Hii ni Blogu ya watu wote...uwe huru kuchangia neno lolote unaloona linafaa kwa ajili ya kuujenga mwili wa Kristo
Tuesday, July 21, 2009
Kadhi ni nani?
Wakristo tunayo HAKI ya kushiriki kyk kutazama mahakama ya kadhi kabla ya kuiruhusu/kukubali itumike ktk kutoa hukumu hapa nchini Tanzania.
Hii ni kwa sababu itakapoanza kutoa hukumu hapa nchini haitakuwa juu ya waislamu tu bali hata kwa wengine kwa sababu za kizazi.Hii ni kwa maana wapo wapo wakristo waliooa na kuzaa na waislamu pia wapo waislamu waliooa na kuzaa na wakristo hivyo hukumu kupitia vitabu vya dini ya kiislamu haigusi waislamu tu bali hat jamii ya wakristo.
Ni vema tuanze kwa kumtazama huyu mtu aitwae KADHI je ni nani na anabeba sifa zipi ili tuwe huru kumpa madaraka ya kuhukumu.
BIBLIA;LUKA 18;2-6
(Akasema palikuwa na KADHI katika mji fulani hamchi Mungu wala hajali watu.Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane aliyekuwa akimwendea endea akisema.Nipatie HAKI na adui wangu Nae kwa muda alikataahalafu akasema japokuwa simchi Mungu wala sijali watu lakini kwa kuwa mjane huyu ananiudhi nitampatia haki yake asije akanichosha kwa kunijiadaima.Bwana akasema sikilizeni anayosema yule KADHI dhalimu).
Katika neno hilo tunazipata sifa kuu nne za KADHI nazo ni
1HAMCHI MUNGU.
2.HAJALI WATU.
3HUTOA HAKI PALE ANAPOSUMBULIWA.
4.NI DHALIMU.
Ikiwa kama ameshindwa kumpa HAKI yake mjane ambaye ana HAKI YA KUSAIDIWA, Je ataweza kutoa HAKI ya HUKUMU ya KWELI hapa TANZANIA?
HAPANA KWA SABABU HANA SIFA ZINAZOSTAHILI.
swala jingine la kujifunza ni kuwa waislamu wanalalamika kuwa serikali imewanyima HAKI YA KUABUDU(majira 7/7/2009. je ni haki gani hiyo ya kuabudu wakati kila siku tunasikia AZANA misikitini nao huenda huko kuabudu?
Moja ya mikakati ya serikali yetu hapa tanzania katika kulinda amani na utulivu imetoa UHURU WA KUABUDU KWA WATU WOTE kama ilivyo kwa watu wote je ni uhuru gani wa kuabudu waislamu wamenyimwa?
Ikiwa kama kweli wamenyimwa basi wasiende misikitini lakini ikiwa hawajanyimwa basi watubu kwa watanzania kwa kusema uongo.ikifuatiwa na BAKWATA kutengua kauli hiyo katika gazeti la majira 7/7/2009.
Vilevile waislamu huko UK nao wanalalamika kwa kunyimwa haki(Daily News july 15,2009 pg 25.je unajifunza nini katika hili???
Yafaa kutambua kuwa tuko kwenye nyakati za KUNG'ANG'ANIA ULICHO NACHO KWA KUKISHIKIRIA SANA ILI ASIJE MWOVU ..........................
Mkristo yafaa kutembea huku TAA ikiwaka ili kutazama hatua tunazopita kama tunakanyaga mahali sahihi au la.
Hivyo kwawakristo wote wanaoiamini BIBLIA hapa duniani yafaa kufahamu kuwa KRISTO NI MWISHO WA SHERIA.
RUMI 10;1-4
(Ndugu zangu nitakayo sana moyoni mwangu na dua yangu nimuombayo Mungu ni kwa ajili yao ili waokolewe.Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudikwa ajili ya Mungu lakini si katika MAARIFA.Kwa maana wakiwa hawaijui haki ya Mungu na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe hawakujitia chini ya haki ya Mungu.Kwa maana KRISTO NI MWWA SHERIA ili kila aaminie ahesabiwe HAKI.
NA BARAKA ZA MUNGU MWENYEZI,ZA BABA,ZA MWANA NA ZA ROHO MTAKATIFU ZAWASHUKIE NA KUKAA NANYI DAIMA.
AMEN.
Charles Kabaka
Thursday, July 16, 2009
MBUNGE wa kuteuliwa na mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale Mwiru ameushambulia waraka wa kichungaji uliotolewa na Kanisa Katoliki nchini, unaoelekeza namna ya kupata kiongozi anayefaa kuchaguliwa katika Uchaguzi Mkuu ujao adai kuwa utaligawa Taifa.Kingunge alitoa kauli hiyo alipokuwa akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, ambayo iliwasilishwa na George Mkuchika bungeni mjini Dodoma jana.
Hata hivyo, Kanisa Katoliki kupitia Baraza lake la Maaskofu (TEC), limekuwa na utamaduni wa kutoa mwongozo kama huo wakati Taifa linapoelekea Uchaguzi Mkuu, huku kumbukumbu zikionyesha kuwa pia lilifanya hivyo mwaka 2005.
Katika kikao hicho cha jana kilichokuwa chini ya Mbunge wa Peramiho, Jenister Mhagama aliyekuwa mwenyekiti, Kingunge alizungumza kwa msistizo huku akiwataka wabunge wamsikilize kwa makini na kutahadharisha kwamba asinukuliwe vibaya.
``Na sasa nimalize, nina jambo moja kubwa, naomba mnisikilize kwa makini, lakini msininukuu vibaya. Kanisa Katoliki, viongozi wake rafiki zangu, wale wa juu nawafahamu sana, Kanisa hilo limetoa mwongozo kuelekeza anayefaa kuchaguliwa katika uchaguzi ujao.
“Mimi nikautafuta na kuusoma. Sasa hili Kanisa Katoliki linatoa mwongozo wa kuchagua kiongozi wa kisiasa, kwa maana hiyo huu ni mwongozo wa Wakatoliki. Si utakuwa mwongozo wa Wakatoliki pekee?” alisema Kingunge akihoji.
