Friday, January 30, 2009

Mchungaji awa Mbunge mbeya vijijini

Mbunge mpya wa Mbeya Vijijini Mchungaji Luckson Mwanjale akila kiapo Bungeni Mjini Dodoma leo.



Mchungaji Mwanjale anakuwa ni mchungaji wa kwanza nchini kuchaguliwa kushindana katika kinyang'anyiro cha uchaguzi na kupiga kampeni na hatimaye kuibuka mshindi wa kiti hicho kwa kupitia tiketi ya CCM.

Waziri mkuu aangua kilio bungeni

Hoja ya wapinzani kumtaka ajiuzulu yayeyuka

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda ameangua kilio bungeni kuonyesha uchungu alio nao dhidi ya vitendo vya mauaji ya kikatili ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), hivyo kuyeyusha hoja ya wabunge wa upinzani waliokuwa wamepania kumbana, ili ajiuzulu kwa madai kwamba, alitoa amri ya kuua wauaji ambayo ni kinyume na katiba ya nchi.
Hali hiyo ilitokea jana bungeni, wakati Pinda akielezea yaliyomfanya atoe kauli hiyo tata kikatiba na misingi ya haki za binadamu.
Pinda alisema alipokuwa katika ziara katika mikoa ya Kanda ya Ziwa, alipata taarifa za kusikitisha kuhusu mauji ya albino na mara kesho yake habari zikatoka kwenye vyombo vya habari kwamba, albino mwinge kauawa.
"Jamani jamani taarifa za matukio hayo kibinadamu zinatia uchungu sana na kumfanya mtu ashindwe kujizuia….," mara akaanza kutokwa machozi na kukatisha maelezo yake akatoa miwani na kujifuta huku wabunge wakiwa kimya.
Waziri Mkuu alisema hayo baada ya Kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni, Hamad Rashid Mohamed, kumtaka atoe ufafanuzi kuhusu kauli aliyoitoa hivi karibuni akiwa katika ziara Kanda ya Ziwa, kuwaruhusu wananchi kuwaua watu watakaokutwa wakimchinja albino.
Hamadi alisema katiba ya nchi inamlinda mtu kupewa nafasi ya kujitetea, hivyo akamtaka waziri afafanue maana ya kauli yake, kwa kuwa ni kinyume na taratibu ambazo nchi imejiwekea katika kuhakikisha haki inapatikana.
Pinda alisema mtu anaposikia au kusoma taarifa za mauaji ya albino, hawezi kupata hisia juu ya mateso wanayoyapata, sawa na anayewasikiliza watu walionusurika kufa au walioshuhudia vitendo hivyo vikitendeka.
“Mimi walinihadithia, aah! Samahani," alisema kwa masikitiko Pinda huku akiwataka radhi wabunge kwa kushindwa kuendelea kueleza kwa jinsi alivyoguswa na matukio hayo. Mara akaanza kububujikwa na machozi na baada ya sekunde kama 15, alichukua kitambaa chake akajifuta.
Aliendelea kuelezea jinsi maalbino wanavyouawa kikatili, akisema wengi walikufa kwa kushindwa kupata huduma mapema ya kuzuia damu baada ya ama kukatwa mikono ama miguu na majitu hayo katili yenye imani potofu kwamba, viungo hivyo vinaweza kumpatia mtu utajiri.
Alisema alielezwa kuwa, wauaji wanachokifanya ni kumshambulia albino na kumkata kiungo wanachokitaka kwa kutojali hali wanayomuacha nayo kama ni mateso, kufa au kupona hivyo alipatwa na uchungu kiasi cha kujikuta anatamka kuwa, watu wanaokutwa wakitenda hayo nao wanapaswa kuadhibiwa papo hapo.
Alifafanua kuwa wakati akiwa kwenye ziara hiyo iliyokuwa maalumu kwa ajili ya kukemea na kupanga mikakati ya kukabaliana na vitendo hivyo, idadi ya maalbino waliouawa walikuwa 30 na baada ya kukemea vitendo hivyo, ghafla akapewa ripoti ya kuuawa wengine wawili, jambo ambalo lilizidi kumuudhi na kumchanganya.
Waziri Pinda aliwaomba radhi watu walioudhika kutokana na matamshi na pia akimuomba Mungu amsamehe iwapo amewakosea.
"Kama mnaona kile nilichofanya ni makosa naomba mnivumilie. Naomba Mungu anisamehe kama nimewakosea," aliomba Waziri Mkuu na kuongeza kuwa serikali imechukizwa sana na mauaji hayo ya kikatili.
Alisema Tanzania imekuwa ikiheshimika sana katika jumuiya ya kimataifa, lakini mauaji ya albino na ya vikongwe katika eneo hilo yameitia doa.
Alielezea pia kuhuzunishwa zaidi na tamko la Bunge la Jumuiya ya Ulaya (EU) la kulaani mauaji hayo, kana kwamba wao wanaguswa sana na suala hilo kuliko Serikali ya Tanzania.
