Monday, July 30, 2007

Mchungaji ashinda kesi ya kumbaka muumini wake

MCHUNGAJI wa Kanisa la Pentecoste Tanzania (KLPT) Kibaha Maili Moja, Fredrick Makulala (48) ameachiwa huru na Mahakama ya Hakimu Mkazi Mwandamizi mkoani Pwani Bi. Pelegia Khodai, baada ya kuthibitika kuwa madai dhidi yake ya kumbaka Bi. Consolata Ngonyani (25) si ya kweli.
Katika hukumu iliyotolewa hivi karibuni katika mahakama hiyo, Hakimu Khodai, amesema kuwa ameridhishwa na vielelezo vyote villivyotolewa na daktari na mashahidi wa mlalamikiwa kuwa hapakuwa na ushahidi wowote wa kuthibitisha kuwa Bi. Consolata alikuwa amebakwa.
"Mahakama inakuachia huru baada ya kuthibitika kuwa madai (ya madai) hayakuwa na vielelezo (vya kutosha) kukutia hatiani kuwa umebaka". Hakimu Khodai ameandika katika taarifa ya hukumu yake.
Akisoma maelezo ya mlalamikaji, Hakimu Khodai alisema kuwa mnamo Desemba 4, 1997 saa 5.00 asubuhi huko nyumbani kwa Bi. Consolata Kibaha Maili Moja, Mchungaji alikuja kwa nia ya kusuluhisha ugomvi waliokuwa nao na mumewe Samwell Bandeke.
Taarifa ya Hakimu inaseama mshtakiwa alidai kuwa Mchungaji alipofika nyumbani kwa mlalalmikaji alimuulizia mumewe na alipojibiwa kuwa hakuwepo, waliongea naye mazungumzo ya kuwaida kuhusiana na ugomvi wao kwa muda, lakini baadaye alimvuta chumbani na kumbaka. Naye Mchungaji Makulala akitoa utetezi wake alisema yeye alifika nyumbani kwa mlalalmikaji akiwa pamoja na Mjumbe wa Shina Bw. Omari kwa ajili ya kusuluhisha ugomvi wao, ambao Bi. Consolata aliuleta kwake.
Taarifa ya hukumu inasema Bi. Consolata alileta ugomvi huo kwa Mchungaji kwa kuwa hao wanokorofishana ni waumini wake yaani Bi. Consolata na Bw. Samweli.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo Bw. Omari aliitwa kutoa utetezi wake na yeye alikiri kuwa Mchungaji hakuwa amembaka kwa vile muda huo walifika wote nyumbani kwa mlalamikaji.
Shahidi wa pili wa Mchungaji alidai kuwa yeye aliwasikia watu waliokuwa na chuki na Mchungaji huyo wakipanga njama za kumdhalilisha.
Shahidi huyo alisema kuwa alimsikia Bw.Bandeke, akimshurutisha mkewe Bi. Consolata aende
polisi kushitaki kuwa Mchungaji amembaka, na asingefanya hivyo Bw. Bandeke angempiga vibaya.
Naye shahidi wa tatu na wa mwisho wa Mchungaji ambaye ni mkewe aliiambia mahakama kuwa Bi. Consolata, alifika nyumbani kwake na kumlalamikia kuwa mumewe ‘anamfosi’ aende polisi kushtaki kuwa mchungaji amembaka, na asingefanya hivyo angepigwa vibaya.
Bi. Consolata na mumewe Samwel ambao wana ugomvi wa muda mrefu unaosemekana kuwa unatokana na wivu, sasa hivi wametoroka na hawajulikani walipo, na mara baada ya kutoa ushahidi wao wakawa hawahudhurii mahakamani mpaka hukumu ilipotolewa.
Mwandishi wa habari hizi allipozungumza na mchungaji Makulala nyumbani kwake maili moja, kuwa ni kwa nini kuna kikundi cha waumini wanaompinga kanisani kwake, alisema waumini hao ni vibaraka tu wanaotumiwa na uongozi wa juu kumsakama.
Amesema mara baada ya taarifa za kuwa amebaka zilipofikishwa polisi viongozi wa juu wa kanisa hilo walifika kanisani hapo Desemba 7 mwaka 1997 toka Der Es Salaam.
Aliwataja viongozi hao kuwa ni makamu wa Askofu Nkhandda, katibu mkuu wa KLPT, Bw, Aron Mabondo na katibu mtendaji Bw,Shekihiyo.Anasema walipokuja aliwaeleza hali halisi ya mambo yalivyokuwa, wakati wanaendelea na kikao hicho ndipo alipokuja huyo jirani yake ambaye ndiye aliyekuwa shahidi wake wa jadi na kueleza mbele yao kuwa ‘’twendeni mukamuone bi. Consolata na mumewe pamoja na kikundi chao.

No comments: