Wednesday, February 25, 2009

JE UNAFAHAMU FAIDA ILIYOPO KATIKA KUIMBA NYIMBO ZA ROHONI?--2

KUIMBA NA KUSIFU –SILAHA KUBWA KATIKA VITA.

Ndugu katika Kristo, Nakusalimu katika Jina lipitalo majina yote, Jina ambalo kwalo sisi wanadamu wote tunaokolewa kutoka dhambini, Jina linalotubariki, Jina linalotuweka huru, Jina zuri la Yesu Kristo. Nakutakia neema na amani tele katika kumjua Mungu na Yesu Bwana wetu. (1Peter 1:2)

Wiki iliyopita kwa msaada wa Roho Mtakatifu tulijifunza sehemu ya kwanza ya somo hili, linalotuonesha umuhimu wa sisi tumwaminio Kristo kuimba nyimbo za rohoni. Ninaamini Roho Mtakatifu alikuwa juu yako kukufundisha na ukaelewa vizuri, ninanamshukuru Yeye hata kwa ajili ya wale walionitumia shuhuda zao. Kati ya hao, ndugu mmoja alinieleza kuwa kuna wakati alikuwa kiimba nyimbo za Tenzi za Rohoni akiwa anaishi katika nyumba za kupanga, na ikawa inatokea kuwa kuna wakati akiwa anaimba, mapepo yanawapagawa na kuwatoka baadhi ya wapangaji wengine, pamoja na kuwa alipewa notice kwenye nyumba hizo.

Leo tunaendelea na sehemu hii ya pili na ya mwisho ya somo hili, na leo tuangalia Faida za kuimba nyimbo za sifa&kushukuru mara tuwapo katika mapito magumu.

Leo tutazama vita ya ajabu kama ilivyorekodiwa katika kitabu cha 2 Mambo ya Nyakati sura ya 20. Ili kukusaidia wewe kuelewa vizuri zaidi habari hii ninakupa shauri, pata muda na usome vizuri sura nzima hii ya 20, mimi hapa nitataja mistari michache tuu.

Habari hii inaanza katika mstari wa kwanza kabisa, ambapo tunaona kuwa mataifa matatu yalitoka na kwenda kujipanga kuwavamia wana wa Israeli (kabila lile la Yuda) katika nchi yao waliyopewa kukaa na Mungu Baba. Ndipo mtu mmoja akatoka na kwenda kumpa mfalme wa Israel (Yehoshafati) habari hizi za uvamizi. Hizi zilikuwa ni habari za kusikitisha na kuogopesha sana, kwa ilikuwa ni mataifa matatu yaliyojiandaa yanawavamia wana wa Israeli, wale wa Yuda, taifa moja.

Biblia inatuambia wazi kabisa katika mstari wa tatu kuwa hata Yehoshafati mwenyewe aliogopa, lakini kulikuwa na jambo moja zuri katika kuogopa kwake- yeye alikwenda kumwomba Mungu Baba juu ya uvamizi huu na akatangaza kufunga katika nchi nzima (ingekuwa baraka namna gani kama leo Taifa zima la Tanzania, au angalau hata kanisa tuu tukapanga kufunga siku Fulani kwa ajli ya jambo Fulani katika nchi yetu?) na tunaona kuwa walitoka katika miji ya Yuda na wakakusanyika pamoja kumwomba Mungu Baba kwa ajili ya hili.

Tunaona kuwa baada ya kukutana mbele za mfalme, mfalme aliomba maombi ambayo yalifanya hata wana wa Israeli wakatiwa moyo. Kisha Roho Mtakatifu akashuka juu ya nabii mmoja naye akasimama na kuwaeleza watu wote kuwa wasiogope kwani Baba Mungu anasema kuwa vita sio vyao bali ni vya Bwana(mstari wa 15)-{Ni vyema na wewe ukajisemea na kuamini hili kila mara unapokutana na majaribu mbalimbali katika maisha yako}. Kwa maana nyingine, Mungu alikuwa amekuja kuwasaidia katika vita vile. Kisha yule nabii akaendelea kuwaambia kuwa hawatahitaji kupigana vile vita, bali wao wafike tuu katika uwanja ule wa mapambano na waoune wokovu wa Bwana. Wakamwabudu Bwana (inawezekana waliimba nyimbo za kuabudu) na wakalala usiku ule kwa amani.
Wakaamka asubuhi iliyofuata, ambayo ilikuwa ndiyo siku ya kwenda vitani, sasa kwa namna tuliyozoea sisi, tungejipanga kwa kila mtu kupewa silaha na kufundishwa namna ya kupigana-hata kama tumeshaambiwa kuwa vita ni vya Bwana na sio vyetu, lakini alichofanya mfalme Yehoshafati ni tofauti kabisa na ndio hasa ninataka ujifunze wiki hii nzima.

Biblia inatuambia kuanzia mstari wa 21 kuwa, mfalme aliamka asubuhi ili kuongea na watu juu ya vita vilivyo mbele yao, na badala ya kuwapanga namna ya kupigana, yeye aliwapanga watu kwa ajili ya kuimba nyimbo za kumsifu Bwana kwa uzuri wa utakatifu wake. Tena akawaambia watangulie mbele ya jeshi lao wakiimba na kusema “Msifuni Bwana kwa maana fadhili zake zadumu milele”

Mstari wa 22 unasema “ Na walipoanza kuimba na kusifu, Bwana akaweka waviziao kinyume cha wana wa Amoni,Moabu na mlima Seiri waliokuja kupigana kinyume cha Yuda; nao wakauawa” Biblia haiweki wazi kuwa hawa “waviziao” ni kina nani lakini inavyoonesha, hawa ni malaika ambao Bwana aliwateremsha kuja kuwasaidia Yuda. Na kilichotokea ni wale wa mataifa waliokuja kuwashambulia wana wa Yuda walianza kupigana wao kwa wao hadi wakamalizana. Wana wa Yuda walipofika hapo walipo, walikuta maiti zao tuu, maadui zao wote walikufa! Huu ni ushindi mkubwa sana ambao Bwana aliwapatia bila nguvu zao hata kidogo na tunaambiwa kuwa wana wa Yuda walitumia siku tatu kukusanya nyara (mali) walizokuwa nazo wale maadui zao na kisha wakamshukuru Bwana.
Hebu utazame tena huo mstari wa 22. Utaona kuwa umeanza na maneno “na walipoanza kuimba na kusifu, Bwana akaweka waviziao………..” Maana ya haya maneno ni nini katika mstari huu?
Maana yake ni kwamba, Bwana hakuanza kuwapigania wao ila mpaka pale walipanza kuimba na kusifu. Yaani muda wote Bwana alikuwa kimya anawatazama watafanyaje, walipoanza kuimba na kusifu ndio akawapigania. Tupo pamoja?

Je unajifunza nini hapa? Hii ina maana kuwa wasingeanza kuimba na kusifu, Bwana angekaa kimya kabisa, nap engine wangeamua kupigana vita vile kwa nguvu za jeshi lao na wangeshindwa kwa sababu huo ulikuwa siyo mpango wa Mungu Baba kuwasaidia (sio kila mpango ni mpango wa Bwana kukusaidia pale upatapo shida). Hivyo Bwana alikaa kimya hadi pale walipoanza kuimba na kusifu.

Sasa nataka ujiulize, ni kwa nini Bwana awasubiri hadi waimbe na kusifu? Kwa nini sio hadi waombe na kufunga siku kadhaa? Kwanini kuimba?
Ukijiuliza swali hili utaona tena faida nyingine ya kumsifu Bwana pale unapopita katika magumu ya ulimwengu huu.

Sababu iliyopo ni kwa kuwa “Uimbaji ni sauti ya Imani” (“Praise is the voice of faith”). Yaani, unapoimba wimbo Fulani katika Roho, kwa kumaanisha, unaonesha imani iliyo ndani ya moyo wako kwa Bwana. Baada ya kumwomba Baba Mungu juu ya jambo fualani, je unaamini kuwa atakufanyia kama ulivyomwomba? Je, unaioneshaje imani yako? Njia mojawapo ya kuonesha imani ya mtu anapopita katika hali Fulani ngumu ni kwa kusikiliza maneno anayosema juu ya hali ile ngumu. Ukimsikia anasema maneno ya kukata tamaa, kuwa haamini kuwa Bwana atamsaidia hapo, basi ujue imani yake imekufa (na hiyo ni hali ya hatari) lakini ukimsikia anakiri ushindi kutoka kwa Bwana hata kama hali ni mbaya kiasi gani, basi mtu huyu anayo imani iliyo hai na Bwana atamsaidia mara moja.

Kwahiyo unapopita katika majaribu au hali yoyote ngumu usiyoipenda, ni vyema kumwomba Bwana kwa Jina la Yesu, na baada ya kumwomba, Atataka kuona imani yako, kwa hiyo anza kuimba nyimbo kadha wa kadha za kumsifu Bwana, uziimbe kwa kumaanisha na moyoni mwako ukimsifu Bwana kwa kukusaidia katika hali ngumu unayopitia, maana hiyo ndiyo imani yako. Ukifanya hivyo, wewe utakuwa ni sawa na wale wana wa Yuda walipoanza kuimba na kusifu, na Bwana akaja na kuwasaidia. Bwana atakusaidia na wewe. Na hilo ndilo kusudi la Roho Mtakatifu kukuletea ndani ya moyo wako nyimbo za kusifu kama tulivyoona kwenye sehemu ya kwanza ya somo hili.

Ninaamini kuwa umeona faida nzuri zilizo katika kumwimbia Bwana nyimbo katika Roho, kwa kumaanisha. Ukijisomea Biblia zaidi pia unaweza ukaona namna huduma ya uimbaji ilivyo ya muhimu sana katika kuujenga mwili wa Kristo. Na ninaamini kuwa utabarikiwa sana ukiyaweka haya katika matendo.
Watu wote tumshukuru na kumsifu Mungu Baba kwa kutuletea somo hili kwa wakati huu, na hapa ikiwa ni mwisho wa somo hili, Amen.
********************

SEMINA YA MWAKASEGE ARUSHA
Tangazo: Kwa wale wakazi wa jiji la Arusha, tunamshukuru Mungu kwa kuwa semina ya Neno la Mungu ya Mwalimu Christopher Mwakasege imeanza hapa Arusha tarehe 22 mwezi huu na itamalizika tarehe 1 mwezi wa tatu. Kwa wale wakazi wa Arusha na maeneo ya jirani, huu ni wakati wa kwenda kupata maarifa ya Neno la Mungu pale. Lakini pia kwa wale waishio nje ya Arusha na wangependa kupata mafundisho ya semina hii yake katika kanda za redio, kanda za video(VHS), Audio CDs, au DVD basi wawasiliane nami ( savedlema2 at yahoo dot com) ili nione namna naweza kuwasaidia kwa kuwatumia.

****************
Je una ushuhuda wowote wa matendo ambayo Bwana amekufanyia katika maisha yako au familia yako na ungependa watu wengine wauosome na imani yao kwa Bwana iongezeke? Kama ndivyo basi ingia katika website yangu
www.lema.or.tz na kisha click ukurasa wa “Shuhuda” na uandike ushuhuda wako hapo.

********************
Tuzidi kuombeana tafadhali,
Frank Lema
www.lema.or.tz
Arusha.

Thursday, February 19, 2009

JE UNAUFAHAMU UMUHIMU AU FAIDA YA KUIMBA NYIMBO ZA ROHONI?


Bwana Yesu Kristo asifiwe!

“Nakutakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.”(1Kor1:4)

JE UNAUFAHAMU UMUHIMU AU FAIDA YA KUIMBA NYIMBO ZA ROHONI?

Bwana Yesu asifiwe tena! Ninamshukuru Mungu,Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo kwa wema wake ulio mkuu sana kiasi kisichoweza kuelezeka kwa namna ya kibinadamu, kwa kunilinda mimi na wewe pia mpaka kufikia hapa, tunajua kuwa hii ni neema tunayotakiwa kumshukuru Mungu kwayo.

Ni muda mrefu umepita tangu nikuletee ujumbe wa Neno la Mungu kwa njia hii(kwa wale waliokwishajiunga na huduma hii tayari), na kama wewe ndio umejiunga na huduma hii karibuni, basi karibu na ubarikiwe.

Leo ninakuletea kwa uwezo wa Roho Mtakatifu ujumbe huu unaosema “Je, unaufahamu umuhimu wa kuimba nyimbo za rohoni?”