Hata hivyo, alisema kuwa katika ziara hiyo, ambayo iliwahusisha pia baadhi ya mawaziri, wabunge, viongozi wa polisi, viongozi wa dini na kisiasa, waliahidi kushirikiana kuhakikisha kuwa wanakabiliana na kulimaliza tatizo.
Isitoshe alisema aliwataka viongozi wa vijiji kurejesha ulinzi wa jadi, maarufu kama sungusungu ili kukabiliana na wauaji.
Pinda alisema kuwa serikali ipo tayari kupokea maoni kutoka kwa watu mbalimbali, yanayoweza kusaidia kupata mbinu ya kukomesha kabisa mauaji hayo, ili kuiokoa jamii hiyo ya albino.
Alisema katika kumbukumbu za serikali, hadi mwishoni mwa mwaka jana vikongwe 2,866 walikuwa wameuawa kwa imani potofu kuwa ni wachawi.
Alisema serikali imeliagiza jeshi la polisi kutumia maarifa yake, hata kama itabidi kutumia gharama kubwa, ili kuwatia mbaroni watu wote wanaojihusisha na mauaji hayo.
Wapinzani pia walimtaka Pinda atoe maelezo yanayodaiwa kuwa yalitolewa na Rais Jakaya Kikwete kisiwani Pemba kwamba, aliwashangaa wakazi wa eneo hilo kuwachagua watu ambao hawawezi kuunda serikali na ambao watachukua muda mrefu kupata nafasi hiyo.
Pinda alisema anapata taabu kujibu swali hilo, kwa sababu hawezi kuyatolea maelezo mambo yaliyozungumzwa na bosi wake na wala hajui kama ni kweli rais alisema kama vyombo vya habari vilivyoripoti.
Mbunge wa Konde, Dk Ali Tarab Ali (CUF) alimtaka Pinda aeleze kama kitendo cha Rais Kikwete kutumia magari ya serikali kisiwani Pemba na kuonekana akifanya shughuli za chama ni matumizi mabaya ya fedha za serikali.
Pinda alimjibu akisema kuwa, ni vigumu rais kutofautisha vyombo vya usafiri anavyovitumia wakati akifanya ziara za kisiasa ama za kiserikali na kutoa mfano kwamba, hata rais wa Marekani hutumia ndege aina ya Air Force one bila kuchagua kuwa ni shughuli ya kisiasa au kiserikali.
Wakati hayo yakitokea bungeni, baadhi ya viongozi wa dini nchini, wamemtaka Waziri Pinda kukiri kosa, kufuta kauli yake na kuomba radhi kwa mamlaka za kisheria, Bunge na Wananchi.
Akizungumza na Mwananchi jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislaam, Sheikh Ramadhan Sanze alisema Pinda alifanya kosa la kiufundi kwa kuwa yeye ni mtendaji mkuu wa serikali, hivyo hakupaswa kusema jambo linalopingana na msimamo wa serikali, sheria na katiba ya nchi.
"Kwa vile kauli hiyo haijaleta madhara mpaka sasa Waziri Mkuu ana uchochoro wa kupita ili kujisafisha. Cha msingi ni kukiri kosa, kufuta kauli yake na kuomba radhi kwa mamlaka za kisheria, Bunge na Wananchi" alishauri Sheikh Sanze.
Alisema, hajafuatilia vizuri kuhusu hoja za kambi ya upinzani bungeni na kwamba, kujiuzulu inaweza isiwe suluhisho la tatizo hilo kwa kuwa, hata kama atajiuzulu kauli haitafutika na tatizo litabaki palepale.
"Nchi hii haina dini na kwa hiyo haingozwi na sheria za dini bali inaongozwa na sheria za nchi, kwa hiyo Pinda alipaswa kuangalia sheria ya nchi kwanza kabla ya kutoa agizo lake," alisema Sheikh Sanze.
Alifafanua kuwa, Waziri Pinda ametengeneza mazingira ya uchafuzi na uchochezi, kutokana na kauli yake hiyo kwani baadhi ya watu wanaweza kuitumia vibaya kwa kumuua mtu kwa sababu ya chuki tu baina yao.
Alisema, athari ya kauli kama hizo zinaweza kusababisha migogoro kati ya dini na dini nyingine, kabila moja na jingine au dhehebu moja na jingine kama wananchi watautumia wito huo.
Alisema vita dhidi ya mauaji ya albino imekuwa ikitumika kisiasa zaidi kuliko kitaalamu na kuongeza kuwa, mamlaka husika ziliangalie tatizo hilo kitaalamu badala ya kuliacha likitumika kisiasa.
Naye Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Valentino Mokiwa alisema kauli ya Pinda ya kutaka aliyeua albino auawe si sahihi kwa sababu mtu akimuua aliyeua ni muuaji na ana kosa kisheria.
Mauaji ya albino yamekuwa yakitikisa nchi na hasa katika eneo la Kanda ya Ziwa, licha ya juhudi mbalimbali zilizofanywa na serikali kupitia jeshi la polisi, mashirika ya kutetea haki za binadamu, vyama vya walemavu na watu binafsi.
Source:Mwananchi

Tuesday, January 27, 2009

Jan 2009:KWAHERI NDUGU YETU SEDEKIA.