Aliendelea kusema: “Kwa hiyo KKKT (Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania) nao watoe mwongozo kwa sababu wao hawaongozwi na Kanisa Katoliki, ni Wakristo ndiyo, lakini mantiki tu. KKKT wakitoa, Pentekoste watatoa wakwao na Anglikana bado, nao watatoa wakwao, Waislamu bado na wao watoe wa kwao.”
Kingunge ambaye ni mmoja wa wabunge wa muda mrefu ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tangu enzi za Mwalimu Nyerere Rais wa Kwanza wa Tanzania aliongeza kuwa anazungumza hayo kwa kuzingatia mantiki ya mwongozo huo.
“Ni mantiki tu, nasema kwa heshima zote nawaomba viongozi wa Kanisa Katoliki, nawapenda sana, nawaomba warudishe ule mwongozo wao, sisi tunataka nchi moja na tuishi pamoja kwa kushikamana, hatutaki kugawanyika kama Lebanon,” alisema Kingunge bila kufafanua zaidi kuwa waurudishe wapi na kwa vipi.
Kauli hiyo ya Kingunge imetolewa wakati waraka huo wa Kanisa Katoliki umezua mjadala miongoni mwa watu wa kada mbalimbali, huku baadhi wakilishutumu kanisa hilo wakidai kuwa linaingilia masuala ya kisiasa.
Hata hivyo, juma lililopita Askofu Msaidizi wa Kanisa hilo Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Methodius Kilaini alisema mafisadi wanauhofia mwongozo huo.
Kwa mujibu wa Kilaini mwongozo huo unaweka vipaumbele vya nchi katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, ndiyo maana wanaupinga.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya misa ya upadrisho iliyofanyika Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph jimboni humo, Kilaini alisema mwongozo huo ulianza kutumika tangu uchaguzi wa mwaka 1995 na kusisitiza kuwa kwa mwaka huu watu wengi wameshtuka kutokana na kugusa masuala ya ufisadi.
Kanisa hilo lilitoa vitabu viwili vya mwongozi na vipaumbele vya nchi kabla ya kuuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2010, mwongozo ambao umekumbana na vipingamizi kutoka kwa baadhi ya wanasiasa kwa madai kuwa dini inaingilia mambo ya siasa.
“Kwanza napenda watu waelewe kuwa mwongozo hauna lolote kuhusu dini kama watu wanavyodhani, kwa sasa jamii imeshituka kuhusu vitendo vya rushwa na ndiyo sababu baadhi ya wanasiasa wanapinga muongozo huo kwa kuwa unalenga kuwafungua watu macho na kukemea vitendo vya ufisadi,” alisema Kilaini na kuongeza.
“Ninachowataka wanasiasa wote washiriki kupiga vita ufisadi. Asiyetaka kupigana na ufisadi tusimchague na ndivyo mwongozo huo unavyosema,” alisema.
Alifafanua kuwa mwongozo huo unazungumzia juu ya serikali na msimamo wake na wala si kumchangua mtu fulani wala chama fulani kwa ajili ya kumpa uongozi.
“Watu wausome mwongozo huo kwa moyo mweupe na ninaamini wataufurahia, utakuza ufahamu juu ya masuala ya kidemokrasia,” alisema Kilaini.
Awali Mbunge wa Kigoma Kusini, Manju Msambya alishutumu mwongozo huo aliouita kuwa ni "Waraka wa Kiaskofu" wakati akichangia hotuba ya makadirio na matumizi ya Wizara ya Sheria na Katiba, akisema unawafundisha waumini wake kuhusu namna ya kuchagua viongozi kwa imani zao na kuonya kuwa nchi inaweza kuingia kwenye vurugu.
Msambya ambaye hakutaja moja kwa moja dhehebu la dini lililotoa waraka huo, alisema unapingana na kanuni inayosema watu wasichanganye dini na siasa.
Lakini Askofu Kilaini alisema mwongozo huo haukutungwa na maaskofu wala mapadri wa Kanisa hilo na kufafanua kuwa umetungwa na Chama cha Wataalam wa Kanisa Katoliki (CPT) na kwamba wao waliupa baraka zote baada ya kuusoma na kuona unafaa.
Source: Mwananchi
DIGITALBRAIN NA SOMO LA UBONGO

Wednesday, July 8, 2009
Mufti Simba asisitiza mchakato wa Mahakama ya Kadhi bado unaendelea
Mufti Simba ametoa kauli hiyo baada ya serikali kutangaza Juni 30 kuwa haitaunda Mahakama ya Kadhi na badala yake itatafsiri sheria za Kiislamu na kuzijumuisha kwenye sheria za nchi ili zitumike kwenye mahakama za kawaida.
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) jijini Dar es Salaam jana, Mufti Simba alisema walikutana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Waziri wa Sheria na Katiba, Mathias Chikawe na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam William Lukuvi juzi usiku na kukubaliana baadhi ya mambo ambayo yataharakisha kuundwa kwa mahakama hiyo.
“Tumekubaliana kwamba hoja ya Mahakama ya Kadhi haijazikwa, ila serikali inahitaji msaada wa masheikh katika suala hilo na sisi tumekubali kutoa msaada huo,” alisema Mufti.
"Hivyo jopo la masheikh litaundwa na serikali itaunda jopo lake la wataalamu halafu tutakutana, ili kuratibu mfumo ambao utatumika katika Mahakama ya Kadhi nchini.”
Hatua ya serikali kutangaza kuzika mpango huo wa kuanzisha Mahakama ya Kadhi ilipingwa vikali na Waislamu ambao walidai CCM iliwahadaa wakati wa kampeni za mwaka 2005 na hivyo kusema hawatakiunga mkono chama hicho kwenye uchaguzi ujao na pia kupanga kuandamana Ijumaa ijayo.