Kuna faida kubwa sana tunayoipata pale tunapoimba nyimbo mbalimbali za rohoni katika Kristo Yesu. Ninaposema kuimba hapa, siyo lazima uwe umepewa huduma na karama ya uimbaji kama tunavyowaona waimbaji wengi wakiimba na kurekodi nyimbo zao, hapana. Kila mtu aliyeokoka amepewa ndani yake aina Fulani ya uimbaji, hata kama siyo karama yake, japokuwa unaweza kuimba kidogo tuu, lakini Baba Mungu ndiye ameweka hicho kitu ndani ya kila aliyeokoka. Kwanini Baba Mungu ametupa aina hii ya uimbaji hata kwa watu ambao huduma yao wanayomtumikia Mungu kwayo siyo ya uimbaji? Hii ina maana zipo faida za kipawa hiki Mungu alichoweka ndani yetu na inapaswa tukitambue na tukitumie vyema.

Kwanza hebu soma na UITAFAKARI mistari hii hapa chini:

“Je, pana mtu yeyote miongoni mwenu aliye na shida? Anapaswa kusali. Je, yuko mwenye furaha? Anapaswa kuimba nyimbo za sifa”.(Yakobo 5:13)

“Ujumbe wa Kristo ukae ndani yenu pamoja na utajiri wake wote. Fundishaneni na kushauriana kwa hekima yote. Imbeni zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Mungu mioyoni mwenu kwa shukrani.”-(Kolosai 3:16)

1Samweli 16:23 : “Ikawa, ile roho mbaya kutoka kwa Mungu ilipomjilia Sauli, ndipo Daudi akakishika kinubi, akakipiga kwa mkono wake, naye Sauli akaburudishwa na ile roho mbaya ikamwacha”


Bila shaka baada ya kuitafakari mistari hiyo hapa juu umeanza kupata picha kidogo juu ya jambo hili.
Mungu ametupa aina hii ya uimbaji ndani yetu kwa ajili ya kutusaidia katika maeneo mbalimbali tunayopitia hapa duniani.

Unaona katika mstari ule wa Yakobo 5:16, Roho Mtakatifu anasema kuwa kama mtu ana shida basi anapaswa kuomba, kisha akasema kuwa, kama mtu ana furaha basi anapaswa kuimba nyimbo za sifa. Bila shaka nyimbo hizi kwa ajili ya kumsifu na kumshukuru Mungu kwa jambo alilolifanya hata ukawa na furaha. Je, unafikiri Roho Mtakatifu ametoa agizo hili bure? La Hasha! Lazima jambo hili ni la muhimu sana ndio maana ametuagiza tufanye hivyo.
Naandika waraka huu wa leo kukuhimiza kuhusu kuimba nyimbo za rohoni kwa Bwana. Wakati wowote unapokuwa mahali na ukaona tuu kuwa ndani ya moyo wako unajisikia furaha, basi pata muda mahali wewe mwenyewe au na watu wengine na uimbe nyimbo zozote utakazokuwa nazo za kumsifu Baba Mungu na utaona matunda yake, Mungu atafurahi na ataendelea kukupa hiyo furaha zaidi.

Ukitazama ule mstari wa kwenye kitabu cha Samweli 16:23 unaona kuwa mfalme Sauli alijiwa na roho mbaya iliyomsumbua, na ukisoma mistari inayotangulia utaona kuwa, Sauli alipoona tatizo hili, hakumwita kuhani aje kumwombea, bali baada ya kushauriwa, aliagiza aletwe mtu wa kumpigia kinubi pale roho ile itakapomjia, na akaletwa Daudi. Na ikawa kuwa kila roho ile ilipomjia, Daudi alikipiga kinubi chake na roho mbaya ikamwacha Sauli. Hebu tazama tofauti ya jambo hili lililotokea hapa na lile liliagizwa katika mstari ule wa Yakobo! Kwa waraka wa Yakobo tunaagizwa kuomba pale tunapopatwa na jambo lisilo jema, lakini hapa kwa Samweli, Sauli ameshauriwa kupata mtu wa kumwimbia!

Ni wazi kuwa, kuna mahali Mungu Baba ataamua kukusaidia kwa kukuongoza kuomba, na mahali pengine Atakuongoza kuimba tuu nyimbo katika Roho. Unachotakiwa ni kusikiliza ndani ya moyo wako unasukumwa kufanya kipi.

Unapoimba nyimbo za kiroho mahali popote kuna mambo mazuri yanatokea. Nafsi yako inaponywa majeraha yoyote uliyoyapata, iwe ni kwa kuonewa, kutukanwa au majeraha yoyote yale ya kwenye nafsi. Pia unajazwa nguvu za Roho Mtakatifu ndani yako kwa namna ya ajabu.

Siku moja kuanzia mida ya mchana hivi, niliona kuwa kuna wimbo Fulani wa kwenye kitabu cha Tenzi za Rohoni unakuja sana moyoni mwangu bila hata kusikia mtu akiuimba popote japokuwa hata sifahamu beti zake vizuri. Hali hii iliendelea kwa siku nzima, wimbo huo ulikaa sana moyoni mwangu na kila mara nilipokuwa free nilijikuta tuu naanza kuuimba kidogo. Nikapanga kuwa baadaye nitauimba. Jioni niliporudi kupumzika, nilichukua kitabu changu cha Tenzi za Rohoni na nikaanza kuuimba huo wimbo. Nilipofika katikati ya ule wimbo, ghafla niliona nimeteremkiwa na kujazwa nguvu za Roho Mtakatifu kwa namna niliyoishangaa sana, kwani hata sikuomba hata kidogo kabla ya tukio hili. Baada ya hapo ndio nikagundua ni nini maana yake mtu anapokuwa katika shughuli zake na ghafla anasikia ndani yake wimbo Fulani umekuja hata kama haufahamu wote. Kwa hiyo tangu hapo mimi huwa karibu na vitabu vyangu viwili vya nyimbo (Tenzi za Rohoni na Holiness Song Book) na kila nisikiapo Roho Mtakatifu ameweka wimbo Fulani ndani yangu, ninahakikisha kuwa nimepata muda mzuri wa kuuuimba mimi mwenyewe au na wenzangu, na mara kwa mara nipatapo nafasi hukaa na kuimba nyimbo kadhaa kwenye vitabu hivi. Kama naona sifahamu sauti ya wimbo Fulani basi huwa natafuta mtu anayeujua namwomba tuuimbe, au natafuta ala (Midi files) za huo wimbo na kuimba kwa kuzifuatia. Na baada ya kuuimba huwa ninajua kwa hakika kabisa kuwa kuna kitu Mungu amenifanyia wakati nikiuuimba. Yaweza kuwa ni moyo wangu umeponywa, maombi yangu yamejibiwa au imani yangu imeongezwa wakati nilipoimba ule wimbo. Sasa utaona ni kwa nini Biblia inatushauri tufarijiane kwa nyimbo hizi hata wakati wa maombolezo, mioyo yetu inaponywa na tunaongezewa imani.

Wakati mwingine unapomwomba Mungu Baba jambo, anakutaka uonyeshe imani kuwa unaamini kuwa kile ulichoomba ni chako tayari (kama Biblia isemavyo) na ili kukusaidia uonyeshe imani yako, anakuwekea ndani ya moyo wako wimbo wa kumshukuru Mungu Baba, hata kama wimbo wenyewe hujawahi kuuimba miaka kadhaa, na utajikuta tuu unataka kuiimba na utashangaa pia kuwa wala hakuna mtu yeyote aliyekutajia huo wimbo, na wala hujamsikia mtu akiuimba huo wimbo.


Je, na wewe umeshakutana na jambo kama hili? Ulichukua hatua gani? Watu wengi hujikuta wanapuuzia tuu na kusema “Ah! Huu wimbo umetoka wapi tena saa hizi na mimi nipo na kazi zangu?” Nimekuletea waraka huu kwa Roho Mtakatifu ili kukusaidia, kuanzia sasa unapoona hali ya namna hii, hakikisha kuwa unapata muda mzuri uliotulia na ukae na kuziimba nyimbo hizi, ni za muhimu sana. Ninakupa shauri sasa, nunua vitabu vyako vya nyimbo (kama Tenzi za Rohoni) ukae nacho pale ulipo, na unapopata muda, tafuta wimbo mmojawapo na uuimbe, baada ya muda mfupi utaona faida yake njema. Kama unafamilia yako, tengeni muda wa kuomba kila siku usiku (kwa mfano) kabla ya kulala, na kabla ya kuomba, changueni nyimbo chache za rohoni kutoka kwenye vitabu mlivyonavyo na mziimbe wote kwa pamoja. Baada ya muda mfupi mtagundua kuwa upendo na mshikamano ndani ya familia (au kundi lolote) unaongezeka kwa namna msiyoijua na Mungu anajibu maombi yetu kwa namna mnayofurahi zaidi.

Huu ndio ujumbe Bwana aliouweka moyoni mwangu siku hii ya leo kwa ajili yako na ninaamini kuwa utafanyika baraka kubwa sana kwako pale utakapouweka katika matendo, na hayo ndio maombi yangu kwa Baba Mungu.

“….Je yuko mwenye furaha? Anapaswa kuimba nyimbo za sifa”

Mungu Baba akubariki na tuzidi kuombeana daima.

Ni mimi katika Kristo,
FRANK LEMA.
www.lema.or.tz
Arusha Tanzania.


// Kupokea ujumbe huu kwa email jiunge na mailing lists kwa kutembelea www.lema.or.tz //

Wednesday, February 18, 2009

Mchungaji Auwawa kwa baada ya kufumaniwa

MCHUNGAJI wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Mtaa wa Manundu mjini hapa, Bw. Ernest Mngazija (52) ameuawa kwa kuchomwa kisu baada ya kufumaniwa na mke wa mtu akifanya naye mapenzi ndani ya nyumba yao. Tukio hilo lilitokea juzi saa 2. 30 usiku baada ya Mchungaji huyo kukutwa katika nyumba yenye namba HMK/MT/86 iliyopo mtaa wa Mtonga nje kidogo ya mji wa Korogwe. Mchungaji huyo aliyeacha mke na watoto zaidi ya watano, alikutwa na Bi. Happy Temu (19) ambaye ni mke wa Bw. Mandia. Mwandishi wa habari hizi alipofika katika eneo la tukio jana alishuhudia michirizi ya damu kutoka nyumba aliyofumaniwa mchungaji huyo hadi sehemu aliyoangukia kiasi cha mita 100 baada ya kukosa nguvu kutokana na damu kumtoka nyingi. Akizungumzia tukio hilo, Bw. Herman Kiluu ambaye ni Balozi wa mtaa wa Mtonga Juu (Meco) alisema, Mchungaji huyo alikutwa akifanya mapenzi na mke huyo nyakati za usiku. Alisema baada ya kijana huyo kumkuta mchungaji alikwenda kutoa taarifa kwa Mwenyekiti wa Mtaa huo, Bw.Hassan Mndolwa 'Segere Kuu'ambaye naye alifika nyumbani kwake ambapo walivunja mlango wa nyumba hiyo baada ya mke kukataa kufungua na hivyo kuingia ndani kujua kulikoni. "Mchungaji alipotoka alikatwa kisu cha shingo na Mandia, akakatwa tena huku akitafuta njia za kukimbia na vijana walikuwa wakipiga kelele za mwizi," alisema Bw. Kiluu. Alisema hata hivyo, baada ya Mchungaji kukatwa visu vingi alikosa nguvu na kuanguka jirani na nyumba yake ambapo walimpeleka Hospitali ya Magunga kupitia Polisi lakini alifariki akiwa njiani kabla ya kufikishwa hospitali kutibiwa. Tukio hilo limeibua maswali mengi kwani wiki iliyopita, Mchungaji huyo aliongoza misa ya marehemu Salmin Karata ambaye alikuwa dereva wa World Vision aliyekufa kwa ajali ambapokatika mahubiri yake alisema watu wajiandae na kifo. "Leo hii Salmin kesho mimi au wewe," alikaririwa akisema. Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga, Bw. Sirro Nyakoro alithibitisha kutokea kwa mauaji hayo na kusema mtuhumiwa anasakwa na Polisi kwani alikimbia baada ya mauaji hayo. Alisema Happy alihojiwa na Polisi na kuachiwa na atakuwa shahidi kesi hiyo itakapoanza kusikilizwa. Shahidi mwingine atakuwa Balozi aliyeitwa na mtuhumiwa kushuhudia ugoni. Kamanda alisema, marehemu alichomwa visu mara nne katika sehemu mbalimbali za mwili na kutokwa damu nyingi na alikutwa uchi wa mnyama akivaa chupi mlango ulipovunjwa. Alipoulizwa walijiridhishaje Mchungaji alikuwa amefanya mapenzi na Bi. Happy Kamanda alisema 'mtu amekutwa uchi wa mnyama anavaa chupi maana yake alikuwa anafanya nini".