TUKIO LA JANUARY 2009:

KWAHERI NDUGU YETU SEDEKIA.


Jina la Bwana litukuzwe milele na milele, na tena atukuzwe Yeye ambaye anatuwazia mema kuliko yale sisi tuyawazayo.

Ndugu wana Sayuni popote pale mlipo, nadhani wote mnakumbuka msiba tulioupata wa kutwaliwa kwa ndugu yetu Fanuel Sedekia akiwa kule katika nchi ya baba zetu, Israel.

Mimi nilifuatilia tukio lile na kuhudhuria ibada ya kuuaga mwili wake hapa Arusha ila nilishindwa kuwaletea habari hizi kwa muda kutokana na kubanwa sana na mambo hapa, ila nimezileta leo ili tujikumbushe ikiwa ni tukio kubwa kabisa katika mwezi huu.

Kama wengi tulivyojua, ndugu yetu huyu alifariki akiwa katika safari muhimu sana ya kiroho kule Israel, akiwa pamoja na timu ya huduma ya MANA ya mwalimu Christopher Mwakasege.

Siku hiyo ya kuuga mwili wake na mazishi (January 10) tulikutana katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid hapa Arusha, na watu walikuwa ni wengi kiasi ambacho hakikutegemewa. Mwili wake uliingizwa uwanjani, ukiwa umebebwa kwenye gari, na gari lingine lilikuwa likifuata nyumba yake likiwana speakers kubwa huku wakiwa wameweka ule wimbo wa “Bwana ametoa na Bwana ametwaa” aliouimba Sedekia mwenyewe. Hii ikiwa ni baada ya kuwasili jana yake kwa ndege kutokea Israel ambapo mamia ya wakazi wa Arusha walijipanga pembeni mwa barabara ya moshi-arusha huku wakiutazama msafara uliokuwa na mwili wake uliopata magari yasiyopungua 40, na wengine walikwenda hadi hospitali ya mkoa ya Arusha na walisikika wakipiga mayowe ya vilio walipoona jeneza lake. Mara baada ya kuingia uwanjani,ulipokelewa kwa utulivu na timu ya waimbaji wa muziki wa Injili kutoka Dar na maeneo mbalimbali kama unavyoweza kuona katika picha. Baada ya hapo, watu mbalimbali walipewe nafasi ya kuzungumza kwa ufupi namna walivyomfahamu Sedekia. Na hapa kwa ufupi natata nieleze kile alichosema Mwl. Mwakasege.
Mwalimu alielezea namna walivyoondoka na Sedekia hapa uwanja wa ndege wa Arusha, ya kuwa alikuwa amemaliza kutumia doze ya malaria iliyomsumbua muda kidogo na kuwa alisema alikuwa ok kwa safari. Waliondoka hadi Israel walipoanza kutembelea maeneo muhimu ya kibiblia huko, na baada ya siku chache, Sedekia alionekana kuwa mdhaifu na alisema hali yake si nzuri sana. Baadaye, walimua kumpeleka hospitali waliyoshauriwa na madaktari akiambatana naye na daktari waliyekuwa naye safarini pia. Baada ya uchunguzi ilifahamika kuwa alisumbuliwa na Sukari na pia homa ya mapafu (Pneumonia),na hivyo akalazwa katika hospitali ile ya Poriya.

Mwakasege aliendelea kusema kuwa kabla ya Sedekia kuugua, walitembelea kanisa moja huko Israeli na Sedekia alikuwa amekwenda na kinanda chake (japokuwa ilikuwa ni safari ya mafundisho ya ndoa) hivyo alikitoa kinanda chake na akapewa nafasi ya kuimba. Aliimba wimbo ule wa “Bwana Mungu nashangaa kabisa” (Tenzi no. 114) na huo ndio ulikuwa wimbo wa mwisho wa Sedekia kuimba upande huu (kwani upande ule mwingine bado anaimba)
Mwalimu aliendelea kueleza namna Sedekia alivyougua, muda wa safari yao ulipokwisha ilibidi Mwl. Mwakasege abaki Israel kumuuguza Sedekia na wengine kurudi nyumbani.
Alieleza kuwa madaktari walijitahidi na kurekebisha hali ya sukari yake (iliyokuwa juu sana) na mapafu,lakini alipoteza fahamu na hakupata tena fahamu hadi uimbaji wake ulipohamishiwa mbinguni.

Katika ibada ile ileyohudhiriwa na watu wengi kuliko hata anapokuja rais wa nchi yetu huku Arusha, ilijawa na watu wa rika zote, na watu kutoka nchi mbalimbali. Mbunge mmoja alieleza pia namna walivyofahamiana na Sedekia, na mkenya mmoja aishiye Norway alieleza namna walivyokuwa wamepanga kwenda kupeleka Injili katika nchi zaidi ya tano za Afrika wakiwa na Sedekia, na kwamba aliwaambia anakwenda Israel na akirudi ndio wataanza safari hizo.

