Thursday, July 31, 2008

mazishi ya wangwe yaahirishwa kwa ghasia








Mazishi ya Mh. Chacha Wangwe, aliyekuwa Mbunge wa Tarime aliyefariki dunia kwa ajali ya gari majuzi huko Dodoma, yameshindwa kufanyika leo kijijini kwake Kamokorere baada ya kufumuka kwa vurugu kubwa ambapo wabunge na viongozi wa serikali na vyama vya siasa walohudhurian ilibidi watoke bomba kusalimisha maisha yao.
Vurugu hiyo ilianza dakika chache baada ya kuwasili kilioni hapo kwa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Mh. Freeman Mbowe, katika kijiji cha Kemokorere kiasi cha kilomita 20 hivi toka mjini Tarime.
Hali ilipokuwa mbaya, ilibidi Mh. Mbowe na viongozi wote waliohudhuria mazishini waondolewe kilioni chini ya ulinzi mkali wa FFU ukiongozwa na Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Mara Afande Leberatus Barlow ambao walifanya kazi ya ziada kuepusha balaa.
Viongozi wengine waliohudhuria walikuwa ni pamoja na wenyeviti wa vyama vya upinzani Profesa Ibrahim Lipumba (CUF), Augustino Lyatonga Mrema (TLP), John Cheyo (UDP) James Mbatia (NCCR-Mageuzi) na Mbunge wa Karatu Mh. Wilbroad Slaa pamoja na kiongozi wa upinzani bungeni, Mh. Hamad Rashid.
Wote hao walisindikizwa chini ya ulinzi mkali wa FFU kuondoka mahali hapo na kuelekea Musoma. Waziri wa Kilimo na Umwagiliaji, Mh. Steven Wassira, na Manaibu Mawaziri ambao ni wabunge wa Kanda ya Ziwa, Dr. James Wanyacha na Gaudensia Kabaka nao ilibidi waondoke.
Ujumbe toka Kenya ulioongozwa na Dr Wilfred Machage ambaye ni mbunge wa jimbo la Kurya na pia Naibu Waziri katika serikali ya mseto ya Kenya pamoja na wakuu wa wilaya wawili nao walikuwepo na ilibidi waondoke kwa kuruka ukuta.
Tofauti na walivyoingia, itifaki haikuweza kufuata kama walipowasili wabunge 20 wakiongozwa na mbunge wa Bumburi Mh. William Lukindo vurugu hilo lilipoanza na ilibidi kila mmoja aondoke chini ya ulinzi mkali.
Maelfu ya waombolezaji, wengi wao wakiwa vijana waliobeba mabango yenye ujumbe mbalimbali unaohoji kifo cha Mh. Wangwe, walitawala hapo kilioni. Juhudi za Mkuu wa mkoa wa Mara Mh. Issa Machibya kuwatuliza hazikuzaa matunda.
Hata juhudi za kututuliza ghasia hizo za Wah. Zitto Kabwe na mmoja wa wanafamilia waandamizi kama vile Profesa Samwel Wangwe na Mkuu wa zamani wa Halmashauri ya Tarime Mh. Peter Wangwe pia hazikuambulia kitu.
Prof Wangwe aliwaambia waombolezaji hao wenye hasira kwamba familia ya Wangwe imeamua kumtafuta mtaalamu huru kuifanyia upya uchunguzi maiti ya hayati Chacha Wangwe ili kubaini alifariki kwa njia ipi.
Wengi ya waombolezaji wanatuhumu kwamba Mh. Wangwe hakufa kwa ajali ya gari. Mtu moja aliyekuwa na marehemu wakati wa ajali, Bw. Mallya, anahojiwa na polisi na uchunguzi wa kina unaendelea.

Source: www.michuzi-blog.com



Wednesday, July 30, 2008

Shuhuda.. Shuhuda.. Shuhuda...!

SAVED FROM SUICIDE


When I was 15 years old I became very depressed and unhappy with my life. My parents had divorced when I was 12 and my mom had gotten remarried to a man that had 3 children which lived with us. The marriage only lasted a year and they got a divorce. After this it was just my mom, me and my sister.
My mom had started dating and went out on the weekends. I would usually go out with my friends. I really didn't have a reason to commit suicide now that I think back on what led me to make that decision. I wasn't as popular as I wanted to be and my best friend was becoming popular and getting all the attention from the guys. She had a boyfriend and I didn't. I had started smoking and drinking. This made me more depressed.
On the day I decided to commit suicide, I had been out with my friend. I had a terrible time and started thinking about suicide. We had met these two guys that we knew while we were out and they said they would take us home. We had all been drinking that night but I didn't know the guy that was driving was as drunk as he was. On the way home, I was thinking about how I would commit suicide once I got home.
My mom had always had problems with her kidneys and she had all kinds of prescription medicine in the cabinet. I decided I would take all the pills in the cabinet. Everything that was in the cabinet I would put on the kitchen table and sit down and start taking pills until I passed out. By the time it was morning and my mom got up, I would be dead.We were just a few miles from home when the driver ran off the road. It had started raining and I guess he must have been driving faster than I realized. The last words I remember being spoken were his friend saying, "Hey man, Get back on the road." The driver must have jerked the truck back on the road because the next thing I remember we were flying through the air.
The truck had hit a row of poles that someone had put up in their yard. The poles were just a few feet high and this caused the truck to go up in the air and flip over. I remember my friend grabbing hold of the steering wheel and saying "Oh my God." I thought to myself maybe I will die in this wreck and then I won't have to go home and take all those pills. This would be easier. It seemed like everything happened in slow motion. I put my hands together and bowed my head and said "Please God don't let this hurt."The next thing I remember was waking up thinking I was at home in my bed and I was waking up from a dream. I suddenly began to remember what had happened. I had been in a wreck. Everything was pitch black dark and I couldn't see. I tried to move but I couldn't. I felt a horrifying fear come over me. I must be dead. I tried harder to get out of the darkness but I couldn't and I became more and more afraid.
Words cannot begin to describe how terrified I was when I realized I must be dead. I had wanted to die and now I had my wish. I didn't want to be dead if this was what it was like. I couldn't see or move; I was just lying there in total darkness with overwhelming fear and loneliness.
I began to call out to God. "Please God don't let me be dead. I promise to stop smoking and drinking and I will quit thinking about committing suicide." As I prayed to God, he quickly came and brought me out of the darkness. I began to crawl out from underneath the truck and I saw my friends standing there.We had landed upside down in front of someone's house. They called the ambulance and I was taken to the hospital. It was a miracle that I wasn't dead. My head was split wide open to the bone and I had broken my back. I was lucky to be alive.
Statistics say that someone thinking about committing suicide will usually not tell anyone. This is why when they do commit suicide, everyone is so shocked. They didn't know that the person was so depressed. When I decided to commit suicide, I didn't tell anyone, not even my best friend. The only one that knew my thoughts and what I was planning to do was God.
If I hadn't got into that wreck, I would have committed suicide and probably would have died but God didn't let me. He saved me but when I was lying there in that terrifying darkness, I think he was showing me of what it would be like if I had committed suicide. I would have went to hell. I don't know till this day where I was at, maybe it was the gates of hell and that is why I felt so horrified. All I know is I never want to go back there again!I urge anyone thinking of suicide to seek help. Trust me you do not want to experience what I did. I am just so thankful that God saved me and didn't let me die. I am grown now and I have two kids and a wonderful husband. My life has been full of trials but God has always been there for me even when I didn't know it.



Dear Reader - are you at peace with God? If not, you can be. Do you know what awaits you when you die? You can have the assurance from the Holy Spirit that heaven will be your home, if you would like to be certain. Either Jesus Christ died for yours sins, or He didn't (He did!). Are you prepared to stand before God on the Judgment Day and tell Him that you didn't need the shed blood of Jesus Christ on the Cross to cover your sins? We plead with you ... please don't make such a tragic mistake

Ushuhuda..Ushuhuda...Ushuhuda...!

Kama nilivyowaahidi watumishi kuwa tutakuwa tunawaletea mbalimbali za matendo makuu ya Mungu anayotenda kwetu sisi watumwa wake..
Wapendwa,
Bwana YESU asifiwe sana!!!! Jina langu ninaitwa Prudence, nimeona ni vema ku share ushuhuda huu wa matendo makuu ya MUNGU kwangu na kwa familia yangu kwa ujumla. Sisi sote ni shuhuda wa matendo makuu ambayo MUNGU hututendea kila kuitwapo leo, pumzi ya uhai, afya njema, chakula na baraka nyingine nyingi. Mimi nimemwona MUNGU zaidi ya hapo. Mwaka 2006 tarehe 12 mwezi Februari, gari letu aina ya Suzuki ESCUDO 5 doors, iligongwa vibaya sana na FUSO hapo Morogoro maeneo ya Mkambarani karibu na Mikese Polixce station.
Ninawaambia wapendwa gari lile liligongwa vibaya sana upande ule wa dereva, nilishuhudia kwa macho yangu ya nyama jinsi dereva alivyo vyunjwavyunjwa miguu na maeneo mengi ya mwili wake. Aliumizwa kichwa na kwa hakika aliumia sana, kiasi kwamba hakuweza kuishi zaidi ya saa moja tangu tupate ajali. Kijana MOSES, ambaye alikuwa dereva, alifariki DUNIA katika hospital ya MOROGORO. Inaniuma sana.
Kwa upande wangu mimi, nilivunjika mkono wa kulia na mikwaruzo michache sehemu za tumboni. Sikuumia sehemu nyingine yoyote na mkono hauna madhara tena ninautumia kama kawaida na huwezi jua kama uliwahi kuvunjika. Wapendwa hebu angalieni wenyewe hizo picha halafu mniambie kama si MUNGU aliye niokoa ni nani hasa??? Nina mshangaa MUNGU, nina muogopa na ninamheshimu. MUNGU anaweza yote, hata pale unapoona imeshindikana kwa akili za kibinadamu yeye bado anaweza.!!!!!!!!!!!!!!!!!
Mimi na familia yangu tumemwona BWANA YESU!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
shuhuda
Kama unao ushuhuda na unapenda kushirikisha wapendwa wengine mahali hapa katika mlima huu wa sayuni , usisite kuniandikia kwa email: miwlc@yahoo.com

Sunday, July 27, 2008

Be A Faithful Operator.--Lema Mailing Lists

Be A Faithful Operator.--Pray!
A prayer is just like a telephone call. When the Lord puts the thought in your mind about a certain person, that's a message from God. He's putting in a phone call to you, & He wants you to be the operator to connect the call to the person He wants to reach.
God initiates the call! Then you are like the telephone operator, & you have to transfer the call. God plugs the call in & if you are willing to plug it out, you can reach whoever He's trying to help. Your faith is the hand that flips the switch so they can receive God's message! You are the link between God & them, so if you fail to pass the call on, they will never get the message!
Of course, the person on the other end of the line has to pick up the phone when it rings & they have to listen & receive the call. You can't make them receive it, you can't make them pick up the phone. That's their responsibility! There are all kinds of reasons why you, as the operator, sometimes can't get through, but you have to keep trying!
Please pray! You're the Operator. It's your responsibility to pass on the message. Please don't fail!--Or someone will miss God's important call!
Hopeful you are blessed by these devotions,please invite others to join this mailing list by going to
www.lema.or.tz and selecting "Mailing Lists"

Frank Lema

Thursday, July 24, 2008

Pambio la Leo

Kiongozi wa sifa: Hakunaaa...X 3
Kama weweeee...
Hakunaaa...X 3
Kama weweeee...
Wote:Hakunaaa...X 3
Kama weweeee...
Hakunaaa...X 3
Kama weweeee...