Lakini Mufti Simba alisema kikao chao na Waziri Pinda, kilichohudhuriwa na wajumbe zaidi ya 20, likiwemo jopo la masheikh aliloliteua kutoka madhehebu yote ya Kiislamu , wamekubaliana suala hilo liendelee kushughulikiwa.
"Niliandaa jopo la masheikh kutoka madhehebu yote nchini. Nashukuru kwa kuitikia wito wangu. Tulienda kwa Waziri Mkuu tukazungumza kwa mapana zaidi kuhusu Mahakama ya Kadhi na amekubali kuwa mahakama haijafa na mchakato unaendelea,” alisema Mufti Simba.
Alifafanua pia wamekubaliana na Waziri Pinda kwamba atazungumza bungeni kukanusha kauli iliyotolewa na Waziri Chikawe Juni 30 mwaka huu bungeni mjini Dodoma kuhusu uamuzi wa kuzika hoja ya mahakama hiyo.
Mahakama ya Kadhi hushughulikia hasa masuala ya mirathi na ndoa kulingana na misingi ya dini ya Kiislamu.
"Kimsingi serikali haijakataa mahakama ya kadhi, lakini inahitaji msaada wa masheikh na tumekubaliana na Waziri Pinda akafute usemi wa kwamba serikali haitaunda tena mahakama hii na yeye amekubali," alisema Mufti Simba.
"Kitakachoendelea ni kujadili mfumo gani wa mahakama unafaa kutumika.”
"Tunayo matumaini makubwa ya kuipata Mahakama ya Kadhi kwa sababu ni haki yetu na tutaendelea kuidai hadi pumzi yetu ya mwisho (mpaka kufa), mchakato unaendelea.
"Jazba hazifai na tutumie hoja au kwa msemo wa kisasa tutumie nguvu ya hoja.”
Mufti Simba pia alitoa onyo kali kwa Imamu Mkuu wa Msikiti wa Mnyamani uliopo Buguruni, Sheikh Muhammad Idd Muhammad kwa kuzungumza katika vyombo vya habari yale yaliyozungumzwa juzi katika kikao baina ya serikali na jopo la masheikh, kabla ya Mufti kuzungumza.
"Mzungumzaji wa suala la Mahakama ya Kadhi kwa upande wa Waislamu ni mimi tu, hakuna mzungumzaji mwingine. Hivyo namuonya Muhammad Idd kwa kitendo chake cha kutangulia kuzungumzia yaliyojiri katika kikao chetu kabla mimi kuzungumza,” alionya Mufti.
Akizungumza katika kipindi chake cha Arrisala kinachorushwa na kituo cha televisheni cha Channel Ten juzi usiku, Sheikh Idd alieleza kwa ufupi yale yaliyozungumzwa katika kikao cha masheikh na Waziri Pinda.
Sheikh Idd alikiri kosa na kumuomba radhi Mufti Simba, masheikh wenzake pamoja na Waislamu, lakini aliongeza kuwa hakufanya hivyo kwa nia mbaya.
"Nakiri kosa; lakini pia namuomba radhi Mufti, masheikh na Waislamu licha ya kwamba sikufanya vile kwa nia mbaya. Hata Mufti atajua baadaye kuwa sikufanya kwa nia mbaya,” alisema Sheikh Idd.
Baada ya kumaliza kutoa tamko lake, Mufti Simba alikataa maswali akisema suala hilo la Mahakama ya Kadhi linahitaji umakini wa hali ya juu katika kulizungumza.
"Leo sitaki maswali... sitaki kubabaishwa katika majibu. Nakataa maswali ili haya yakaandikwe kama vile nilivyosema bila ya kupotoshwa,” alisema Mufti.
Kabla ya Mufti kuzungumza na waandishi, Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum aliwatahadharisha waandishi kuacha kuandika na kunukuu kauli za watu wengine, badala yake wachukue yale ya Mufti Simba tu kwa sababu yeye ndiye msemaji mkuu katika tukio hilo.
"Waandishi waondoke na kauli ya Mufti tu yeye ndiye msemaji mkuu wa Waislamu Tanzania kupitia chombo chao cha Bakwata. Hakuna msemaji mwingine,” alisema Sheikh Salum.
Hoja ya Mahakama ya Kadhi imekuwa ikidaiwa na Waislamu kwa takriban miaka 20 sasa huku serikali ikitoa ahadi ya kulipatia ufumbuzi, lakini awamu zote za serikali zimekuwa zikipiga danadana.
Wakati huohuo, katibu wa Kamati ya Kutetea Haki za Waislamu, Sheikh Ponda Issa Ponda amesema maandamano ya amani waliyopanga kuyafanya Ijumaa wiki hii, yatafanyika kama yalivyopangwa.
Sheikh Ponda alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na Mwananchi na kwamba maandamano hayo yataanzia Viwanja vya Mnazi Mmoja na kuhitimishwa katika viwanja vya Biafra vilivyo Kinondoni jijini Dar es Salaam.
“Hakuna kitakachotubadili msimamo wetu. Sisi tunafanya maandamano hayo ya amani kuonyesha hisia zetu na kitu gani ambacho Waislamu tunahitaji,” alisema.
Alisema pamoja na kuwapo na kauli mbalimbali za kuwataka Waislamu wawe na subira, hawatakubali kwa kuwa kauli hizo sio mpya na kwamba wameshazizoea.
“Kauli kama hizo zimekuwa zikitolewa mara kwa mara na viongozi," alisema.
Alieleza kwamba maandamano hayo yataanzia Viwanja vya Mnazi Mmoja na kupitia barabara za Bibi Titi, Morogoro na Kawawa,” alisema.
Naye Katibu wa Kamati Maalum ya Kutetea Mali za Waislamu, Sheikh Khalifa Khamis alisema maandamano hayatakuwa na maana kwa sababu suala hilo limeshazungumzwa na masheikh na serikali.
“Mimi nipo pamoja na Mufti kwa kuwataka Waislamu wawe na subira kwa kuwa hivi sasa anayesubiriwa ni Mufti kuipeleka timu yake kwa waziri wa sheria,” alisema.
“Nina uhakika mahakama hii itapatikana mapema kwa kuwa mazungumzo tumeshamaliza na kinachofuata ni utekelezaji tu,” alisema Sheikh Khamis.
Sheikh Khalifa aliwataka Waislamu kuendelea kuwa na subira kwa kuwa uanzaji wa mahakama hiyo unaweza kuwa kwa awamu na kutoa mfano kwamba inaweza ikaanza Dar es Salaam ama wilaya ya Ilala na mikoa mingine ikafuata.
Alipotafutwa na Mwananchi, Waziri Chikawe alikataa kuzungumza kwa njia ya simu akidai hana uhakika kama anayezungumza naye ni mwandishi kweli wa gazeti hili.
“Nitajuaje kama wewe ni mwandishi, nitajuaje,” alihoji Waziri Chikawe na kuongeza: “Come to my office (njoo ofisini kwangu),” alijibu na kukata simu.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi, ambaye imedaiwa kuwa alikuwemo kwenye kikao hicho, alisema: “Muulize aliyewaita masheikh hao mimi sijawaita.”
Source: Mwananchi
Askofu adai mafisadi wanauhofia waraka wa Kanisa Katoliki
ASKOFU msaidizi wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Methodius Kilaini amesema mafisadi wanauhofia mwongozo uliotolewa na kanisa hilo ambao unaweka vipaumbele vya nchi katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, ndiyo maana wanaupinga.Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya misa ya upadrisho iliyofanyika jana kwenye Kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es Salaam, Kilaini alisema mwongozo huo ulianza kutumika tangu uchaguzi wa mwaka 1995 na kusisitiza kuwa kwa mwaka huu watu wengi wameshtuka kutokana na masuala ya ufisadi.
Kanisa hilo lilitoa vitabu viwili vya mwongozo na vipaumbele vya nchi kabla ya kuuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, mwongozo ambao umekumbana na vipingamizi kutoka kwa baadhi ya wanasiasa kwa madai kuwa dini inaingilia mambo ya siasa.
“Kwanza napenda watu waelewe kuwa mwongozo hauna lolote kuhusu dini kama watu wanavyodhani, kwa sasa jamii imeshtuka kuhusu vitendo vya rushwa na ndiyo sababu baadhi ya wanasiasa wanapinga mwongozo huo kwa kuwa unalenga kuwafungua watu macho na kukemea vitendo vya ufisadi,” alisema Kilaini.
“Ninachowataka wanasiasa wote washiriki ni kupiga vita ufisadi. Asiyetaka kupigana na ufisadi tusimchague, na ndivyo mwongozo huo unavyosema,” alisema.
Alifafanua kuwa mwongozo huo unazungumzia juu ya serikali na msimamo wake na wala si kumchagua mtu fulani wala chama fulani kwa ajili ya kumpa uongozi.
Alisema kama kutakuwa na kiongozi wa dini au mtu yeyote wa dini atakayezungumzia masuala ya kumchagua mtu ama chama fulani cha siasa, atakuwa amepotoka na kwamba huo ndio msimamo uliomo kwenye mwongozo huo.
“Watu wausome mwongozo huo kwa moyo mweupe na ninaamini wataufurahia, utakuza ufahamu juu ya masuala ya kidemokrasia,” alisema Kilaini.
Kauli ya Kilaini imetolewa wakati ambapo baadhi ya wabunge wamejitokeza kuitahadharisha serikali kuhusu mwongozo huo kwenye mkutano unaoendelea wa Bunge la Muungano, wakidai kuwa ukiachwa nchi inaweza kuingia kwenye matatizo ya udini.
Mbunge wa Kigoma Kusini, Manju Msambya aliushutumu mwongozo huo aliouita kuwa ni "waraka wa Kiaskofu" wakati akichangia hotuba ya makadirio na matumizi ya Wizara ya Sheria na Katiba, akisema unawafundisha waumini wake kuhusu namna ya kuchagua viongozi kwa imani zao na kuonya kuwa nchi inaweza kuingia kwenye vurugu.
Msambya ambaye hakutaja moja kwa moja dhehebu la dini lililotoa waraka huo, alisema unapingana na kanuni kwamba watu wasichanganye dini na siasa.
Akizungumza kwa jazba, Msambya, ambaye katika mchango wake alitaka tamko la serikali kuhusu sababu za nchi kutojiunga na Jumuiya ya Nchi za Kiislamu (OIC) na kutoundwa kwa Mahakama ya Kadhi, alisema alichukizwa na kitendo cha waziri ambaye hakumtaja jina, kwamba alipoulizwa na waandishi wa habari kuhusiana na waraka huo, aliusifu akisema ni mzuri kwa sababu ni moja ya elimu ya kupiga kura.
Lakini Askofu Kilaini alisema mwongozo huo haukutungwa na maaskofu wala mapadri wa kanisa hilo na kufafanua kuwa umetungwa na Chama cha Wataalamu wa Kanisa Katoliki (CPT) na kwamba wao waliupa baraka zote baada ya kuusoma na kuona unafaa.
Kabla ya kuongea na waandishi wa habari, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo aliwapa daraja la upadri, mashemasi watatu.
Mashemasi hao ni pamoja na Joseph Mkonde, Joseph Mapunda ambao watakuwa mapadri wa jimbo, huku Hendrick Mambwe akienda kulitumikia kanisa hilo nchini Ethiopia.
