Thursday, August 13, 2009

Kingunge atangaza upya vita na Katoliki

MWANASIASA Mkongwe nchini Kingunge Ngombale Mwiru, ameendelea kuung'ang'ania waraka wa Kanisa Katoliki na sasa amelitaka kanisa hilo limwombe radhi kwa kumwita fisadi alipoupinga bungeni.
Waraka huo uliotolewa Machi mwaka huu, ulilenga kuwapa mwongozo waumini wa Kanisa Katoliki wa namna ya kushiriki Uchaguzi Mkuu ujao, vipaumbele vya kitaifa na aina ya kiongozi anayefaa kuchaguliwa.
Akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake jijini Dar es Salaam jana, Kingunge alisema alishangaa kusikia kanisa hilo likisema wanaohofia waraka huo ni mafisadi baada ya yeye (Kingunge) kutoa angalizo bungeni katika Mkutano wa 16 uliomalizika Julai 31 mwaka huu.
"Maaskofu wamenisikitisha sana katika hili. Hatuwezi tukakubali nchi ikapelekwa wanavyotaka wao, tunaomba waache," alisema Kingunge na kuongeza:
"Nashangaa, askofu mzima akazungumza na kuniita fisadi, hiyo ni dhambi. Askofu huyo akaungame. Mimi sipendi neno fisadi ni afadhali kama rushwa iitwe rushwa".
Hata hivyo, Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Method Kilaini jana alikataa kujibu kauli hiyo ya Kingunge akisema hataki kulumbana na mkongwe huyo wa siasa.
"Sitaki kulumbana naye, mzee wa watu ni mzee wa watu tu, hivyo sitaki kuendeleza malumbano naye,"alisema Kilaini.
Kwa mujibu wa Kingunge, viongozi wa Kanisa Katoliki wamemkejeli na kumtukana kuwa hajasoma kwani anaamini kwamba aliusoma waraka huo vizuri na kuulewa kwa kina kabla hajatoa kauli hiyo.
'Niliusoma vizuri na kuelewa. Hivi nitashindwa kuelewa walichoandika, nimesoma maandiko ya dini ya Kiislam, Kihindu na nyingine, siwezi kushindwa kusoma na kuelewa waraka huu." alisema Kingunge juzi alipokuwa akihojiwa na kituo cha Channel 10 na kuongeza:
"Sikutaka kuingia katika maudhui, maana nikiingia katika maudhui ningelumbana nao kwamba dini inakuaje na ilani, ilani inapaswa kuandaliwa na vyama vya siasa tu na si vinginevyo," alisisitiza.
Kingunge alisema ni vizuri kanisa likaelewa kuwa lenyewe sio chama cha siasa na kwamba, halina uwezo wa kuandaa ilani ya uchaguzi.
Alifafanua kwamba, wakati anazungumzia waraka huo bungeni hakuwa anataka uhasama na kanisa kwa kuwa anaheshimu imani, ila alikuwa akitoa angalizo kwa kuwa dini haiongozi nchi kama serikali.
"Ukiona vyaelea, jua vimeundwa" angekuwepo Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere hapa, kanisa hilo lisingethubutu kuandaa waraka huo, mimi pia ni mkongwe, hivyo hakuna yeyote ambaye anaweza kusimama na mimi kuhusu historia ya nchi hii.
Nataka niwaambie kwamba, tunajua mambo ya Kanisa Katoliki, lakini kwa bahati mbaya mwalimu hayupo,"alisema.
Kingunge aliendelea kulishambulia kanisa hilo akidai kuwa linataka kuwatoa Watanzania katika utamaduni wao na kulishauri kuunda chama cha siasa kama linaona ni vyema.
Alisisitiza kuwa dini si chombo cha kuunganisha watu, bali kuwatenganisha ndiyo maana kila mtu ana dini yake, lakini serikali ni moja, hivyo nchi yenye dini nyingi haiwezi kuunganishwa na dini bali siasa.
Katika malumbano hayo yaliyodumu kwa muda sasa, kanisa liliutetea waraka huo likisema kuwa sio mara ya kwanza kuutoa kwa waumini wake.
Lilisema huu umekuwa utaratibu wa kanisa hilo tangu mwaka 1995 ukiwa na lengo la kuwaelimisha waumini wake kuhusu namna ya kutekeleza haki yao ya kupiga kura.

Source: Mwananchi

Ubatizo wa maji mengi au maji machache?

Yohana 3:3 “Yesu akamwambia, "Amen nakwambia, mtu asipozaliwa upya hataweza kuuona ufalme wa Mungu."
Kuhusu ubatizo wa maji:
“Yesu akamjibu, "Kweli nakwambia, mtu asipozaliwa kwa maji na Roho, hawezi kamwe kuingia katika ufalme wa Mungu.” [Yohana 3:5]
Bwana Yesu asifiwe!
Ninaamini kuwa wewe unaendelea vyema na Yesu ni mwema kwako pia, ndiyo, Yesu ni mwema.
Ndugu mmoja aliniandikia na kuomba ufafanuzi kuhusu suala zima la ubatizo kwetu sisi WaKristo. Ndugu huyu ameuliza ni ubatizo upi sahihi, wa maji mengi au maji kidogo? na akauliza je, mtu anatakiwa kubatizwa akiwa mdogo au mtu mzima ajuaye mema na mabaya? Anasema ameuliza hivi kutokana na mapokeo/imani zinazohubiriwa na makanisa mbalimbali tunayosali. Na mimi nimeona nimjibu kwa njia hii ili iwe faida kwa wote. Na nitamjibu kwa kadri Roho Mtakatifu alivyonipa kuelewa na kuamini ndani yangu. Kama ujuavyo, huduma hii ya mtandaoni haifungamani na dhehebu lolote lile.
Ubatizo ni agizo la Mungu kama tusomavyo katika Biblia, kwa mfano Mathayo 28:19:"Basi enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa Jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu......" na pia mstari huo hapo juu wa Yohana 3:5.
Tunajua kuwa madhehebu mengi yamekuwa yakihubiri mengi kuhusu uwingi au uchache wa maji ya kubatizwa, lakini sijasikia waliojaribu kufikiri ni kwa nini Mungu anataka maji yatumike katika ubatizo, na isiwe kimiminika kingine chochote, na Bwana Yesu hakulizungumza hili. Lakini ninaamini kiini cha jambo hili ndio kimetajwa katika Waraka wa Kwanza wa Yohana 5:8-9 "Kwa maana wako watatu washuhudiao mbinguni, Baba, na Neno na Roho Mtakatifu na watatu hawa ni umoja. Kisha wako watatu washuhudiao duniani, Roho na maji na damu, na watatu hawa hupatana kwa habari moja....."
Hakuna mahali Biblia inapotaja tutumie kiasi gani cha maji katika ubatizo, kama tulivyoona, Biblia inasema tuu kuwa tutumie maji. Ili mradi maji yapo, mbatizaji anaweza kuamua atumie maji kiasi gani. Anaweza kubatizia baharini, ziwani, mtoni au kwa matone machache ya maji, mradi tuu maji yawepo pale kwani ni mojawapo ya washuhudiao hapa ulimwenguni.
Ubatizo wa maji kidogo ni sawa, na ubatizo wa maji mengi ni sawa (huo wingi wa hayo maji unatofautiana pia).Hivyo ndivyo tunavyotakiwa kuamini na kutokukubali kuyumbishwa na mtu yeyote pasipo ridhaa yetu.Wazungu wana msemo usemao "A man living by the river never uses spittle of water for washing", yaani mtu aishiye kando ya mto hatotumia matone ya maji kwa kuoshea, kwa sababu anayo maji mengi.Hali kadhalika,Yohana Mbatizaji angeweza kuamua kubatizia watu mtoni kwa sababu alikuwa karibu na mto Yordani. Mtu ana uchaguzi huru wa kuamua kubatizwa kwa maji kidogo au mengi kiasi gani, kama atakavyopenda yeye mwenyewe. Kwa mfano leo, tukiamua sisi tuliookoka wa Tanzania, tukajikusanya na kuamua kwenda kuhubiri injili kule Darfur, Sudan, na tukaambiwa na waandaji wa huduma hiyo kuwa kule tutakapokwenda kuhubiri injili ni jangwa tupu, hakuna maji mengi kama tulivyonayo huku kwetu, je tutafanyaje basi? Je, tutakataa kwenda kuhubiri kwa sababu kule hakuna maji mengi ya kubatizia? Je, tutaacha kufungasha Biblia katika mabegi yetu na badala yake tutabeba maji ili tukifika kule tutengeneze mto wa kubatizia? La Hasha! Ukisoma kitabu cha "A table in the presence" kilichoandikwa na Lt.Carey H. Cash, ambaye ni Mchungaji wa Jeshi la Marekani (Military Chaplain) aliyeshiriki vita ya Iraq, utaona kuna mahali ameeleza habari za Mchungaji mwanajeshi mwingine aliyekuwepo katika vita ya Vietnam, alijiwa na askari wakitaka kubatizwa kabla ya kuelekea kwenye mapambano, lakini wakati huo hakuwa na hata tone la maji, na alijua wazi kuwa kwa mazingira ya vita,baadhi ya wale askari waliotaka kubatizwa anaweza asiwaone tena baada ya pale kwani wanaweza kufa vitani, hivyo hawezi kuwaambia "Njooni baadaye",ungekuwa wewe ungefanyaje? Anasema yule mchungaji katika hali ile (kwa alivyoamini) aliamua kutumia mate yake kuwabatiza, na akawabatiza!
Ninafikiri kinachotokea katika mwili wa Kristo sasa hata watumishi wa Mungu hawashirikiani katika kuujenga mwili wa Kristo ni mbinu tuu za shetani za kutaka kututenganisha ili tusiwe na umoja Bwana aliotuombea katika Yohana 17.Nafikiri unaweza ukawa umeona namna madhehebu yalivyojitenga, kila mmoja akieleza ubaya wa dhehebu lingine badala ya kueleza ubaya wa shetani. Shetani anataka kumfanya kila Mkristo ajione kuwa bora kuliko mwenzake na tusiweze kuungana katika kumpinga ibilisi.
Kuhusu kiasi cha maji ya kubatizia kiasi chochote kinafaa, kila mtu na afanye kama apendavyo,mradi tuu maji yatumike.
Kuhusu ubatizo wa watoto au watoto wazima, ninaona pia kuwa kila watu na wafanye wapendavyo wenyewe. Wapo wanaoamini kuwa mtoto hawezi kubatizwa,na kwamba lazima mtu aokoke kwanza ndio kisha abatizwe (kwa sababu Biblia imesema kuwa "Aaminiye na kubatizwa ataokoka"), na wapo wanaoamini mtoto mchanga anaweza kubatizwa (“Yesu akamjibu, "Kweli nakwambia, mtu asipozaliwa kwa maji na Roho, hawezi kamwe kuingia katika ufalme wa Mungu.” [Yohana 3:5] -ameanza kwa maji, yaani kubatizwa na kisha kwa Roho(kuokoka)) hivyo hawa huanza kubatiza kwanza na kisha wokovu, ingawa akitokea mtu mzima katika madhehebu hayo hajabatizwa (kwa mfano mshirika mpya) hubatizwa pia.
Siyo lazima mtu awe mdogo au awe mkubwa ili abatizwe,ubatizo ni kwa yeyote yule. Ndiyo maana kuna baadhi ya watu walipata neema ya kuokoka wakiwa bado watoto wadogo sana, hadi miaka sita,je hawa wakiokoka tuwazuie kubatizwa kwa sababu ni wadogo? Hebu soma kilichotokea kwa Mtume Petro katika Matendo 10:44-48.
Ushauri wangu mimi, Ubatizo wa maji mengi ni sawa na wa maji kidogo ni sawa, mradi maji yanatumika hakuna ulio bora kuliko mwingine, pia, kubatiza watoto wadogo ni sawa, kubatiza wakubwa ni sawa,hakuna ulio bora kuliko mwingine, nami ninaamini kuwa nina Roho Mtakatifu.
Tusikubali tena shetani aendelee kututenga sisi tulio viungo katika mwili mmoja wa Kristo, ndiyo kusema, Tujenge madaraja (ya kutuunganisha) na siyo kuta (za kututenga). Na tukumbuke, siku ya mwisho watakaoingia mbinguni ni wale ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima, yaani waliookoka,na siyo waliobatizwa. Wapo waliobatizwa ambao hawataingia mbinguni kwa sababu hawajaokoka.(Kwa hivyo unajua ni wapi pa kuweka bidii kubwa)
"Mtu yeyote ambaye jina lake halikupatikana limeandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika ziwa la moto.”-Ufunuo wa Yohana 20:15.
Kwa utukufu wa Mungu,
Frank Lema
www.lema.or.tz
savedlema2@yahoo.com

Monday, August 10, 2009

Use Your Gifts To Serve Others

Use Your Gifts To Serve Others

By Eric Elder

I once belonged to a church that had 3,500 ministers! That’s a lot of ministers! But it wasn’t because they had 3,500 people on staff. It was because they considered every member a minister. They expected and encouraged every member to minister to others, to serve others, with the particular gifts that God had given them.

That was the church where I finally decided to put my faith in Christ. It wasn’t just because of the great sermons, or the powerful Sunday School lessons, which were important. It was also because of the various members who reached out to me, who invited me to Bible studies in their homes, who prayed for me, and who served me-- ministered to me--in various other ways.

When the truth of God’s love for me in Christ finally broke through to my heart and mind, I decided to devote the rest of my life to serving Him, too. That didn’t mean that I went immediately into “professional” ministry. It meant that I had now become the three- thousand, five hundred and first minister at that church, using the gifts God had given me to minister to others.

This is how the Bible describes ministry. While there are certainly specific gifts--or “graces,” as the Bible sometimes refers to them-- that are given to some to preach or teach, to prophesy or evangelize, or to oversee the workings of the church, these gifts are simply a means to an end: to equip the rest of God’s people for works of service.

Here’s how the Apostle Paul puts it in Ephesians chapter 4:

“But to each one of us grace has been given as Christ apportioned it.... It was He who gave some to be apostles, some to be prophets, some to be evangelists, and some to be pastors and teachers, to prepare God’s people for works of service, so that the body of Christ may be built up until we all reach unity in the faith and in the knowledge of the Son of God and become mature, attaining to the whole measure of the fullness of Christ” (Ephesians 4:7, 11-13).

The Apostle Peter puts it like this, in 1 Peter chapter 4:

“Each one should use whatever gift he has received to serve others, faithfully administering God’s grace in its various forms. If anyone speaks, he should do it as one speaking the very words of God. If anyone serves, he should do it with the strength God provides, so that in all things God may be praised through Jesus Christ” (1 Peter 4:10-11a).

When I first put my faith in Christ and received the gift of eternal life, I was surprised to find out that God still had more gifts to give me! I thought eternal life was enough! But it wasn’t enough for God. He still had more He wanted to do in and through me, so He poured other gifts into my life, gifts that were not just for me, but to equip me to serve others.

If you’ve already received the gift of eternal life by putting your faith in Christ, God still has more He wants to do in and through you, too.

For some of you, God has called you, gifted you, and equipped you with the ability to teach, preach, evangelize, prophesy and oversee His work here on the earth. If so, God wants you--He needs you--to use those gifts to equip others, “to prepare God’s people for works of service.”

For some of you, God has called you, gifted you, and equipped you with gifts of faith, mercy, encouragement, serving, giving, leadership, administration--and the list goes on and on (just read Paul’s letters to the Corinthians, chapters 12 and 13, or to the Romans, chapter 12, for more about spiritual gifts and how to use them). But all gifts are given for the same reason, “so that the body of Christ may be built up until we all reach unity in the faith and in the knowledge of the Son of God and become mature, attaining to the whole measure of the fullness of Christ.”

Your church doesn’t have just one minister, or two, or ten or twenty. Every member is a minister, when you use your gifts to serve others.

Let’s pray...

Father, thank You for giving me the gift of eternal life, and thank You for going further and giving me even more gifts beyond that! Help me to think of ways today to use the gifts You’ve given me to serve others. Help me to not neglect those gifts, but to put them into practice so they can grow better and stronger, not only for my sake, but for those You want to touch through me. In Jesus’ name, Amen.

A breakthrough requires a trial to break through.

A breakthrough requires a trial to break through.

It would be nice to simply wake up one day and suddenly be a mature Christian, but in order to grow up in God, we will have to go through trials. There is no other way to grow strong spiritually than to go through trials.

1 Peter 5:10 says, And the God of all grace, who called you to his eternal glory in Christ, after you have suffered a little while, will himself restore you and make you strong, firm and steadfast. You may not like trials, but this verse says that when you are going through trials after you have suffered a little while, you will grow to be firmly rooted and grounded (strong, firm and steadfast) in God.

Similarly, James 1:12 says, Blessed is the man who perseveres under trial, because when he has stood the test, he will receive the crown of life that God has promised to those who love him. Here again, you don't get the rewards (the crown of life) until you have persevered under trial and stood the test.

So, learn to be thankful in your trials, because in order to get your breakthrough, you need a trial to break through.

Therefore, don't be discouraged during times of suffering. Know that after you have suffered a little while, God himself will make you strong firm and steadfast.

Pray for persecuter Christians..

And pray in the Spirit on all occasions with all kinds of prayers and requests. With this in mind, be alert and always keep on praying for all the saints. - Ephesians 6:18

VOM-USA Prayer Update for August 7, 2009

PAKISTAN – Muslim Mob Attacks Christians – VOM Sources

On July 30, Muslim extremists attacked Christians, burning more than 50 homes and animals in Faisalabad, Pakistan, according to The Voice of the Martyrs contacts. Muslims falsely accused Christians of burning the Quran during a wedding ceremony the previous day. Muslim extremists claimed they attacked believers because police did not arrest anyone for their complaints about a burned Quran. This is the fifth incident of persecution against Christians in two months. Muslims are threatening more attacks. Pray for believers who have lost their homes and livestock. Ask God to provide for and encourage them. Pray false accusations by Muslims will draw believers closer to the Lord and for their faithfulness to draw non believers into faith with Christ.

Psalm 91

ERITREA- Christian Dies in Prison – Compass Direct News

On July 23, Yemane Kahasay Andom, a Christian imprisoned for his faith in Eritrea died after authorities denied him medical treatment, according to Compass Direct News. Yemane is the third Christian to die in prison this year. He died at Mitire Confinement Center from complications with malaria and was reportedly tortured while in prison. It is believed his body was secretly buried at the camp. According to Compass Direct, two weeks prior to his death, Yemane was allegedly weakened by continuous physical torture and solitary confinement because he refused to sign a recantation form. Though Compass reports it is not clear what was written on the recantation form, most Christians interpret the signing of such a form as the denouncement of their faith in Christ. Pray for the Andom family and believers in Eritrea. Ask God to comfort others who have lost loved ones. Pray that Eritrean Christians will continue to follow Christ's example of faithfulness, even at great cost. Pray that Eritrea's leaders will repent and come to faith in Christ.

Romans 8:34-36

CHINA – Youth Camp Raided – China Aid Association

On July 23, Public Security Bureau (PSB) and Religious Affairs Bureau (RAF) officials raided a Christian youth camp in Nanyang city, Henan province. PSB and RAF officers took away all 20 students attending the camp for further investigation . The students, each under 18 years old, were released to their families that afternoon. Two instructors, 40 year-old Cheng Ping, and 30 year-old Miao Miao, were arrested and sent to the Yongan Lu Detention Center in Nanyang city. They were reportedly sentenced to administrative detention. The lengths of their sentences are unknown. Officials told church leaders who organized the camp not to speak publicly about the case. Pray the young people who had this strenuous experience remain faithful to Christ. Pray for their instructors who remain in prison. Pray believers in China will continue trusting God despite increased persecution.

2 Corinthians 12:9-11

Please pray.

God bless you,
Sayuni.