Ilifahamika kuwa Sedekia alikuwa na maono makubwa sana kwa ajili ya huduma yake kumtukuza Mungu huko mbeleni. Alikuwa na mpango wa kufungua studio yake ya muziki ya Injili, jambo ambalo, wote waliokuwepo siku ile waliazimia kuwa maono haya yasimamiwe na mke wake hadi studio ijengwe. Tukio hili wali walilitumia pia kusisitiza waimbaji waimbe katika roho kama alivyofanya Sedekia, na pia umoja kati yao ulisisitizwa sana jambo ambalo limeonekana kuanza kukua katika msiba ule.

Muda wote wa tukio hili, kwaya ya pamoja “Mass Choir” ilikuwa ikiimba nyimbo mbalimbali alizoimba Sedekia, lakini wimbo wa “Nimemwona Bwana….” Uliimbwa sana.
Tulipewa nafasi ya kutoa michango yetu kwa upendo kama sehemu ya kusema “pole” kwa familia yake.

Kumalizia mazungumzo yake, mwalimu Sedekia alianza kwa kumshukuru Mungu kwa kumpa Neema ya kuwa na Sedekia katika siku zake za mwisho (kwani aliwahudumia wengi lakini Mungu alipenda siku za mwisho wake awe na Mwakasege) na kuwashukuru watu wengine wote.

Alizungumza zaidi na kusema kuwa hakuna awezaye kuyapindisha mapenzi ya Mungu, na ya kuwa, mawazo ya Mungu yapo juu sana kuliko mawazo yetu sisi wanadamu. Ni nani ajuaye kuwa uimbaji wa Sedekia sasa unatakiwa zaidi mbinguni na Mungu kuliko hapa duniani?

Mwalimu Mwakasege alituonya ya kuwa “MUNGU ANAENDELEA KUWA MUNGU HATA KAMA HAKUJIBU TULIVYOTAKA, hivyo: Usimvunjie Mungu heshima yake ndani ya moyo wako, mwache aendelee kuwa Mungu daima” japokuwa Sedekia aliombewa nchi nzima ili asife,lakini Yeye Mungu anajua zaidi yetu.

Alimalizia kwa kutusihi watu wote tulioguswa na msiba huu, kila mtu ajiulize maswali haya matatu na apate jibu lake leo hii.(Ninamnukuu)

1. Kwanza jiulize, ukifa unataka ukumbukwe kwa lipi?
2. Baada ya kifo, zipo sehemu mbili tuu za kwenda, mbinguni na jehanam, je unataka ukifa uende wapi?
3. Je, Yesu Kristo akirudi leo, utanyakuliwa na Yeye au utabaki? (mwisho wa kunukuu)

Mwishoni ilitolewa nafasi ya watu wote kupita kwa mstari kwenda kutoa heshima za mwisho kwa mwili wake. Watu tulijipanga kwenye mistari iliyoanzia mwanzo hadi mwisho wa uwanja lakini watu hawakukata tamaa hata kidogo. Tulijipanga na kuanza zoezi hili ambalo halikuweza kufanikiwa kwani baadhi ya watu walishindwa kujizuia kwa vilio na kufanya hali kuwa ngumu, hali iliyopelekea zoezi hili kusitishwa na mwili wake kuchukuliwa na kupelekwa kuzikwa.

Ile siku ya mwisho, wote tuliookoka tutanyakuliwa na Bwana wetu Yesu Kristo, na tunaambiwa kuwa tutakutana wote ng’ambo ya mto, kama maneno ya ule wimbo wa “Shalll we gather at the river” (Ati twonane mtoni), tutakumbatiana na walioolewa wa vizazi vyetu na kisha tutaungana pamoja na tutakaribishwa kuingia katika karamu iliyoandaliwa katika Mji ule wa Yerusalemu mpya ambao hata sasa upo tayari kwa ajili yetu. Tuliookoka wote tusife moyo, Sedekia yupo na Bwana, na uzuri mmoja ni kwamba ipo siku tutakutana naye na kukaa naye pamoja na Bwana. Kusema ukweli, sasa yupo anaendelea kumwabudu Mungu huko juu kwa Baba yetu. Tushike sana tulichonacho.

Haya ndiyo niliyopenda kuwashirikisha siku hii ya leo.

“KWAHERI KAKA SEDEKIA, KATIKA SAA YA BWANA TUTAKUTANA PALE NG’AMBO YA MTO ULE”



www.lema.or.tz na Sayuni blog inamwomba Mungu Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo amtunze mke wake, watoto na familia yote, na Bwana atutie sisi wote NGUVU. Amen.

Frank Lema.
Arusha.

