Wednesday, March 16, 2011

Mwingira amlaani mchungaji Loliondo

Mtume na Nabii Josephat Mwingira wa Kanisa la Efatha amemuombea mabaya Mchungaji Ambikile Mwasapile anayetoa tiba ya magonjwa sugu katika eneo la Samunge, Loliondo kwamba anapaswa kulaaniwa hadi kufa kutokana na kutoa huduma hiyo.

Mwingira alisema hayo katika mahubiri ya ibada ya Jumapili aliyoyatoa katika Makao Makuu ya Kanisa hilo lililoko Mwenge jijini Dar es Salaam. “Imeandikwa katika Biblia kwamba,ukipewa bure nawe toa bure. Iweje yeye anauza dawa hiyo, ikiwa Mungu amesema aponye watu. Hakuna sababu ya kuwatoza fedha yoyote wagonjwa.

“Hizi ni roho za kishetani zinazotaka kuwaangusha walio wengi ambao hawamjui Yesu Kristo kwani haiwezekani mtu atumiwe na Mungu halafu hata siku moja asimtaje Yesu. Asitumie Biblia hata kuwahubiria watu wamtumaini muumba wao,”alisema Mwingira.

Mwingira alisema huduma hiyo ni uongo na kwamba haina tofauti na Deci iliyokuja kiujanja ujanja na kuteka watu wengi baadaye walijutia maamuzi yao. “Kama mpakwa mafuta wa Bwana niliyeitwa kwa kusudi lake.

Nailaani Loliondo ife pamoja na Mchungaji wake na itoweke kama Deci ilivyotoweka,” alisema Mwingira. Mwingira alisema Mchungaji Mwasapile ni mwongo, anataka kuwadanganya watu na kuwapoteza kiimani.

Alisema kama alivyoilaani Deci na ikafa, anailaani huduma ya Loliondo ili ife kwa kuwa mchungaji huyo ni roho ipotezayo, inayotaka kuwateka watu walioko gizani na kuwaangamiza. Alisema baadhi ya viongozi tayari wamepigwa ngwara na roho hiyo na kunywa dawa, bila wao kujijua.

“Sitakubali kuendelea kuona roho hiyo ikipoteza watu. Nailaani itoweke Loliondo na iangamie kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti,”alisisitiza. Mwingira alisema haiwezekani kwa mtu aliyeitwa na Mungu kuwahudumia watu wake, baadhi ya watu hao wafe kwenye huduma yake.

“Ni wagonjwa wangapi wamepelekwa kule na wengine wamefariki nyumbani kwake kabisa na wengine njiani, je mlishawahi kujiuliza? alihoji Mwingira. Mwingira alitoa kauli hiyo siku chache baada Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo kulieleza gazeti hili:"Miujiza haiji kwa urahisi hivyo na watu kuponya kiasi hicho, huenda wanaweza kuponywa kwa ‘Illusion’ na baade ikaleta madhara."

Alisema cha msingi watu wanapaswa kuwa makini na serikali pia kwa sababu, wingi wa watu kuponywa huenda baadaye ukaleta vifo vingi zaidi kutokana na dawa yenyewe.


Pengo alisema: “Ninachoamini miujiza haiji kwa urahisi na watu wakaponywa kiasi hicho kwa mara moja, huenda ikawa ni kuponya kwa ‘illusion’ na baadae watu wakapata madhara makubwa.

“Ila sina jibu la kutoa kuhusu uponyaji huo, nabaki tu kushangaa nayayotendeka kwa Mchungaji huyo hadi kufikia watu kuamini kiasi hicho,”alisema. Pengo alisema huenda akawa ameamua kutumia njia hiyo akawavuta hata wa waumini waingie kwenye imani yake na kuacha dini zao.

Source:mwananchi.co.tz

Lowassa apata kikombe Loliondo

WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa juzi alipata tiba ya magonjwa sugu inayotolewa na Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwasapile katika Kijiji cha Samunge, Tarafa ya Sale, Loliondo, mkoani Arusha.Lowassa alifika katika eneo hilo mchana akiwa na viongozi kadhaa wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro na Serikali kisha kupata kikombe kimoja chenye dawa kinachotolewa na mchungaji huyo kwa ajili ya tiba.

Tofauti na viongozi wengine, Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli (CCM), Jimbo linalopakana na Kijiji cha Samunge, alikwenda huko akiwa na viongozi mbalimbali wakiwamo viongozi wa dini na baadhi ya wapigakura wake.

Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, Lowassa alithibitisha kwenda Loliondo na kuwataja viongozi wa dini alioambatana nao katika msafara wake kuwa ni Askofu Msaidizi wa KKKT, Dayosisi ya Kaskazini, Dk Frederick Shoo na Mkuu wa Jimbo la Masai Kaskazini, Dayosisi ya Kaskazini Kati (Arusha), Mchungaji John Nangole.