Rudia rudia hadi upako ushuke then anza kuomba....
Ubarikiwe

Tuesday, July 22, 2008

VITA YA KIDINI UKRISTO NA UYAHUDI, ISRAELI.

Hii ni habari ambayo inaweza kumshangaza kila mmoja asikiaye na kuisoma. Lakini ndo ukweli halisi kwamba hata sasa Ukristo (Christianity) na dini ya kiyahudi ni vitu viwili visivyofungamana.

Wayahudi kupitia vipeperushi vinavyoweka kwenye magari, nguzo za simu na maeneo mbalimbali ya matangazo wamekuwa wakiupiga vita ukristo ndani ya nchi yao. Kwao ukristo ni sawa na imani potofu. Vipeperushi hivyo vimekuwa vikisomeka katika hali ya kuwatahadharisha watu kutokana na wale wenye jitihada za kuuneza ukristo: "Beware! These are the members of the Jewish Missionary Cult. They are baptizing Jews into Christianity." Ndani ya Israel nchi ambayo wengi tungetaraji iwe na wakristo wengi, lakini wakristo ni kati ya 6,000 na 15,000 tu.

Wengi tungelitaraji kwamba Israeli iunge mkono Ukristo lakini sivyo. Na hii yote ni kutimizwa kwa maandiko kwamba hata sasa kwao Masihi bado hajafunuliwa na wanamtarajia Masihi mwingine wakati ukweli ni kwamba Yesu Kristo alikwisha kuja nao wakamkataa ikiwa ni pamoja na kumsulibisha.
Waenda kwa miguu wakipita kando ya ukuta wa mji mkongwe wa Jeriusalemu.

Habari za hivi karibuni zinaonesha kwamba mchungaji mmoja David Ortiz, kutoka maeneo ya Ariel, Israeli na ambaye yuko mstari wa mbele kueneza injili alitegeshewa bomu la kutengenezwa kwa mkono kwa mfano wa kifurushi cha zawadi na ambalo lilimjeruhi vibaya mtoto wake baada ya kulitegua wakati akitoa chocolate.

Wengi wa wapinzani wakiwamo waalimu wa dini ya kiyahudi na kanisa la ORTHODOX wanasimamia vigezo kwamba kuruhusu kusambaa kwa Ukristo ni kutimiza unabii na kumfanya Kristo aje mapema.

Mstahiki meya wa mji wa Or Yehuda, mji ulio karibu na Tel Aviv aliamuru kukusanya na kuchoma biblia zote za agano jipya baada ya kuwaona wakristo (”Messianic Jews” kama wajulikanavyo huko) wakigawa biblia kwa wayahaudi wenye asili ya Ethiopia (KUSHI). Mambo hayo ya kunyanyaswa kwa wakristo yanafanyika pia katika miji mingine mingi tu ndani ya Isreali.

Israel na uongozi mzima wa nchi hiyo umejikuta katika hali ya kukanganya kwani kwa upande mmoja imekuwa mstari wa mbele kukaribisha mahujaji wa kikristo kutoka maeneo mbalimbali ya dunia na kwa wakati huohuo ikishuhudia ugandamizaji mkubwa wa haki za binadamu – wakristo kunyanyaswa ndani ya nchi hiyo. Naam pia imekuwa mstari wa mbele katika kujaribu kupinga wamisionari kueneza injili ya Kristo ndani ya israeli.

Inasikitisha kuona taifa hili ambalo ni chanzo cha wakristo wengi duniani kuwa katika hali ya namna hiyo. Na tuendelee kuwaombea wale wachache walioamua kuyatoa maisha yao kwa Kristo ndani ya nchi hiyo ili Kristo ajapo waende nae. Kweli wanatakiwa kusimama maana mazingira yao ni magumu kwani hakuna adui aliye mbaya kama wa nyumbani mwako.

JE! WAFAHAMU KWAMBA WAISRAELI WAISHIO MAREKANI NI KARIBU SAWA NA WALIOKO ISRAEL KWENYEWE?

Kulingana na takwimu zilizotolewa mwaka huu na idara ya takwimu ya Israel (Central Bureau of statistics-CBS), kwenye sherehe za kutimiza miaka sitini ya uhuru wa nchi hiyo,Israel ina jumla ya watu 7,282,000. Kati ya hao 5,499,000 (75.5%) ni Wayahudi, 1,461,000 (20.1%) waarabu na 322,000 (4.4%) wengineo.

Pamoja na idadi hiyo, taifa hili ambalo lilianzishwa na watu kiasi cha 806,000 mwaka 1948 kwa sasa limekuwa kwa kiasi kikubwa na ni taifa ambalo historia yake na habari zinasomwa na kusikika karibu duniani kote kila siku.

Pamoja na kuwa na idadi hiyo ndani ya nchi ijulikanayo kama Israel bado wengi wa wayahudi wanaishi nje ya nchi hiyo. Marekani ni nchi inayoongoza kwa kuwa na wayahudi wengi kwa karibu sawa na wale walio ndani ya Israel kwenyewe. Kama takwimu zinavyoonesha: Marekani 5,275,000 (40.3% ya wayahudi wote duniani), Ufaransa 491,500 (3.8%), Canada 373,500 (2.9%) na nchi nyinginezo nyingi. Kwa takwimu hizo inaonesha kwamba bado wayahudi wengi wanaishi katika utawanyiko.

Wataalamu wa maandiko katika hili mnasemaje? Je kuja kwa Kristo ni mpaka Israeli wote warejee kwao au ishara kubwa ni ile ya habari njema kuhubiriwa ulimwenguni pote kama inenavyo mathayo 24 na sura nyinginezo za kinabii au?

Friday, July 18, 2008

Bwana asifiwe...

Tangu tutangaze maombezi kupitia mlima huu wa sayuni watu wengi wamekuwa wakituma maombi yao na wengi wamekuwa wakipokea mahitaji yao kupitia mlima huu.
Wadau wengi wamekuwa wakiniomba wawe wananipigia simu direct katika namba yangu badala ya utaratibu uliokuwepo wa kunitumia sms tu.Kwa hivi sasa ninaomba wadau muwe huru kunipigia tu katika namba yangu ya +255-713-427857 .
Pia kwa wale wanaopenda kuchat na mimi au watumishi wengine wa sayuni waweza kutuadd na katika yahoo messenger yako kwa kutumia email zetu hapa chini kama ifuatavyo.
Mtade : miwlc@yahoo.com
Maranatha: chalujohn@yahoo.com
SavedLema: savedlema@yahoo.com

Tumeamua kutumia utaratibu huu wa kuchat ili kupunguza gharama za simu hasa zile za nje ya nchi na zile ambazo si za line ya tigo ambayo ni rahisi zaidi kupiga kwa hapa Tanzania.

Mungu awabariki sana.

Wimbo wa kuabudu wa leo

Kiongozi wa sifa:Nigusee tenaaa...X 2
Ninaombaaa Babaa....uniguseeee tenaaa...
Niguseeee......
Wote:Nigusee tenaaa...X 2
Ninaombaaa Babaa....uniguseeee tenaaa...
Niguseeee......


Rudia rudia pambio hilo la kuabudu ukisikia upako umeshuka anza kububujika katika Roho na Bwana atakutana na mahitaji yako

Tuesday, July 15, 2008

BREAKING NEWS

ALIYEKUA MUIMBAJI WA INJILI NA HABARI ZAKE KUANDIKWA KUTOKA VYOMBO VYA HABARI KUWA NI MGONJWA, DEBORA SHABAN AMEFARIKI SIKU YA IJUMAA TAREHE 11, MSIBA UKO MAGOMENI MIKUMI NA ATAZIKWA SIKU YA JUMATATU TAREHE 14 JULAI. MUNGU AWE FARAJA KWA WAPENDWA WOTE.


Source: http://strictlygospel.wordpress.com

Mtikila na milioni 3 za Rostam Aziz

Mchungaji wa Kanisa la Wokovu Kamili, Christopher Mtikila, amesema atamfungulia kesi mahakamani Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz. Alidai mashitaka hayo yatakuwa ni pamoja na ya kughushi saini katika stakabadhi ya malipo anayodai alilipwa kama mkopo na si sadaka au mchango wa Kanisa kama inavyodaiwa. Wakati Mtikila akiyasema hayo, suala la Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kutangaza kutotambua mchango alioutoa Rostam alipoalikwa kwenye uzinduzi wa kwaya, limeleta changamoto mpya baada ya baadhi ya taasisi za dini kutaka zipewe namba ya mbunge huyo ili zimwalike azichangie fedha.
Mmoja wa Wainjilisti kutoka Huduma ya Biblia ni Jibu kutoka Morogoro, Damian Ndimbo aliomba apewe namba ya simu ya Rostam kwa lengo la kumpigia na kumwomba aipatie msaada wa kifedha taasisi yake. “….Mbunge Rostam Aziz kuchangia kanisa yupo sahihi, kwani kanisa limesababisha hayo yote na kama mna namba yake mnitumie aje asaidie na huduma yetu,” alisema Ndimbo kwa njia ya simu. Aliongeza, “Wakristo wenye fedha wako wengi lakini hawachangii kanisani wala kusaidia, kazi yao ni kuchangia mambo ya ajabu kama pombe, lakini huyu Rostam amejitolea, tunaomba namba yake atusaidie na sisi huku Morogoro.” Mtikila, akizungumza na na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, aliibua masuala ya uraia na kusema kuwa miongoni mwa kesi atakazofungua ni pamoja na kuhoji uraia wa mbunge huyo. Mtikila, ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Democratic (DP), alisisitiza jana kuwa Sh milioni tatu alizopokea kutoka kwa Rostam zilikuwa za mkopo na kwamba atamrudishia. “Mimi nitazirudisha hizo fedha na akizikataa ina maana nizitafune, na mimi nina meno 32 kama binadamu wengine nitazitafuna,” alisema. Akirejea kwenye Biblia, Mtikila alisema huo ulikuwa mkopo kama ambavyo Mungu alivyomtumia Farao kugharamia maandalizi ya Musa na kwamba na yeye aliutumia katika maandalizi ya kuwashtaki waliofilisi nchi na kuwafanyia utafiti. Alisema alipochukua mkopo yeye ndiye aliyesisitiza asainishwe akiwa na uhakika wa kuurudisha, kwa kuwa mkopo ni kama biashara hivyo hauna dhambi na unachukuliwa kwa mtu yeyote ili mradi masharti yasiwe mabaya. Mtikila alisema kila stakabadhi halali ya malipo inatakiwa iwe na jina kamili la mlipwaji, maelezo sahihi ya sababu za malipo, tarehe ya malipo, saini ya mlipaji na mlipwaji na namba na mhasibu hawezi kugonga mhuri kama stakabadhi hiyo haina namba kwa kuwa itakuwa ni malipo hewa. “Na huyu aliyesaini stakabadhi hii aanze kutroti kwenda Keko”. Alidai Rostam ametumia stakabadhi hiyo kwa ajili ya kujisafisha kwa kuitumia KKKT na kwamba yote aliyofanya ni halali. Alisema hata makanisa ambayo mbunge huyo anadai kuwa alishayachangia tangu awali, yalipokea fedha hizo za sadaka kabla ya Rostam hajatuhumiwa kuhusika na masuala ya Richmond na EPA. Pia alimtaka mbunge huyo naye kwenda mahakamani kama anaona anaonewa au kuchafuliwa kufuatia kauli zinazotolewa dhidi yake kuhusu mwaliko wake na kauli zake alizozitoa hivi karibuni katika KKKT, Usharika wa Kinondoni
Source: Habari leo;Globalpublishers

Nyimbo za Injili

Jina la wimbo: Mbele ninaendelea...