Tuesday, July 21, 2009

Kadhi ni nani?

Ndg mpendwa.

Wakristo tunayo HAKI ya kushiriki kyk kutazama mahakama ya kadhi kabla ya kuiruhusu/kukubali itumike ktk kutoa hukumu hapa nchini Tanzania.
Hii ni kwa sababu itakapoanza kutoa hukumu hapa nchini haitakuwa juu ya waislamu tu bali hata kwa wengine kwa sababu za kizazi.Hii ni kwa maana wapo wapo wakristo waliooa na kuzaa na waislamu pia wapo waislamu waliooa na kuzaa na wakristo hivyo hukumu kupitia vitabu vya dini ya kiislamu haigusi waislamu tu bali hat jamii ya wakristo.
Ni vema tuanze kwa kumtazama huyu mtu aitwae KADHI je ni nani na anabeba sifa zipi ili tuwe huru kumpa madaraka ya kuhukumu.
BIBLIA;LUKA 18;2-6
(Akasema palikuwa na KADHI katika mji fulani hamchi Mungu wala hajali watu.Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane aliyekuwa akimwendea endea akisema.Nipatie HAKI na adui wangu Nae kwa muda alikataahalafu akasema japokuwa simchi Mungu wala sijali watu lakini kwa kuwa mjane huyu ananiudhi nitampatia haki yake asije akanichosha kwa kunijiadaima.Bwana akasema sikilizeni anayosema yule KADHI dhalimu).
Katika neno hilo tunazipata sifa kuu nne za KADHI nazo ni


1HAMCHI MUNGU.
2.HAJALI WATU.
3HUTOA HAKI PALE ANAPOSUMBULIWA.
4.NI DHALIMU.

Ikiwa kama ameshindwa kumpa HAKI yake mjane ambaye ana HAKI YA KUSAIDIWA, Je ataweza kutoa HAKI ya HUKUMU ya KWELI hapa TANZANIA?

HAPANA KWA SABABU HANA SIFA ZINAZOSTAHILI.

swala jingine la kujifunza ni kuwa waislamu wanalalamika kuwa serikali imewanyima HAKI YA KUABUDU(majira 7/7/2009. je ni haki gani hiyo ya kuabudu wakati kila siku tunasikia AZANA misikitini nao huenda huko kuabudu?
Moja ya mikakati ya serikali yetu hapa tanzania katika kulinda amani na utulivu imetoa UHURU WA KUABUDU KWA WATU WOTE kama ilivyo kwa watu wote je ni uhuru gani wa kuabudu waislamu wamenyimwa?

Ikiwa kama kweli wamenyimwa basi wasiende misikitini lakini ikiwa hawajanyimwa basi watubu kwa watanzania kwa kusema uongo.ikifuatiwa na BAKWATA kutengua kauli hiyo katika gazeti la majira 7/7/2009.



Vilevile waislamu huko UK nao wanalalamika kwa kunyimwa haki(Daily News july 15,2009 pg 25.je unajifunza nini katika hili???


Yafaa kutambua kuwa tuko kwenye nyakati za KUNG'ANG'ANIA ULICHO NACHO KWA KUKISHIKIRIA SANA ILI ASIJE MWOVU ..........................
Mkristo yafaa kutembea huku TAA ikiwaka ili kutazama hatua tunazopita kama tunakanyaga mahali sahihi au la.
Hivyo kwawakristo wote wanaoiamini BIBLIA hapa duniani yafaa kufahamu kuwa KRISTO NI MWISHO WA SHERIA.
RUMI 10;1-4
(Ndugu zangu nitakayo sana moyoni mwangu na dua yangu nimuombayo Mungu ni kwa ajili yao ili waokolewe.Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudikwa ajili ya Mungu lakini si katika MAARIFA.Kwa maana wakiwa hawaijui haki ya Mungu na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe hawakujitia chini ya haki ya Mungu.Kwa maana KRISTO NI MWWA SHERIA ili kila aaminie ahesabiwe HAKI.

NA BARAKA ZA MUNGU MWENYEZI,ZA BABA,ZA MWANA NA ZA ROHO MTAKATIFU ZAWASHUKIE NA KUKAA NANYI DAIMA.
AMEN.


