HII NDIO HISTORIA YA MAREHEMU ASKOFU MOSES KULOLA
Marehemu Askofu Moses Kulola enzi za uhai wake
MOSES KULOLA, aliyezaliwa mwaka 1928 katika familia ya watoto kumi, na kufariki mwezi Agosti 2013 katika hospitali ya AMI (African Medical Investments) iliyopo Slipway jijini Dar es Salaam. Ambapo kwa sasa wamebaki ndugu zake wanne.
Moses Kulola alijiandikisha katika shule ya kwanza mnamo mwaka 1939. Shule hiyo ilikuwa inaitwa Ligsha Sukuma, ilikiwa ni shule ya Misheni. Baada ya kumaliza hapo Ligsha Sukuma Mission School, Moses Kulola akajiunga katika Idara ya Uchoraji wa Majengo mnamo mwaka 1949. Na mwaka 1950 alibatizwa katika Kanisa la AIM Makongoro, mjini Mwanza.
Alifanikiwa kumuoa Elizabeth na Mungu aliwajalia kupata watoto 10, ambapo kwa sasa saba (7) bado wako hai. Alianza kazi za Umisionari mnamo mwaka 1950, ingawa alikuwa amesikia wito huo mwaka ule wa 1949!

Faustine Munishi(malebo) Moses Kulola,Emmanuel Mwasota.
Mwaka 1959 aliajiriwa serikalini.
Lakini pamoja na kuajiriwa huko Moses
Kulola aliendelea na kuhubiri Injili
katika Miji na Vijiji. Utumishi wake kama mwajiriwa wa Serikali
ulikwisha mwaka 1962 baada ya kuwa amekabidhi nguvu, mwili na nafsi
yake katika kazi ya Mungu! Ilipofika mwaka 1964 aliamua kusoma na akajiunga katika Chuo cha Theolojia na kuhitimu katika kiwango cha
Diploma mamo mwaka ule wa 1966.
Endelea kusoma historia hii kwa kubofya hapa chini

No comments:
Post a Comment