Katika ramani ya utendaji kazi ya KKKT, Jimbo la Masai Kaskazini ndipo kilipo Kijiji cha Samunge ambako ni makazi ya Mchungaji Mwasapile.“Ni kweli, nimekwenda pale na wapigakura wangu pamoja na viongozi wa dini, Msaidizi wa Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini, Dk Shoo na Mkuu wa Jimbo la Masai Kaskazini, Mchungaji Nangole,” alisema Lowassa na kuuliza: “Kwani hiyo nayo ni habari jamani?”

Baada ya Lowassa kufika katika kijiji hicho akiwa na ujumbe wake, aliongoza moja kwa moja hadi kwa Mchungaji Mwasapile na kuzungumza naye kisha akapata kikombe cha tiba na kuondoka.

Kabla ya Lowassa kwenda kupata tiba, amekuwa akitoa msaada wa nauli kwa wagonjwa mbalimbali wa jimbo lake kwenda kwa mchungaji huyo ambaye dawa yake inadaiwa kutibu magonjwa ya saratani, kisukari, pumu, shinikizo la damu na Ukimwi.Lowassa ni miongoni mwa wanasiasa maarufu nchini ambao wameshafika kwa mchungaji huyo kupata tiba hiyo wakiwamo mawaziri, naibu mawaziri, wabunge, wakuu wa mikoa na wilaya.


Katika jitihada za kudhibiti usalama na kuhakikisha kwamba wananchi wanapata huduma kwa mchungaji huyo bila matatizo, Serikali imeimarisha ulinzi kwa kuweka askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), katika kijiji hicho na kusimamia magari. Pia imepeleka wauguzi kusaidia wagonjwa mahututi kabla ya kumfikia mchungaji na imetoa pia jenereta kwa ajili ya kufua umemeKaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Raymond Mushi alisema jana kuwa, sasa walau hali ni nzuri kwani msongamano umepungua.


"Ni kweli sasa hali inaridhisha na jana watu wamekwenda kupata tiba na kurejea makwao mapema hili ndilo serikali inalolitaka. Tunaomba watu wanaopeleka wagonjwa wawe wanauliza kwanza hali ya msongamano," alisema Mushi.Mushi alisema inawezekana watu wanaokwenda katika kijiji hicho kusubiriana katika Mji wa Mto wa Mbu ambako kuna huduma nyingi muhimu kuliko wote kwenda huko kwa wakati mmoja.

Alitoa wito kwa watu wenye wagonjwa mahututi kuacha kuwapeleka moja kwa moja kwa mchungaji huyo kabla ya kupata ushauri wa kitaalamu kuhusu afya zao.Katika hatua nyingine, wagonjwa kadhaa waliolazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili wameanza kutoroka wodini na kwenda Loliondo kupata matibabu ya magonjwa sugu yanayotolewa na Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwaisapile, Mwananchi imeelezwa.

Habari zilizopatikana hospitalini hapo jana zimeeleza kuwa wagonjwa hao walianza kuondoka Muhimbili juma lililopita baada ya Serikali kubariki matibabu hayo. Ofisa mmoja mwandamizi wa hospitali hiyo ambaye aliomba jina lake lisiandikwe gazetini, amesema kuwa wakati baadhi ya wagonjwa hao wakiwa wanatoroka wodini, wengine wamekuwa jasiri kwa kuwaaga madaktari wao.

“Wagonjwa wameanza kuondoka na wengine bila hata ya kuaga, hivyo hatujui hatima yao kama watafika salama huko Loliondo,” alisema.Ofisa huyo alisema juma lililopita, mgonjwa mmoja aliyekuwa amelazwa chumba namba 15 katika Wodi ya Kibasila, aliondoka baada ya kusikia taarifa kuhusu huduma hiyo.

“Kuna mgonjwa mmoja aliyekuwa amelazwa Kibasila Wodi namba 15 aliondoka aliposikia kuwa Babu ameanza tena kutoa matibabu hayo ambayo awali yalisitishwa,” alisema.Hata hivyo, Ofisa Habari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Aminiel Aligaisha alisema hana taarifa za kutoroka wodini kwa wagonjwa hao na kwenda kufuata tiba huko Loliondo... “Sina taarifa zozote za kuondoka kwa wagonjwa hapa hospitalini.”

Matibabu Loliondo yapandisha nauli Ubungo
NAULI za kwenda Arusha kutoka Ubungo, Dar es Salaam zimepanda kwa kasi katika siku za hivi karibuni kutokana na wingi wa wasafiri wanaoelekea Loliondo kupata tiba hiyo ya magonjwa sugu.Habari zilizolifikia gazeti hili jana kutoka kituoni hapo zimeeleza kuwa, nauli hizo zimepanda kutoka Sh18,000 hadi Sh30,000 tangu juma lililopita.

Mmoja wa mawakala wa mabasi ya abiria katika kituo hicho ambaye hakutaka kutajwa gazetini alisema ongezeko hilo la nauli limetokana na baadhi ya mawakala kukodi mabasi na kuwasafirisha abiria.“Nikupe siri moja tu ambayo inatufanya tupandishe nauli. Lengo letu ni kupata faida, ujue sisi tunakodi basi zima kisha tunakatisha tiketi kwa bei yetu ili na sisi tupate faida,” alisema.

Mmoja wa abiria aliyekuwa akisafiri kuelekea Arusha, Charles Manyama alisema mabasi yaendayo huko yamegawanyika katika madaraja matatu yale ya bei ya juu, bei ya kati na bei ya chini lakini kwa sasa bei imekuwa ni moja kwa mabasi yote.

Kwa mujibu wa abiria huyo, zamani nauli za Arusha zilikuwa Sh25,000 kwa basi la daraja la juu, Sh18,000 kwa mabasi ya daraja la kati na Sh15,000 kwa daraja la chini, lakini sasa mabasi yote yanatoza kati ya Sh25,000 hadi Sh30,000.“Mawakala hawa wanadhani kila mtu anayepanda magari haya anakwenda Loliondo lakini siyo kweli, wengine tuna safari nyingine kabisa," alisema Manyama na kuongeza:

"Unakuta bei zinashangaza na kupanda sana. Hata hivyo, inashangaza kuona wanadamu tunakosa utu. Watu wanakwenda kupata matibabu wanapandishiwa nauli, walipaswa kuwaonea huruma wagonjwa hawa,” alisema Manyama.Jitihada za kumtafuta Meneja wa kituo cha mabasi Ubungo ziligonga mwamba baada ya taarifa kutoka ofisi kwake kueleza kuwa alikuwa nje kikazi.

Polisi Arusha wadhibiti usafiri wa Loliondo
Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limeitaka Halmashauri ya Jiji la Arusha kuweka vituo vinavyotambulika kwa ajili ya wagonjwa wanaokwenda kupata matibabu kwa Mchungaji Mwasapile ili kuepuka utapeli.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Akili Mpwapwa alisema jana kuwa kutokana na idadi kubwa ya watu kutaka kwenda Loliondo, kumezuka vituo vingi ambavyo vinaweza kuwa chanzo cha utapeli kwa watu wanaotoka mikoani."Nafahamu hili ni jambo ambalo manispaa wanahusika nalo, wahakikishe kuwa hakuna vituo visivyo rasmi ili wananchi wasije kudanganywa na watu wabaya," alisema.

Katika kituo kilichoibuka ghafla baada tiba ya magonjwa sugu kuanza kutolewa cha Chini ya Mti, kulizuka vurugu za madereva na madalali waliokuwa wakibishania kiwango cha nauli, hatua iliyosababisha polisi wenye silaha kupelekwa katika eneo hilo.

Hatua ya polisi kuonekana katika kituo hicho, ilisababisha wasiwasi kwa wananchi kuwa huenda Serikali imesimamisha utaratibu wa wananchi kwenda Loliondo, jambo ambalo kaimu kamanda huyo alilikanusha.

"Tunachokifanya ni kuweka utaratibu mzuri, polisi wanasimamia sheria. Magari mengine yanazidisha idadi ya watu na kutoza pesa nyingi zaidi. Sumatra wakisema nauli sahihi ni kiwango fulani na madereva wakizidisha basi tunawakamata," alisema.

Wananchi waliozungumza na gazeti hili bila kutaja majina yao walisema kuwa wanashangazwa na bei ya nauli kuwa juu hata baada ya Serikali na KKKT, Dayosisi ya Kaskazini Kati kuboresha mazingira ya kuwahi kupata tiba na kuondoka kijijini Samunge.

"Mwanzoni walikuwa wanasema magari yanakaa sana huko, kwa hiyo wanafidia hizo siku za kungoja wagonjwa lakini sasa hivi ukienda leo unarudi kesho na nauli bado iko juu," alisema mmoja wa wananchi hao.Nauli ya kutoka Mjini Arusha hadi Samunge, Loliondo ni Sh100,000 kwenda na kurudi kwa magari aina ya Land Cruser ,huku nauli ya mabasi ikiwa pungufu zaidi.

Source: mwananchi.co.tz

Saturday, March 12, 2011

Yanayojiri sayuni

Anonymous DORAH said...

NILIKUWA muumini wa kanisa la EAGT MNAZI MMOJA..CHINI YA MCHUNGAJI andrew.naomba nifahamishwe kanisa hilo limehamia wapi..nikija TANZANIA NAHANGAIKA KUTAFUTA SEHEMU YA KUABUDU..NAOMBA TAARIFA.

March 10, 2011 12:48 AM

Delete
Blogger Mtade said...

Mtumishi Dora, Kanisa la Pastor Andrew kwa sasa lipo mnazi mmoja kati ya jengo la ushirika lumumba na ilipokuwa sukita zamani.Kuna jengo jeupe la ghorofa saba.karibu kabisa na mabasi ya hekima au sumry yanayotokea mbeya.Ukifika hapo pandisha ghorofa ya tatu utakuwa umefika.Kanisa linaitwa faith word church.Kwa maelezo zaidi ukifika piga namba hii utafika 0713-427857

Barikiwa

March 12, 2011 4:07 PM

Loliondo kwa babu

Msafara wa magari kuelekea Loliondo kwa Mchungaji Ambilikile Mwasapile.

WAKATI Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Haji Mponda akieleza kuwa ameagiza Serikali ya Mkoa wa Arusha kuzuia tiba ya magonjwa sugu inayotolewa na Mchungaji Ambilikile Mwasapile, Kaimu Mkuu wa Mkoa huo, Raymond Mushi amesema ni vigumu kusitisha huduma hiyo.

Mushi alisema pamoja na kutopata barua yoyote inayomwagiza asimamishe huduma za mchungaji huyo, ni vigumu katika mazingira yaliyopo katika Kijiji cha Samunge, Loliondo kufanya hivyo ikizingatiwa kwamba hivi sasa kuna maelfu ya watu hasa wagonjwa walioko hapo na wengine wakiendelea kumiminika.

“Hata mimi nimemsikia Waziri Dk Mponda, lakini siwezi kuanza kufanya kazi bila kupokea barua na maelekezo. Lakini hili jambo ni gumu kidogo kwani watu bado wanakwenda na tukipata barua tutajua jinsi ya kukabiliana na hali hii,” alisema Mushi.

Kaimu Mkuu huyo wa Mkoa alisema kama akipokea barua na maelekezo watakaa na watendaji wengine kuona ni jinsi gani wataweza kukabiliana na hali ya Loliondo. “Pale yule mchungaji anasema anatoa huduma ya tiba na lile jambo ni la kiimani ndiyo sababu anasema wenye imani watapona sasa sidhani kama wataalamu wakipeleka dawa ile maabara wataona kitu,” alisema Mushi.

Mbali ya Kaimu Mkuu wa Mkoa kuonyesha wasiwasi wake juu ya utekelezaji wa agizo hilo la Waziri, Mbunge wa Ngorongoro (CCM), Saning’o ole Telele amepinga hatua hiyo ya serikali kutaka kuzuia kwa muda tiba hiyo akisema badala yake, inapaswa kusaidia watu kupata tiba.“Sikubaliani na Waziri wa Afya kuzuia tiba eti sijui mchungaji ajisajili kwanza.Tunachoomba ni serikali kusaidia watu wafike Ngorongoro, Samunge na kupata tiba katika mazingira bora,” alisema Telele.

Telele alisema watu wengi wamepona kwa kunywa dawa hiyo, hivyo Serikali inapaswa kuomba msaada wa mashirika mbalimbali kama Msalaba Mwekundu yafike kuweka mahema na kutoa huduma ya kwanza.Jana, Dk Mponda alimtaka Mkuu wa Mkoa wa Arusha, kuzuia mara moja matibabu ya magonjwa sugu yanayoendeshwa na Mchungaji Mwasapile hadi serikali itakapojiridhisha ubora na usalama wake kwa watumiaji.

Akizungumzia tamko hilo la Waziri, Msaidizi wa Mchungaji Mwasapile, Paulo Dudui alisema amepotoshwa kwa vitu vingi: "Kwanza siyo kweli kuwa wagonjwa wote wanatumia kikombe kimoja na pia si kweli kwamba wanatumia maji ya mto."

"Kila mgonjwa anatumia kikombe chake na tuna vikombe zaidi ya 100 ambavyo baada ya kutumika vinaoshwa na wagonjwa wanaona na pale kuna maji ya bomba yanayotoka katika chanzo cha maji cha Samunge.”Lakini Dudui alisema kama wakipokea maelekezo ya serikali kuhusu tiba watakaa na kujadiliana kwani wanaamini huduma ambayo wanatoa ina manufaa makubwa kwa watu na siyo uganga.

“Mchungaji mwenyewe atasema nini cha kufanya ila Waziri kapotoshwa. Hapa serikali ilitakiwa kusaidia huduma kutolewa na siyo kuzuia,” alisema Dudui.Katika hatua nyingine Dudui alisema kwamba mtoto mmoja alifariki dunia jana katika eneo hilo kutokana na kuchelewa kupata tiba.


Source: http://www.globalpublishers.info

Tuesday, March 8, 2011

Ya Mchungaji wa Loliondo

WAKATI idadi ya watu ikizidi kumiminika katika Kijiji cha Samunge, Tarafa Sale, Loliondo kupata kile kinachoaminika kuwa ni tiba dhidi ya magonjwa sugu, mtoa huduma hiyo, Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Ambilikile Masapila ameiomba Serikali imsaidie kupata gari la kubeba dawa, vyombo vya kunywea, kuni na vyombo vikubwa vya kuchemshia dawa hiyo ili kukabili wingi huo.

Mchungaji Masapila ambaye alistaafu utumishi wa Kanisa mwaka 2001, katika Usharika wa Sonjo, alisema licha ya dawa hiyo kutolewa kwa Sh 500, pia kuna tatizo kubwa la barabara hadi kufika kijijini hapo.

"Tunaomba Serikali kutengeneza barabara kwani wagonjwa wanapata shida sana kufika hapa, nasikia hata nauli zimepanda sana," alisema Masapila.