Monday, January 26, 2009

Serikali yapiga marufuku waganga wa jadi Tanzania

SERIKALI imetangaza kufuta leseni zote za waganga wa jadi kuanzia Ijumaa Jan. 23, 2009 ikiwa ni sehemu ya mapambano dhidi ya mauaji ya Albino na Vikongwe nchini.
Amri hiyo ilitangazwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda katika mkutano wa hadhara mjini Shinyanga leo mwishoni mwa ziara yake ya mikoa ya Kanda ya Ziwa kuhamasisha mapambano ya Serikali dhidi ya mauaji hayo.
Waziri Mkuu alisema kuwa aliwasiliana na Mwanasheria Mkuu kuhusu uamuzi wa kuchukua hatua hiyo ya kufuta leseni hizo na Mwanasheria Mkuu akasema jambo hilo linawezekana.
"Kuanzia leo leseni zote za waganga wa jadi futa… Mtu yeyote akiendelea na kazi hiyo mfuatilieni," aliwaagiza Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Wakuu wa Halmashauri zote za Jiji, Miji na Wilaya nchini.
Waganga wa jadi wamekuwa wakituhumiwa kuwa ndiyo chimbuko la mauaji hayo kwa vile wao ndiyo hupiga ramli za kuelekeza hivyo.
Katika mikutano na viongozi wa mikoa ya Kagera, Mwanza, Mara, Tabora na Shinyanga, wachangiaji wengi waliitaka serikali kufuta leseni hizo. Hata baadhi ya waganga wa jadi waliochangia walikiri.
Waganga wa jadi husajiliwa na kupewa leseni za kufanya kazi zao na Halmashari kwa utaratibu wa kiutawala. Ipo sheria ya mwaka 2002 kuhusu Tiba Asilia na Tiba Mbadala (Traditional and Alterntive Medicine Act), lakini Kanuni za utekelezaji wake zilikuwa hazijatengenezwa.
Waziri Mkuu alisema mganga wa jadi ambaye anaweza kuruhusiwa baadaye ni yule ambaye dawa zake za mitishamba au za asili zitakuwa zimethibitishwa na Kitengo cha Uchunguzi wa Tiba Asili cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kuwa kweli zinatibu. Mgonjwa naye atatakiwa awe na cheti kutoka hospitali kitakachothitisha maradhi yake na kuwa tiba yake hopitali imeshindikana. "Waganga hawa ni waongo wakubwa…Siyo lazima kuwa nao.
Wangekuwa waganga wa kweli magonjwa mengi yangepungua nchini, lakini magonjwa yapo na sasa wanapiga ramli na kuwa kichocheo cha mauaji. Mkoa wa Shinyanga unasemekana unaongoza kwa idadi ya waganga wa jadi waliosajiliwa na wako 1,104 na 94 ambao hawakusajiliwa.
Wilaya ya Kahama peke yake ina 763. Waziri Mkuu aliuambia umati uliofurika kwenye uwanja wa Chuo cha Biahshara cha Shinyanga (Shycom) huku akishangiliwa kuwa mapambano dhidi ya mauaji ya Abino ni vita na ndiyo maana anataka ulinzi wa jadi wa Sungusungu urejeshwe kusaidiana na vyombo vya dola kukabiliana na hali hiyo.
Aliwataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na Jeshi la Polisi na Idara ya Usalama wa Taifa kufnya kazi zao kwa ufanisi zaidi na "kujipanga upya na kuteremka hadi ngazi ya chini" kusimamia mapambano dhidi ya mauaji ya Albino na Vikongwe.
"Inapotokea kuwa Albino au Kikongwe anauawa katika eneo fulani, mimi nitamshukia Mkuu wa Mkoa na kumuuliza kwa nini aliacha hali itokee hivyo. Mkuu wa Mkoa naye atamshukia Mkuu wa Wilaya na vivyo hivyo," alisema.
Aliongeza: "Tukijumuika wote kwa pamoja tutashinda vita hii kama tulivyoshinda vita dhidi ya nduli Idi Amin wa Uganda". Waziri Mkuu pia alisema atamwomba Jaji Mkuu kuwa zile kesi za mauaji ya Albino ambazo ziko tayari zinapangiwa majaji maalum ili zikamilike na hatima yake ijulikane haraka.
Tangu Juni mwaka 2007 mpaka Novemba mwaka 2008 jumla ya Albino 34 wameuawa nchini kwa imani za ushirikina kuwa eti viungo vyao vinasaidia kupata utajiri.
Idadi yao kimkoa kwenye mabano ni Mwanza (19) Mara (4) Kigoma (3) Shinyanga (4), Kagera (3) na Mbeya (1). Mwaka huu tayari wameuawa watatu.
Jumla ya vikongwe waliouawa nao kwa kushukiwa wachawi ni 2583 ambapo idadi yao kimkoa kwenye mabano ni Mwanza (696), Shinaynga (522), Tabora (508), Iringa (256), Mbeya (192) Kagera (186), Singida (120) na Rukwa (103).
Ziara ya Waziri Mkuu Pinda katika mikoa ya Kanda ya Ziwa inamalizika leo kwa majumuisho yatakayowahusisha viongozi wa mikoa hiyo. Alianzia Kagera na badaye kutembelea mikoa ya Mwanza, Tabora na Shinyanga.
Mkoa wa Mara ulijumuishwa kwa viongozi wake kuhudhuria mkutano wa viongozi Mwanza.