Mbele ninaendeleaa...
Ninazidi kuteembeaa..
Maombi uuuyasikieeeee...
EeBwanaa uunipaandisheeee... (eeBwanaaa...)


(Korus..)


EeBwanaa uuuniiinueeeee.....
Kwa imaniii...nisimameee...
Nipande miiiilimaa yoteee...
EeBwana uuunipanisheeeee....


Nisikaeee duniaaniiii...
Ni mahaliii pa sheetaniiii..
Natazamiiiiaaaa mbinguniiiiii...
Nitafika kwaa iiiimanii.... (eeBwanaaa...)


(Rudia Korus..)


Nataka niiipanishweee juuu...
Zaidi ya yaleee maaawinguuuuu...
Nitaombaaa nifikishweee....
EeBwanaaa uuunipanisheeee... (eeBwanaa....)


(Rudia Korus..)


Sina tamaaa nikaeeee...
Mahali paaaa shakaaaa kamweee....
Hapo wengiiii wanakaaaa....
kuendeleeeaaa naaaombaaaa...(eeBwanaaa...)

(Rudia Korus..)

Rudia rudia kuimba hadi upako ushuke ...ukiona unaanza kububujika ingia kwenye maombi na ikibidi anza kunena kwa lugha kama umejazwa na Roho Mtakatifu na mwambie Bwana akutane na mahitaji yako yote kwamba mwezi huu usipite kabla hujapokea majibu yako....

Monday, July 14, 2008

KIZUNGUMKUTI BAINA YA ROSTAM AZIZ (MB) NA K.K.K.T.

Haya maoni nimeyapata kwa mtu fulani nami nimeona niyaweke hapa kuhusu sakata la Rostam Azizi (mb) na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (K.K.K.T.). Japo ni marefu lakini huyu mtu ana ujumbe mzito ndani yake.
Mh. Rostam Aziz akizungumza na waandishi wa habari kwenye Hoteli ya Kilimanjaro Kempsinki Jijini Dar.

Kama mtanzania awaye yeyote, nimezopekea taarifa za KKT vs Rostam kwa mtazamo wangu pia. Najua kila mtu anamtazamo wake wa kuwaz na kufikiri jinsi ya hali halisi ya mambo yalivyo.Kila kukicha neno fisadi ni neno la kawaida kabisa na tumekuwa wepesi kufuatilia habari zake usiku na mchana, sina shaka mchango wa vyombo vya habari katujuvya swala hili umetukuka. Sitashangaa pia kuona hata wasanii mbalimbali kuiliimbia hili kukubaliana kuwa awa ni adui wa taifa letu na binadamu mwingine yeyote hapa duniani.

Niliposoma habari ya Rostam kwenda kanisani kama mgeni rasmi sikushtushwa na Kusikia hivyo, hila nilishtushwa na ujasiri, shutuma zikikulemea unaweza pata magonjwa ya moyo,na simanzi nzito. Nakumbuka pale ambapo tulipokuwa watoto na tunamwimbia mtoto aliyekojoa ‘’kikojozi kakojoa na nguo kaitia moto’’ tunamalizia kindumbwendumbwe chalia..Zamani ulikuwa unazungushwa mtaani huku mzazi au mlezi wako akihakikisha unazomewa hili usirudie tena. Naona hawa mafisadi wako hivyo! Lakini kinyume na mtoto kikojozi ambaye anatembea na aidha godoro lilolowa mkojo au nguo zake. Mafisadi hawana alama yoyote ya kutuonyesha kuwa ni mafisadi..Nikitafakari kwa kina swala la KKT, ufisadi na mafisadi serikali na wananchi.Adhabu wanayopata tunaowaita mafisadi haitoshi na haiwastahili, kwa sababu na sisi hatustahili kuwahukumu jinsi inavyowastahili wahukumiwe.

KKT wanaelewa vyema tabia mbaya ya baadhi ya watanzania kujichukulia hatua mkononi ya kuchoma vibaka au wezi huku mitaani mwetu. Sio siri watanzania wengi wasio na hatia wamepoteza maisha yao. Serikali, makanisa , asasi mbali mbali za kijamii zimepiga kelele kuhusu swala hili.Na kwasababu ni tabia iliyojengeka kwa kufikiri polisi hawafanyi kazi vizuri basi wananchi ikiwemo KKT sasa inachukua hatua mkononi.Sio siri, KKT kutoa tamko la kumkataa Rostam kwa kisingizio wako mbele kwenye vita juu ya ufisadi, kwa kumuita mtu fisadi mimi siliungi mkono. walilofanya KKT inaonyesha kuwa wanaunga mkono swala la watu wote wanaoshukiwa wezi wapewe adhabu bila kuwasikiliza. Kwa namna hii,KKT wamekuwa mahakimu, waendesha mashtaka na mashahidi, ila hawajajiweka nafasi ya mtuhumiwa!, wala kuangalia upande wa pili kuwa ni kanisa.

Mtego mkubwa kuliko yote ni pale ambapo KKT inataka ituaminishe kuwa wote wanaoalikwa katika sherehe zao zinazofanana na zile wanakuwa ni watakatifu au hawana madoa yoyote yale. Na pia sitaki kuamini kuwa wote waliowahi kualikwa na watakaoalikwa basi watakuwa watakatifu!. Na kwa namna hii kikanisa tunapata picha ya ajabu ambayo hata Mungu anatushangaa kona dhambi fulani ni kubwa na nyingine ndogo.Tunapofikia kuona mwongo afadhali kuliko muuaji tunahalalisha mambo yasiyofaa kanisani.Kwani vipimo na viwango vya dhambi havipatikani katika biblia ambayo KKT wanayoitumia hakuna dhambi kubwa wala ndogo.Kwa uongo wa shetani kwa Adamu na Eva mpaka leo tunakufa!..Ili kuthibitisha kuwa dhambi zote ni sawa hakuna msahafu unaoeleza adhabu tofauti kwa dhambi tofauti.Ilichofanya KKT ni kuhalalisha dhambi zingine, ili mradi kila mmoja kama aonavyo, ndipo pale watu wanaoamini ndoa za jinsia mmoja kwao wataona ni sawa. KKT wao dhambi kubwa ya kumfukuza mtu ni ufisadi. Nasubiri kwa hamu kuona nani ataalikwa na KKT ambapo lenzi zao zitawaonyesha kuwa huyo mtakatifu.

Siamini ninaposikia kuwa kumbe haikuwa mara ya kwanza kwa Rostam Aziz kualikwa katika kanisa hilohilo.Tunataka tujue 2005 wakati Rostam anachangia ujenzi hakuwa fisadi?? (kama mnavyomuita). Na je fedha zilipokelewa ? na je leo mkitambua kuwa fedha zilikuwa za kifisadi ilikuthibitisha mnachukizwa na ufisadi basi kanisa libomolewe! Maana kama hela yake ilinunua sementi, mchanga au maji tusemeje?. Na lisiishie kubomolewa kanisa la KKT kinondoni bali makanisa yote ambayo misingi yake na fedha zake zilitoka kwa wenye dhambi.Maana sitaki kuamini kuwa wanaotoa fedha zisizo halali ni Rostam pekee! Ndipo pale katika tamko la KKT sijaona wakisema watarudisha fedha! Inabidi kuweka mashine kwenye chombo cha sadaka ambacho kitazikataa hela zisizo halali!

Tamko la kanisa linachanganya zaidi pale linapoamua kupinga ujio wa Rostam kwa sababu ya presha za wananchi juu ya ufisadi.Hii kwa KKT ni udhaifu, ni udhaifu wa ajabu kutoa maamuzi kwa sababu ya presha ya watu fulani wenye malengo mazuri ila bila mbinu nzuri juu ya ufisadi. vikitokea vikundi vya watu fulani vikawapa presha KKKT wapitishe ndoa za mashoga watakubali?. Je haikutosha kusema Rostam hatujafurahishwa na aliyoyazungumza, bila kuondoa dhana ya kuwa kanisa ni la kila mtu.Maana tunavyomwona sisi Rostam sivyo Mungu anayomwona! Kanisa inabidi lijifunze jinsi ya kujibu bila kuondoa dhana nzima ya ukristo.

Paulo mtume alikuwa muuaji! Daudi alizaa na mke wa mtu cha ajabu mtoto wa nje ndiye aliyejenga hekalu, Rahabu alikuwa kahaba ! akamzaa Boazi(Mathayo 1:5) ambapo tunapata ukoo wa Yesu!.Msingi mkubwa wa Yesu ni kuwafanya watu watoke katika hali zao za dhambi, kwa sababu wote tumefanya dhambi na tumeshindwa kuishinda dhambi tufikie hatua ya kuishinda dhambi(Ufunuo 12:11). Kwa maana dhambi haitawatawala ninyi,kwa sababu hamwi chini ya sheria, bali chini ya neema(Rumi 6:14).Na kwa sababu mpango wa Mungu hataki mtu apotee, Yesu hakusita kukutana na Zakayo mtoza ushuru maana huyu alikuwa fisadi mwingine wa kipindi hicho.Zakayo kwa kukutana na Yesu alishawishika kurudisha mara nne ya mali alizozifisadi, na zingine akawagawia maskini(Luka 19).Lakini cha ajabu Yesu alipohuzunishwa na mambo ya biashara mahekaluni hakusubiri vyama vya upinzani, wala asasi mbalimbali yeye mwenyewe aliingia na kuwafukuza wote waliofanya biashara ndani ya hekalu! Hapa ndipo tunapomwona Yesu katika upeo wa kitofauti.Hakumbagua mtu kutokana na hali zao.Ilipofika swala la kodi aliwaeleza ya Mungu mpeni Mungu ya kaisari mpe kaisari!.Katika dhana nzima hii ya Yesu na mpango wake naona kanisa liko mbali kabisa!.Kwa hiyo tamko la kanisa lilitakiwa kutokukiuka misingi ya kanisa lakini bila kuondoa vita ya ufisadi.Hapa ndipo KKT walitakiwa wakae chini na kuwaza sana.Tukiuliza ni viongozi wangapi wa KKT ambao kwa nyazfa zao walienda kwa watuhumiwa wa ufisadi angalau kuwahubiria injili.Je kumualika kwenye sherehe kama hiyo pengine kungetoa nafasi kama hiyo?.Paulo anasema ni muhimu kuchangamana na watu fulani ili kuwapata hao watu!.Kuwatenga na kutoa matamko makalikamwe hakutoi nafasi ya watu hao kubadilika.Je Rostam hapaswi kuhubiriwa?

Nachanganyikiwa zaidi pale ninapofikiri kumuita Rostam aje kuzungumza kwenye hafla ya kikristo mlitaka aongee nini??Marko? Luka?Mathayo?? Basi angeandaliwa hotuba ili aisome!Kwa maana nyingine asingesema aliyosema bado angeandamwa na watu kuwa hajasema lolote!.Pia angekaa kimya angekuwa mnafiki wa nafsi yake,watu wamekualika na kila siku unaandikwa kwenye vyombo vya habari bado ukae kimya kama hamna kitu kinachoendelea!.Yeye kisaikolojia anaumizwa na hali hii iwe kweli au si kweli. Au waliomualika ni wanafiki hawamjui Rostam??.Rostam hajawa mbaya kiasi hicho. Watanzania wengi wanataka mtu aseme ndio wafurahi!.Alilosema Rostam kama mimi ningesema amefikia pazuri(mtazamo wa kikanisa).Pale aliposema watoto wake anataka walelewe kwenye misingi mizuri ya dini hapa ni ‘’ushindi’’ wa kikanisa swala je wataenda wapi? Sio siri kiroho zaidi Roho ya Rostam ingeweza kuokolewa kama mpaka ana uwezo wa kufika kanisani lakini mmepoteza na kumrejesha sio rahisi. Yesu anasema adhabu yake ni kufungiwa jiwe shingoni atupwe baharini(Mt 18:6). Hivi mlitaka Rostam aseme nini??