Mchungaji ‘akutwa’ na viungo vya albino

Mchungaji wa Kanisa la Pentecoste lililopo Idiwili Kata ya Iyula, wilayani Mbozi anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kukutwa na mabaki ya mwili wa binadamu yaliyokuwa yakiuzwa Sh milioni 30. Cosmas Mwasenga (39) alikamatwa Februari 13 mwaka huu akiwa na Luseshelo Mwashilindi ambaye inadaiwa alikuwa ameyahifadhi nyumbani kwake mabaki hayo. Mabaki hayo ambayo Polisi inahisi kuwa ni ya albino, ni vipande vinne vinavyosadikiwa kuwa sehemu ya mikono. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Zelothe Stephen alisema leo kuwa watuhumiwa hao walikamatwa katika eneo la Mlowo, Mbozi. Akizungumzia tukio hilo, Kamanda Zelothe alisema Februari 12 mwaka huu, polisi walipata taarifa kuwa kuna kikundi cha watu Mlowo, wana vipande vya mabaki ya mwili wa mwanadamu vinavyosadikiwa kuwa ni mabaki ya mwili wa albino. Alisema taarifa hizo zilidai kuwa kikundi hicho kilikuwa kinatafuta wateja ili kuwauzia vipande hivyo na kwamba watu waliokuwa wanatafuta wateja waligawanyika katika Wilaya ya Mbozi na baadhi ya mitaa ya Jiji la Mbeya. “Tuliweka mtego na kukutana na watu hao ambao walisema wanauza viungo vya ‘kunguru mweupe’ wakimaanisha albino, ambapo walikubaliana na kukutana na Mwashilindi ambaye alikuwa anahifadhi viungo na kufikia makubaliano ya kuvinunua kwa Sh milioni 30,” alisema. Alisema Februari 13, taratibu za kupata kiasi hicho cha fedha zilikamilika na walipofika kwa Mwashilindi alitoka akiwa na vipande vinne vya mabaki ya binadamu vikiwa vimefungwa katika karatasi, na Polisi wakamkamata. “Baada ya kupekua katika nyumba ya Mwashilindi tulifanikiwa kupata dawa za binadamu, maji ya kuchanganya na dawa na koti jeusi mali ya Mchungaji Mwasenga,” alisema. Aliongeza kuwa watuhumiwa wote wawili wanashikiliwa na watafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika. Kamanda Zelothe alisisitiza umuhimu wa wananchi kutoa taarifa Polisi na kusema kwa kufanya hivyo, ndipo vitendo vya mauaji ya albino vitapungua. “Tunapenda kuwaomba wananchi waendelee kutoa taarifa za siri kwa viongozi wa juu, ili ziweze kufanyiwa kazi haraka,” alisema.

Friday, February 6, 2009

Mchungaji afungwa kwa kukataa kuapa mahakamani

Mchungaji wa Kanisa la EAGT lillilopo mtaa wa Ichenjezya mjini Vwawa wilayani Mbozi mkoani Mbeya Simon Kitwike (48) jana alijikuta akihukumiwa kifungo cha miezi sita gerezani, baada ya kudharau mahakama kwa kukataa kuapa ili atoe ushahidi kutokana na imani ya Dini.Mchungaji huyo aliyevunjiwa nyumba yake mwishoni mwa mwaka jana na kuibiwa mali kadhaa za nyumbani kwake alifika katika mahakama ya wilaya ya Mbozi ili kutoa ushahidi wake, lakini alikataa kuapa kabla ya kutoa ushahidi wake akidai ni dhambi.Hakimu wa mahakama ya wilaya Kajanja Nyasige alimwamuru asome kifungu katika Biblia kinachomtaka asiape mahakamani, ndipo mchungaji huyo alifungua Biblia na kusoma kitabu cha Mathayo 5: 35 kuwa ndicho kinachompa msimamo huo.Baada ya kusoma kifungu hicho Hakimu Nyasige alimuuliza tena mshitakiwa (shahidi) kama atakuwa tayari kuapa ili aweze kuendelea na kutoa ushahidi wake mahakamani, hata hivyo mshitakiwa huyo aliendelea kubaki na msimamo wake wa kukataa kuapa.Ndipo Hakimu huyo alimsomea kifungu cha sheria na 198 (1) kama ilivyorekebishwa mwaka 2002 kinachokataza mtu kudharau Mahakama na kuwa kuendelea kukataa kuapa ni kuvunja sheria na hivyo anatenda kosa la jinai.Hata hivyo hakimu Nyasige aliendelea kumvumilia mchungaji huyo ili aweze kubadili msimamo wake kwa kumwamuru asome Biblia hiyo tena Waraka wa Mtume Paulo kwa Warumi 13:1- 5, shahidi huyo alisoma kifungu hicho mbele ya mahakama, lakini alipoulizwa kama amebadili msimamo wake alijibu kuwa hawezi kubadili msimamo wake, kwa aya hiyo ya waraka na akasisitiza kuwa msimamo upo pale pale.Hakimu Nyasige alilazimika kumsomea hukumu na kumtia hatiani kutokana na kosa la kuidharau mahakama, hivyo anamhukumu kwenda jera miezi sita na kuwa atatakiwa kuja kutoa ushahidi wake kwa kesi ya msingi Marchi 2, mwaka huu.Mwandishi wa habari hizi alimhoji Mchungaji mwandamizi wa Kanisa hilo aliyejitaja kwa jina moja la Mwakasaka ambaye alisema amesikitishwa na hukumu hiyo na akadai kuwa mchungaji wake alielewa vibaya vifungu vya biblia vinavyozungumzia viapo.Naye Mchungaji Erasto Makalla wa kanisa la Pentekoste alieleza kusikitishwa kwake na hatua hiyo ya mchungaji kupingana na mamlaka ya serikali na akasema kuna haja ya kuwafanyia semina wachungaji ili waelewe taratibu za serikali.Matukio ya upinzani yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara wilayani hapa ambapo mwaka juzi waumini wa madhehebu ya Mashahidi wa Jehova walikuwa kwenye mgogoro na serikali baada ya kukataza wanafunzi wasiimbe wimbo wa taifa na kuheshimu bendera.

Kikwete na UDOM

Rais Jakaya Mrisho Kikwete ametangaza kuwa amefanya uamuzi kuwa makao makuu ya Serikali mjini Dodoma sasa yatajengwa katika eneo la Chamwino, baada ya eneo lililokuwa limetengwa awali kwa ujenzi huo katika eneo la Chimwaga, kutolewa kwa ajili ya ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), chuo kikubwa zaidi cha umma nchini.
Rais Kikwete pia ameutaka uongozi wa chuo hicho cha UDOM kuelekeza nguvu zaidi katika kufundisha wataalam zaidi wa shahada kubwa zaidi za Uzamili na Uzamivu, badala ya kushikilia kufundisha watu kwa ajili ya kupata shahada la kwanza tu.
Rais Kikwete ameelekeza hayo wakati alipotembelea UDOM, ili kujionea maendeleo ya wa chuo hicho, ikiwa ni mara yake ya kwanza kutembelea chuo hicho tokea alipokwenda kukagua ujenzi wa chuo hicho Agosti 2, 2007.Akizungumza na jumuia ya wanachuo baada kumaliza kutembelea chuo hicho na kukagua ujenzi wake, Rais Kikwete amesema kuwa ameamua kuwa sasa makao makuu ya Serikali yatajengwa katika eneo linalozunguka Ikulu Ndogo ya Chamwino, baada ya kuwa ametoa eneo la awali la ujenzi wa makao makuu hayo kwa ujenzi wa UDOM.
“Kuna sababu mbili za kufanya hivyo. Moja ni kwamba eneo hili sasa tumelitokea kwa ajili ya ujenzi wa chuo hiki maridadi na cha kupendekeza kabisa. Hata kabla ya ujenzi kumalizika, nyie mnajionea kinachovutia,” amesema Rais Kikwete na kuongeza:
“ Pili ni kwamba Rais hawezi kufanya kazi ya kusafiri mwendo mrefu kiasi hiki kati ya makazi yake ya Chamwino na ofisi yake kwenye eneo hilo la Chimwaga,” Rais Kikwete amewaambia wanajumuia hao.
Inakisiwa kuwa kuna umbali wa kiasi cha kilomita 35 kutoka Chamwino kwenda mjini Dodoma. Hivyo, safari ya kutoka Chamwino kwenda Chimwaga na kurudi ni kiasi cha kilomita 70.
Rais Kikwete amewaambia wanajumuia hao wa UDOM kuwa ameshangazwa kweli kweli na hatua ya ujenzi wa Chuo hiki. “Nimepata faraja kubwa moyoni mwangu. Naamini kuwa baada ya ujenzi, eneo hili litakuwa moja ya maeneo ya kuvutia zaidi nchini, na wala sisemi maeneo ya vyuo viku, bali majengo yote.”
Rais Kikwete pia amewaelezea wanajumuia hiyo jinsi wazo la kuanzisha chuo hicho lilivyozaliwa, kwa sababu uamuzi wa kuanzisha chuo hicho ulikuwa uamuzi binafsi wa Rais Kikwete, na wala hilo halikuwa sehemu ya Ilani ya Uchaguzi Mkuu wa CCM, mwaka 2005.
Amesema kuwa aliamua kuanzia chuo hicho kwenye Jengo la Chimwaga lililokuwa mali ya Chama cha Mapinduzi kwa sababu jengo lilikuwa halitumiki ipasavyo. “Unajua tulikuwa tunalitumia jengo hili mara moja ama mara mbili kwa miaka mitano. Kama mkikumbuka hili jengo ndilo lilikuwa limetumike kwa ajili ya Bunge. Ni jengo kubwa sana hili na lilifaa kabisa kuanzia chuo hiki.”Rais Kikwete ametumia zaidi ya saa mbili kutembelea ujenzi wa chuo hicho ambacho kikikamilika kitakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi kiasi cha 40,000 kwa wakati mmoja.
Akipata maelekezo kuhusu maendeleo ya ujenzi na masomo katika Chuo hicho ambacho tayari kina wanafunzi wapatao 7,000 kutoka kwa Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Kikura, Rais Kikwete ameutaka uongozi wa chuo hicho kubadilisha fikra na kuelekeza nguvu kubwa zaidi katika kukifanya chuo hicho Kituo cha Ubunifu kwa kutoa wasomi wengi zaidi wa shahaha za Uzamili na Uzamivu.
“Kwa kuchukua wanafunzi wachache wa shahada hizo za juu, na wakati mwingine kwa kuongozwa tu na hisia zetu, tunaweza kabisa kuwa tunadumaza maendeleo ya taifa,” amesema Rais Kikwete, akitolewa mfano wa uzoefu wake katika Chuo cha Kenyatta cha Nairobi, ambacho mwishoni mwa mwaka uliopita, kilimtunukia shahada ya heshima za Uzamivu.

Friday, January 30, 2009

Mchungaji awa Mbunge mbeya vijijini

Mbunge mpya wa Mbeya Vijijini Mchungaji Luckson Mwanjale akila kiapo Bungeni Mjini Dodoma leo.



Mchungaji Mwanjale anakuwa ni mchungaji wa kwanza nchini kuchaguliwa kushindana katika kinyang'anyiro cha uchaguzi na kupiga kampeni na hatimaye kuibuka mshindi wa kiti hicho kwa kupitia tiketi ya CCM.

