will be encouraged to continue meeting together for worship despite opposition. Pray that Christ will work in the hearts of those who oppose Him, so that they, too, will know the Good news. Hebrews 10:23-25

INDIA - UPDATE - Christians Targeted by Bombs -
VOM Sources OrissaThe Voice of the Martyrs contacts in Orissa state report hat three relief camps housing Christians in Kandhamal district were bombed on the evening of Sept. 29. The explosions began at 7:00 p.m. and bombs went off in the villages of Nuagoan and Mahasinghi and the town of Baliguda. VOM contacts believe Hindu extremists are responsible for the attack. For the sixth week, extremists have continued to use violence and intimidation against Christians in relief camps, in an attempt to forcibly convert believers to Hinduism. Several Christian families in the camps have succumbed to pressure form extremists and "reconverted" to Hinduism in exchange for being allowed to return to their homes in Ladapadar village. Fresh violence also persists outside the Kandhamal camps, including the burning and bombing of homes and church buildings. Pray for safety and protection for believers in the relief camps. Pray that Christians in India will stand firm in their faith despite severe pressure to deny Christ.Joshua 1:8

Dear Sayuni visitors, PUSH! --- ( Pray Until Something Happens!)
God Bless you abundantly.
Sayuni.

Monday, October 6, 2008

This week's sermon:The Power of Faith


At the end of the book of Acts, you’ll see that Paul finally made it to Rome. He stayed there for two years awaiting his trial before Caesar, living in his own rented house under house arrest. He welcomed all who came to see him, preaching boldly about the kingdom of God and teaching about Christ.

And that’s where the book of Acts ends.

In some ways, it seems like the book ends in mid sentence--like there’s a page or two still missing. What happened to Paul? Did he ever make it to his trial? Was he ever able to testify before Caesar?

Even though the Bible doesn’t record what happened next, I believe that Paul did make it to his trial and that he did get to testify before Caesar. Why? Because the same God who brought Paul this far had also told Paul that he would one day testify in Rome. Back in Acts 23, when Paul was first arrested in Jerusalem and when many were plotting to kill him, God said to Paul:

“Take courage! As you have testified about Me in Jerusalem, so you must also testify in Rome” (Acts 23:11).

Then again in Acts 27, when Paul’s shipmates were about to give up hope that they would ever be saved from the storm, an angel of God spoke to Paul again, as Paul told the men:

“Last night an angel of the God whose I am and whom I serve stood beside me and said, ‘Do not be afraid, Paul. You must stand trial before Caesar; and God has graciously given you the lives of all who sail with you.’ So keep up your courage, men, for I have faith in God that it will happen just as He told me” (Acts 27:23-25).

That’s the kind of faith I’ve been praying for myself--and for you as well--all throughout this study, the kind of faith that says, “I have faith in God that it will happen just as He told me.” Because I know, like Paul knew, and like Christ knew, that when you have faith in Christ, nothing will be impossible for you.

In the mid-1900’s, there was a woman who did all kinds of miracles in the name of Christ, seeing people saved, healed and delivered from various addictions. When asked what kind of gift God had given to her to be able to do so many things, she said she didn’t have the gift of evangelism, or healing or prayer. She said she had the gift of faith. And with faith, all kinds of things are possible.

We’ve seen through the book of Acts how faith helped these earliest of believers to do all kinds of things. We’ve seen that faith waits, acts, heals, saves, obeys, fills, speaks, explains, surrenders, gives, includes, prays, fasts, persists, purifies, sings, examines, works, baptizes, resurrects, dies, testifies, keeps a clear conscience, appeals, models, warns and supplies. And I have a feeling that’s just the beginning.

The truth is the book of Acts really is unfinished. Jesus is still alive. He’s still working through people today. And He still wants to work through you. You may be surprised at what you can do when you put your faith in Him. For all the incredible things that Jesus did, here’s what He said you could do if you had faith in Him:

“I tell you the truth, anyone who has faith in Me will do what I have been doing. He will do even greater things than these, because I am going to the Father” (John 14:11-12).

As we finish this study together, my prayer is that the following words of Christ would echo in your ears in the days ahead, words that will give you the faith to do all that Christ still wants you to do:

“I tell you the truth, if you have faith as small as a mustard seed, you can say to this mountain, ‘Move from here to there’ and it will move. Nothing will be impossible for you” (Matthew 17:20).

Let’s pray...

Father, give me the faith to move mountains and more, in Jesus’ name, Amen.


God bless you all, please remember to invite your friends to Sayuni.
Much blessings.