Gharama za magari zimeendelea kuwa juu kwani hivi sasa wale wanaokwenda kwa kutumia magari ya kitalii wanalazimika kulipa kati ya Sh120,000 na 150,000 na mabasi ni kati ya Sh30,000 hadi 50,000.

Magari hayo sasa yamekuwa yakiondoka Arusha usiku ili kufika Samunge usiku wa manane na hatimaye siku inayofuata wagonjwa wapate dawa.

Kuongezeka kwa kasi kwa watu wanaokwenda kutibiwa kwa mchungaji huyo kumeibua hofu ya kutokea kwa magonjwa ya milipuko kama kipindupindu na kuhara kutokana na kukosekana kwa huduma muhimu za kijamii.

Eneo hilo hivi sasa linakabiliwa na tatizo kubwa la huduma muhimu kama vile majisafi, vyoo, nyumba za kulala na vyakula hivyo wageni hao wengi wakiwa wanakabiliwa na maradhi sugu yakiwemo kansa, kisukari, shinikizo la damu, kifua kikuu na Ukimwi.

Akizungumza na Mwananchi jana, Msaidizi wa Mchungaji huyo, Paulo Dudui alisema maafa makubwa yakiwamo magonjwa ya mlipuko yanaweza kutokea kwa sasa... "Tunaomba (Serikali) msaada wa mahema, vyoo vya muda na huduma muhimu kama mawasiliano kwani hapa kuna watu zaidi ya 6,000 ambao wanalala nje hawana sehemu za kujisaidia, vyakula hakuna na hata mawasiliano hakuna."

Alisema gharama za maisha katika eneo hilo zimepanda kwani bei za vyakula hivi sasa ni kubwa mno akisema hali hiyo ni hatari hasa kwa wagonjwa wanaotolewa hospitali ambao hali zao zinaweza kuwa mbaya hata kabla ya matibabu na hivyo kufariki.

Alisema juzi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali aliwatembelea na kujionea hali hiyo na hivyo wana imani suala la msaada litafikishwa katika ngazi za juu.

"Hali ni mbaya sana hapa kama mvua zikinyesha zaidi kunaweza hata kutokea vifo kwani wengi wanaokuja hapa ni wagonjwa," alisema Dudui.

Kuongezeka kwa idadi ya wagonjwa kunatokana na kusambaa kwa taarifa za watu waliopata tiba hiyo na kupona maradhi hayo sugu. Kiongozi mmoja mwandamizi wa CCM Mkoa wa Arusha ambaye hakutaka kutaja jina lake alidai kuwa tangu alipokunywa dawa hiyo, tatizo la sukari ambalo lilikuwa likimsumbua limekwisha.

"Sijui kama nimepona kabisa au la, lakini sasa najisikia vizuri tofauti na mwanzo," alisema kiongozi huyo.

Diwani waViti Maalum (CCM) Wilaya ya Monduli, Dora Kipuyo alidai anamfahamu mgonjwa aliyekuwa na kansa ya mguu ambao ulitakiwa kukatwa, lakini baada ya kupata dawa hiyo sasa vidonda vimekauka.

Baadhi ya watu wenye Virusi Vya Ukimwi (VVU), ambao wamepewa dawa hiyo, licha ya kudai kuwa sasa wana hali nzuri, bado hawajapima kwani wengi waliohojiwa walikuwa hawajatimiza sharti la kukaa siku saba kabla ya kupima ili wajue kama virusi vimekwisha au la.

Mchungaji Masapila alisema dawa hiyo ambayo alioteshwa na Mungu tangu mwaka 1991 na kukumbushwa mwaka 2009, inatokana na maombi na mti wa mgariga ambao unapatikana katika viunga vya Milima ya Sonjo.

Hata hivyo, alisema kupona kwa mgonjwa haraka pia kutokana na imani yake juu ya dawa hiyo ambayo dozi yake ni kikombe kimoja tu kinachonywewa hapo hapo inakotolewa.

Tayari Wizara ya Afya, imekwishatuma wataalam wake kwenda huko kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa dawa hiyo.

Source: Globalpublisherstz.com

Loliondo

WAKATI serikali ikijiandaa kutoa majibu ya kisayansi kuhusiana na tiba ya maajabu ya Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwasapile (75) mkazi wa Kijiji cha Samunge, Ngorongoro mkoani wa Arusha, maajabu zaidi ya tiba yake yameongezeka.

Akizungumza kwa tabu na gazeti hili kutokana na kuzungukwa na kadamnasi iliyokuwa ikihitaji kuponywa, mchungaji huyo alisema kuwa kabla ya kufika katika kijiji hicho Mei, mwaka 2009, alikuwa akiishi mkoani Manyara akitangaza Injili kama mhubiri wa kawaida na baadaye alistaafu.

Mchungaji Mwasapile ambaye ametazamwa na watu kama ‘Nabii mpya’ amekuwa akitoa tiba hiyo kwa staili ya aina yake ambapo mgonjwa anatakiwa anywe maji yenye dawa hiyo hapo hapo kwa kutumia kikombe kidogo.
Aidha, maajabu mengine ni baadhi ya watu kusema kuwa, mti ambao mchungaji huyo anautumia kutibia unajulikana lakini tatizo bila mkono wake kuchimba mizizi yake hakuna kinachoweza kufanyika.

ALIVYOPATA UTABIBU
Mchungaji Mwasapile anasimulia ilivyokuwa hadi akaoteshwa kuhusu mti huo, anasema:

“Ilikuwa mwaka 1999 nikiwa Babati, kuna siku nikiwa nimelala ilinijia sauti ndotoni. Ikaniamuru kuwa, watu wengi wa Kijiji cha Samunge wanakufa na Ukimwi, kisukari presha na magonjwa mengine mbalimbali.
“Sauti hiyo ikanitaka niwatibu watu hao ili waweze kuendelea na maisha yao kama kawaida. Lakini mimi nilipuuzia sauti hiyo na kuendelea na mambo yangu.
“Hata hivyo, mwaka 2009 sauti hiyo ilinijia tena ndotoni ikinipa maagizo yale yale, lakini safari hii ikanipa onyo kuwa, nisipotimiza agizo hilo nitaadhibiwa.

“Niliamka na kutii, nilikuja hapa kijijini na kwenda hadi kwenye mti nilioelekezwa kuwa ndiyo tiba ya magonjwa yote haya.

“Nilianza kazi hiyo mara moja na tangu siku hiyo umati mkubwa wa watu unamiminika kijijini hapa kadiri wanavyopata habari zangu kutoka kwa watu waliofanikiwa kupona,” alisema mchungaji huyo huku wagonjwa wakiona namchelewesha kutoa tiba kwao.
Hata hivyo, mchungaji huyo alifafanua kuwa, ikitokea amekufa leo, Mungu atamtoa mtu mwingine kufanya kazi hiyo na anaweza akawa si ndugu wala mtoto wake.
Alipoulizwa idadi ya wagonjwa aliowatibu, mchungaji huyo alisema ana uhakika na watu 30,000 huku akisema gharama yake ni shilingi 500 tu kama alivyoagizwa kwenye ndoto. Hivi sasa zaidi ya watu 200,000 wanatibiwa hapo.

MUME NA MKE WAFUMANIANA
Mchungaji huyo anapoendelea na tiba hajui kinachofanyika nje ambako kuna umati wa watu.
Mwandishi wetu alishuhudia watu wawili, mke na mume kila mmoja akimuuliza mwenzake amefikaje kijijini hapo bila kutoa taarifa.
Mwanaume aliyejitambulisha kwa mwandishi wetu kwa jina la Isaya John Jeena alisema alikuwa na mpango wa kwenda kwa mtaalamu huyo kutokana na kusumbuliwa na maradhi ya muda mrefu (hakuyataja).

“Nilikuwa safarini Nairobi, nikapanga nikirudi nije huku, sasa, nashangaa kumkuta mke wangu, kwa nini aje bila kunitaarifu mimi mumewe?” Alihoji Jeena.

VIGOGO NAO WAMO
Tangu aanze kutibu watu, idadi kubwa ya vigogo, wakiwemo wana siasa, maofisa wa serikali na wafanyabiashara wa ndani ya nchi wamekuwa wakimiminika kupata tiba.
Mbali na makundi hayo, baadhi ya wagonjwa waliolazwa katika hospitali mbalimbali za mikoa, ikiwemo Kilimanjaro Christian Medical Center (KCMC) ya mjini Moshi, wamekuwa wakiomba ruhusa kutoka wengine wakitumia njia ya kutoroka ili wakatibiwe kwa mchungaji huyo.

Kwa sasa katika Kijiji cha Samunge, watu waliofurika ni wa kutoka Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Singida, Mbeya, Manyara , Dar es Salaam na nchi jirani za Kenya na Uganda.

Magari mengi ya kifahari ya vigogo yalionekana mwishoni mwa wiki iliyopita yakiwa yamezungukwa na askari wa FFU wakishirikiana na mgambo kuhakikisha kuwa hakuna mwandishi wa habari ama mtu yeyote atakayeruhusiwa kupiga picha eneo hilo.

Mabasi kutoka Dar, Arusha na Moshi yamekuwa yakianzisha ‘ruti’ za kwenda Loliondo moja kwa moja kutoka katika miji hiyo.
Hata hivyo, kutokana na idadi kubwa ya watu wanaokwenda eneo hilo huduma ya vyakula imepanda ambapo wageni wanaofika hapo wamekuwa wakilazimika kubeba vyakula vyao baada ya kujikuta wakiuziwa sahani moja ya chakula kwa shilingi kati ya 5,000 na 10,000.
Awali kulikuwa na watu walikuwa wakichinja mbuzi 50,000 kwa siku lakini sasa wamezuiliwa kutoa huduma hiyo.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa, katika eneo hilo hakuna idadi kubwa ya vyoo vya kujisaidia, hivyo watu kujikuta wakienda vichakani.

Aidha, imebainika kuwa, hata ‘madada poa’ wanaofanya biashara ya kuuza miili katika maeneo mbalimbali ya starehe mjini Arusha, nao wamepungua baada ya wengi wao kutimkia kwa mchungaji huyo kutokana na kuamini wana maambukizi ya Virusi vya Ukimwi.
Usafiri wa kutoka mjini Arusha hadi Samunge umepanda ghafla kutoka shilingi 35,000 kwenda na kurudi hadi kufikia shilingi 150,000 kwa magari yanayomudu kufika huko kwani barabara ni mbovu.

Ingawa hakuna taarifa rasmi zilizothibitisha kuwa mgonjwa wa Ukimwi amepona lakini Lilian John (30) mkazi wa kijiji hicho alisema kuwa aligundua ana maambukizi ya Ukimwi mwaka 2006 baada ya kufiwa na mume na mwanaye.

Alisema mwaka 2009 alibahatika kuonana na mchungaji huyo wakati huo alikuwa siyo maarufu na kumpatia dawa hiyo.

Baada ya kuitumia kwa wiki mbili alikwenda kupima katika Hospitali Teule ya Wasso ambapo madaktari walithibitisha kuwa, hana Virusi vya Ukimwi.

SERIKALI INASEMAJE?
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Isidori Shirima amesema serikali haioni sababu ya kuzuia watu kupata tiba za mchungaji huyo kama hazina madhara kwa afya zao.
Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Blandina Nyoni amesema wizara yake imeiagiza ofisi ya mganga mkuu wa mkoa ifanye utafiti wa kimaabara juu ya dawa hiyo kwa kushirikiana na Taasisi ya Taifa ya Uchunguzi wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) ili kubaini ukweli wa kisayansi na watatoa taarifa uchunguzi ukikamilika.

Source: Globalpublisherstz.com

Friday, February 25, 2011

The Secret of Being Great-13


What would happen if I were to follow you with a camera crew 24 hours a
day 7 days a week for the next 100 days while you went for your goals?

I bet 3 things would happen....

1) You would START doing the things you say you need to do.

2) You would STOP doing the things you know you shouldn't be doing.

3) You would MAKE monumental performance gains and change your life.

This is ALL possible through the discipline of accountability.

Accountability serves and protects your character, credibility and
commitments as it ensures that what you want to accomplish gets
accomplished.

The problem however is that the lack of accountability is one of the
biggest constraints you have which prevents goal achievement.

With that reality in mind, I wanted to share with you an exciting
opportunity to achieve every goal you set, to enforce ultimate
accountability into your life, and show you how you can make monumental
performance gains.

Call Me on +255-713-427857 for audio and video books for success.
Mtade (miwlc@yahoo.com)

Friday, February 18, 2011

The Secret of Being Great-12

Why Time is Money but Money is not Time

These are some of the reasons.If you use them in a smart way in faith you will for sure get success in whatever you do.

1.Your future is created by what you do today, not tomorrow

2.The only difference between a rich person and poor person is how they use their time

3.The poor, the unsuccessful, the unhappy, the unhealthy are the ones who use the word tomorrow the most

4.Do today what you want for your tomorrows

5.Tomorrows only exist in the minds of dreamers and losers

6.The most life-destroying word of all is the word tomorrow

7.Today is the word for winners and tomorrow is the word for losers

Call Me on +255-713-427857 for audio and video books for success.
Mtade (miwlc@yahoo.com)

Kwa walioathirika na mabomu ya mbagala

"My Life Is In Your Hands"

You don't have to worry
And don't you be afraid
Joy comes in the morning
Troubles they don't last always
For there's a friend in Jesus
Who will wipe your tears away
And if your heart is broken
Just lift your hands and say

Oh
I know that I can make it
I know that I can stand
No matter what may come my way
My life is in your hands

With Jesus I can take it
With Him I know I can stand
No matter what may come my way
My life is in your hands

So when your tests and trials
They seem to get you down
And all your friends and loved ones
Are nowhere to be found
Remember there's a friend in Jesus
Who will wipe your tears away
And if you heart is broken
Just lift your hands and say

Oh
I know that I can make it
I know that I can stand
No matter what may come my way
My life is in your hands

With Jesus I can take it
With Him I know I can stand
No matter what may come my way
My life is in your hands

Thursday, February 17, 2011

Tuesday, February 15, 2011

Nigerian richest pastors

The common saying, ‘As poor as a church rat’ is fast losing its proverbial essence, given the assets churches and their leaders parade today. To disprove the saying, Opeyemi Adesina, Tayo Salami

and Chika Morkah, using additional Internet sources, identify four Nigerian pastors who are not only rich but are setting the pace in the art of wealth creation and business management.

They labour in the Lord’s vineyard, yet they are stupendously rich. That statement aptly captures the monetary worth of some pastors plying the gospel of Christ in Nigeria today. Not a few people will marvel at the value of the estates and earthly possessions on which they sit and superintend. Although they are many in the wealth circle, four of them clearly stand out, given their carriage, life styles, investments and popularity. Not many will fault the likes of Bishop David Oyedepo of Winners Chapel, Pastor Matthew Ashimolowo of Kingsway International Christian Centre, Pastor Chris Oyakhilome of Christ Embassy, and Prophet Temitope Balogun Joshua of Synagogue Church of All Nation as the ‘Big Four’ among several other affluent ministers of God.