Waziri mkuu aangua kilio bungeni

Hoja ya wapinzani kumtaka ajiuzulu yayeyuka

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda ameangua kilio bungeni kuonyesha uchungu alio nao dhidi ya vitendo vya mauaji ya kikatili ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), hivyo kuyeyusha hoja ya wabunge wa upinzani waliokuwa wamepania kumbana, ili ajiuzulu kwa madai kwamba, alitoa amri ya kuua wauaji ambayo ni kinyume na katiba ya nchi.
Hali hiyo ilitokea jana bungeni, wakati Pinda akielezea yaliyomfanya atoe kauli hiyo tata kikatiba na misingi ya haki za binadamu.
Pinda alisema alipokuwa katika ziara katika mikoa ya Kanda ya Ziwa, alipata taarifa za kusikitisha kuhusu mauji ya albino na mara kesho yake habari zikatoka kwenye vyombo vya habari kwamba, albino mwinge kauawa.
"Jamani jamani taarifa za matukio hayo kibinadamu zinatia uchungu sana na kumfanya mtu ashindwe kujizuia….," mara akaanza kutokwa machozi na kukatisha maelezo yake akatoa miwani na kujifuta huku wabunge wakiwa kimya.
Waziri Mkuu alisema hayo baada ya Kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni, Hamad Rashid Mohamed, kumtaka atoe ufafanuzi kuhusu kauli aliyoitoa hivi karibuni akiwa katika ziara Kanda ya Ziwa, kuwaruhusu wananchi kuwaua watu watakaokutwa wakimchinja albino.
Hamadi alisema katiba ya nchi inamlinda mtu kupewa nafasi ya kujitetea, hivyo akamtaka waziri afafanue maana ya kauli yake, kwa kuwa ni kinyume na taratibu ambazo nchi imejiwekea katika kuhakikisha haki inapatikana.
Pinda alisema mtu anaposikia au kusoma taarifa za mauaji ya albino, hawezi kupata hisia juu ya mateso wanayoyapata, sawa na anayewasikiliza watu walionusurika kufa au walioshuhudia vitendo hivyo vikitendeka.
“Mimi walinihadithia, aah! Samahani," alisema kwa masikitiko Pinda huku akiwataka radhi wabunge kwa kushindwa kuendelea kueleza kwa jinsi alivyoguswa na matukio hayo. Mara akaanza kububujikwa na machozi na baada ya sekunde kama 15, alichukua kitambaa chake akajifuta.
Aliendelea kuelezea jinsi maalbino wanavyouawa kikatili, akisema wengi walikufa kwa kushindwa kupata huduma mapema ya kuzuia damu baada ya ama kukatwa mikono ama miguu na majitu hayo katili yenye imani potofu kwamba, viungo hivyo vinaweza kumpatia mtu utajiri.
Alisema alielezwa kuwa, wauaji wanachokifanya ni kumshambulia albino na kumkata kiungo wanachokitaka kwa kutojali hali wanayomuacha nayo kama ni mateso, kufa au kupona hivyo alipatwa na uchungu kiasi cha kujikuta anatamka kuwa, watu wanaokutwa wakitenda hayo nao wanapaswa kuadhibiwa papo hapo.
Alifafanua kuwa wakati akiwa kwenye ziara hiyo iliyokuwa maalumu kwa ajili ya kukemea na kupanga mikakati ya kukabaliana na vitendo hivyo, idadi ya maalbino waliouawa walikuwa 30 na baada ya kukemea vitendo hivyo, ghafla akapewa ripoti ya kuuawa wengine wawili, jambo ambalo lilizidi kumuudhi na kumchanganya.
Waziri Pinda aliwaomba radhi watu walioudhika kutokana na matamshi na pia akimuomba Mungu amsamehe iwapo amewakosea.
"Kama mnaona kile nilichofanya ni makosa naomba mnivumilie. Naomba Mungu anisamehe kama nimewakosea," aliomba Waziri Mkuu na kuongeza kuwa serikali imechukizwa sana na mauaji hayo ya kikatili.
Alisema Tanzania imekuwa ikiheshimika sana katika jumuiya ya kimataifa, lakini mauaji ya albino na ya vikongwe katika eneo hilo yameitia doa.
Alielezea pia kuhuzunishwa zaidi na tamko la Bunge la Jumuiya ya Ulaya (EU) la kulaani mauaji hayo, kana kwamba wao wanaguswa sana na suala hilo kuliko Serikali ya Tanzania.
Hata hivyo, alisema kuwa katika ziara hiyo, ambayo iliwahusisha pia baadhi ya mawaziri, wabunge, viongozi wa polisi, viongozi wa dini na kisiasa, waliahidi kushirikiana kuhakikisha kuwa wanakabiliana na kulimaliza tatizo.
Isitoshe alisema aliwataka viongozi wa vijiji kurejesha ulinzi wa jadi, maarufu kama sungusungu ili kukabiliana na wauaji.
Pinda alisema kuwa serikali ipo tayari kupokea maoni kutoka kwa watu mbalimbali, yanayoweza kusaidia kupata mbinu ya kukomesha kabisa mauaji hayo, ili kuiokoa jamii hiyo ya albino.
Alisema katika kumbukumbu za serikali, hadi mwishoni mwa mwaka jana vikongwe 2,866 walikuwa wameuawa kwa imani potofu kuwa ni wachawi.
Alisema serikali imeliagiza jeshi la polisi kutumia maarifa yake, hata kama itabidi kutumia gharama kubwa, ili kuwatia mbaroni watu wote wanaojihusisha na mauaji hayo.
Wapinzani pia walimtaka Pinda atoe maelezo yanayodaiwa kuwa yalitolewa na Rais Jakaya Kikwete kisiwani Pemba kwamba, aliwashangaa wakazi wa eneo hilo kuwachagua watu ambao hawawezi kuunda serikali na ambao watachukua muda mrefu kupata nafasi hiyo.
Pinda alisema anapata taabu kujibu swali hilo, kwa sababu hawezi kuyatolea maelezo mambo yaliyozungumzwa na bosi wake na wala hajui kama ni kweli rais alisema kama vyombo vya habari vilivyoripoti.
Mbunge wa Konde, Dk Ali Tarab Ali (CUF) alimtaka Pinda aeleze kama kitendo cha Rais Kikwete kutumia magari ya serikali kisiwani Pemba na kuonekana akifanya shughuli za chama ni matumizi mabaya ya fedha za serikali.
Pinda alimjibu akisema kuwa, ni vigumu rais kutofautisha vyombo vya usafiri anavyovitumia wakati akifanya ziara za kisiasa ama za kiserikali na kutoa mfano kwamba, hata rais wa Marekani hutumia ndege aina ya Air Force one bila kuchagua kuwa ni shughuli ya kisiasa au kiserikali.
Wakati hayo yakitokea bungeni, baadhi ya viongozi wa dini nchini, wamemtaka Waziri Pinda kukiri kosa, kufuta kauli yake na kuomba radhi kwa mamlaka za kisheria, Bunge na Wananchi.
Akizungumza na Mwananchi jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislaam, Sheikh Ramadhan Sanze alisema Pinda alifanya kosa la kiufundi kwa kuwa yeye ni mtendaji mkuu wa serikali, hivyo hakupaswa kusema jambo linalopingana na msimamo wa serikali, sheria na katiba ya nchi.
"Kwa vile kauli hiyo haijaleta madhara mpaka sasa Waziri Mkuu ana uchochoro wa kupita ili kujisafisha. Cha msingi ni kukiri kosa, kufuta kauli yake na kuomba radhi kwa mamlaka za kisheria, Bunge na Wananchi" alishauri Sheikh Sanze.
Alisema, hajafuatilia vizuri kuhusu hoja za kambi ya upinzani bungeni na kwamba, kujiuzulu inaweza isiwe suluhisho la tatizo hilo kwa kuwa, hata kama atajiuzulu kauli haitafutika na tatizo litabaki palepale.
"Nchi hii haina dini na kwa hiyo haingozwi na sheria za dini bali inaongozwa na sheria za nchi, kwa hiyo Pinda alipaswa kuangalia sheria ya nchi kwanza kabla ya kutoa agizo lake," alisema Sheikh Sanze.
Alifafanua kuwa, Waziri Pinda ametengeneza mazingira ya uchafuzi na uchochezi, kutokana na kauli yake hiyo kwani baadhi ya watu wanaweza kuitumia vibaya kwa kumuua mtu kwa sababu ya chuki tu baina yao.
Alisema, athari ya kauli kama hizo zinaweza kusababisha migogoro kati ya dini na dini nyingine, kabila moja na jingine au dhehebu moja na jingine kama wananchi watautumia wito huo.
Alisema vita dhidi ya mauaji ya albino imekuwa ikitumika kisiasa zaidi kuliko kitaalamu na kuongeza kuwa, mamlaka husika ziliangalie tatizo hilo kitaalamu badala ya kuliacha likitumika kisiasa.
Naye Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Valentino Mokiwa alisema kauli ya Pinda ya kutaka aliyeua albino auawe si sahihi kwa sababu mtu akimuua aliyeua ni muuaji na ana kosa kisheria.
Mauaji ya albino yamekuwa yakitikisa nchi na hasa katika eneo la Kanda ya Ziwa, licha ya juhudi mbalimbali zilizofanywa na serikali kupitia jeshi la polisi, mashirika ya kutetea haki za binadamu, vyama vya walemavu na watu binafsi.
Source:Mwananchi

Tuesday, January 27, 2009

Jan 2009:KWAHERI NDUGU YETU SEDEKIA.


TUKIO LA JANUARY 2009:

KWAHERI NDUGU YETU SEDEKIA.


Jina la Bwana litukuzwe milele na milele, na tena atukuzwe Yeye ambaye anatuwazia mema kuliko yale sisi tuyawazayo.

Ndugu wana Sayuni popote pale mlipo, nadhani wote mnakumbuka msiba tulioupata wa kutwaliwa kwa ndugu yetu Fanuel Sedekia akiwa kule katika nchi ya baba zetu, Israel.

Mimi nilifuatilia tukio lile na kuhudhuria ibada ya kuuaga mwili wake hapa Arusha ila nilishindwa kuwaletea habari hizi kwa muda kutokana na kubanwa sana na mambo hapa, ila nimezileta leo ili tujikumbushe ikiwa ni tukio kubwa kabisa katika mwezi huu.

Kama wengi tulivyojua, ndugu yetu huyu alifariki akiwa katika safari muhimu sana ya kiroho kule Israel, akiwa pamoja na timu ya huduma ya MANA ya mwalimu Christopher Mwakasege.

Siku hiyo ya kuuga mwili wake na mazishi (January 10) tulikutana katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid hapa Arusha, na watu walikuwa ni wengi kiasi ambacho hakikutegemewa. Mwili wake uliingizwa uwanjani, ukiwa umebebwa kwenye gari, na gari lingine lilikuwa likifuata nyumba yake likiwana speakers kubwa huku wakiwa wameweka ule wimbo wa “Bwana ametoa na Bwana ametwaa” aliouimba Sedekia mwenyewe. Hii ikiwa ni baada ya kuwasili jana yake kwa ndege kutokea Israel ambapo mamia ya wakazi wa Arusha walijipanga pembeni mwa barabara ya moshi-arusha huku wakiutazama msafara uliokuwa na mwili wake uliopata magari yasiyopungua 40, na wengine walikwenda hadi hospitali ya mkoa ya Arusha na walisikika wakipiga mayowe ya vilio walipoona jeneza lake. Mara baada ya kuingia uwanjani,ulipokelewa kwa utulivu na timu ya waimbaji wa muziki wa Injili kutoka Dar na maeneo mbalimbali kama unavyoweza kuona katika picha. Baada ya hapo, watu mbalimbali walipewe nafasi ya kuzungumza kwa ufupi namna walivyomfahamu Sedekia. Na hapa kwa ufupi natata nieleze kile alichosema Mwl. Mwakasege.
Mwalimu alielezea namna walivyoondoka na Sedekia hapa uwanja wa ndege wa Arusha, ya kuwa alikuwa amemaliza kutumia doze ya malaria iliyomsumbua muda kidogo na kuwa alisema alikuwa ok kwa safari. Waliondoka hadi Israel walipoanza kutembelea maeneo muhimu ya kibiblia huko, na baada ya siku chache, Sedekia alionekana kuwa mdhaifu na alisema hali yake si nzuri sana. Baadaye, walimua kumpeleka hospitali waliyoshauriwa na madaktari akiambatana naye na daktari waliyekuwa naye safarini pia. Baada ya uchunguzi ilifahamika kuwa alisumbuliwa na Sukari na pia homa ya mapafu (Pneumonia),na hivyo akalazwa katika hospitali ile ya Poriya.

Mwakasege aliendelea kusema kuwa kabla ya Sedekia kuugua, walitembelea kanisa moja huko Israeli na Sedekia alikuwa amekwenda na kinanda chake (japokuwa ilikuwa ni safari ya mafundisho ya ndoa) hivyo alikitoa kinanda chake na akapewa nafasi ya kuimba. Aliimba wimbo ule wa “Bwana Mungu nashangaa kabisa” (Tenzi no. 114) na huo ndio ulikuwa wimbo wa mwisho wa Sedekia kuimba upande huu (kwani upande ule mwingine bado anaimba)
Mwalimu aliendelea kueleza namna Sedekia alivyougua, muda wa safari yao ulipokwisha ilibidi Mwl. Mwakasege abaki Israel kumuuguza Sedekia na wengine kurudi nyumbani.
Alieleza kuwa madaktari walijitahidi na kurekebisha hali ya sukari yake (iliyokuwa juu sana) na mapafu,lakini alipoteza fahamu na hakupata tena fahamu hadi uimbaji wake ulipohamishiwa mbinguni.