Thursday, July 2, 2009
Exclusive Interview of Pastor Chris Oyakhilomme about Prophet T.B Joshua
The humility and success of the founder of Christ Embassy is simply phenomenal. In a few years, the ministry has grown from a campus fellowship of a few hundreds to an international ministry making world-wide impact. And in nearly every country of the world, the gospel according to Pastor Chris is spreading fast. Oyakhilome talks about Jesus and the Holy Spirit as though they live together. Handsome and debonair, he delivers the message of the one he said sent him with a passion. In Nigeria his name has become synonymous with miracle healing. And when he talks about prosperity, he really is unapologetic. Hear him “I will never be broke in my life”. Since the debut of its TV programme in 1996, the ministry has remained on the cutting edge, pioneering new ways of doing things in the industry, that has become the envy of long established television stations. It has the largest Christian television network in Africa, and with its recently launched satellite station is reaching out to about a quarter of the world's population. Aside miracle healing, Oyakhilome is also many things to different people. To some, he is controversial and to others, he is mysterious. And the man of God doesn't help matters as he has consistently refused to grant press interviews. He would rather talk about the Christ he seeks to introduce than Pastor Chris. Last week, National Standard in line with our avowed commitment to letting you hear from notable Nigerians got Pastor Chris to talk. He spoke with Editor-in-Chief, Ambrose Isesele. We serve you the first of a two part series. You will be glad to read this.

I think they are doing their job the best way they know how, but I do not know what their aims and objectives are, and I have a vision that is unique.The Pentecostal Fellowship of Nigeria has its beliefs. I am not a Pentecostal and therefore don't have to be a part of it. It's like they are not Baptists, else, why did they not join the Baptist Fellowship of Nigeria? Why? We all believe in Jesus; why did they not join the Baptist? Because of their beliefs! So they feel they are different from the Baptists and there is nothing wrong with that. I think it depends on beliefs. I do not believe everything from the Pentecostal stand point, because there is nothing Pentecostal in Christianity.
Wanaotumia dawa za kukuza matiti,matako hatarini kupata saratani
Mkaguzi wa dawa vipodozi na vifaa vya tiba wa TFDA Kissa Mwamwita alisema kumekuwa na wimbi kubwa la wanawake wanaotumia vipodozi hivyo ambavyo havijasajiliwa na mamlaka hiyo.
Akizungumza na mwandishi wa habari hii, Mwamwita alisema vipodozi hivyo vimekuwa vikiingizwa nchini na kuuzwa kwa kificho huku ikidaiwa kuwa wateja wake wakubwa ni wanafunzi wa sekondari na wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu.
Mwamwita aliwataka wanawake wanaotumia vipodozi kuwa makini wakati wanaponunua vipodozi kwa kuangalia kama vimesajiliwa kwani vipo vipodozi vinavyouzwa kwa kificho.
“Matumizi ya vipodozi hivyo vinavyoongeza ukubwa wa makalio na matiti ni hatari kwa afya na pia yanawaweka katika hatari ya kupata magonjwa ya saratani,” alisema Mwamwita.
Alisema watumiaji wa vipodozi wanatakiwa kuwa makini wanapotaka kununua bidhaa hizo ili kuepuka kununua vipodozi vyenye viambata vya sumu.
Hata hivyo TFDA imetoa tahadhari kwa wananchi wanaoendelea kutumia vipodozi vyenye viambata vya sumu zikiwemo ‘losheni’ kuacha kutumia kwa kuwa kiafya vina madhara makubwa.
Mwamwita alitaja baadhi ya vipodozi vyenye viambata kuwa ni Chloqinone,Chloroform na Mercury Compound.
Source: Mwananchi
Mahakama ya Kadhi yakoroga Waislamu, Wanasiasa
Wadau mbalimbali kutoka taasisi za kidini, wanasiasa na wasomi waliambia gazeti hili jana kwamba, uamuzi huo wa serikali unakwenda kinyume na kilichomo katika ilani ya uchaguzi ya CCM ambayo ina kipengele kinachoruhusu kuanzishwa kwa mahakama hiyo.
Juzi Waziri wa Sheria na Katiba, Mathia Chikawe aliliambia Bunge Tanzania haitaunda Mahakama ya Kadhi badala yake sheria za Kiislamu zitaingizwa katika sheria za nchi ili zitumike katika mahakama ya kawaida.
Katibu wa Kamati ya Kutetea Mali za Waislamu Tanzania, Sheikh Khalifa Khamisi alisema kamati hiyo inatarajia kupinga hatua ya serikali kufuta ombi la kuanzishwa Mahakama ya Kadhi na kutoa tamko lake rasmi Jumapili hii.
Sheikh Khamisi aliliambia gazeti hili jana kuwa, hoja ya serikali kwamba yenyewe haina dini ndiyo maana imeamua kupinga hatua hiyo, siyo sahihi.
"Serikali imesema kuwa haina dini, kwa nini basi iwazuie Waislamu kuanzisha mahakama ambayo wanaitambua kwa mujibu wa imani ya dini yao?"alihoji Sheikh Khamisi na kuongeza:
"Tena mambo haya wanafanyiwa Waislamu tu na sio dini nyingine hasa baada ya maaskofu kutishia kujitoa katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya kufutiwa misamaha ya kodi," alisema Khamisi.
Alisema kamati yake inaipinga vikali kauli hiyo ya serikali iliyotolewa juzi bungeni na Waziri wa Sheria wakati akiwasilisha makadirio na matumizi ya wizara yake kwa mwaka 2009/10.
"Serikali inawaogopa sana maaskofu na kuwadidimiza Waislamu hata pale wanapokuwa na haki sawa na wengine na imekuwa ikiwapuuza na kuwasahau," alisema.
Alidai kuwa wameziona taasisi kadhaa za dini ya kikristo zikifanyabiashara kwa kivuli cha kutoa huduma za kiroho, lakini serikali imekaa kimya tena.
“ Tena baadhi ya makanisa yanafanya mambo kinyume na taratibu za nchi, serikali imeshindwa kuyakemea, lakini wanaliona hili la Waislamu ambao wanyonge kuwa halifai," alisema Sheikh.
Alisisitiza kuwa suala la kuwapo kwa Mahakama ya Kadhi ni haki ya Waislamu kama ilivyo katika nchi nyingine ambazo wamepewa uhuru kamili wa kuabudu wanachoamini.
Nalo Baraza kuu la Waislamu Tanzania, (Bakwata) limesema litatoa tamko rasmi kuhusu kauli ya serikali kufuta mpango wa kurudisha mahakama hiyo.