Charles Kabaka

Thursday, July 16, 2009

MBUNGE wa kuteuliwa na mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale Mwiru ameushambulia waraka wa kichungaji uliotolewa na Kanisa Katoliki nchini, unaoelekeza namna ya kupata kiongozi anayefaa kuchaguliwa katika Uchaguzi Mkuu ujao adai kuwa utaligawa Taifa.
Kingunge alitoa kauli hiyo alipokuwa akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, ambayo iliwasilishwa na George Mkuchika bungeni mjini Dodoma jana.
Hata hivyo, Kanisa Katoliki kupitia Baraza lake la Maaskofu (TEC), limekuwa na utamaduni wa kutoa mwongozo kama huo wakati Taifa linapoelekea Uchaguzi Mkuu, huku kumbukumbu zikionyesha kuwa pia lilifanya hivyo mwaka 2005.
Katika kikao hicho cha jana kilichokuwa chini ya Mbunge wa Peramiho, Jenister Mhagama aliyekuwa mwenyekiti, Kingunge alizungumza kwa msistizo huku akiwataka wabunge wamsikilize kwa makini na kutahadharisha kwamba asinukuliwe vibaya.
``Na sasa nimalize, nina jambo moja kubwa, naomba mnisikilize kwa makini, lakini msininukuu vibaya. Kanisa Katoliki, viongozi wake rafiki zangu, wale wa juu nawafahamu sana, Kanisa hilo limetoa mwongozo kuelekeza anayefaa kuchaguliwa katika uchaguzi ujao.
“Mimi nikautafuta na kuusoma. Sasa hili Kanisa Katoliki linatoa mwongozo wa kuchagua kiongozi wa kisiasa, kwa maana hiyo huu ni mwongozo wa Wakatoliki. Si utakuwa mwongozo wa Wakatoliki pekee?” alisema Kingunge akihoji.
Aliendelea kusema: “Kwa hiyo KKKT (Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania) nao watoe mwongozo kwa sababu wao hawaongozwi na Kanisa Katoliki, ni Wakristo ndiyo, lakini mantiki tu. KKKT wakitoa, Pentekoste watatoa wakwao na Anglikana bado, nao watatoa wakwao, Waislamu bado na wao watoe wa kwao.”
Kingunge ambaye ni mmoja wa wabunge wa muda mrefu ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tangu enzi za Mwalimu Nyerere Rais wa Kwanza wa Tanzania aliongeza kuwa anazungumza hayo kwa kuzingatia mantiki ya mwongozo huo.
“Ni mantiki tu, nasema kwa heshima zote nawaomba viongozi wa Kanisa Katoliki, nawapenda sana, nawaomba warudishe ule mwongozo wao, sisi tunataka nchi moja na tuishi pamoja kwa kushikamana, hatutaki kugawanyika kama Lebanon,” alisema Kingunge bila kufafanua zaidi kuwa waurudishe wapi na kwa vipi.
Kauli hiyo ya Kingunge imetolewa wakati waraka huo wa Kanisa Katoliki umezua mjadala miongoni mwa watu wa kada mbalimbali, huku baadhi wakilishutumu kanisa hilo wakidai kuwa linaingilia masuala ya kisiasa.
Hata hivyo, juma lililopita Askofu Msaidizi wa Kanisa hilo Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Methodius Kilaini alisema mafisadi wanauhofia mwongozo huo.
Kwa mujibu wa Kilaini mwongozo huo unaweka vipaumbele vya nchi katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, ndiyo maana wanaupinga.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya misa ya upadrisho iliyofanyika Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph jimboni humo, Kilaini alisema mwongozo huo ulianza kutumika tangu uchaguzi wa mwaka 1995 na kusisitiza kuwa kwa mwaka huu watu wengi wameshtuka kutokana na kugusa masuala ya ufisadi.
Kanisa hilo lilitoa vitabu viwili vya mwongozi na vipaumbele vya nchi kabla ya kuuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2010, mwongozo ambao umekumbana na vipingamizi kutoka kwa baadhi ya wanasiasa kwa madai kuwa dini inaingilia mambo ya siasa.
“Kwanza napenda watu waelewe kuwa mwongozo hauna lolote kuhusu dini kama watu wanavyodhani, kwa sasa jamii imeshituka kuhusu vitendo vya rushwa na ndiyo sababu baadhi ya wanasiasa wanapinga muongozo huo kwa kuwa unalenga kuwafungua watu macho na kukemea vitendo vya ufisadi,” alisema Kilaini na kuongeza.
“Ninachowataka wanasiasa wote washiriki kupiga vita ufisadi. Asiyetaka kupigana na ufisadi tusimchague na ndivyo mwongozo huo unavyosema,” alisema.
Alifafanua kuwa mwongozo huo unazungumzia juu ya serikali na msimamo wake na wala si kumchangua mtu fulani wala chama fulani kwa ajili ya kumpa uongozi.
“Watu wausome mwongozo huo kwa moyo mweupe na ninaamini wataufurahia, utakuza ufahamu juu ya masuala ya kidemokrasia,” alisema Kilaini.
Awali Mbunge wa Kigoma Kusini, Manju Msambya alishutumu mwongozo huo aliouita kuwa ni "Waraka wa Kiaskofu" wakati akichangia hotuba ya makadirio na matumizi ya Wizara ya Sheria na Katiba, akisema unawafundisha waumini wake kuhusu namna ya kuchagua viongozi kwa imani zao na kuonya kuwa nchi inaweza kuingia kwenye vurugu.
Msambya ambaye hakutaja moja kwa moja dhehebu la dini lililotoa waraka huo, alisema unapingana na kanuni inayosema watu wasichanganye dini na siasa.
Lakini Askofu Kilaini alisema mwongozo huo haukutungwa na maaskofu wala mapadri wa Kanisa hilo na kufafanua kuwa umetungwa na Chama cha Wataalam wa Kanisa Katoliki (CPT) na kwamba wao waliupa baraka zote baada ya kuusoma na kuona unafaa.