Tuna nchi dhaifu kwa sababu makanisa na misikiti yetu ni dhaifu,familia ni dhaifu,kwa sababu tuna akina baba na akina mama dhaifu.Dhana nzima ya dini haifuatwi.wengi yuko dini fulani kwa sababu wazazi walikuwa dini hiyo au mazoea.Hii imepelekea kuwa na wasanii makanisani kuwa na mafisadi wa imani.Kufungisha ndoa za wajawazito, kuingia na nguo zisizo na heshima makanisani, kufanyiana fitina na kupigana makanisani,utapeli kupindisha maneno ya Mungu, hawa wote sio bora kuliko Rostam.Wale walio kwenye ile orodha ya mafisadi wamo makanisani na misikitini mwao, wengine ni vongozi makanisani! Kwa hiyo hao wote wafukuzwe! Hapa naona KKT iko mtegoni..Nilifikiri katika tamko lao watasema kuanzia sasa hakuna kwaya yoyote inayozindua albamu kumualika mtu yeyote kama mgeni rasmi. Hili siliongelei kwa sasa ila nafikiri ni wakati mzuri kwa watu wajiitao wakristo kufikiria swala la kumualika mtu mwenye hela ili atoe pesa za michango.KKT wangeanzia hapo.Maana kama hivyo basi hamna imani na kama haana imani hamumpendezi Mungu!.Amelaaniwa amtegemeaye mwanadamu!!.Nafikiri mkiomba tu kwa imani kanda zitauzika.Hili nalo linathibitisha makanisa yetu mengi ni taasisi za kibiashara na watu kukusanyikia ili wajuane maana kama uko kanisani na huna mpango wa kwenda mbinguni nachelea kusema a ni kupoteza muda na kufuga wezi ,mafisadi hawa wote wametoka makanisani na misikitini.

Kwa sababu ni KKT wametoa tamko hili,afadhali kidogo maana angekuwa ni askofu mkuu wa KKT ingekuwa hatari, naamini anabusara zake na nimjuavyo ni mlokole mzuri. Kwa wadhifa wake anakutana na viongozi wengi, siku anasimikwa walikuwapo viongozi wengi wa serikali wenye tuhuma za ufisadi. Je waliusimika ufisadi? , je asihudhurie wala kuchangamana na hao watu maana kwa kufanya hivi kunamfanya naye kuwa mmoja wa mafisadi? Si kweli. Je angekuwa raisi amehudhuria?KKT ingetoa tamko kama hilo? Mbona naye yumo katika ile orodha ya mafisadi?

Watanzania wengi tunafurahi sana kusikia na kununua habari kuhusu mafisadi. Gazeti ambalo haliandiki habari za mafisadi yanaonekana wasaliti na yale yaandikayo wanaonekana mashujaa, yote yanaweza kuwa sawa kutegemea na nini sisi tunataka, Je nikijua huyu mtu fisadi basi inatosha?? Nikimzuia asiseme popote pale huku wanakula hela walizoiba nimetatua tatizo ? Magazeti hayaandiki habari za kifisadi kama udaku, tatizo wengi wanachukulia habari hizi za ufisadi kama udaku.ukishajua fulani fisadi basi moyo wako unasuuzika! Nadhani kazi ya vyombo vya habari na baadhi ya wapinzani ni kueleza tatizo na kulitatua.Tangu habari za ufisadi zimeanza mpaka leo hatua gani zimechukuliwa? Je Rostam angekuwa jela hao wanakwaya wa amkeni wangempata wapi?. Tatizo ni mamlaka tulizo nazo nani anahusika? akina nani wako TAKUKURU wakristo na waislamu, akina nani mapolisi? Wakristo na waislamu! Mawaziri na wabunge hawa makanisa yao yapo mwezini? Hapana. Sasa tatizo liko wapi?

Nadhani wote tumekutana na mbwa wanaobweka sana, ukitishia unataka kuokota jiwe anakimbia ni kama sisi tulio wengi.Ni hodari sana kusema ufisadi hatuchukui hatua yoyote.Kuna msomi mmoja yeye anataka Rostam akusanye waandishi wa habari awaambie anavyohusika kwenye ufisadi!akikusanya waandishi wa habari na akasema basi mioyo yetu itaridhika kabisa!eti ajibu tuhuma huu mamlaka zilizowekwa kisheria kuweka usalama wa raia na watu wao zipo!.Ukiona nchi ambayo wasomi, wapinzani makanisa hayana chochote cha kufanya isipokuwa kusema ujue nchi hiyo bado sana ukombozi kupatikana, kuna watu wanasema mpaka mitume wote warudi labda tutabadilika.

Wasomi,makanisa,misikiti waliunga mkono CCM na ikashinda kwa asilimia kubwa.Vyama vya siasa vinaongezeka na vinajulikana wiki moja kabla ya uchaguzi ,ukiona watu wanawapokea kwa vigelegele watuhumiwa wa ufisadi huku wengine wakiwatetea, ukiona makanisa yako kimya hayasemi lolote juu ya ufisadi au la wanasema wakati wengine wameshasema! ujue jamii hii ina tatizo.Mapinduzi ya kifikra yanapaswa yafanywe na mtu mmoja mmoja kasha yahamie katika ngazi ya jamii na baadae kufikia hatua jukumu la mwanandamu duniani.Kuzungumza swala la ufisadi bila kuchukua hatua yoyote ni kupoteza muda.

Kila mmoja kwa nafasi yake likiwamo kanisa linapaswa lijiulize mara mbili jinsi tunavyowachagua viongozi wetu kuanzia ngazi ya mjumbe wa nyumba kumi kumi mpaka taifa, sio hapo tu makazini mashuleni, kila mahali viongozi wetu tunawapataje?.KKKT wananichekesha pale wanaposema taratibu hazikufuatwa na kwamba wao ni wakubwa zaidi kiasi kusema waliomualika ni kikundi cha watu fulani.Viongozi wengi makanisani ni miungu watu, hawakosolewei wala hawashauriki. Wanapeana uzee wa kanisa, ushemasi, uaskofu kulingana na fedha za mtu, kazi ya mtu na urafiki na mtu na siyo mtu huyo ana uwezo gani wa kuongoza watuki-Mungu.Si tunakurupuka leo na kutaka mtu fulani ajiuzulu wakati hatujalelewa katika tamaduni hizo, kuanzia ngazi ya familia na kanisa.

Muda umefika wa kubadilisha mifumo yetu,tujiulize je mafisadi wanapaswa wakamatwe na nani? Na je wakikamatwa mahakama zetu zina uwezo wa kuwahukumu? Na je wakienda gerezani hawatatoroswa kwenda nje ya nchi?.Mwakyembe aliposema Rostam na wengine wengi wanahusika , TAKUKURU,polisi na usalama wa taifa walitakiwa wachukue hatua haraka na tungeona matokeo.Tukishaona hivi tujue tunapaswa kuifumua mifumo yote kuanzia ngazi ya rais mpaka balozi wa nyumba kumi kumi.Mapinduzi hayaleti demokrasia , demokrasia inaleta mapinduzi.Tukishafanya mapinduzi kama mifumo bado mibaya bado hatujafanya kitu, Kenya mashahidi wa hili.Ni wakati mzuri wa kupigia kelele swala la katiba, tume za uchaguzi na misingi mingine mingi.. Hili linawezekana kwa sababu tunauwezo wa kupiga kura. Kama tuko tayari tupige kura si kwa kusema fulani nimchanga katika uongozi , maana hata Nyerere hakuwahi kuwa rais kabla ya kuwa rais, tunaangalia uwezo wa mtu,je alifanya nini siku za nyuma na atatufanyia nini.Hapa ndipo ninashawishika kusema hata vyama vyetu vingi vya upinzani bado ni visaliti . Natamani ruzuku isiwepo ili tupate viongozi waliojitoa na kuuza sera zao tutazinunua kwa michango yetu, huu utaratibu wa fedha kutoka serikalini ni kunyong’onyesha upinzani! ama sivyo watu wa aina ya Odinga na Tsavangirai tutawasikia tu.

Maaskofu wa makanisa kaeni chini nendeni kwa rais mkamuulize mafisadi wanachukuliwa hatua gani na mumpe muda, maana mafisadi hawa ni kaka na dada zetu, ni wajomba zetu, watoto wetu, waumini wenu wanacheza nao,hata nyie mnakula nao, Kama vithibitisho vyenu viko sahihi kwa nini hawafunguliwi mashtaka?.Mkishindwa kupata majibu inabidi mkubali hata kuandamana ili haki itendeke.Kumsimamisha Mchungaji siyo kutatua tatizo! Na si kikanisa tena hii ni siasa kanisani.Nachelea siku moja KKT kufanya maamuzi kuwaridhisha watu mtafika pabaya! Mtoto aliyekuwa anacheza nyumba ya jirani akarudi analia sio unampiga mtoto na kumwambia kwa nini ulienda kucheza kwa jirani,labda kama ulimkataza asiende ,sidhani kama KKT imewaambia waumini wake wawakwepe mafisadi na kwa namna hiimakanisania hawatabaki watu!

Tunaishi katika criminalised society(jamii ambayo wengi wao wanamakosa ya jinai)) ambapo ufisadi wanafanya watu wengi, pengine asilimia 40 ya watanzania sio waaminifu katika maeneo yao ya kazi,katika mali za serikali na jamii, wengine hawajajulikana , wengine wakati huu bado wanaiba mabilini ya shilingi!. Na hiyo asilimia wengi wao wasomi na wana uwezo.Wengi wa hawa hawana mpango na siasa wala kinachoendela nchini maana wanakula wanavaa na wana magari. Katika hawa wengi hawapigi kura. Kulalamika kuwa raisi hatufai kwa maneno mengine japo inauma kusema ni kujitukana wenyewe. Tunawezo wa kuchagua tumtakaye.Kama unalalamikia uongozi na hukupiga kura nao ni ufisadi mwingine afadhali anayelalamika alipiga kura, hata kama kwa macho masikio na utashi wake alimchagua asiyefaa! Dhana ya kikristo ya kuheshimu mamlaka inaanzia hapa, kuwa wanaotuongoza ndio tuliowachagua. La si hivyo basi lawama zote wanachi wanapaswa kuzibeba! KKKT wakiwemo hapa. Na hapa sio siri katika wapiga kelele za ufisadi wengi sio wakweli ili mradi siku ziende. Ukiwaambia haya sasa maandamano ya kupinga ufisadi wengi hawajitokezi, lakini ndio wa kwanza kongelea juu ya ufisadi.

Watanzania wengi sio wapole kama inavyojulikana, ila kinachoonekana ni kuwa hakuna matatizo sana ya kuwaua watu(there is no critical problem).Nauli zikipanda wataongea siku mbili lakini watalipa, vitu vikipanda watafanya hivyo hivyo, mali asili zinaondoka, kilimo hamna anayefuatilia. Ikitokea asilimia 70 ya wananchi wanashindwa kusafiri,kula na matibabu kwa sababu gharama ya maisha imepanda,ikifikia mpaka mfagizi kariakoo ni mchina.Wengi ndio wataamka na kushtuka lakini tutakuwa tumechelewa.Kipindi hicho mwenye nguvu ataishi, hata kama tutawapeleka mafisadi gerezani lakini tayari mali asili zetu zitakuwa zimeondoka.Upole wetu na kutojali mambo yetu kipindi hiki kutaangamiza vizazi vijavyo.Hapa uzalendo hauhitaji elimu.

Furaha yangu ni kuona wanaotuhumiwa na ufisadi wanachukuliwa hatua na kuthibitishwa kuwa ndio halafu wapate adhabu sawia na makosa yao.Furaha yangu ni kuona makanisa yanachukua hatua nzito juu ya mafisadi kwa kuangalia kiini cha tatizo.KKT inapaswa ijue kuwa watanzania wengi wako kama wale wayahudi waliosema ona Yesu anakula na Zakayo mwenye dhambi, itambue kama ambavyo wale wayahudi hawakuwa na uwezo wa kumfanya lolote Zakayo, ndivyo ilivyo watanzania wengi wanaishia kusema tu. Lakini KKT wakati wanamzogoa Rostam(kama Zakayo) walipaswa wachukue nafasi kama ya Yesu, watimize wajibu a kikanisa na sio walivyofanya.Niko tayari kukosolewa pale nilipoandika kinyume,Mungu ibariki Tanzania.

MdauUDSM

WANAMAOMBI KUTAKA KULIOMBEA BUNGE KUFUKUZA NGUVU ZA GIZA (UCHAWI)

Kamati ya Umoja wa Makanisa ya Kikristo nchini, imemuandikia barua Spika wa Bunge, Bw. Samwel Sitta, ikimuomba awaruhusu waende Dodoma kulizunguka Bunge kwa ajili ya maombi na kusisitiza kwamba hawaamini taarifa iliyotolewa na Polisi kwamba unga uliopatikana ndani ya jengo hilo haukuwa na uchawi.

Kadhalika, Kamati hiyo imewashauri mawaziri na wabunge wenye hirizi kuzisalimisha kwao kabla ya kuanza maombi kwani wanaweza kuumbuka.

Pia Kamati hiyo imesema hatua ya Naibu Spika kufunga mjadala kuhusu `unga wa uchawi` haiwakatishi tamaa kufanya maombi hayo. Kamati hiyo imesema taarifa ya polisi imewachanganya na sio sahihi kwa sababu dola haiamini mambo ya uchawi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Kamti hiyo, Askofu Isack Kalenge alisema uchunguzi huo wa Polisi, Mkemia Mkuu, Bunge na Usalama wa Taifa ni batili kwa kuwa vyombo hivyo ambavyo viko chini ya serikali, havina uwezo wa kutambua uchawi.

Askofu Kalenge, ambaye ni kiongozi wa Kanisa la Pentekoste International, alisema wanaamini kuwa bado uchawi upo bungeni na wabunge wengi wanateswa na nguvu hizo za giza.

``Uchawi ni jambo la kiroho, haliwezi kupimwa kwa kamera wala uchunguzi wa Mkemia Mkuu, tunaamini tatizo la uchawi bungeni halijapatiwa ufumbuzi, tunakwenda Dodoma kulimaliza tatizo hilo ili lisitokee tena,``alisema. Akizungumza katika mkutano huo, Mchungaji Wilbert Ngowi alisema kamati hiyo haiwezi kufumbia macho taarifa hizo, kwa vile zimeliaibisha Taifa.

``Umefika wakati sasa kanisa liseme yale ambayo lilikuwa linayafumbia macho na lifanye mambo ambayo yalikuwa hayafanyiki, japokuwa hatua hii inaweza kutafsiriwa kwamba tunachanganya dini na siasa, lakini si vibaya.

Kuanzia sasa tumeamua kuchanganya dini na siasa kwa sababu maandiko matakatifu yanasema kufanya hivyo sio dhambi,``alisema.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mchungaji Christopher Mtikila alisema iwapo watapata ushirikiano wa Spika wataenda bungeni wiki ijayo. Akifafanua, kiongozi huyo alisema wamemuomba Spika awape kibali cha kuingia bungeni kuwaombea wabunge na `kuharibu` nguvu za giza zilizojaa humo. Mchungaji Mtikila alisema kabla hawajatia mguu Dodoma, wanawataka Wabunge, mawaziri na yoyote ambaye anatembea na hirizi aisalimishe kabla hawajaanza maombi.

``Ni matarajio ya Kamati kwamba wabunge wazalendo, hususan wale ambao hawatembei na hirizi vibindoni, watafurahia kazi hii njema ya watumishi wa Mungu yenye lengo la kuwaponya,``alisema. Kiongozi huyo alisema iwapo watakataliwa kufanya mambo hayo, watalizunguka jengo la Bunge hilo na kurusha `makombora ya sala` na kuahidi kwamba hakuna mwanga wala hirizi itakayosalimika.

Aliahidi kuwa wabunge na mawaziri, ambao ni wapenda uchawi, wataumbuka vibaya kutokana na sala hizo. Alisema tayari waumini mbalimbali wameshaanza kufunga kwa ajili ya kujiandaa na sala hiyo. Alisema hawatarajii upinzani kutoka kwa Bw. Sitta kwa sababu hivi karibuni Spika huyo alinukuliwa akiwataka viongozi wa dini, kuliombea Bunge kutokana na kuwa katika wakati mgumu.

``Sisi tumeamua kwenda kuliombea Bunge kama alivyosema, ila sisi tutaenda na mamlaka makubwa, ambayo yatasambaratisha kila roho chafu. Sisi wenye macho ya kiroho tumejua kwamba pale ndani pametundikwa kila aina ya uchawi, lakini hakuna hata mmoja ambao utasalimika,``alisema.

Sorce: Nipashe, 14.07.2008

Saturday, July 12, 2008

Church reverend suspended over Rostam Aziz incident

A DAR ES SALAAM Church leader has reportedly been suspended for inviting the Igunga Member of Parliament on a CCM ticket, Rostam Aziz, to speak at a prayer mass last Sunday without following proper procedure.
Reverend Joseph Masege of the Kinondoni Lutheran Church is understood to have been so disciplined by the church for allowing the politician to address worshippers without being given the relevant go-ahead by his superiors.
Rostam used the occasion to deliver what has been widely interpreted as a highly-controversial speech, including remarks that may be interpreted as part and parcel of the ongoing political fallout and subsequent wrangling over the findings of the parliamentary committee that investigated the Richmond corruption scandal.
The MP was one of the most prominent casualties of the committee’s final report, along with ex-prime minister Edward Lowassa and ex-cabinet ministers Nazir Karamagi and Dr Ibrahim Msabaha. Rev. Masege and one of the church’s choir groups, Amkeni, were reportedly suspended from the church after they were found to have been somehow behind the politician’s presence at the Sunday prayer mass, apparently as a VIP guest. When contacted on his mobile phone yesterday, Rev. Masege himself declined to comment on his reported suspension, abruptly hanging up the phone instead.
Rostam reportedly donated a total of 7.6m/- to the Amkeni choir group, and was given the honour of addressing the church gathering. In his remarks that received prominent coverage in a number of local newspapers, the MP said the country was passing through difficult times, claiming further that some people were being unfairly accused of corruption and thereby apparently demonised by political foes.
A statement issued earlier yesterday by the Kinondoni Lutheran Church distanced itself from Rostam’s remarks, saying his presence at the church did not follow proper procedure. ’’It has been established that Rostam was invited by a group that has no authority to issue such invitations,’’ said the church statement signed by its secretary general, Ambassador Richard Mariki.
The statement said the church had been dismayed by, and strongly rejected, the MP’s remarks to the congregation to the effect that he was a ’’clean politician.’’ The church also refused to be associated with any statements made by Rostam inside the church, saying the ’House of God’ should never be used to cleanse people from corruption allegations. ’’The church does not allow its congregations to be used as political platforms to cleanse corruption suspects.
The Evangelical Lutheran Church of Tanzania has been at the forefront in the fight against corruption,’’ said the strongly-worded statement. The church apologised to its worshippers for the incident, saying it would make sure such things never recur in future.