Friday, January 23, 2009

PLEASE SAY EVEN JUST A WORD....

Thank you for joining with us as we pray for the persecuted church around the world. "Confess your trespasses to one another, and pray for one another, that you may be healed. The effective, fervent prayer of a righteous man avails much." -James 5:16


CHINA
- Deathly Ill Husband Denied Visitation with his Imprisoned Wife

– China Aid AssociationChinese government authorities have denied Hua Zaichen, 91, visitation with his imprisoned wife, 79-year-old Shuang Shuying, according to China Aid Association (CAA).Zaichen, who is deathly ill, requested a final meeting with his wife to say his goodbyes, but officials refused to grant the request. “Authorities say Shuang Shuying is not allowed to leave prison before February 8, 2009, the end of her two-year sentence. Officials stated that if her husband died before then, she would be allowed to see his body for 10 minutes and would have to be chained, handcuffed, shackled and wearing a prison uniform,” CAA added. Pray for this family that has endured many hardships for the sake of their faith. Pray for Shuang Shuying to be released. Praise God for their courage!Joshua 1:9

INDIA
- Four Christians Arrested in Madhya Pradesh – VOM SourcesOn Jan. 5, police arrested four Christians in the village of Kushalpura, Madhya Pradesh, India on false charges of forcible conversion. At 10:00 a.m., Pastor Kantilal Bhuria went to the home of a local Christian where 25 believers were gathered for prayer. During the service, a mob of Hindu extremists barged into the house and accused Pastor Bhuria of forcibly converting Hindus. The extremists verbally abused those present and beat a Christian woman. The police arrived on scene after receiving a phone call from the attackers and arrested four believers. At last report, these Christians remained in detention. Pray for the release of these Christians. Ask God to give them and other suffering believers in India grace, wisdom and endurance as they serve Him.1 Peter 5:10-11

KAZAKHSTAN

– President Sends Repressive Law for Constitutional Review – Forum 18 NewsPresident Nursultan Nazarbaev of Kazakhstan has sent a repressive new law which aims to severely limit freedom of religion or belief to the country's Constitutional Council, Forum 18 News Service reported. Meanwhile, the government continues to repress the exercise of freedom of thought, conscience and belief. In January a Baptist pastor, Aleksandr Kerker, was fired from his job because he led worship without state permission. Pastor Kerker lost his job after authorities visited his employer. Pray for believers in Kazakhstan facing the possibility of harsher conditions if this repressive law is passed. Ask God to provide for Pastor Kerker and his family during this challenging time. Pray this pastor forgives his persecutors and for God to touch the heart of these authorities.Philipians 4:6-7

UZBEKISTAN

– Children and Parents Threatened for Attending Services – Forum 18 News
Police in southeast Uzbekistan have begun a campaign against children attending places of worship, Forum 18 News Service reported. The authorities' campaign, which also uses the state-controlled mass media, attacks schools and parents who allow children to attend religious "sects." Pray for Christian families who have come under scrutiny in Uzbekistan. Ask God to give them courage to continue serving the Lord despite what authorities say.Psalm 91.

PLEASE TAKE TIME TO SAY EVEN JUST A WORD.
-Team at Sayuni.

Tuesday, January 20, 2009

DigitalBrain yajitolea kuidhamini mlima sayuni

Ile kampuni kubwa ya kizalendo ya DigitalBrain sasa imejitolea kuudhamini mlima sayuni kwa kuutengenezea website yake itakayogharimu zaidi ya dola 5000.Website hiyo itakayokuwa ni web portal ya aina yake kuwahi kutokea hapa Tanzania itakuwa na kila kitu kinachopaswa kuwapo katika website za kisasa.Kwa muda wa zaidi ya mwaka mmoja na nusu mlima sayuni umekuwa ukipatikana kwenye blog na kwa kuwa kwenye blogu lakini sasa DigitalBrain wameamua kugharamikia shughuli zote za kuitengeneza website hii kubwa na ya kipekee kabisa barani Afrika.
Katika website hiyo itakayokuwa tayari kabla ya mwisho wa mwezi huu,kutakuwa na mahubiri LIVE mbali mbali,muziki wa injili na pia utawaona LIVE wahubiri mbalimbali na wachungaji mbalimbali wanaotumiwa na Bwana hapa nchini.
Pia utaweza kusikiliza radio mbalimbali za kikristo kama Radio WAPO FM, Praise Power FM na Upendo FM zote za jijini Dar.
Kwa wale walio ughaibuni kaeni mkao wa kupokea baraka hizi ambazo wengi mmekuwa mkizisubiria kwa muda mrefu.
Pia utaweza kushiriki mijadala mbalimbali ya wapendwa na mambo ya kisiasa na kijamii.Kuchat na wapendwa mbalimbali,kununua na kuuza bidhaa mbalimbali, kupata taarifa za nyumba za kupangisha na kununua, na mambo mengine mengi mengi mengi ya kujenga.
Kwa hivi sasa DigitalBrain wanarusha vipindi vyao kupitia radio WAPO FM na unaweza kuwasikiliza LIVE kupitia mtandao wao wa http://www.digitalbraintz.com/ . Waweza kusikiliza kipindi chao kilichorushwa jumatau ya jana na jumatatu zingine zilizopota.
Akiongea na Mlima sayuni mkurugenzi wa Ufundi wa DigitalBrain Mr. Marco Salimu amesema kuwa wameamua kufanya kitu kizuri kwa ajili ya mwili wa Kristo na wamejitolea kiasi hicho cha fedha kwa kuwa wanaamini katika kutoa na kubarikiwa katika kipimo cha kujaa,kushindiliwa,kusukwasukwa kumwagika jinsi Bwana YESU atakavyowabariki.
...DigitalBrain..By the renewing of your mind..