Katika ibada ile ileyohudhiriwa na watu wengi kuliko hata anapokuja rais wa nchi yetu huku Arusha, ilijawa na watu wa rika zote, na watu kutoka nchi mbalimbali. Mbunge mmoja alieleza pia namna walivyofahamiana na Sedekia, na mkenya mmoja aishiye Norway alieleza namna walivyokuwa wamepanga kwenda kupeleka Injili katika nchi zaidi ya tano za Afrika wakiwa na Sedekia, na kwamba aliwaambia anakwenda Israel na akirudi ndio wataanza safari hizo.

Ilifahamika kuwa Sedekia alikuwa na maono makubwa sana kwa ajili ya huduma yake kumtukuza Mungu huko mbeleni. Alikuwa na mpango wa kufungua studio yake ya muziki ya Injili, jambo ambalo, wote waliokuwepo siku ile waliazimia kuwa maono haya yasimamiwe na mke wake hadi studio ijengwe. Tukio hili wali walilitumia pia kusisitiza waimbaji waimbe katika roho kama alivyofanya Sedekia, na pia umoja kati yao ulisisitizwa sana jambo ambalo limeonekana kuanza kukua katika msiba ule.

Muda wote wa tukio hili, kwaya ya pamoja “Mass Choir” ilikuwa ikiimba nyimbo mbalimbali alizoimba Sedekia, lakini wimbo wa “Nimemwona Bwana….” Uliimbwa sana.
Tulipewa nafasi ya kutoa michango yetu kwa upendo kama sehemu ya kusema “pole” kwa familia yake.

Kumalizia mazungumzo yake, mwalimu Sedekia alianza kwa kumshukuru Mungu kwa kumpa Neema ya kuwa na Sedekia katika siku zake za mwisho (kwani aliwahudumia wengi lakini Mungu alipenda siku za mwisho wake awe na Mwakasege) na kuwashukuru watu wengine wote.

Alizungumza zaidi na kusema kuwa hakuna awezaye kuyapindisha mapenzi ya Mungu, na ya kuwa, mawazo ya Mungu yapo juu sana kuliko mawazo yetu sisi wanadamu. Ni nani ajuaye kuwa uimbaji wa Sedekia sasa unatakiwa zaidi mbinguni na Mungu kuliko hapa duniani?

Mwalimu Mwakasege alituonya ya kuwa “MUNGU ANAENDELEA KUWA MUNGU HATA KAMA HAKUJIBU TULIVYOTAKA, hivyo: Usimvunjie Mungu heshima yake ndani ya moyo wako, mwache aendelee kuwa Mungu daima” japokuwa Sedekia aliombewa nchi nzima ili asife,lakini Yeye Mungu anajua zaidi yetu.

Alimalizia kwa kutusihi watu wote tulioguswa na msiba huu, kila mtu ajiulize maswali haya matatu na apate jibu lake leo hii.(Ninamnukuu)

1. Kwanza jiulize, ukifa unataka ukumbukwe kwa lipi?
2. Baada ya kifo, zipo sehemu mbili tuu za kwenda, mbinguni na jehanam, je unataka ukifa uende wapi?
3. Je, Yesu Kristo akirudi leo, utanyakuliwa na Yeye au utabaki? (mwisho wa kunukuu)

Mwishoni ilitolewa nafasi ya watu wote kupita kwa mstari kwenda kutoa heshima za mwisho kwa mwili wake. Watu tulijipanga kwenye mistari iliyoanzia mwanzo hadi mwisho wa uwanja lakini watu hawakukata tamaa hata kidogo. Tulijipanga na kuanza zoezi hili ambalo halikuweza kufanikiwa kwani baadhi ya watu walishindwa kujizuia kwa vilio na kufanya hali kuwa ngumu, hali iliyopelekea zoezi hili kusitishwa na mwili wake kuchukuliwa na kupelekwa kuzikwa.

Ile siku ya mwisho, wote tuliookoka tutanyakuliwa na Bwana wetu Yesu Kristo, na tunaambiwa kuwa tutakutana wote ng’ambo ya mto, kama maneno ya ule wimbo wa “Shalll we gather at the river” (Ati twonane mtoni), tutakumbatiana na walioolewa wa vizazi vyetu na kisha tutaungana pamoja na tutakaribishwa kuingia katika karamu iliyoandaliwa katika Mji ule wa Yerusalemu mpya ambao hata sasa upo tayari kwa ajili yetu. Tuliookoka wote tusife moyo, Sedekia yupo na Bwana, na uzuri mmoja ni kwamba ipo siku tutakutana naye na kukaa naye pamoja na Bwana. Kusema ukweli, sasa yupo anaendelea kumwabudu Mungu huko juu kwa Baba yetu. Tushike sana tulichonacho.

Haya ndiyo niliyopenda kuwashirikisha siku hii ya leo.

“KWAHERI KAKA SEDEKIA, KATIKA SAA YA BWANA TUTAKUTANA PALE NG’AMBO YA MTO ULE”



www.lema.or.tz na Sayuni blog inamwomba Mungu Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo amtunze mke wake, watoto na familia yote, na Bwana atutie sisi wote NGUVU. Amen.

Frank Lema.
Arusha.

Monday, January 26, 2009

Serikali yapiga marufuku waganga wa jadi Tanzania

SERIKALI imetangaza kufuta leseni zote za waganga wa jadi kuanzia Ijumaa Jan. 23, 2009 ikiwa ni sehemu ya mapambano dhidi ya mauaji ya Albino na Vikongwe nchini.
Amri hiyo ilitangazwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda katika mkutano wa hadhara mjini Shinyanga leo mwishoni mwa ziara yake ya mikoa ya Kanda ya Ziwa kuhamasisha mapambano ya Serikali dhidi ya mauaji hayo.
Waziri Mkuu alisema kuwa aliwasiliana na Mwanasheria Mkuu kuhusu uamuzi wa kuchukua hatua hiyo ya kufuta leseni hizo na Mwanasheria Mkuu akasema jambo hilo linawezekana.
"Kuanzia leo leseni zote za waganga wa jadi futa… Mtu yeyote akiendelea na kazi hiyo mfuatilieni," aliwaagiza Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Wakuu wa Halmashauri zote za Jiji, Miji na Wilaya nchini.
Waganga wa jadi wamekuwa wakituhumiwa kuwa ndiyo chimbuko la mauaji hayo kwa vile wao ndiyo hupiga ramli za kuelekeza hivyo.
Katika mikutano na viongozi wa mikoa ya Kagera, Mwanza, Mara, Tabora na Shinyanga, wachangiaji wengi waliitaka serikali kufuta leseni hizo. Hata baadhi ya waganga wa jadi waliochangia walikiri.
Waganga wa jadi husajiliwa na kupewa leseni za kufanya kazi zao na Halmashari kwa utaratibu wa kiutawala. Ipo sheria ya mwaka 2002 kuhusu Tiba Asilia na Tiba Mbadala (Traditional and Alterntive Medicine Act), lakini Kanuni za utekelezaji wake zilikuwa hazijatengenezwa.
Waziri Mkuu alisema mganga wa jadi ambaye anaweza kuruhusiwa baadaye ni yule ambaye dawa zake za mitishamba au za asili zitakuwa zimethibitishwa na Kitengo cha Uchunguzi wa Tiba Asili cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kuwa kweli zinatibu. Mgonjwa naye atatakiwa awe na cheti kutoka hospitali kitakachothitisha maradhi yake na kuwa tiba yake hopitali imeshindikana. "Waganga hawa ni waongo wakubwa…Siyo lazima kuwa nao.
Wangekuwa waganga wa kweli magonjwa mengi yangepungua nchini, lakini magonjwa yapo na sasa wanapiga ramli na kuwa kichocheo cha mauaji. Mkoa wa Shinyanga unasemekana unaongoza kwa idadi ya waganga wa jadi waliosajiliwa na wako 1,104 na 94 ambao hawakusajiliwa.
Wilaya ya Kahama peke yake ina 763. Waziri Mkuu aliuambia umati uliofurika kwenye uwanja wa Chuo cha Biahshara cha Shinyanga (Shycom) huku akishangiliwa kuwa mapambano dhidi ya mauaji ya Abino ni vita na ndiyo maana anataka ulinzi wa jadi wa Sungusungu urejeshwe kusaidiana na vyombo vya dola kukabiliana na hali hiyo.
Aliwataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na Jeshi la Polisi na Idara ya Usalama wa Taifa kufnya kazi zao kwa ufanisi zaidi na "kujipanga upya na kuteremka hadi ngazi ya chini" kusimamia mapambano dhidi ya mauaji ya Albino na Vikongwe.
"Inapotokea kuwa Albino au Kikongwe anauawa katika eneo fulani, mimi nitamshukia Mkuu wa Mkoa na kumuuliza kwa nini aliacha hali itokee hivyo. Mkuu wa Mkoa naye atamshukia Mkuu wa Wilaya na vivyo hivyo," alisema.
Aliongeza: "Tukijumuika wote kwa pamoja tutashinda vita hii kama tulivyoshinda vita dhidi ya nduli Idi Amin wa Uganda". Waziri Mkuu pia alisema atamwomba Jaji Mkuu kuwa zile kesi za mauaji ya Albino ambazo ziko tayari zinapangiwa majaji maalum ili zikamilike na hatima yake ijulikane haraka.
Tangu Juni mwaka 2007 mpaka Novemba mwaka 2008 jumla ya Albino 34 wameuawa nchini kwa imani za ushirikina kuwa eti viungo vyao vinasaidia kupata utajiri.
Idadi yao kimkoa kwenye mabano ni Mwanza (19) Mara (4) Kigoma (3) Shinyanga (4), Kagera (3) na Mbeya (1). Mwaka huu tayari wameuawa watatu.
Jumla ya vikongwe waliouawa nao kwa kushukiwa wachawi ni 2583 ambapo idadi yao kimkoa kwenye mabano ni Mwanza (696), Shinaynga (522), Tabora (508), Iringa (256), Mbeya (192) Kagera (186), Singida (120) na Rukwa (103).
Ziara ya Waziri Mkuu Pinda katika mikoa ya Kanda ya Ziwa inamalizika leo kwa majumuisho yatakayowahusisha viongozi wa mikoa hiyo. Alianzia Kagera na badaye kutembelea mikoa ya Mwanza, Tabora na Shinyanga.
Mkoa wa Mara ulijumuishwa kwa viongozi wake kuhudhuria mkutano wa viongozi Mwanza.

Friday, January 23, 2009

PLEASE SAY EVEN JUST A WORD....

Thank you for joining with us as we pray for the persecuted church around the world. "Confess your trespasses to one another, and pray for one another, that you may be healed. The effective, fervent prayer of a righteous man avails much." -James 5:16


CHINA
- Deathly Ill Husband Denied Visitation with his Imprisoned Wife

– China Aid AssociationChinese government authorities have denied Hua Zaichen, 91, visitation with his imprisoned wife, 79-year-old Shuang Shuying, according to China Aid Association (CAA).Zaichen, who is deathly ill, requested a final meeting with his wife to say his goodbyes, but officials refused to grant the request. “Authorities say Shuang Shuying is not allowed to leave prison before February 8, 2009, the end of her two-year sentence. Officials stated that if her husband died before then, she would be allowed to see his body for 10 minutes and would have to be chained, handcuffed, shackled and wearing a prison uniform,” CAA added. Pray for this family that has endured many hardships for the sake of their faith. Pray for Shuang Shuying to be released. Praise God for their courage!Joshua 1:9

INDIA
- Four Christians Arrested in Madhya Pradesh – VOM SourcesOn Jan. 5, police arrested four Christians in the village of Kushalpura, Madhya Pradesh, India on false charges of forcible conversion. At 10:00 a.m., Pastor Kantilal Bhuria went to the home of a local Christian where 25 believers were gathered for prayer. During the service, a mob of Hindu extremists barged into the house and accused Pastor Bhuria of forcibly converting Hindus. The extremists verbally abused those present and beat a Christian woman. The police arrived on scene after receiving a phone call from the attackers and arrested four believers. At last report, these Christians remained in detention. Pray for the release of these Christians. Ask God to give them and other suffering believers in India grace, wisdom and endurance as they serve Him.1 Peter 5:10-11

KAZAKHSTAN

– President Sends Repressive Law for Constitutional Review – Forum 18 NewsPresident Nursultan Nazarbaev of Kazakhstan has sent a repressive new law which aims to severely limit freedom of religion or belief to the country's Constitutional Council, Forum 18 News Service reported. Meanwhile, the government continues to repress the exercise of freedom of thought, conscience and belief. In January a Baptist pastor, Aleksandr Kerker, was fired from his job because he led worship without state permission. Pastor Kerker lost his job after authorities visited his employer. Pray for believers in Kazakhstan facing the possibility of harsher conditions if this repressive law is passed. Ask God to provide for Pastor Kerker and his family during this challenging time. Pray this pastor forgives his persecutors and for God to touch the heart of these authorities.Philipians 4:6-7

UZBEKISTAN

– Children and Parents Threatened for Attending Services – Forum 18 News
Police in southeast Uzbekistan have begun a campaign against children attending places of worship, Forum 18 News Service reported. The authorities' campaign, which also uses the state-controlled mass media, attacks schools and parents who allow children to attend religious "sects." Pray for Christian families who have come under scrutiny in Uzbekistan. Ask God to give them courage to continue serving the Lord despite what authorities say.Psalm 91.