Source: THISDAY

Wasabato wenye imani kali na safari ya ulaya

WAUMINI 17 wa dhehebu la Wadiventista Wasabato Masalia, kutoka mikoa mbalimbali nchini, akiwemo mtoto mwenye umri wa miaka (16) na wanawake wawili wameweka kambi kando ya Uwanja vya Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam kwa lengo la kusubiri usafiri kwenda nchi za nje kuhubiri Injili bila kuwa na nyaraka zozote za kusafiria.
Waandishi wa gazeti hili jana walifika eneo hilo la Uwanja wa Ndege majira ya saa 4:30 asubuhi na kuwaona waumini hao wakiwa wamepiga kambi wakiwa na mizigo yao.
Mwananchi lilipofika katika eneo hilo, waumini hao walianza kuwafokea kuwa wanakiuka haki zao za msingi kwa kuanza kuwapiga picha bila idhini yao.
Kutokana na mtafaruku huo, waandishi wa Mwananchi waliwaomba radhi na kuwaelewesha kwamba, lengo lao halikuwa baya, bali walitaka kuandika habari na kuchapisha picha zao ili jamii ielewe walichokuwa wakifanya katika eneo hilo.
Baada ya mazungumzo hayo, hatimaye waumini hao walikubali kuzungumza na Mwananchi, lakini wanawake waliokuwa miongoni mwa kundi hilo waliondoka. Walipoulizwa wale wanawake wameenda wapi, walijibu kuwa hawatakiwi kuelewa.
Wakizungumza na Mwananchi kwa nyakati tofauti waumini hao walisema, wapo katika viwanja hivyo kwa muda wa siku tano sasa wakisubiri usafiri kwenda nchi za nje kuhubiri neno la Mungu.
Kusekwa Daudi, ambaye ni mmoja wa waumini waliopiga kambi katika viwanja hivyo, alisema lengo lao ni kusafiri na kwenda nchi za nje ambazo wameelekezwa na Mungu waende wakaeneze Injili kama neno la Mungu linavyosema, enendeni ulimwenguni mkaihubiri Injili.
''Tupo hapa kwa maelekezo ya Mungu, tunasubiri usafiri kwenda kuhubiri Neno la Mungu, mimi naenda Iran, Mungu kanituma huko,'' alisema Daudi.
Daudi alifafanua kuwa, Mungu kawapanga watu wawili wawili kila sehemu na kwamba, tiketi zao na viza ni Biblia, hivyo hawana wasiwasi wa kuondoka eneo hilo.'' Tutaondoka hapa tulipo, hatuna chakula, lakini Mungu atatupa,'' alisema.
Naye Daniel Masinde (16) ambaye alimaliza elimu ya msingi mwaka jana katika shule ya Bunda na kudai kufaulu kujiunga na sekondari, alisema hakutaka kuendelea na masomo hayo kwani aliamua kumtumikia Mungu kwanza na mambo mengine yatafuata baadaye.
''Nilifaulu, lakini sioni umuhimu wa elimu, kwanza nimtumikie Mungu, mimi amenituma kwenda Ufaransa na muda wowote nitaondoka kuanzia sasa,'' alisema Masinde.
Aliendelea kudai kuwa, amewaacha wazazi wake mkoani Mara kwani Biblia inaeleza kuwa mtu asipoacha vyote na kumfuata Mungu amepotea.
Mtoto huyo ambaye alionekana akiongea kwa ujasiri na kujiamini zaidi, alisoma mistari katika Biblia na kutolea maelezo ikiwa ni pamoja na Bahari ya Hindi itakuwa damu siku ya uchungu.
Mtoto huyo alipoulizwa na mwandishi wa habari hizi kuhusiana na lugha atakayotumia wakati akieneza Injili huko Ufaransa wakati hajui Kifaransa, alisema Mungu atamjaza Roho Mtakatifu ili kuweza kuongea lugha yoyote ile.
''Suala la lugha halina shida kabisa, Mungu atanijaza Roho Mtakatifu nitaongea tu lugha yeyote,'' alisema Masinde.
Mwingine aliyejulikana kwa jina la Kibunda Masige alisema kuwa, Kristo atawakatia tiketi za ndege wataondoka muda wowote kuanzia sasa (wakati wa mahojiano jana).
Awali, waumini hao walieleza kuwa maamuzi ya kwenda kuhubiri Neno la Mungu katika nchi za nje yalitolewa katika Mkutano Mkuu wa dhehebu hilo uliofanyika Mwanza Aprili mwaka huu ambapo walifikia maamuzi hayo.
Walifafanua kuwa katika msafara wao hawana kiongozi wao wala mkuu wa msafara, kwani kiongozi wa msafara wao ni Mungu.
Waumini hao walipoulizwa kuhusu sehemu wanapolalala, walijibu kuwa Mungu ndiye anajua wanapolala hata wao hawaelewi.
Waumini hao wamedai kuwa wale ambao wanakwenda nchi za jirani ambazo hazihitaji ndege, wameshafika huko, lakini wao wanakwenda nchi za mbali ndio maana wanasubiri usafiri Dar es Salaam.
Waumini hao wa dhehebu la Waadiventista Wasabato, walianza kuingia Dar es Salaam mmoja baada ya mwingine kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania ikiwemo Mwanza, Shinyanga na Kigoma Jumamosi wiki iliyopita.
Badaa ya kufika uwanjani hapo walikaa ndani ya Uwanja wa Ndege kwa siku mbili na baadaye uongozi uliwafukuza ndipo walipoamua kwenda pembeni ya baa ya Night Park jirani na uwanja huo na kuweka kambi eneo hilo.
Kwa upande wake, Afisa Usalama wa Uwanja wa Ndege, Julius Muungwana, alithibitisha kuwepo kwa kundi la waumini hao katika maeneo ya viwanja hivyo kwa muda wa siku mbili na kueleza kwamba waliwafukuza.
''Ni kweli kundi la watu hao lilifika katika viwanja hivi, sheria zetu haziruhusu mtu kukaa katika maeneo haya bila kazi yoyote, hivyo tuliwafukuza, lakini sasa hatuelewi nini kinaendelea juu yao,'' alisema Muungwana.
Hivi karibuni kundi jingine la waumini hao lilipiga kambi porini mkoani Mbeya likisubiri siku ya kurudi kwa Yesu. Waumini hao walidaiwa kuuza vitu vyao wakisubiri mwisho wa dunia kwa maelezo kwamba, Yesu asingeshuka mijini ambako kumejaa maovu ndiyo maana wakawa wanamsubiri porini.
Hata hivyo, baada ya muda waumini hao waliondoka porini bila Yesu kushuka.
Source: mwanachi

Thursday, July 10, 2008

Pambio ya leo

Kiongozi wa sifa:......"Wote waliompokea aliwapa uwezo kuwa wanaaa......"
Wote:"Wote waliompokea aliwapa uwezo kuwa wanaaa........."
Kiongozi wa sifa:...."Wote waliompokea aliwapa uwezo kuwa wanaaa.........."
Wote:"Wote waliompokea aliwapa uwezo kuwa wanaaa......
Kiongozi wa sifa:.."Aliwapa uwezooo...."
Wote:"Kuwa wanaaaa...."
Kiongozi wa sifa:...."Walitupa uwezooooo....."
Wote:"Kuwa wanaaaaa....."
Kiongozi wa sifa:......"Wote waliompokea aliwapa uwezo kuwa wanaaa......" Wote:"Wote waliompokea aliwapa uwezo kuwa wanaaa........."
Rudia rudia mara nyingi pambio hiyo hadi uone upako umeshuka ndo uache...anza kuimba basi hapo ulipo......

Mbarikiwe...

Iran wafanya jaribio la kombora linalofika Israel

Iran test-fired nine missiles Wednesday, including ones capable of hitting Israel, making a dramatic show of its readiness to strike back if the United States or Israel attacks it over its nuclear program.
The launches sparked strong U.S. criticism and a jump in oil prices — underlining fears Iran might seal off the Strait of Hormuz, the Gulf waterway through which 40 percent of the world's crude passes, if military conflict does break out.
The tests of the long- and medium-range missiles did not appear to mark a significant advance in Iran's missile capability — similar ones have been tested previously. But the timing and location were clearly aimed to send a message, coming as Iran has sharply stepped up the tone of its warnings of retaliation if attacked. This week, a top official of Iran's Revolutionary Guards, Ali Shirazi, warned Tel Aviv would be "set on fire" in any Iranian retaliation.
The tests took place amid a military exercise that Iran has been conducting in the Hormuz strait, where Tehran has threatened to block oil traffic in response to any U.S. or Israeli military action.
Iran has long warned it would strike back for any attack against it. But it has sharpened its rhetoric since Israel's military sent warplanes over the eastern Mediterranean in June for a large military exercise that U.S. officials described as a possible rehearsal for a strike on Iran's nuclear facilities.
Gen. Hossein Salami, the Revolutionary Guards air force commander, said Iran's war games this week — code-named "Noble Prophet" — "demonstrate our resolve and might against enemies who in recent weeks have threatened Iran with harsh language," state TV reported.
"Hundreds and maybe thousands of missiles are ready to be fired at specified targets," he said. "A small part of our defense options was put on display for the world today. Our real reaction against enemy threats will be quicker and stronger."
The West needs to "assess Iran's might accurately," he added.
State TV aired footage of at least six missiles being fired simultaneously, and said the barrage included a new version of the Shahab-3 missile, which officials have said has a range of 1,250 miles and is armed with a 1-ton conventional warhead. That would put Israel, Turkey, the Arabian peninsula, Afghanistan and Pakistan within striking distance. The TV report did not say whether the test took place near the Hormuz strait.
The U.S. Defense Department said it was studying the test to determine exactly what was launched and what it shows about Tehran's missile capabilities.
Secretary of State Condoleezza Rice called Wednesday's tests "evidence that the missile threat is not an imaginary one."
"Those who say that there is no Iranian missile threat against which we should build a missile defense system perhaps ought to talk to the Iranians about their claims," Rice said while traveling in Sofia, Bulgaria.
On Tuesday, Rice and Czech counterpart Karel Schwarzenberg signed a deal allowing the U.S. to base a missile defense shield in the Czech Republic.
Defense Secretary Robert Gates said the test bolsters the U.S. argument that Tehran is a threat and a missile defense system is needed in Europe.
A White House spokesman called the tests "completely inconsistent with Iran's obligations to the world" and said they further isolate the country.
Iran should "refrain from further missile tests if they truly seek to gain the trust of the world," said Gordon Johndroe, spokesman for the National Security Council, speaking from Japan where President Bush is attending the Group of Eight summit.
Democratic presidential candidate Barack Obama said Iran's missile tests highlight the need for direct diplomacy as well as tougher threats of economic sanctions and strong incentives to persuade Tehran to change its behavior.
John McCain, the Republican seeking the presidency, said the tests demonstrate a need for effective missile defense, including missile defense in Europe and the defense system the U.S. plans with the Czech Republic and Poland. Oil prices rose Wednesday on news of the tests, along with a U.S. government report showing crude stockpiles fell more than expected. Light, sweet crude for August delivery rose $1.50 to $137.54 a barrel in early afternoon trading on the New York Mercantile Exchange.
Israeli defense officials said there were no major surprises in the latest Iranian missile tests. The officials said they appeared to be more of an exercise in psychological warfare than a breakthrough in military technology.
"Israel does not desire hostility and conflict with Iran," Israeli government spokesman Mark Regev said. "But it is clear that the Iranian nuclear program and the Iranian ballistic missile program is a matter of grave concern."
The test could also be aimed to show the West there cannot be a military solution to the standoff with Iran over its nuclear ambitions. Iran denies U.S. accusations it seeks to build nuclear weapons, and earlier this week it sent a response to a Western package of economic incentives aimed at pushing it to halt uranium enrichment. EU officials have said they are still evaluating the response, but Tehran has insisted it will not suspend enrichment.
Iranian leaders have said they don't believe the U.S. or Israel will attack, citing U.S. problems in Iraq and the effect on already soaring oil prices. President Mahmoud Ahmadinejad on Tuesday called the idea of an attack a "funny joke."
But at the same, Iran has been more vocal in warning of the fallout of any U.S. or Israeli strike.
The semi-official Fars news agency, which is believed to be close to the Revolutionary Guards, reported details on the missiles tested Wednesday, saying they included a "newly upgraded" Shahab-3, first tested in its longest-range version in 2004.
The Shehab-3 tested Wednesday has been designed with a "cluster" warhead, that allows it to release multiple bombs over a wider area, Fars said, without elaborating. It also boasts a more accurate navigational system that allows a control room to bring the missile back on route if it strays or destroy it if it goes too far off course, it said.
The other missiles tested included the Zelzal, versions of which have a range of 130-185 miles, and the Fateh, with a range of 105 miles.

Zitto Kabwe alazwa muhimbili

*Asumbiliwa na homa ya matumbo
* Madaktari wasema anaendelea vizuri

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe amelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) akisumbuliwa na ugonjwa wa homa ya matumbo.
Akizungumza na Mwananchi jana jijini Dar es Salaam hospitalini hapo jana, Msaidizi wa Mbunge huyo, Omary Ilyas, alisema Kabwe alilazwa tangu juzi usiku katika jengo la Mwaisela, wodi namba nane, chumba 312 baada kuugua ghafla, lakini sasa anaendelea vizuri kufutia huduma kutoka kwa madaktari wa hospitali hiyo.
''Alifikishwa hapa saa tatu usiku wa kuamkia jana. Tunadhani tatizo lake linatokana na uchovu wa safari madaktari wake wameshachukua vipimo vyote, tunasubiri ni majibu na anaweza kuruhusiwa kwani kwa sasa anaendelea vizuri,'' alisema Ilyas na kuongeza:
''Mheshimiwa Mbunge amekuwa na ziara mfululizo, bila kupata mapumziko kwa kipindi kirefu, hivyo inawezekana ndizo ziliyomsababishia maumivu makali ya mwili kiasi cha kumlazimu alazwe hapa kwa ajili ya mapumziko na uchunguzi zaidi''.