Saturday, January 10, 2009

KWA HERI SEDEKIA

Hakika mtumishi wa Mungu alale kwa amani!

Kama kuna watu walibariki moyo wangu ni Fanuel Sedekia na naomba niamini vivyo hivyo kwa mioyo ya watu wengi kama jinsi ambavyo umati wa watu ulivyojihudhurisha pale kwenye viwanja vya Sheikh Amri abeid Karume, Arusha mjini. Mtu huyu alipendwa na wengi na huo ni udhihirisho tosha namna ambavyo mwili wake uliheshimiwa kwenye kuagwa na hata mazishi yake.

Yatosha kwa siku maovu yake na Bwana ampe faraja haswa mjane na watoto wake pasipo kusahau wote walioguswa na msiba huu kwa namna moja ama nyingine!!

Hebu basi tujikumbushe walao kwa nyimbo hizi wakati tukiendelea na maombelezo.

KWAHERI KAKA YETU SEDEKIA


BWANA YESU ASIWE WAPENZI WOTE WA SAYUNI NA PIA WOTE WALIOMPENDA NDUGU FANUEL SEDEKIA.

Hatimaye leo tarehe 10,January 2008, ile safari ya mwisho kwa hapa duniani ya kaka yetu mpendwa, muimbaji Fanuel Sedekia imefanyika leo hapa jijini Arusha.

Mwili wa kaka Sedekia (36) uliletwa kwa ndege maalumu jana na kufika hapa Arusha hospitali ya mkoa majira ya saa 12 kamili jioni ulipohifadhiwa hadi leo asubuhi.

Leo asubuhi mwili wake uliletwa katika uwanja wa mpira wa Sheikh Amri Abeid hapa Arusha ulipowekwa kutoa nafasi kwa watu walioweza kufika kutoa heshima zao za mwisho kwa kaka yetu.
Baadaye mwili wake ulipelekwa kuzikwa katika makaburi yaliyopo Njiro hapa Arusha.

Zoezi hilo limefanyika leo na hii ni taarifa fupi tuu kwenu kuwajulisha kilichotokea. Kesho nitawaletea picha kadhaa na maelezo zaidi kuhusu tukio hili la aina yake.

"Yes, brother Sedekia, We will meet on that beatiful shore when the time of the Lord comes"

MUNGU UNABAKIA KUWA MUNGU HATA KAMA HUKUJIBU KAMA TULIVYOTAKA SISI.

Wednesday, January 7, 2009

DigitalBrain waanza kusikika live kwenye Internet

Ile kampuni inayokuja juu na kwa kasi katika maswala ya teknolojia ya habari na mawasiliano ya DigitalBrain imeanza kurusha vipindi vyake vya radio kupitia kwenye mtandao live.
Akizungumza na Sayuni , mkurugenzi wa ufundi wa kampuni hiyo Bw. Marco Salimu amesema kuwa wameamua kurusha vipindi hivyo vya radio kwenye mtadao ambavyo hurushwa na radio Wapo FM ya jijini Dar es Salaam ili kuwapa fursa wasikilizaji walioko maeneo kusikofikika na mawimbi ya radio hiyo kuweza kupata elimu hiyo inayotolewa na wataalamu wa kampuni hiyo.
DigitalBrain ni kampuni ya wazawa inayojihusisha na maswala ya ICT iliyojizolewa umaarufu mkubwa miongoni mwa jamii kwa hivi sasa kutokana na kipindi hicho.Kipindi hicho hurushwa na radio hiyo kila siku ya jumatatu saa mbili kamili usiku hadi saa tatu kamili.
Waweza kusikiliza matangazo hayo hapa kwenye link hii www.digitalbraintz.com

Mungu awabariki DigitalBrain kwa kazi njema.

Tuesday, January 6, 2009

Every action you take is a seed you sow, and every seed you sow is a harvest you'll reap

Every action you take is a seed you sow, and every seed you sow is a harvest you'll reap.