PLEASE TAKE TIME TO SAY EVEN JUST A WORD.
-Team at Sayuni.

Tuesday, January 20, 2009

DigitalBrain yajitolea kuidhamini mlima sayuni

Ile kampuni kubwa ya kizalendo ya DigitalBrain sasa imejitolea kuudhamini mlima sayuni kwa kuutengenezea website yake itakayogharimu zaidi ya dola 5000.Website hiyo itakayokuwa ni web portal ya aina yake kuwahi kutokea hapa Tanzania itakuwa na kila kitu kinachopaswa kuwapo katika website za kisasa.Kwa muda wa zaidi ya mwaka mmoja na nusu mlima sayuni umekuwa ukipatikana kwenye blog na kwa kuwa kwenye blogu lakini sasa DigitalBrain wameamua kugharamikia shughuli zote za kuitengeneza website hii kubwa na ya kipekee kabisa barani Afrika.
Katika website hiyo itakayokuwa tayari kabla ya mwisho wa mwezi huu,kutakuwa na mahubiri LIVE mbali mbali,muziki wa injili na pia utawaona LIVE wahubiri mbalimbali na wachungaji mbalimbali wanaotumiwa na Bwana hapa nchini.
Pia utaweza kusikiliza radio mbalimbali za kikristo kama Radio WAPO FM, Praise Power FM na Upendo FM zote za jijini Dar.
Kwa wale walio ughaibuni kaeni mkao wa kupokea baraka hizi ambazo wengi mmekuwa mkizisubiria kwa muda mrefu.
Pia utaweza kushiriki mijadala mbalimbali ya wapendwa na mambo ya kisiasa na kijamii.Kuchat na wapendwa mbalimbali,kununua na kuuza bidhaa mbalimbali, kupata taarifa za nyumba za kupangisha na kununua, na mambo mengine mengi mengi mengi ya kujenga.
Kwa hivi sasa DigitalBrain wanarusha vipindi vyao kupitia radio WAPO FM na unaweza kuwasikiliza LIVE kupitia mtandao wao wa http://www.digitalbraintz.com/ . Waweza kusikiliza kipindi chao kilichorushwa jumatau ya jana na jumatatu zingine zilizopota.
Akiongea na Mlima sayuni mkurugenzi wa Ufundi wa DigitalBrain Mr. Marco Salimu amesema kuwa wameamua kufanya kitu kizuri kwa ajili ya mwili wa Kristo na wamejitolea kiasi hicho cha fedha kwa kuwa wanaamini katika kutoa na kubarikiwa katika kipimo cha kujaa,kushindiliwa,kusukwasukwa kumwagika jinsi Bwana YESU atakavyowabariki.
...DigitalBrain..By the renewing of your mind..

Saturday, January 10, 2009

KWA HERI SEDEKIA

Hakika mtumishi wa Mungu alale kwa amani!

Kama kuna watu walibariki moyo wangu ni Fanuel Sedekia na naomba niamini vivyo hivyo kwa mioyo ya watu wengi kama jinsi ambavyo umati wa watu ulivyojihudhurisha pale kwenye viwanja vya Sheikh Amri abeid Karume, Arusha mjini. Mtu huyu alipendwa na wengi na huo ni udhihirisho tosha namna ambavyo mwili wake uliheshimiwa kwenye kuagwa na hata mazishi yake.

Yatosha kwa siku maovu yake na Bwana ampe faraja haswa mjane na watoto wake pasipo kusahau wote walioguswa na msiba huu kwa namna moja ama nyingine!!

Hebu basi tujikumbushe walao kwa nyimbo hizi wakati tukiendelea na maombelezo.

KWAHERI KAKA YETU SEDEKIA


BWANA YESU ASIWE WAPENZI WOTE WA SAYUNI NA PIA WOTE WALIOMPENDA NDUGU FANUEL SEDEKIA.

Hatimaye leo tarehe 10,January 2008, ile safari ya mwisho kwa hapa duniani ya kaka yetu mpendwa, muimbaji Fanuel Sedekia imefanyika leo hapa jijini Arusha.

Mwili wa kaka Sedekia (36) uliletwa kwa ndege maalumu jana na kufika hapa Arusha hospitali ya mkoa majira ya saa 12 kamili jioni ulipohifadhiwa hadi leo asubuhi.

Leo asubuhi mwili wake uliletwa katika uwanja wa mpira wa Sheikh Amri Abeid hapa Arusha ulipowekwa kutoa nafasi kwa watu walioweza kufika kutoa heshima zao za mwisho kwa kaka yetu.
Baadaye mwili wake ulipelekwa kuzikwa katika makaburi yaliyopo Njiro hapa Arusha.

Zoezi hilo limefanyika leo na hii ni taarifa fupi tuu kwenu kuwajulisha kilichotokea. Kesho nitawaletea picha kadhaa na maelezo zaidi kuhusu tukio hili la aina yake.

"Yes, brother Sedekia, We will meet on that beatiful shore when the time of the Lord comes"

MUNGU UNABAKIA KUWA MUNGU HATA KAMA HUKUJIBU KAMA TULIVYOTAKA SISI.

Wednesday, January 7, 2009

DigitalBrain waanza kusikika live kwenye Internet

Ile kampuni inayokuja juu na kwa kasi katika maswala ya teknolojia ya habari na mawasiliano ya DigitalBrain imeanza kurusha vipindi vyake vya radio kupitia kwenye mtandao live.
Akizungumza na Sayuni , mkurugenzi wa ufundi wa kampuni hiyo Bw. Marco Salimu amesema kuwa wameamua kurusha vipindi hivyo vya radio kwenye mtadao ambavyo hurushwa na radio Wapo FM ya jijini Dar es Salaam ili kuwapa fursa wasikilizaji walioko maeneo kusikofikika na mawimbi ya radio hiyo kuweza kupata elimu hiyo inayotolewa na wataalamu wa kampuni hiyo.
DigitalBrain ni kampuni ya wazawa inayojihusisha na maswala ya ICT iliyojizolewa umaarufu mkubwa miongoni mwa jamii kwa hivi sasa kutokana na kipindi hicho.Kipindi hicho hurushwa na radio hiyo kila siku ya jumatatu saa mbili kamili usiku hadi saa tatu kamili.
Waweza kusikiliza matangazo hayo hapa kwenye link hii www.digitalbraintz.com

Mungu awabariki DigitalBrain kwa kazi njema.

Tuesday, January 6, 2009

Every action you take is a seed you sow, and every seed you sow is a harvest you'll reap

Every action you take is a seed you sow, and every seed you sow is a harvest you'll reap.

Have you ever had a thought like this: "Nobody would ever notice"? Or this: "It's just a little thing"? But to God, every action -- big or small -- is important, because every action you take is a seed you sow.

For example, say that you tell your boss you worked eight hours when really you only worked six. But on the other hand, it's only two hours, and "nobody will ever notice." However, you're sowing seeds of dishonesty in your life that will reap a harvest of the very same thing.
Do not be deceived: God cannot be mocked. A man reaps what he sows. The one who sows to please his sinful nature, from that nature will reap destruction; the one who sows to please the Spirit, from the Spirit will reap eternal life. (
Galatians 6:7-8) Don't think that you can lie to someone (i.e. sow a seed of dishonesty), but yet expect to reap a harvest of truth in your life.
Proverbs 22:8 warns that He who sows wickedness reaps trouble.

Therefore, be very careful about how you act in every area of life, because every action you take is a seed you sow, and every seed you sow is a harvest you'll reap.

God Bless you as you put this into actions.
If you want to receive weekly wisdoms in your email go to
www.lema.or.tz and click "Mailing Lists to join"

pray for the persecuted church


Thank you for joining with us as we pray for the persecuted church around the world. "Confess your trespasses to one another, and pray for one another, that you may be healed. The effective, fervent prayer of a righteous man avails much." -James 5:16


VOM Prayer Update for December 30, 2008On Wed. Dec 31 2008 at 07:59 AM Moderator wrote: CHINA - 40 Christian Leaders Detained, 16 Sentenced to Administrative Detention - China Aid AssociationOn Dec. 16, 40 pastors and house church leaders were detained at a Christian leaders gathering in Taoling village, Henan province, according to China Aid Association. Officials told the Christian leaders they needed to pay between a 1,000 to 2,00 yuan fine (US $11.20-$22.40). Some of the Christians were released after paying the fine. However, 16 leaders were sentenced to 10 to 15 days administrative detention for engaging in an "illegal religious gathering." Mr. Yan Linshan, the host of the meeting, received 10 days of administrative detention and a 1,000 yuan fine. Pray for the imprisoned Christian leaders. Ask God to encourage them and their families during this difficult time. Pray God protects Christians in China and for them to forgive their persecutors.Psalm 27:1

INDIA

- Hindu Extremists Attack Christians in Karnataka - Compass Direct NewsOn Dec. 14, Hindu extremists from the Bajrang Dal group attacked a Christmas program organized by the Helping Hands organization and accused the director of forcible conversion. Extremists disrupted the program which helps rural women and children, accusing Samuel Moses of trying to forcibly convert women and children. The extremists burned gospel literature and took Moses and his accountant to the Bangarapet police station. The Christians were detained in the police station for about nine hours, with the incident publicized on local broadcast and print media. The Christians were later released without charges. Police Inspector Chinnana Swami told Compass Direct that the Christians were detained for questioning, but police found no forcible conversion and the case has been closed. Praise God the Christians were released. Ask God to protect Christians in India who face intimidation and sometimes imprisonment because of their faith in Christ.Romans 8:31

VIETNAM

- Authorities Destroy Church Building - Compass Direct NewsOn Dec. 17, local government officials destroyed a new wooden church building built by Hmong Christians in Cu Hat village, Dak Lak province, Compass Direct News reported. A large contingent of government officials, police and demolition workers arrived at the church in the morning and destroyed it. Police with electric cattle prods beat hundreds of distraught Christians who rushed to the site to protect the building. Five people were injured in the atack, including a child who suffered a broken arm and a woman who was poked in the stomach with a cattle prod. Pray for those injured in this attack. Pray believers will be able to rebuild the church building.Romans 8:11

MWIMBAJI WA INJILI FANUEL SEDEKIA KATUTOKA. HABARI ZA KUSIKITISHA ZIMEINGIA SASA HIVI KWAMBA MWIMBAJI MAHIRI WA NYIMBO ZA INJILI, FANUEL SEDEKIA, AMEFARIKI DUNIA JANA KATIKA HOSPITALI YA PORIYA TIBERIA, HUKO ISRAEL.
HABARI ZINASEMA MAREHEMU ALIKUWA AMELAZWA KWA WIKI TATU HOSPITALI HAPO AKISUMBULIWA NA KISUKARI PAMOJA NA NIMONIA. ALIKUWA HUKO KATIKA MSAFARA WA MAHUBIRI NA MCHUNGAJI MWAKASEGE.

MIPANGO YA KUULETA MWILI WAKE NYUMBANI KWA MAZISHI UNAFANYWA NA TUTAENDELEA KUWAFAHAMISHA HABARI ZINAPOTUJIA. KWA SASA KINACHOFAHAMIKA NI KWAMBA MSIBA UTAKUWA NYUMBANI KWAKE ARUSHA NA ATAKAPOZIKIWA BADO HAIJAJULIKANA KWANI YEYE KWAO NI KIGOMA.
BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA...JINA LA BWANA LIBARIKIWE..
source: swahilitime.blogspot.com

Wednesday, December 31, 2008

SAYUNI WEEKLY WISDOMS

Shalom and Praise the Lord!

Oh, what a pleasure is to see this day (31st December 2008)! It is as it was said "This is the day the Lord has made, we will rejoice in it" Yes, we rejoice but also be thankful for it for we can earn it by our own.

As we live in this end day of the 2008 year, I would like to share with you these two Christian Weekly Wisdoms to take you through the years.

This Week's Weekly Wisdoms are:


1) God is not necessarily looking for ability, He is looking for availability.
2) Are you so hungry to own more money that your money owns you?


Please click here now to go to www.lema.or.tz where you can read the messages.
I wish you a Prosperous 2009 year, a year in which you will know the Lord more deeply and have all success in Him.