Source: Mwananchi

Kanisa la KKKT lamkana Rostam Aziz

KANISA la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) limesema taratibu zilikiukwa katika kumwalika Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz (CCM) kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa albamu ya kwaya ya Usharika wa Kinondoni, Dar es Salaam Jumapili iliyopita. Taarifa ya Dayosisi ya Mashariki na Pwani (DMP) ambako Usharika huo upo, imesema kanisa hilo halitambui usafi wake. Katika hafla hiyo, Rostam ambaye si Mkristo, alichangia Sh milioni tano kwa ajili ya ununuzi wa seti za muziki za kwaya hiyo na jenereta yenye thamani ya Sh milioni 2.6. Taarifa hiyo inawaomba radhi waumini wake ambao huenda walikwazwa na taarifa za ugeni na matamshi ya Rostam katika Usharika wa Kinondoni, ambako alinukuliwa akiipongeza KKKT kwa kutambua usafi wake. Katibu Mkuu wa KKKT wa Dayosisi hiyo, Balozi Richard Mariki amesema katika taarifa hiyo jana kuwa katika tukio lililomhusisha Rostam, taratibu za kuwaalika wageni kwenye shughuli za kanisa hazikufuatwa na kanisa limesikitishwa na matamshi yake. “Rostam alialikwa na kikundi ambacho hakikuwa na mamlaka ya kumwalika". Alisema kutokana na ukiukwaji wa taratibu hizo, madai yaliyonukuliwa katika vyombo vya habari kwamba ugeni wa Rostam katika usharika wa Kinondoni na tafsiri ya kuwapo kwake kuwa kanisa linatambua usafi wake, si sahihi na ni madai potofu. “Msimamo wa kanisa hauruhusu usharika zake zitumike kama majukwaa ya siasa kujisafisha au kuwasafisha watuhumiwa wa ufisadi,” ilisema taarifa hiyo ya KKKT ambayo imetolewa na Halmashauri Kuu ya DMP. Katibu mkuu huyo alisema KKKT imekuwa mstari wa mbele katika kupinga na kukemea ufisadi na linaunga mkono juhudi za kutokomeza uovu. Mariki alisema kanisa litachukua tahadhari kuhakikisha kwamba jambo kama hilo halitokei tena na kusisitiza kuwa jukumu la kanisa ni kuokoa roho za watu na si kukumbatia aliodai kuwa ni “mafisadi na wala rushwa”. “DMP inapenda kuwaomba radhi waumini wote wa DMP, KKKT na wale wote wenye mapenzi mema kwa nchi yetu ambao kwa namna moja ama nyingine wamekwazwa na tukio hilo,” alisema Mariki katika taarifa hiyo. Kwa mujibu wa Mariki, juzi Halmashauri ya DMP ilifanya kikao cha dharura ambacho kilijadili taarifa zilizoandikwa na vyombo mbalimbali Jumatatu kuhusu Rostam kulipongeza kanisa hilo kwa kutambua usafi wake, licha ya mlolongo wa tuhuma na kashfa zinazoelekezwa dhidi yake. Taarifa hiyo ilieleza kuwa kama kanisa kuna taratibu za kualika wageni kwenye shughuli mbalimbali za kanisa kuanzia ngazi ya mtaa, usharika, jimbo na ofisi ya Dayosisi. Mwishoni mwa wiki iliyopita Rostam alialikwa na kwaya ya Amkeni ya Usharika wa Kinondoni kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi ambako alisema taifa liko katika wakati mgumu katika siasa na jamii na akawaomba watu watumie makanisa kulirejesha katika mstari sahihi. Alisema waumini wa dini hawamtuhumu mtu, hawamshutumu, hawapendi wenye wivu na wenye chuki, bali wanapenda haki na hivyo ni vizuri wakaitumia fursa hiyo kuliombea taifa. “Nawashukuru kwa kunialika kuwa mgeni rasmi leo hii…ni ishara kwamba mmeamua kupuuza vijimaneno na upuuzi wa vijiweni,” alisema Rostam. Haikuwa mara ya kwanza kwa Rostam kushiriki na kuchangia katika Usharika huo, kwani mwaka 2005 alichangia ujenzi wa jengo la kanisa hilo ambalo sasa linatumika kama sehemu ya Chuo Kikuu cha Tumaini.
***************************************************************

Maswali ni mengi sana kuliko majibu katika sakata hili la Rostam Aziz.

1.Hivi ni kweli imethibitishwa kisheria au kiroho kuwa Rostam Aziz fisadi?

2.Kwa nini KKKT wasirudishe sadaka hizo za Rostam Aziz na jenereta lake alilolitoa?

3.Hivi kama akialikwa mwanasiasa mwingine anayetuhumiwa kwa ufisadi KKKT bado wanaweza kutoa tamko la namna hii?(Tunajua wapo wengi wanaotuhumiwa kwa ufisaidi --epa,meremeta,tangold,kiwira,richmond n.k)

4.Hivi dhambi ya kuishupalia ni hii tu ya ufisadi?

5.mbona kuna wazinizi,walevi,wachawi,wezi na wauwaji wanaoalikwa makanisani na hata ndani ya KKKT na huwa wanatoa michango mingi sana na huwa inapokelewa kwa vifijo na nderemo.Kwa nini KKKT wasirudishe hizo nazo?

6.KKKT wamethibitisha vipi kama Rostam Aziz ni Fisadi?

7.Nani anayetakiwa kuingia kanisani? Je ni watakatifu pekee au pamoja na wenye dhambi?

8.Ni matamko mangapi ya wanasiasa yamewahi kutolewa kanisani na KKKT ika react kama hivi?

Kwa kweli maswali ni mengi sana ya kujiuliza hapa...nahisi majibu ni machache sana katika maswali haya...Nadhani imefika wakati sasa kwa makanisa kuangalia upya utaratibu wa kuwaalika wanasiasa na matajiri makanisani hata kama ni hawajampa YESU maisha yao kwa kisingizio cha changizo na kupokea mapesa...hivi hakuna wageni rasmi waliokoka wanaomjua Mungu?

Hivi kumkaribisha mlevi,mzinzi na kahaba katika madhabahu ya Mungu na kumwacha akitoa hutuba yake ni sawa kweli mbele za Mungu?Tumeshuhudia wafanyabiashara au wanasiasa wakipandishwa madhabahuni na kutoa hotuba zao mara nyingi...

Siungu mkono ufisadi ila ninasema kuwa lazima tufike kipindi tuwe tunapima mambo kabla ya kukurupuka na kutoa matamko ili kuufurahisha umma bila kujali kuwa hatutendi haki mbele za MUNGU wetu..


Mbarikiwe....

Wednesday, July 9, 2008

Pastors Attacked, Accused of Forcible Conversion

Pastor Murugan was beaten by Hindu militants who ambushed him and two other believers while returning home from a prayer meeting in Moodalpalya, Karnataka, India.
According to The Voice of the Martyrs contacts, "The other two managed to flee and escape any harm.
The militants accused the pastor of forcibly converting people and 'spoiling the minds of the children' and took him to the local police station where he was detained."
In an unrelated incident on June 26, Hindu militants barged into the home of a local believer in Hubli, Karnataka; shouted curses at the Christians gathered for a prayer meeting and beat Pastor Vinod Talakere.
VOM sources added, "They dragged the pastor and another believer to the local police station where the men were detained on accusations of forcibly converting people, kidnapping local girls and enrolling them in Bible college."
Pray for the release of these pastors. Ask God to bless their ministry and the work of other Christians spreading the gospel in India.
Philippians 4:13

Pambio ya leo

Kiongozi wa sifa:......"Utukufuu kwake Yesuuuu....haleluyaaa...X 2"
Wote:"Utukufuu..kwake Yesuuuu...haleluya.....X2"
Kiongozi wa sifa:...."Vijanaa nauliza mnijibu sifa na utukufuuu tumpe nani....?"
Wote:"Utukufuu..kwake Yesuuuu...haleluya.....X2"
Kiongozi wa sifa:.."Umeombea wagonjwaa...wameponaa...usibebe utukufuuu..mwachie Yesuuu..."
Wote:"Utukufuu..kwake Yesuuuu...haleluya.....X2"
Kiongozi wa sifa:...."Umehubiri vizuri watu wamebarikiwaaa..usibebe utukufu...umpe Yesuu..."
Wote:"Utukufuu..kwake Yesuuuu...haleluya.....X2"

Rudia rudia mara nyingi pambio hiyo hadi uone upako umeshuka ndo uache...
anza kuimba basi hapo ulipo......
Mbarikiwe...

Tuesday, July 8, 2008

Rostam Aziz ajisafisha kanisani

**Asema watu wanachukiana na kuombeana vifo Adai wanazushiana uchawi, anapakaziwa fisadi **Aomba kanisa litumike kurejesha taifa katika mstariDar es Salaam,

MBUNGE wa Igunga, Bw. Rostam Aziz amesema taifa liko katika wakati mgumu kisiasa na kijamii na ameomba watu watumie makanisa kulirejesha katika mstari ulio sahihi.
Bw. Rostam ametoa mwito huo leo jijini Dar es Salaam katika hafla ya uzinduzi na kuweka wakfu albamu ya kwaya ya Amkeni ya Kanisa la Kiinjili la Kulutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kinondoni, iliyofanyika katika viwanja vya kanisa hilo ambapo alikuwa mgeni rasmi.
Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz akionyesha kanda za video, kaseti na dvd za kwaya ya Amkeni ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kinondoni wakati wa hafla ya uwekaji wakfu katika kanisa hilo, Dar es Salaam leo. Kulia ni Mwenyekiti wa maandalizi ya hafla hiyo, Justine Mugangala
Amesema waumini wa dini hawamtuhumu mtu, hawamshutumu, hawapendi wenye wivu na wenye chuki bali wanapenda haki, na kwamba licha ya kashfa za ufisadi anazozushiwa, wamepuuza hilo na wamejenga imani kwake.
“Nawashukuru kwa kuamua kunialika kuwa mgeni rasmi… ni ishara kwamba mmeamua kupuuza maneno na upuuzi wa vijiweni. Nafurahi kuwa miongoni mwenu…. hamtuhumu, hamshutumu, hampendi wenye wivu na wenye chuki, mnapenda haki. Ninao watoto watatu na nataka niwalee katika misingi hii,” alisema Rostam huku akishangiliwa na umati wa watu waliofurika katika hafla hiyo.
Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz akizungumza na waumini wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kinondoni wakati wa hafla ya uwekaji wakfu katika video, kaseti na dvd ya kwaya ya Amkeni ya kanisa hilo, Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mchungaji wa kanisa hilo, Joseph Masege na kulia ni Mwenyekiti wa maandalizi ya hafla hiyo, Justine Mugangala
Rostam alisema watu wanachukiana mpaka kufikia hatua ya kuzushiana uchawi na kuombeana vifo. “Tutumie makanisa kukemea vitu hivi ili kurejesha taifa katika mstari ulio sahihi,” alisema.
Rostam alisema licha ya matatizo ya kisiasa, kuna matatizo ya kijamii ambayo alisema ni ndoa kuvunjika kila kukicha, watoto wa mitaani kuongezeka, madanguro na dawa za kulevya kukithiri, mambo ambayo yanasababishwa na mmomonyoko wa maadili.
Katika hafla hiyo ya kuweka wakfu kanda za video, kaseti na dvd, Mbunge huyo alitoa mchango wa sh. milioni 5 kuchangia seti za vyombo vya muziki kwa kwaya ya Amkeni pamoja na jenereta yenye thamani ya sh. milioni 2.6. Hiyo ni albamu ya kwanza ya kwaya ya Amkeni iliyodumu kwa miaka 24 sasa.
Mwaka 2005, Rostam pia alishiriki katika harambee ya ujenzi wa jengo la Kanisa la KKKT Kinondoni ambalo kwa sasa linatumika kama Chuo Kikuu cha Tumaini.
Waimbaji wa kwaya ya Amkeni ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kinondoni wakitumbuiza wakati wa hafla ya uwekaji wakfu katika kanda zao za video, kaseti na dvd, leo jijini Dar es Salaam . Mgeni rasmi alikuwa Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz aliyeichangia kwaya hiyo sh. milioni 5 na kuahidi kuinunulia jenereta yenye thamani ya sh. milioni 2.6.