Source: Mwananchi

DIGITALBRAIN NA SOMO LA UBONGO


**Je, Unajua jinsi ubongo wako unavyofanya kazi?

**Unafahamu kwamba 75% ya ubongo wako ni maji? kwa hiyo mtu akikuita kichwa maji hajakosea?

**Unafahamu jinsi ya kuutumia ubongo wako kwa mafanikio ?

**Unajua kuwa wewe upo hivyo ulivyo kwa sababu ya matumizi ya ubongo wako wewe mwenyewe kwa hiyo huna wa kumlaumu?

**Wewe ni matokeo ya mawazo yako na matumizi ya ubongo wako..


Fuatana na wataalam wa Digitalbrain katika mfululizo wa vipindi vyao radio WAPO FM 98.0 kupitia kataka website yao http://www.digitalbraintz.com/ na ujifunze kwa undani zaidi kutoka kwa Mtaalamu na Ujasiliamali Mr. Mbutho Chibwaye.

Waweza pia kupata cd za mafundisho yake kwa kuwasiliana naye kwa simu namba + 255 713 427857. au kwa email: mbutho@digitalbraintz.com

Wednesday, July 8, 2009

Mufti Simba asisitiza mchakato wa Mahakama ya Kadhi bado unaendelea

SHEIKH Mkuu wa Tanzania, Mufti Issa Shaaban bin Simba amesema kuwa hoja ya Mahakama ya Kadhi haijazikwa bali itaendelea kujadiliwa na serikali kwa msaada wa masheikh.
Mufti Simba ametoa kauli hiyo baada ya serikali kutangaza Juni 30 kuwa haitaunda Mahakama ya Kadhi na badala yake itatafsiri sheria za Kiislamu na kuzijumuisha kwenye sheria za nchi ili zitumike kwenye mahakama za kawaida.
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) jijini Dar es Salaam jana, Mufti Simba alisema walikutana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Waziri wa Sheria na Katiba, Mathias Chikawe na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam William Lukuvi juzi usiku na kukubaliana baadhi ya mambo ambayo yataharakisha kuundwa kwa mahakama hiyo.
“Tumekubaliana kwamba hoja ya Mahakama ya Kadhi haijazikwa, ila serikali inahitaji msaada wa masheikh katika suala hilo na sisi tumekubali kutoa msaada huo,” alisema Mufti.
"Hivyo jopo la masheikh litaundwa na serikali itaunda jopo lake la wataalamu halafu tutakutana, ili kuratibu mfumo ambao utatumika katika Mahakama ya Kadhi nchini.”
Hatua ya serikali kutangaza kuzika mpango huo wa kuanzisha Mahakama ya Kadhi ilipingwa vikali na Waislamu ambao walidai CCM iliwahadaa wakati wa kampeni za mwaka 2005 na hivyo kusema hawatakiunga mkono chama hicho kwenye uchaguzi ujao na pia kupanga kuandamana Ijumaa ijayo.
Lakini Mufti Simba alisema kikao chao na Waziri Pinda, kilichohudhuriwa na wajumbe zaidi ya 20, likiwemo jopo la masheikh aliloliteua kutoka madhehebu yote ya Kiislamu , wamekubaliana suala hilo liendelee kushughulikiwa.
"Niliandaa jopo la masheikh kutoka madhehebu yote nchini. Nashukuru kwa kuitikia wito wangu. Tulienda kwa Waziri Mkuu tukazungumza kwa mapana zaidi kuhusu Mahakama ya Kadhi na amekubali kuwa mahakama haijafa na mchakato unaendelea,” alisema Mufti Simba.
Alifafanua pia wamekubaliana na Waziri Pinda kwamba atazungumza bungeni kukanusha kauli iliyotolewa na Waziri Chikawe Juni 30 mwaka huu bungeni mjini Dodoma kuhusu uamuzi wa kuzika hoja ya mahakama hiyo.
Mahakama ya Kadhi hushughulikia hasa masuala ya mirathi na ndoa kulingana na misingi ya dini ya Kiislamu.
"Kimsingi serikali haijakataa mahakama ya kadhi, lakini inahitaji msaada wa masheikh na tumekubaliana na Waziri Pinda akafute usemi wa kwamba serikali haitaunda tena mahakama hii na yeye amekubali," alisema Mufti Simba.
"Kitakachoendelea ni kujadili mfumo gani wa mahakama unafaa kutumika.”
"Tunayo matumaini makubwa ya kuipata Mahakama ya Kadhi kwa sababu ni haki yetu na tutaendelea kuidai hadi pumzi yetu ya mwisho (mpaka kufa), mchakato unaendelea.
"Jazba hazifai na tutumie hoja au kwa msemo wa kisasa tutumie nguvu ya hoja.”
Mufti Simba pia alitoa onyo kali kwa Imamu Mkuu wa Msikiti wa Mnyamani uliopo Buguruni, Sheikh Muhammad Idd Muhammad kwa kuzungumza katika vyombo vya habari yale yaliyozungumzwa juzi katika kikao baina ya serikali na jopo la masheikh, kabla ya Mufti kuzungumza.