Blessings from Arusha,
Frank Lema
www.lema.or.tz

IJA

Tuesday, December 30, 2008

Mtoto umleavyo..!

Picha hapan chini ni mtoto aliyekutwa huko Coco Beach akinywa pombe huku mama yake akifurahia hali hiyo na kumuunga mkono kwa kumsifia kuwa huwa anamaliza bia chupa mbili kwa siku na wala halewi.

Wazazi tunawajibu mkubwa kwa watoto wetu hasa kuwaombea na kuwafundisha njia ipasayo katika misingi ya kibiblia.



Kwa hisani ya mrokim.blogspot.com

Monday, December 29, 2008

“SEIZE THE DAY!”

I confess that I am guilty of using phrases like, “should of”, “If only”, “could have”, etc. way too much. This means, I am living in the past. I also confess that I live too much of my life in the future. Unfortunately, if most of my time is spent wondering if I should have made a different decision in the past, and hoping and praying about the decision I have to make next month, TODAY is lost. I am trying (after all these years) to learn to “embrace the moment”. Carpe Diem….”Seize the Day.”
Lately, I have found myself in conversations with my wife, one of my children or a friend talking about this subject. It’s so easy to second guess ourselves on what we did or said yesterday or we find ourselves waiting for the “miracle check” in the mail, (hopefully coming tomorrow) that will change everything. I realized that I am not living in the moment. God is in the moment! He is with you…, RIGHT NOW! Yes, He is in your past and He is in your future. He holds your future in His hands. But let’s not forget that God has something for you, for me, in this day….in this moment.
A friend sent something to me yesterday that I would like to share with you. Here is an excerpt of the letter:
Read something recently from a book called “the Shelter of the Most High” that I thought was kind of interesting & I’d share. There’s a chapter in there entitled “The Valley of Fruitfulness”. Quoting from 1 Kings 20:28, the author wrote (various extracts):
No matter what the enemy tries to tell you, Christ is God of the mountains AND God of the valleys. He has not stopped being God because you happen to be in a valley. In fact, these valleys are often as much the plan of God as our mountaintop experiences.
When we are on the “mountaintops” of our Christian experience, we can see our future clearly. We have perspective & confidence. When we are in one of life’s valleys, however our vision is limited & our future seems hidden. Yet valleys are also the most fertile places on earth. Valleys produce fruitfulness. You can expect there to be a harvest of virtue when God dwells with you in the valleys.
From Ps 84:5-6, each of us has times of weeping when our hearts & hopes seem crushed. Because God has placed in our hearts “highways to Zion”, however, we pass through valleys; we do not live in them. Once we are on the other side of weeping, our Redeemer makes our valley experience into “a spring”. The very things that overwhelmed us will, in time, refresh us with new life.
Consider Gen. 41:52. God made Joseph fruitful in the very things that afflicted him. In the land of your affliction, your battle, is the place where God will make you fruitful. Just as He allowed Joseph to go through many trials, so He allows us to go through great conflicts as well. For He knows that our lives - what we have become through His grace - will help others find the shelter of the Most High God in their lives.
Consider even now the area of greatest affliction in your life. In that area God will make you fruitful in such a way that your heart will be fully satisfied & God’s heart fully glorified. Ultimately, the Lord will touch many other with the substance of what you have gained. In a world that is superficial, Christ will produce something within you that is deep & living.
God has not promised to keep us from valleys & sufferings but He has promised to make us fruitful in them. Without a doubt we each will pass through valleys before we reach our final goal in God. As we remain faithful to Him in trails, the character & nature of Christ Jesus will emerge in our spirits; & Christ will be revealed to those around us. He intends to make your life a key that unlocks God’s shelter for others.
I trust this will bless you today. No matter what you are facing, remember that God has not forsaken you, He has not forgotten you, He is there with you right now in the middle of the night, in the middle of the storm, in the valley.
This is my prayer today. “Lord, forgive me for living in the past or waiting for the future. Help me embrace this moment, this day. I believe You have something special for me to learn this day. Through the storm, in the darkest night, in the deepest valley, You are with me, You will sustain me. Be glorified through my life this day. Help me see You in every situation, and if I can’t see You, increase my faith so I can trust you through the darkness, through the silence and know, by faith, that You are with me. I give you praise for all You have done for me and for all You are doing today! In Jesus’ Name…..amen.”
God bless you, my friend.
Hope this connects with some of you.

Power of the Blood

“Here’s a definition of holiness that I submit for your thoughtful consideration. Holiness is: proximity to the throne.
At the throne of God are myriads of creatures. Those with the greatest honor seem to be those who live closest to God, living inside & around the throne itself. These beings are given various names in Scripture such as angels, cherubim, seraphim, & living creatures. When referring to al of them at once, the Bible uses an interesting phrase. It calls them the “holy ones” (see Daniel 4:17, Job 5:1)
I want to suggest they’re not holy because of who they are; they’re holy because of where they are. They reside in the Holy Place, the place where God dwells, & they are made holy because of their proximity to God.
They’re not holy because of who they are; they’re holy because of who God is. They’re not holy because of something inherent to them, but because of something inherent to God. God alone has holiness as an inherent attribute. He alone is “The Holy One”. All others who surround His throne are holy as a derived quality. They derive their holiness from their proximity to The Holy One. Everything close to God is holy. Why? Because God radiates holiness, & everything close to Him becomes holy by virtue of its nearness to Him. In other words, He brings them into that quality or state which enables them to live in His immediate presence without being destroyed.
If you get close enough to God, you too will become holy. Not because of who you are, but because of where you are. You have received the sprinkling with blood, you have entered with boldness into the throne room, you have drawn near to God; & now the holiness that defines God’s personhood permeates every atom of your being & makes you holy, too. You’re holy because you’re in the presence of The Holy One.
When you understand this principle, you have no hesitation in saying, “I am a holy man (or woman) of God”. Being “a holy man of God” loses its mystique, its sense of elitist superiority, or the connotation of “exceptional spiritual maturity”. Some people define as holy the person who has achieved complete victory over the world the flesh, & the devil. Such a definition makes holiness a formidable mountain that appears almost impossible to climb. If I define holiness as complete spiritual victory, I’ll probably see myself as never able to attain it in this life. Holiness, in that distorted model, becomes mostly a list of things that one must not do. But making your list you don’t do isn’t able to make you holy.
I’m suggesting that holiness is not much what I don’t do, as it is what I do do. I get sprinkled with blood, step into the throne room, & stay there. That’s what I do, & that’s what makes me holy.
Holiness is more than simply an absence of defilement. You can focus on cleaning up your act, removing all that defiles, & still not find holiness. Why? Because holiness is not merely the absence of sin; it’s the presence of fire.
To illustrate, suppose I want to build a bonfire. I gather branches & sticks from the woods & place them in a heap. But the sticks I’ve collected are muddy & wet. So I take time to clean off the mud & allow the wood to dry out Eventually I have a pile of wood that is clean & dry. But just because I’ve gotten rid of everything that could quench the fire does not mean I have a bonfire. Getting rid of the fire-retardants does not give me a bonfire. I don’t have a bonfire until there’s - fire!
Holiness is a bonfire, because our God is a consuming fire. You can get rid of everything that might extinguish your spiritual flame, but just getting rid of the negative does not mean you’re ablaze with holiness. You’re not a living bonfire of holiness until you step into the Holiest, get kindled with the living flame upon the altar of God, & burn with a holy fire in the presence of His glorious holiness.”

Wednesday, December 24, 2008

In what year was Jesus born?

It is good that we want to know about Jesus. One can never learn too much about the greatest man to have ever walked on earth.
The exact day of Jesus' birth is difficult to establish beyond all doubt. The fact of Jesus' birth, the place, the nature, and the purpose are clearly taught in the scriptures (Matt. 1; 2). However, God did not see fit to explicitly reveal the date. We do know that Jesus was born during the reign of Herod the King (Matt. 2: 1). History informs us that this Herod died in 4 B. C. Hence, Jesus would have been born no later than 4 B. C. We also learn from the Bible that a census was being taken at the time of Jesus' birth, in fact, Joseph and Mary were at Bethlehem to enroll when Jesus was born (Lk. 2: 1-7). Quirinius, the Governor of Syria, conducted this census. Based on the believed date of this census, some place Jesus' birth at 6 B. C. Some scholars believe Jesus was born in 5 B. C. In the center column reference of some versions of the King James Translation, we read regarding the time of Matthew 2, "The fourth year before the common account called Anno Domini (A. D., dm)." This date, I believe, is the product of the work of Dionysius Exiguus, a sixth century monk.
The real matter of importance. The matter of great consequence is that Jesus was born of a virgin, just as prophesied 700 years earlier (Matt. 1: 23; Isa. 9: 6). Jesus lived a sinless life and died a sacrificial death (Heb. 4: 15; Matt. 26: 28). Jesus claimed to be the Son of God and proved that claim by many undeniable miracles (Jn. 20: 30, 31).
Christians celebrate the glorious death and resurrection of Jesus each Lord's Day when they observe the Lord's Supper (Matt. 26: 26-29, Acts 20: 7). Jesus is the truth, the way, and the life (Jn. 14: 6). This same Jesus who experienced such a humble birth is coming back as the exalted judge of all men (Matt. 25: 31-46).
Mlima Sayuni unawatakia Heri ya Chrismas na mwaka mpya wenye furaha na fanaka.

Merry Christmas! from Frank Lema

Nothing steals your joy like thinking, "I will enjoy my life when ..."It's very tempting to think that happiness will come to me once I get something: "I would be happy if I just had a bigger house, another car, a better job, more money, a different wife, a nicer family, a new TV...." But such thoughts are very deceptive.In truth, all those things we want actually make us miserable; we fight and quarrel about what we want, and then we're upset when we don't get it (see James 4:1-4). Don't get caught up in things that you want or need. Instead, you should not worry about getting what you need; rest assured your heavenly Father will take care of what you need (see Matthew 6:30-32).It's foolish to make your enjoyment of life hinge upon anything. There will always be one more thing for you to acquire before you can "enjoy life." The more you have, the more you have to worry about, which makes life that much harder to enjoy.Instead of expecting possessions or circumstances to give you joy, seek the only source of everlasting joy—Jesus. Jesus says he came to Earth "so that may have the full measure of my joy within " (John 17:13). Similarly, Jesus said, "I have told you this so that my joy may be in you and that your joy may be complete" (John 15:11).Jesus offers to make our joy complete and to give us the full measure of his joy. Since Jesus is wholly God, His joy is complete and whole joy. That Jesus offers us such joy is astonishing.Therefore, find your joy in God for in his presence is fullness of joy (see Psalm 16:11). Don't let your joy depend on getting all the things you want because there will always be more things that you don't have, and therefore there will always be more things that will prevent you from enjoying life. Let Jesus be your joy, rather than waiting to enjoy life "when...."God loves you not because of what you do, but because of who He is.God is love (1 John 4:8). God doesn't have to pretend to love you; He can't not love you, because He is love.In fact, the very actions of God exemplify what love is. The apostle John explains that this is how we know what love is: Jesus Christ laid down his life for us (1 John 3:16). Only a few verses later, he further defines love: This is love: not that we loved God, but that he loved us and sent his Son as an atoning sacrifice for our sins (1 John 4:9).Notice that God's love for you is independent of how you behave, who you are, or how you respond to that love.Romans 5:6-8 reminds us that God loves us regardless of where we are: You see, at just the right time, when we were still powerless, Christ died for the ungodly. Very rarely will anyone die for a righteous man, though for a good man someone might possibly dare to die. But God demonstrates his own love for us in this: While we were still sinners, Christ died for us.Jesus represents God's love for us in what we now call the Parable of the Prodigal Son (see Luke 15:11-24). In that allegory, the father openly and lovingly receives his son even though the son had run away, squandered all of his money, and insulted the father. In the same way, God loves us unconditionally.There is nothing you can do to get God to love you -- He already does. There is nothing you can do to deserve God's love, because, by sinning, you have turned your back on God and are fundamentally no different than the prodigal son. That parable is a clear reminder that God loves you not because of what you do, but because of who He is.
I pray that these will be a blessing to you, Amen.
Here is something for you, for this Christmas season. Please move your cursor to here, and click here.

God Bless you
-In His Service,
Frank Lema.

Monday, December 22, 2008

Umejiandaaje kumalizia mwaka 2008 na kuanza mwaka mpya wa 2009?