Katibu Mkuu wa Bakwata, Sheikh Suleiman Lolila aliliambia gazeti hili ofisini kwake Kinondoni jijini Dar es Salaam jana kwamba, tamko hilo litatolewa baada ya Mufti Mkuu, Sheikh Issa bin Shaaban Simba kukutana na baraza la Masheikh, ili kujadili suala hilo.
“Tamko rasmi la Bakwata kuhusu kufutwa kwa mpango wa kurudisha Mahakama ya Kadhi litatolewa na Mufti kesho (leo) saa nne asubuhi baada ya kukutana na Baraza la Masheikh,” alisema Sheikh Lolila.
Sheikh Lolila alisema kuwa, Baraza la Masheikh wa mkoa wa Lindi limemteua, Sheikh Mohammed Said Mushangani kuwa kaimu Sheikh wa Mkoa wa Lindi ili kuziba pengo la Marehemu Sheikh Gorogosi aliyefariki kwa ajali ya gari hivi karibuni mkoani humo.
Kwa mujibu wa Sheikh Lolila, Sheikh Mushangani atashika wadhifa huo hadi uchaguzi utakapokamilika mwezi Agosti.
“Kwa sasa tuko kwenye uchaguzi ambao utakamilika mwezi Agosti, hapo ndipo Lindi watakuwa na Sheikh wao rasmi,” alisema Lolila.
Wakati huo huo aliyekuwa Mwenyekiti wa Bakwata, Sheikh Khamis Mataka alisema kauli ya serikali kuizima hoja ya Mahakama ya Kadhi ina mapungufu mengi na kwamba, wanaisubiri katika mkutano ambao iliahidi kukutana na viongozi wa dini ya kiislamu kujadiliana kuhusu jambo hilo.
"Tunafanya busara sana kuisubiri serikali kwa kuwa imeahidi kukutana na viongozi wa dini ya kiislamu. Ndipo sisi wanazuoni tutakapotoa hoja zetu na kuweka wazi mapungufu ya maamuzi hayo ya kuifuta mahakama,"alisema.
Naye Katibu Mkuu wa Baraza Kuu, Jumuiya na Taasisi zote za Kiislamu Tanzania, Ramadhani Sanze alisema wameisikia kauli hiyo ya serikali kupitia kwa waziri wake ya Sheria na katiba, Mathias Chikawe.
Alifahamisha kuwa masheikh wanafanya mkutano wa siku mbili kujadili suala hilo na kwamba, watatoa tamko lao Ijumaa wiki hii.
Alisema hawana haja ya kuyafanya mambo hayo kuwa marefu, isipokuwa serikali itaona ni nini Waislamu wanahitaji kifanyike kwa mujibu wa imani ya dini yao na kuridhika nacho.
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba alimtaka Rais Jakaya Kikwete kuwaomba radhi Watanzania kutokana na kutotekeleza moja ya vipengele vya Ilani ya CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, ambayo inaeleza kuwa itaruhusu kuwepo na Mahakama ya Kadhi nchini.
Profesa Lipumba aliliambia gazeti hili jana kuwa moja ya vipengele katika Ilani ya CCM ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, ilikuwa ni pamoja na kuruhusu kuwepo kwa mahakama hiyo; hivyo kitendo cha serikali kushindwa kutekeleza ahadi hiyo, rais Kikwete anatakiwa awajibike kwa kuwaomba radhi Watanzania waliompigia kura.
"Ni jambo ambalo lipo wazi kabisa, kwa sababu ilani ya uchaguzi inajadiliwa na kupitishwa na chama, hivyo kutokana na hili serikali imeonyesha ni jinsi gani ilivyowadanganya Watanzania. Huu ni 'usanii' kabisa wanaonyesha kuwa hawako makini katika masuala mazito kama hili," alisema Lipumba na kuongeza:
"Wananchi humchagua mtu kutokana na sera zake, hivyo wapo watu walioichagua CCM kwa sababu tu katika kampeni zao walisema watatekeleza suala la Mahakama ya Kadhi".
Katika hotuba yake juzi Chikawe alisema mchakato wa kufikia hatua ya kuzijumuisha sheria hizo za Kiislamu kwenye sheria za nchi lazima upate maoni kutoka kwa madhehebu yote ya Kiislamu nchini.
Naye Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Samwel Ruhuza alilieleza gazeti hili jana kuwa Ilani ya CCM katika uchaguzi wa mwaka 2005, ilisema itashughulikia kuwepo kwa Mahakama ya Kadhi kama moja ya ajenda kubwa za kuwashawishi wapiga kura.
"Hoja hii ilitumiwa na CCM mwaka 2005 na iliungwa mkono na mmoja wa maaskofu wa Kanisa Katoliki ambaye alitamka kuwa Rais Kikwete ni chaguo la Mungu, hivyo watu wengi walimchagua" alisema Ruhuza na kuongeza:
"Siyo kwamba tunalazimisha kuwepo kwa Kadhi Mkuu, lakini kama suala la Mahakama ya Kadhi lilitumiwa katika ilani ya uchaguzi, basi litekelezwe".
Hoja ya kuwepo kwa mahakama ya kadhi ilianzishwa wakati wa serikali ya awamu ya tatu lakini ilizimwa, baada ya miaka mitatu iliyopita sakata hilo lilifufuliwa tena na kuwagawa wanasiasa na wananchi katika makundi mawili (wanaounga mkono na wanaopinga).
Wako waliounga mkono na wengine waliipinga kwa maelezo kwamba itasababisha vurugu na mgawanyiko katika jamii.
Source: Mwananchi
Wednesday, July 1, 2009
Waraka wa Kanisa, Uchaguzi wahojiwa
Source: Habari leo
Mahakama ya Kadhi yayeyuka
source: habari leo
CCM wafanya mkutano kanisani, wampiga kiongozi wa kigango
Tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 3:00 asubuhi wakati wafuasi hao wa wanawake wa CCM, wakiongozwa na mtu mmoja aliyejulikana kwa jina moja la John, walipoingia kanisani humo kwa madhumuni ya kuchukua viti kwa ajili ya mkutano wao. Badala ya kuchukua viti, waliamua kutotoka na kufanyia mkutano huo kanisani.