Have you ever had a thought like this: "Nobody would ever notice"? Or this: "It's just a little thing"? But to God, every action -- big or small -- is important, because every action you take is a seed you sow.

For example, say that you tell your boss you worked eight hours when really you only worked six. But on the other hand, it's only two hours, and "nobody will ever notice." However, you're sowing seeds of dishonesty in your life that will reap a harvest of the very same thing.
Do not be deceived: God cannot be mocked. A man reaps what he sows. The one who sows to please his sinful nature, from that nature will reap destruction; the one who sows to please the Spirit, from the Spirit will reap eternal life. (
Galatians 6:7-8) Don't think that you can lie to someone (i.e. sow a seed of dishonesty), but yet expect to reap a harvest of truth in your life.
Proverbs 22:8 warns that He who sows wickedness reaps trouble.

Therefore, be very careful about how you act in every area of life, because every action you take is a seed you sow, and every seed you sow is a harvest you'll reap.

God Bless you as you put this into actions.
If you want to receive weekly wisdoms in your email go to
www.lema.or.tz and click "Mailing Lists to join"

pray for the persecuted church


Thank you for joining with us as we pray for the persecuted church around the world. "Confess your trespasses to one another, and pray for one another, that you may be healed. The effective, fervent prayer of a righteous man avails much." -James 5:16


VOM Prayer Update for December 30, 2008On Wed. Dec 31 2008 at 07:59 AM Moderator wrote: CHINA - 40 Christian Leaders Detained, 16 Sentenced to Administrative Detention - China Aid AssociationOn Dec. 16, 40 pastors and house church leaders were detained at a Christian leaders gathering in Taoling village, Henan province, according to China Aid Association. Officials told the Christian leaders they needed to pay between a 1,000 to 2,00 yuan fine (US $11.20-$22.40). Some of the Christians were released after paying the fine. However, 16 leaders were sentenced to 10 to 15 days administrative detention for engaging in an "illegal religious gathering." Mr. Yan Linshan, the host of the meeting, received 10 days of administrative detention and a 1,000 yuan fine. Pray for the imprisoned Christian leaders. Ask God to encourage them and their families during this difficult time. Pray God protects Christians in China and for them to forgive their persecutors.Psalm 27:1

INDIA

- Hindu Extremists Attack Christians in Karnataka - Compass Direct NewsOn Dec. 14, Hindu extremists from the Bajrang Dal group attacked a Christmas program organized by the Helping Hands organization and accused the director of forcible conversion. Extremists disrupted the program which helps rural women and children, accusing Samuel Moses of trying to forcibly convert women and children. The extremists burned gospel literature and took Moses and his accountant to the Bangarapet police station. The Christians were detained in the police station for about nine hours, with the incident publicized on local broadcast and print media. The Christians were later released without charges. Police Inspector Chinnana Swami told Compass Direct that the Christians were detained for questioning, but police found no forcible conversion and the case has been closed. Praise God the Christians were released. Ask God to protect Christians in India who face intimidation and sometimes imprisonment because of their faith in Christ.Romans 8:31

VIETNAM

- Authorities Destroy Church Building - Compass Direct NewsOn Dec. 17, local government officials destroyed a new wooden church building built by Hmong Christians in Cu Hat village, Dak Lak province, Compass Direct News reported. A large contingent of government officials, police and demolition workers arrived at the church in the morning and destroyed it. Police with electric cattle prods beat hundreds of distraught Christians who rushed to the site to protect the building. Five people were injured in the atack, including a child who suffered a broken arm and a woman who was poked in the stomach with a cattle prod. Pray for those injured in this attack. Pray believers will be able to rebuild the church building.Romans 8:11

MWIMBAJI WA INJILI FANUEL SEDEKIA KATUTOKA. HABARI ZA KUSIKITISHA ZIMEINGIA SASA HIVI KWAMBA MWIMBAJI MAHIRI WA NYIMBO ZA INJILI, FANUEL SEDEKIA, AMEFARIKI DUNIA JANA KATIKA HOSPITALI YA PORIYA TIBERIA, HUKO ISRAEL.
HABARI ZINASEMA MAREHEMU ALIKUWA AMELAZWA KWA WIKI TATU HOSPITALI HAPO AKISUMBULIWA NA KISUKARI PAMOJA NA NIMONIA. ALIKUWA HUKO KATIKA MSAFARA WA MAHUBIRI NA MCHUNGAJI MWAKASEGE.

MIPANGO YA KUULETA MWILI WAKE NYUMBANI KWA MAZISHI UNAFANYWA NA TUTAENDELEA KUWAFAHAMISHA HABARI ZINAPOTUJIA. KWA SASA KINACHOFAHAMIKA NI KWAMBA MSIBA UTAKUWA NYUMBANI KWAKE ARUSHA NA ATAKAPOZIKIWA BADO HAIJAJULIKANA KWANI YEYE KWAO NI KIGOMA.
BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA...JINA LA BWANA LIBARIKIWE..
source: swahilitime.blogspot.com