Bwana Yesu asifiwe sana!
Ninamshukuru Mungu kwa Neema zake kuu na Upendo wake usio na kipimo kwa nafasi hii aliyotupa ya kujifunza Neno lake la Uzima kwa njia hii. Sifa ni kwake.
Ninamshukuru Mungu Baba kwa kutufikisha tena mwezi huu wa mwisho wa mwaka 2008. Naamini kuwa hata wewe mwenyewe unaona kuwa hii ni Neema kubwa sana. Neema ambayo hatukulipa chochote kupewa, ni zawadi kutoka kwa Baba Mungu kwa upendo wake. Ni wazi kuwa watu wengi sana walifikiri kuwa watafika siku kama hii ya leo lakini leo hawapo hai. Sisi tumefika hapa kwa sababu Baba Mungu ana kazi nasi tena, na ni kwa upendo wake tuu.
Tunapoelekea kuumaliza huu mwaka, ni vizuri tukitafakari pamoja mambo machache.Kwa wale walioweze kutembelea website yangu mwanzoni mwa mwaka huu, niliweka ujumbe maalumu wa "Salamu za mwaka mpya 2008" na nilizungumza kwa Roho Mtakatifu mambo muhimu sana kwa ajili ya mwaka 2008. Miongoni mwa mambo hayo, Roho Mtakatifu alitufundisha kuwa, Tuweke malengo kwa ajili ya mwaka mzima wa 2008, kisha tuweke mikakati ya namna ya kuyatimiza malengo hayo, tuyaombee malengo yetu kwa Mungu, n.k. Tena tuyaandike malengo yetu kwenye karatasi na kuyatunza. Je wewe ulifanya hivyo?
Kama uliweka malengo yako kwa mwaka 2008, sasa tumefikia mwisho wa mwaka, ni wakati sasa wa kukaa chini kwa utulivu na kuanza kuyapitia tena malengo yako, utathmini mafanikio yako.
Unapoyapitia malengo uliyojiwekea, tafakari ni kwa kiasi gani umefanikiwa kutimiza mipango uliyojiwekea ndani ya mwaka huu, ni kwa kiwango gani hujafanikiwa kuyatimiza malengo yako, na umwombe Mungu akuonyeshe ni sababu zipi zimekufanya usiweze kuyatimiza malengo yako. Hii ni muhimu kwani itakusaidia kujua ni mbinu gani uzitumie kufanikiwa mwaka ujao wa 2009.
Tafakari pia baraka na mambo yote mema ambayo Mungu amekukirimia kwa mwaka huu wa 2008. Kwa maneno mengine "HESABU BARAKA ZAKO" Angalia baraka Mungu alizokupa na maneno uliyokuwa unayakiri kuhusu mwaka 2008. Inawezekana umekuwa ukisema kuwa "Ah, mwaka huu siyo mzuri bwana!" Sasa je, ukiangalia Neema Mungu alizokupa, kauli hiyo ni sawa?? Mshukuru Mungu kwa baraka zake zote hizo, hata kama unaziona kuwa chache na ndogo, kumbuka ni Neema hiyo. Tenga muda maalumu kumshukuru Mungu kwa yote.
Tafakari pia mambo ambayo umeyaona kuwa ni mabaya kwa mwaka 2008. Pengine umemlaumu Mungu kwa kuyaacha mambo hayo kukutokea, lakini jiulize, Je, ni makosa ya nani? Wewe mwenyewe unajua kuwa Mungu huwa hafanyi makosa, kwa hiyo ni wazi kuwa inawezekana uzembe wako au kutokuwa makini kumechangia, pamoja na adui yetu shetani kutupinga. Hapo ndipo kunatokea umuhimu wa kutubu kwa kila mwezi wa mwaka 2008, mwombe Mungu akusamehe kwa uzembe wote ulioufanya, naye atakusamehe hakika.
Baada ya mambo hayo, sasa tumia siku zilizobakia kuanza kumwomba Mungu aanze kukuonyesha mambo ya 2009. Sasa anza kuweka tena malengo yako kwa ajili ya mwaka 2009. Panga mikakati ndani ya Kristo ambayo unataka kuitimiza mwaka 2009. Kumbuka namna unavyojiwekea malengo kuna athiri namna utakavyofanikiwa. Usipoweka malengo ni hatari, kwani ukiweka malengo na kuyaandika mahali, hayo malengo yatakuwa yanakuhimiza na kukumbusha kuongeza bidii ili kuyatimiza yote. Ni kama usemavyo msemo wa kiingereza "No man is greater than his vision" Hakikisha unaweka malengo kwa ajili ya mwaka ujao.
Hatua nyingine ni kuweka mikakati, yaani ni namna gani utakavyoweza kuyatimiza malengo hayo uliyojiwekea? Kwa mfano, kama wewe ni mzazi na unataka mwaka unaokuja uwe karibu zaidi na watoto wako ili kuzungumza nao na kuwafundisha mambo mbalimbali, hii ina maana kuwa unatakiwa uwe mwangalifu zaidi kutunza muda, ili upate muda wa kukaa na watoto wako. Weka mikakati.
Kumbuka kumwomba Mungu kwanza kabla ya kufanya tathmini yote hiyo.
Haya ndiyo mambo ambayo siku ya leo nimehimizwa nikushirikishe kwa kipindi hiki cha mwaka. Mungu akipenda hivyo, nitaendelea kukushirikisha zaidi na zaidi kupitia Huduma hii ya Mailing Lists. Kama una maswali au ushauri wowote tunavyoelekea mwisho wa mwaka, karibu.
Tuendelee kuombeana katika Jina la Yesu Kristo.
Ni mimi katika Utumishi,
Frank Lema.

Thursday, December 4, 2008

Mchungaji kortini

Mchungaji wa Kanisa la Pentekoste Kimara jijini Dar es Salaam Jonathani Ilunga anayekabiliwa na Kesi ya Utapeli kwenye Mahakama ya Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, jana aliwekwa chini ya ulinzi mkali baada ya kubaikika kuwa aliyemuwekea dhamana alikuwa ameghushi nyaraka.
Mchungaji huyo anakabiliwa na kesi ya utapeli wa mamilioni ya pesa kutoka kwa wananchi mbalimbali akiwemo Shabani Kassimu mfanyabiashara aliyedai kutapeliwa mali zenye thamani ya shilingi milioni 2.5 na mtumishi huyo wa Mungu.Baada ya kufika mahakamani hapo jana na kusomewa mashtaka yake, Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo Bi.Hellen Riwa alieleza kuwa amepokea barua kutoka kwa msajili wa kesi kwamba hati za dhamana zilizowasilishwa na mdhamini wake aitwaye Sharif Mohamed zilikuwa za kughushi, jambo lililoifanya mahakama hiyo kumfutia dhamana.Katika hali ya kushangaza Mchungaji huyo alikana mbele ya Hakimu kutokumjua Mdhamini wake Sharif ambaye inadaiwa kughushi nyaraka hizo na hivyo kuwasilisha nyaraka zake binafsi ambazo hata hivyo zilitupiliwa mbali.Baada ya dhamana yake kufutwa mchungaji huyo alitoa kioja kingine cha kugoma kutoka nje ya mahakama jambo lililowalazisha polisi kumtoa kwa nguvu na kumsweka lupango, hadi Desema 27 kesi yake itakaposikilizwa tena.

Friday, November 28, 2008

Let's pray for this:

Thank you for joining with us as we pray for the persecuted church around the world. "Confess your trespasses to one another, and pray for one another, that you may be healed. The effective, fervent prayer of a righteous man avails much." -James 5:16

CHINA

– Trial for Detained Christian Delayed – China Aid Association Chinese officials have yet to declare a new court date for Alimujiang Yimiti, a Christian house church leader and ethnic Uyghur in China’s northwest province of Xinjiang, detained since his arrest on Jan. 12, China Aid Association reported. In mid-October, Chinese state prosecutors returned Yimiti’s case to a Xinjiang court for consideration. Charges against Yimiti include “inciting secessionist sentiment to split the country” and “collecting and selling intelligence for overseas organizations,” CAA reported in June. Yimiti converted from Islam to Christianity more than 10 years ago and became active in the growing Uyghur church. Media reports state that Yimiti’s friends have said they believe his faith is the real reason for his arrest. Officials have threatened to hand down a sentence ranging from six years in prison to the death penalty. Pray for Yimiti and his family during this difficult time. Ask God to protect and comfort them and for believers in China to continue living out their faith unashamedly. Philippians 4:6-7

ALGERIA

– Christians Acquitted in Blasphemy Case – Compass Direct News On Oct. 29, a court in northwestern Algeria acquitted three Christians charged with blaspheming Islam and threatening a member of their congregation who reconverted to Islam, Compass Direct News reported. The defendants believe the judge’s decision to acquit was due to the spurious evidence used against them. The acquittal also comes as part of a larger trend of the Algerian government bowing to negative international media attention and government condemnations of such cases, they said. Defendant Youssef Ourahmane said that as a result, a recent government crackdown against evangelical Christians has eased off in recent months. “We had noticed the last four or five months the government is trying to back down a little bit,” Ourahmane said. “I think the pressure on them has been strong, such as condemnations from the U.S. and foreign ministries from France, Italy, Switzerland, Austria and Spain. This pressure from outside has embarrassed the Algerian government very much,” he added. Pray for believers in Algeria who face intense challenges when they live their lives for Christ. Ask God to encourage them and for grace to forgive their persecutors. Isaiah 54:17

KAZAKHSTAN

– Pastor Sentenced to Community Service for Leading Unregistered Church – Forum 18 News Baptist pastor Andrei Blok has been sentenced to 150 hours of compulsory community service following his refusal to pay a fine for leading an “unregistered congregation,” Forum 18 News reported. “If not for many telephone calls to the court and city officials from around the world, Andrei could have been put into prison for several months," his family told Forum 18 News. Yuliya Merkel of the local Justice Department insisted to Forum 18 that Blok "needs" to register his church, and refused to say what would happen if the church continues to worship without registration. Pray for Pastor Blok, his family and congregation. Ask God to bless and encourage them during this challenging time. Pray they will be a witness of Christ’s love to their persecutors. 1 Corinthians 15:57

Now that we have the freedom to worship our Mighty God without inteferences, let's pray for our fellow brothers and sisters around the world who are being persecuted daily.
I am sure God will bless us all.

Lema.

Thursday, November 27, 2008

Is There a Mansion in Heaven for You?


One of these days, if you're faithful, you'll own a mansion that won't cost you anything!--No rent or expenses! Jesus said, "In My Father's House are many mansions. I go to prepare a place for you." (Jn.14:2)--And your rewards There will be proportioned according to your works here. Whatever you have There, you will have already sent ahead in the way of souls won, victories won, battles won & rewards won for your service here!It's like the well-known tale about the rich woman being led to her Heavenly Home by an Angel: They walked past many beautiful mansions where other Christians were living, until finally they got to a poor section of shanties, & the Angel led her through a gate into the yard of a tiny hut. "What's the big idea?" she said, "I'm used to very fine living!" "Well," the Angel answered, "the abodes up here are built of what each person sends on before, & this is all you sent!"--Whereas others had sacrificed & lived their whole lives for the Lord & helped many others, & great was their reward in Heaven!So just be faithful, & one day you'll find that whatever you've paid here is not worthy to be compared with the glory to be revealed there in that Heavenly place that He's gone to prepare!

KUKAMATWA KWA VIONGOZI WA SERIKALI TANZANIA WAKRISTO TUFANYE NINI?

Shalom watu wa MUNGU!


Nimekuwa nikifuatilia hali ya mambo ya kisiasa na matukio ya kupelekwa mahakamani kwa watu ambao hakika tusingeweza dhania kwa siku za huko awali. Hivi punde tumesikia juu ya watuhumiwa wa EPA na pia juzijuzi Mh. ndugu Mramba na Daniel Yona na tetesi zinasema bado wengine wengi wako mbioni kuelekea mkono wa sheria.

Sasa basi kama kanisa na watu wa MUNGU, Je! Tuhesabu kwamba huu ni ushindi wa maombi mengi ya watu ambayo wamekuwa wakifanya mfano yakiwa yale yaliyofanyika Jangwani na mengineyo? Na kama kanisa je kipindi hiki tufanye nini? Tumshukuru au ndo tukaze kamba kuhakikisha kwamba hawa watu wanafungwa wote? Mh.Daniel Yona (l) na Mh. Basil Mramba wakiwa Mahakama ya Kisutu, DSM.
Nachelea sana kwa hali hii kwani isije leta namna ya mtafaruku wa amani nchini mwetu haswa pale watakapoanza kukaangana wenyewe kwa wenyewe walio kwenye mamlaka maana ndio wahusika wakuu. Ni maombi yangu kitu chochote cha kutishia uvunjaji amani kisitokee kamwe! Japo najua adui hafurahii hili kabisa!

Kama watu wa Mungu hebu tushauriane hapa Mlimani Sayuni ili tujue tunaipekaje nchi yetu TANZANIA mbele za Baba yetu aliye mbinguni.