Akizungunza na Mwananchi katekista wa kigango hicho ambacho kipo katika parokia ya Kaniha, jimbo la Kahama, Faustine Damas alisema wafuasi hao wa CCM waliingia kanisani na kuchukua meza ya kuendeshea ibada na kuigeuza kuwa meza ya wageni wao na baadaye kuendesha mkutano wao.
Alieleza kuwa alipofika kanisani alistaajabu kusikia nyimbo wa 'Tieni, tieni' ukiimbwa na baada ya kuingia ndani alikuta wakiwa wanaendelea na mkutano wao huku wakitumia meza kuu ya ibada, jambo ambalo lilimfanya ampigie simu katibu wa kigango hicho, Festus Masumbuko ambaye baada ya kuwaomba waondoke na kuwanyang'anya meza hiyo ya ibada, wafuasi hao wa CCM walianza kumpiga.
"Waliamua kugoma kuondoka na ndipo alipowanyang'anya meza ya ibada, lakini wakamvamia na kumpiga mateke na ngumi. Wamemjeruhi vibaya na pia wamemchania shati," alieleza katekista huyo.
Alisema kutokana na hali hiyo alilazimika kupiga kelele na ndipo wananchi walipofika na kumwokoa. Lakini wakati hali hiyo ikiendelea, mfuasi mmoja wa CCM alipiga simu polisi na kuwaeleza kuwa walikuwa wakifanyiwa vurugu na ndipo polisi walipoenda eneo hilo na kuwakamata wananchi waliokuwa wanataka kumuokoa katibu.
Wananchi hao wanashikiliwa na polisi kwa kufanya vurugu katika mkutano huku wana CCM wakiachiwa huru na kuondoka zao.
Kutokana na hali hiyo paroko wa parokia ya Kaniha, Padri Isaya Bahati ambaye pia ni msaidizi wa askofu wa jimbo la Kahama, alisema muda mfupi baadaye akiwa polisi kuwa amesikitishwa na vurugu hizo na kusisitiza kuwa kanisa kama nyumba ya ibada inapaswa kuheshimika kwa vile si uwanja wala ukumbi wa mikutano.
Alipoulizwa kuhusu suala hilo, naibu katibu mkuu wa CCM, George Mkuchika alisema hana taarifa ya vurugu za wafuasi wake kanisani na kwamba kwa kuwa amepokea taarifa hizo, atazifuatilia kwa kina.
“Ngoja nifuatilie kwa kina kujua ni nini kimetokea,” alieleza Mkuchika.
Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera Henry Salewi alisema kuwa hakuwa kwenye eneo la uchaguzi na kumtaka mwandishi awasiliane na kamishina Telesphol Anaclet ambaye ndiye amekuwa akishughulikia masuala hayo. Hata hivyo, kamishna huyo alisema jeshi la polisi linaendelea na masuala yake hivyo lipewe nafasi ya kufanya kazi.
“Naomba mtuache tufanye kazi yetu sina cha kukueleza kwa sasa,” alisema kamishina huyo wa oparesheni maalumu ya uchaguzi na akakata simu.
Waliokamatwa na jeshi hilo la polisi wametajwa kuwa ni Evarist Dotto, Semen Elias, Mosha Makoye, Batista na Timetheo ambao walitambulika kwa jina moja
source: mwananchi
Saturday, June 20, 2009
E-Club
Usikose hapa hapa sayuni..inakuja kuleta mapinduzi ya kifikra mapema iwezekanavyo
Thursday, June 11, 2009
Kongamano la Wajasiliamali lafana sana
Kongoma kubwa la wajasiliamali lililoandaliwa na kampuni inayokua kwa kasi sana hapa nchini ya DigitalBrain lilifana sana siku ya jumamosi tarehe 6/6/2009.
Akizungumza katika kongamano hilo mgeni rasmi ambaye ni mbunge wa Mbinga mashariki -CCM Mheshimiwa Gaudency Kayombo, alisema kuwa amefurahishwa sana na hatua iliyochukuliwa na DigitalBrain ya kuwaleta wajasiliamali kwa pamoja na kuwafundisha masomo hayo ambayo yanalenga katika kuwakomboa watanzania na wimbi la umaskini.Friday, May 22, 2009
Obama akutana na Rais Jakaya KIkwete
SEMINA YA UJASILIAMALI NCHINI
Semina hiyo ambayo itakuwa ni ya siku moja kuanzia saa 2 asubuhi hadi saa 12 jioni itakuwa na lengo la kuwainua wajasiliamali wadogo na wale ambao badi hawajaanza ujasiliamali na wanataka kuingia kwenye ujasiliamali.
Kutakuwa na waalimu mbalimbali ambao ni wajasiliamali kwa vitendo.Kitu cha tofauti katika semina hiyo ni kwamba baadhi ya walimu wake ni watu wasio na elimu kubwa ya darasani lakini wanaelimu kubwa na uzoefu mkubwa wa jinsi ya kufanya ujasiliamali.Ni watu waliofanikiwa sana sana katika biashara na watashiriana na wewe utakaye hudhuria matamu na mahcungu ya ujasiliamali.
Kiingilio katika semina hiyo ni TSh. 20,000/- tu na formu za kujiunga zinapatikana katika ofisi za DigitalBrain pale Samora Avenue, Kelvin House, 2nd Floor, (jirani na ilipokuwa salamander -opposite na duka la simu la sapna).
Unaweza kusikiliza baadhi ya matangazo ya semina hiyo live kutoka WAPO Radio FM kwa kutembelea tovuti ya DigitalBrain ambayo ni www.digitalbraintz.com .
Kwa maelezo zaidi wasiliana na DigitalBrain kwa namba hii 0713-427857 au +255-713-427857 au email info@digitalbraintz.com
DigitalBrain---By the renewing of your mind...