"Mzungumzaji wa suala la Mahakama ya Kadhi kwa upande wa Waislamu ni mimi tu, hakuna mzungumzaji mwingine. Hivyo namuonya Muhammad Idd kwa kitendo chake cha kutangulia kuzungumzia yaliyojiri katika kikao chetu kabla mimi kuzungumza,” alionya Mufti.
Akizungumza katika kipindi chake cha Arrisala kinachorushwa na kituo cha televisheni cha Channel Ten juzi usiku, Sheikh Idd alieleza kwa ufupi yale yaliyozungumzwa katika kikao cha masheikh na Waziri Pinda.
Sheikh Idd alikiri kosa na kumuomba radhi Mufti Simba, masheikh wenzake pamoja na Waislamu, lakini aliongeza kuwa hakufanya hivyo kwa nia mbaya.
"Nakiri kosa; lakini pia namuomba radhi Mufti, masheikh na Waislamu licha ya kwamba sikufanya vile kwa nia mbaya. Hata Mufti atajua baadaye kuwa sikufanya kwa nia mbaya,” alisema Sheikh Idd.
Baada ya kumaliza kutoa tamko lake, Mufti Simba alikataa maswali akisema suala hilo la Mahakama ya Kadhi linahitaji umakini wa hali ya juu katika kulizungumza.
"Leo sitaki maswali... sitaki kubabaishwa katika majibu. Nakataa maswali ili haya yakaandikwe kama vile nilivyosema bila ya kupotoshwa,” alisema Mufti.
Kabla ya Mufti kuzungumza na waandishi, Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum aliwatahadharisha waandishi kuacha kuandika na kunukuu kauli za watu wengine, badala yake wachukue yale ya Mufti Simba tu kwa sababu yeye ndiye msemaji mkuu katika tukio hilo.
"Waandishi waondoke na kauli ya Mufti tu yeye ndiye msemaji mkuu wa Waislamu Tanzania kupitia chombo chao cha Bakwata. Hakuna msemaji mwingine,” alisema Sheikh Salum.
Hoja ya Mahakama ya Kadhi imekuwa ikidaiwa na Waislamu kwa takriban miaka 20 sasa huku serikali ikitoa ahadi ya kulipatia ufumbuzi, lakini awamu zote za serikali zimekuwa zikipiga danadana.
Wakati huohuo, katibu wa Kamati ya Kutetea Haki za Waislamu, Sheikh Ponda Issa Ponda amesema maandamano ya amani waliyopanga kuyafanya Ijumaa wiki hii, yatafanyika kama yalivyopangwa.
Sheikh Ponda alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na Mwananchi na kwamba maandamano hayo yataanzia Viwanja vya Mnazi Mmoja na kuhitimishwa katika viwanja vya Biafra vilivyo Kinondoni jijini Dar es Salaam.
“Hakuna kitakachotubadili msimamo wetu. Sisi tunafanya maandamano hayo ya amani kuonyesha hisia zetu na kitu gani ambacho Waislamu tunahitaji,” alisema.
Alisema pamoja na kuwapo na kauli mbalimbali za kuwataka Waislamu wawe na subira, hawatakubali kwa kuwa kauli hizo sio mpya na kwamba wameshazizoea.
“Kauli kama hizo zimekuwa zikitolewa mara kwa mara na viongozi," alisema.
Alieleza kwamba maandamano hayo yataanzia Viwanja vya Mnazi Mmoja na kupitia barabara za Bibi Titi, Morogoro na Kawawa,” alisema.
Naye Katibu wa Kamati Maalum ya Kutetea Mali za Waislamu, Sheikh Khalifa Khamis alisema maandamano hayatakuwa na maana kwa sababu suala hilo limeshazungumzwa na masheikh na serikali.
“Mimi nipo pamoja na Mufti kwa kuwataka Waislamu wawe na subira kwa kuwa hivi sasa anayesubiriwa ni Mufti kuipeleka timu yake kwa waziri wa sheria,” alisema.
“Nina uhakika mahakama hii itapatikana mapema kwa kuwa mazungumzo tumeshamaliza na kinachofuata ni utekelezaji tu,” alisema Sheikh Khamis.
Sheikh Khalifa aliwataka Waislamu kuendelea kuwa na subira kwa kuwa uanzaji wa mahakama hiyo unaweza kuwa kwa awamu na kutoa mfano kwamba inaweza ikaanza Dar es Salaam ama wilaya ya Ilala na mikoa mingine ikafuata.
Alipotafutwa na Mwananchi, Waziri Chikawe alikataa kuzungumza kwa njia ya simu akidai hana uhakika kama anayezungumza naye ni mwandishi kweli wa gazeti hili.
“Nitajuaje kama wewe ni mwandishi, nitajuaje,” alihoji Waziri Chikawe na kuongeza: “Come to my office (njoo ofisini kwangu),” alijibu na kukata simu.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi, ambaye imedaiwa kuwa alikuwemo kwenye kikao hicho, alisema: “Muulize aliyewaita masheikh hao mimi sijawaita.”

Source: Mwananchi