Angela Deo Lubala awa miss Temeke

Yule mtoto wa askofu wa kanisa la World Alive Mchungaji Deo Lubala anayechunga kanisa lililopo sinza mori jijini Dar jana amechaguliwa kuwa miss Temeke.Soma habari zaidi na picha za tukio nzima hapa chini.
Angela Luballa (18) ameunyaka Miss Temeke 2008, baada ya kuwashinda wenzake 11 na anatarajiwa kuungana na washiriki wenzake katika kambi ya Miss Tanzania wiki hii.
Angela, alitwaa taji hilo, katika shindano liliyofanyika kwenye viwanja vya TCC Changombe Temeke Dar es Salaam jana usiku.Mwandaaji wa shindano hilo, Benny Kisaka ndiye aliuyemtangaza mshindi huyo ambaye anayemfuatia ni Rona Swai aliyeshinda pia taji la kipaji ‘Miss Talent’ akifuatiwa na Florence Josephat, huku Lilian Shayo akishika nafasi ya nne na Caroline Joseph ya tano.Wanamuziki baba na mwana, Zahir Ally Zoro na Baba Zoro, walipamba onyesho hilo kwa nyimbo ya kusindikiza warembo huku Big Brother II Richard, akiwa mgeni mwalikwa pamoja na miss Temeke 1997, Miriam Odemba na warembo kadhaa waalikwa wakiwamo wachezaji wa timu ya The Express walihudhuria.Washiriki waliopanda jukwaani juzi ni Zainabu Ally, Frolence Josephat, Evanuv Isaac, Caroline Sechuma, Lilian Shayo, Groly Charles, Radhia Omary, Angella Luballa, Rona Swai, Shabia Ally, Nunu Hussein na Mwasha Ramadhan.Pichani Miss Temeke 2008, Angela Luballa (katikati) katika picha ya pamoja na mshindi wa pili Rona Swai (kulia) mshindi wa tatu, Florence Josephat ( kushoto) .Picha nyingine ni ya Richard akijiandaa kumtangaza Miss Talent na nyingine mamisi wakijimwayamwaya ukumbini

Habari hii tuliwahi kuwaletea hapa mlimani sayuni wakati Angela alipochaguliwa kuwa miss Chang'ombe na ushindi wake kuzua mjadala mzito hapa jijini kwa mtoto huyo wa mchungaji wa kanisa la kipentecoste nchini kushiriki mashindano hayo huku akikungwa mkono kwa asilimia 100 na baba yake na mama yake ambao ni watumishi wa Mungu.Wakati anashinda miss Chang'ombe Mchungaji na Askofu Deo Lubala alipoulizwa kuhusu kuunga mkono mtoto wake huyo anayedai kuwa ameokoka alisema kuwa hakuna ubaya wowote kwa binti yake kushiriki mashindano hayo kwani ni njia ya kumhubiri YESU.

Picha chini Angela Deo Lubala (mwenye namba 8 kiunoni) akiwa na washiriki wengine wa miss Temeke wakifanya mazoezi makali ya kunengua kabla la shindano hilo mapema week iliyopita.






Monday, July 7, 2008

FURAHIA WOKOVU WAKO (ENJOY YOUR SALVATION)

MUNGU ASIFIWE SANA!
Pamoja na kuurithi uzima wa milele,kuna ahadi nyingi sana ambazo Mungu amewaahidi wale wamchao yeye,yaani waliokoka,kwahiyo ni jukumu letu sisi kumuuliza Mungu ili azitimize ahadi zake.
Kuna watu wengi sana ambao wameokoka kweli lakini wanaishi maisha duni,ya kimasikini kabisana ya kinyonge kabisa,ukiwauliza wanafikiri kuwa wameokoka ili tuu wasiende Jehanamu,kwahiyo hawahitaji kuishi maisha mazuri hapa duniani.Jambo hilo si kweli na wanamsingizia Mungu wetu tuu.Ukweli Mungu anataka mtu aliyeokoka afaidi maisha yote ya hapa duniani pamoja na yale yajayo.Mungu hataki mtu wakeasumbuliwe na umasikini,magonjwa,kuonewa kwa namna yeyote ile,kudharauliwa kufeli au hali yoyote mbaya maana hebu jiulize mtu wa Mungu,kuna faida gani basi kuokoka kama mtu utaendelea kuonewa na shetani?Ukweli ni kwamba mtu akishaokoka anakaa ndani ya Yesu na Yesu anakaa ndani yake,na ufahamu kuwa Yesu si masikini bali ni tajiri,na akiaa mahali,umasikini hauna nafasi,Yesu si mgonjwa bali ni Daktari bingwahivyo magonjwahayakai sehemu alipo Yesu.Ndio maana wakimbizi hukimbia kutoka kwenye nchi zenye vita nakwendakwenye nchi zenye amani na utulivu kuliko za kwao.
Ingekuwa nia ya kokoka ni kwenda mbinguni tuu,basi Yesu asingeponya watu,kutoa pepo,kubariki wala asingetupa karama za uponyaji kutoka kwa MUNGU.
Hebu tujifunze namna ya kufurahia maisha ya wokovu baada ya kuokoka.
BAADA YA KUOKOKA:
1. Watu wengi wamakuwa hawamini ya kuwa Mungu amewasamehe dhambi zao zote pale wanapokoka,jambo hili limekuwa likiwarudisha wengi nyuma.Unapookoka amini kuwa umeokoka na kwamba Mungu baba amekusamehe dhambi zako zote na kuzisahau kabisa tena zote kabisa,haijalishi ni dhambi ya namna gani uliwahi kuifanya,Mungu anasamehe na kuzisahau kabisa.Soma ISAYA43:25,ISAYA 1:18,ISAYA 44:22.
2. Kuwa na ushirika na watu wengine ambao watakujendakiroho,kama vile vikundi vya maombi na vile vya uamsho.SomaWAEBRANIA10:25,MATENDO YA MITUME 2:42.
3. Hakikisha kuwa unasoma na kutafakari neno la Mungu katika Biblia kila siku,mara nyingi iwezekanavyo,neno la Mungu litakupa mwongozo wa namna ya kuenenda katika wokovu,pia litakufundisha namna ya kuufurahia wokovu wako,hebu soma1PETRO2:2,WAEBRANIA 4:12,ZABURI 119:7&41&43.
4. Dumu kwenye maombi mara zote ukimueleza Mungu mahitaji yako yote kwakuamini kuwa anakusikia na atakupa yale yote unayomuomba.
5. Fahamu kuwa sasa umekuwa mtoto wa Mungu na kwa hiyo Mungu ndiye baba yako(YOHANA1:12),WARUMI8:16)
6. Mkimbie shetani na kazi zake zote,na tamaa zake zote kwa ujasiri(ZABURI 1:1)
7. Usisite kuwafahamisha wengine juu ya uamuzi wako wa kuokoka,watu wengi wamekuwa waoga wa kukiri mbele za watu kuwa wameokoka ,hilo ni jambo la hatari sana katika maisha ya kiroho.Wote waliokoka ni ndugu ndani ya Kristo.Je,wewe hupendi kufahamiana na ndugu zako??Yesu akusadie ili uweze kumkiri mbele ya watu wote.
8. Sasa fuata maagizo yote ambayo Mungu amekupa kwenye neno lake(BIBLIA) ISAYA 44:22.
MKUMBUSHE MUNGU AHADI ZAKE:
Ikiwa umeamua kumfuata Mungu,yeye anakusikiliza kama mtoto wake,kumbuka Biblia inasema"wote waliompokea aliwapa uwezo kuwa wana…"(YOHANA1:12)Kwa hiyo sasa zungumza na Mungu katika maombi ukimkumbusha ahadi zake ambazo amesisema katika Biblia.Ukishaokoka Mungu anakuwa karibu na wewe kuliko baba yako wa duniani alivyokaribu na wewe. Liamnini jina la Yesu.1PETRO2:3-5,MARKO 16:17-18,1WAKORINTHO3:16-17.
MAOMBI:Narudia tena ya kuwa ni muhimu sana kuzungumza na Mungu kwa maombi mara kwa mara kila siku.Hebu soma mistari ifuatayo,ISAYA43:26.".njoo tuhojiane,nikumbushe shida zako,eleza shida zako upate kupewa haki yako…",YEREMIA29:12.
Mtu waMungu unayefuatilia somo hili kumbuka siku zote kwambamaombi bila neno ni sawa na ndege aliyevunjika bawa moja .Sikuzote Mungu huwa hajibu maombi bali huwa anajibu neno lake ambalo limo huko ndani ya maombi yako wewe muombaji,tazamaYEREMIA 1:12,Kwa hiyo,
Siku zote ingiakwenye Maombi ukiwa na neno la Mungu(mstari au mistari ya Biblia inayoelezea ahadi ya Mungu juu ya lile unaloomba k wake) Unapomuomba Mungu usiangalie majibu yako kwa jinsi ya kimwili,wewe unachotakiwa kufanya ni kuamini tuu kuwa umeshapewa.Ukisoma kitabu cha 1WAFALME 18,utaona namna ambavyo Eliya aliomba kwa Mungu ili mvua inyeshe juu ya ile nchi.Nabii Eliya aliomba akamtuma mtumishi wake kwenda kutazama kama kuna dalili zozote za mvua(mawingu)lakini hazikuwepo,akandelea kuombakwa juhudi,Hebu sema"akaendelea kuomba kwa juhudi"akafanya hivyo mara saba na ile mara ya saba akaona mawingu angani madogo kiasi cha kiganja cha mkono.Nabii Eliya alipoona ishara hiyo ndogo aliamini kuwa mvua itanyesha na akafurahi sana kwa kuwa Mungu amejibu maombi yake.Hata wewe unayesoma somo hili sasa hivi uwe na tabia kama ya Eliya.Kama bado hujaona ishara yoyote ile,endelea KUOMBA KWA JUHUDI.Ukiona ishara kidogo sana,ANZA KUMSHUKURU MUNGU UKIAMINI KUWA AMESHAKUJIBU OMBI LAKO.BWANA YESU ASIFIWE SANA!!!! Na baada ya muda mfupi sana utayaona majibu yako waziwazi kabisa.HALELUYA!!
AHADI ZA MUNGU:Ndugu yangu katika Kristo Yesu,hapa nitakupa kwa kifupi tuu baadhi ya ahadi ambazo Mungu amezisema kwa ajili yangu na yako.Ahadi za Mungu zinapatikana katika Biblia.Nakushauri usome Biblia zaidi ili uweze kufahamu ahadi nyingine kwa maana zipo nyingi SANA.
Ahadi hizo nimeziandika katika website yangu www.lema.or.tz click hapa kuzisoma. Kumbuka kuwa mwananchi asipofahamu haki zake, hataweza kuzidai, hali kadhalika mtu aliyeokoka (mlokole) asipozifahamu haki zake, hawezi kuzidai kwa Mungu. Ninakushauri usome Neno la Mungu kwa bidii KILA SIKU ili uone ahadi ambazo Mungu amekuwekea na uanze kuziomba kwa Mungu.
Imetosha sasa watu kuwadharau walokole.

Naamini utalisoma hili somo kwa wiki hii nzima na litakusaidia sana.Waalike na wengine kujiunga na mailing lists hii.
Tafadhali endelea kuniombea.

Mungu akubariki sana.
Frank Lema,
Arusha