Saturday, May 9, 2009
Waziri Mkuu wa Kenya-Raila Odinga abatizwa
Pastor David Owuor comes across as one of the more colourful and esoteric voices in Kenya’s growing legion of fire-and-brimstone evangelical preachers.His long dreadlocked beard lends him instant recognition, but there can be nothing that more vividly marks his acceptance into the mainstream than his new standing as the preacher who baptised Prime Minister Raila Odinga.
Having made a career out of constant predictions of earthquakes, Pastor Owuor now has the keys to the corridors of power where his prescriptions to avert doomsday might find sympathetic ears.
Repentance day
Indeed soon after immersing Mr Odinga in water, the preacher announced he would be convening a meeting between himself, the PM and President Kibaki to plan a national day of repentance.
Mr Odinga concurred: “Very soon, the President and I are going to announce the specific date on national repentance in which I will ask all people to observe a day of repentance in seeking God’s intervention and direction,” he said.
It would indeed be a major feat if Pastor Owuor becomes the main preacher on such an occasion, usually the preserve of the Catholic, Anglican, Islamic, Presbyterian and other mainstream denominations.

Pastor Owuor first came to the limelight with his October 2005 predictions of an earthquake that would bring down Nairobi’s tallest buildings. It did not come to pass.
Still, the pastor has not been discouraged from regular prophesies. He also has not been shy to seize upon events, like the earth tremors in 2007, as proof that his prophecies are accurate.
On Monday evening, Pastor Owuor dipped the PM into the water of a swimming pool at a residence on Riverside Drive, Nairobi, and was catapulted to the national limelight.
His future predictions will not be so easy to dismiss henceforth, if he is seen to have the devoted followers amongst the high and mighty.
Followers of his Holiness and Repentance Ministries began trooping into the home at around 11am.

The women wore long dresses and scarves that covered the hair. In the crowd were a few Asian women in saris. The men were in suits and ties and soon, the choir began belting out Gospel tunes as a pianist ran his fingers over an electronic keyboard.
The baptism ceremony was set to begin at 2pm. A tent was set up behind the house, just next to the pool, and decorated with blue and white ribbons and balloons. The pool was a glittering clean, and the breeze formed ripples on the water.
After sodas and cakes, the congregation settled to wait for the PM as journalists began to arrive. It turned out to be a long wait and a few hours later, at 5.35pm, the PM’s motorcade entered the compound.
The ceremony was fulfilment of a promise more than a month earlier, on March 28, when the PM showed up at one of Pastor Owuor’s huge rallies in Nakuru and declared that he was born-again.
On arrival, Mr Odinga greeted the congregation and then went into a private meeting with Pastor Owuor, to emerge having changed from the dark business suit he wore earlier at his meeting with President Kibaki, into a spotless white ankle-length tunic ready for baptism.
Prayers and sermons and a reading from the book of Matthew on the baptism of Jesus Christ by John at the River Jordan followed.
Monday, May 4, 2009
Azimia baada ya kusikia kishindo cha nyundo-Mbagala
MKAZI wa Mbagala Kuu, Grace Songo jana alianguka chini ghafla na kupoteza fahamu baada ya kusikia kishindo cha nyundo kilichofanana na mlipuko wa mabomu.
Songo alipoteza fahamu baada ya kusikia kishindo cha nyundo wakati mmoja wa waathirika wa mabomu hayo alipokuwa akifanya marekebisho ya nyumba ili apate sehemu ya kuwahifadhi watoto wake baada ya kukosa msaada wa mahema tangu alipokumbwa na maafa hayo.
Hata hivyo saa tatu baadaye Mwananchi ilimfuata mama huyo nyumbani kwake na kuzungumza naye baada ya kupata nafuu alisema "bado tumekumbwa na wasiwasi hasa ukizingatia kwamba wakati mlipuko wa mabomu unatokea nilikuwa hapa nyumbani na nyumba yangu pia imeathirika."
Alisema hali hiyo haimtokei yeye peke yake bali ni watu wengi wanazimia baada ya kusikia mlipuko ama kishindo chochote kinachotokea karibu na maeneo hayo.
Wasiwasi huo umezidi kuwakumba baadhi ya wakazi wa maeneo hayo ikiwa ni siku sita tangu kutokea kwa mlipuko wa mabomu katika kambi ya Jeshi la Wananchi Tanzania kikosi cha 671 na kuteketeza kaya zaidi ya 800 na watu zaidi ya 20 kupoteza maisha.
Kuhusu hali ya msaada Songo alilalamikia utaratibu unaotumika katika kugawa misaada hiyo.
"Tangu tukumbwe na janga hili hatujapata msaada wowote tunalala nje na tunashinda njaa ingawa misaada inatolewa kila siku, lakini baadhi ya watu wanaonufaika si waathirika halisi wa tukio hili,”alisema Songo.
Hata hivyo Mwananchi pia ilishuhudia baadhi ya waathirika wanaoishi mbele ya kituo cha kugawa msaada wakimlalamikia msimamizi wa chama cha msalaba mwekundu, Stella Marealle pamoja na Afisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Temeke na mwenyekiti wa ugawaji wa misaada John Bwana kuwa hajapata msaada wowote huku akilala nje na watoto wake.
Mmoja wa waathirika Daniel Kisa ambaye nyumba yake imeharibiwa na mabomu hayo alisema kuwa "tangu nyumba yangu iharibiwe na mabomu ninaishi kwa wasiwasi mkubwa wa bomu kuwepo eneo hili hasa baada ya askari wa JWTZ kuchimbua bomu ambalo halijalipuka nyuma ya nyumba yangu hii inazidi kunipa wasiwasi."
Source: Mwananchi
Tamasha la kuwachangia walemavu wa ngozi lafana Dar es Salaam








Mlima Sayuni unaungana na serikali yetu katika kulaani vikali mauaji ya maalbino hapa nchini na popote pake duniani.