It may pose a surprise that a few others who are head-to-head, or even heads above these four are not included, it is for no other reason than that their churches are more institutional and non-hereditary as churches of these four are likely to be. It’s on that ground that Pastor Enoch Adejare Adeboye of The Redeemed Christian Church of God, in particular, is not included.

Bishop David Oyedepo

Based on the parameters earlier listed, the richest pastor in Nigeria can be said to be the President and Founder of the Living Faith World Outreach Ministry, aka Winners Chapel, Bishop David O. Oyedepo. The church has the largest worship centre in the country, a 50,000-seat auditorium located at Canaanland, Ota, Ogun State.

Bishop Oyedepo is reported to own two private jets (Gulfstream 1 & Gulfstream 4), a Rolls Royce phantom among other luxury cars, an expensive university (Covenant University), a massive church auditorium, over 1000 branches locally and internationally. He’s also reported to be collecting through his church an average tithe income of 30 million Naira per Sunday (excluding offerings and other levies), franchises including literatures, e.t.c.

Whenever he or Faith, his wife is going out in the town, either separately or together, they usually go out with a convoy of vehicles and blaring of siren to beat the traffic. The couple like riding in posh jeeps with one or two vehicles in front and a similar number of cars following the one occupied by either of them.

Although the Winners’ Chapel is one of Africa’s fastest-growing Pentecostal churches, Oyedepo is often invited for crusades by other churches. He has a global vision of evangelism and has taken the gospel outside the shores of Nigeria, which have yielded a lot of financial rewards. “Your financial revolution is tied to what you do with your finances on the gospel,” he often tells his congregation.

As part of his outreach programmes, Oyedepo acquired a multi-million naira aircraft in 1996 to facilitate his evangelism programmes to countries outside Nigeria. This earned him the appellation “Jet-Age pastor”. He believes he is sent to a generation and not just a denomination to work signs and wonders. He established the Covenant University in Ota, Ogun State, thereby using his wealth for the promotion of tertiary education in Nigeria.

Prophet T. B. Joshua

Temitope Balogun Joshua, born June 12, 1963 and commonly referred to as T. B. Joshua, is the founder of The Synagogue, Church of All Nations (SCOAN), a Christian organisation headquartered in Ikotun, Lagos State. A Christian pastor, humanitarian and author, Joshua broadcasts Christian televangelism via SCOAN’s Christian television station Emmanuel TV, and on the Internet via the Streaming Faith Broadcast Portal. His sprawling church building on Ikotun/Egbe Road is reported to worth billions of naira.

Prophet T.B. Joshua

Joshua is said to have started a church with just a handful of members, naming it ‘The Synagogue, Church Of All Nations’—a name he says God divinely revealed to him. Since 1987 the church has grown far beyond the shores of Nigeria . More than 15,000 members attend the weekly Sunday service, and visitors from outside Nigeria are accommodated in the church facilities.

The church currently has branches in Ghana, the United Kingdom, South Africa, and Greece. He is also mentoring many evangelists from around the world in the church premises, saying: “The biggest reward God can give to His servant... is to make disciples who will do better than what we are presently doing.”.

‘Another Ministry’ is the humanitarian arm of SCOAN, with projects catering to the needs of widows, dwarfs, the elderly, physically challenged, orphans and the destitute. The church provides scholarships to orphans and children of the less privileged, with educational support promised from primary to tertiary levels. There is also a rehabilitation programme for armed robbers and prostitutes.

Often, the church financially supports them to secure a practical vocation. During his 45th birthday on June 12, 2008, T. B. Joshua made a large donation to the less privileged. Joshua has also provided scholarships for numerous physically challenged students and sponsored many physically challenged athletes. He is known to help people, irrespective of faith or denomination.

Joshua recently floated a football club ‘My People FC’ as part of his efforts to help the youth, the young team already making a mark on the Nigerian football scene. Already, three players have been sponsored abroad to play professional football in Sweden.

Two players from My People FC played for Nigeria’s Golden Eaglets in the last FIFA U-17 World Cup,were raised at Synagogue. Sani Emmanuel, who was raised in The SCOAN and worked as an altar boy, was Nigeria’s top-scorer and the tournament’s MVP, winning the Golden Ball and Silver Shoe. Emmanuel and his colleague Ogenyi Onazi have since expressed plans to have a foundation to help other less privileged youths, where ‘every proper means will be used to discover the talented’.

At a thanksgiving service in The SCOAN held after the cadet World Cup, Golden Eaglet’s goalkeeper, Dami Paul, also testified to receiving healing through Joshua’s prayers before the tournament’s commencement.

Pastor Chris Oyakhilome

Chris Oyakhilome, Pastor of Believers’ LoveWorld Incorporated otherwise called Christ Embassy Church, is not only winning souls but has built an expansive business empire from which he is making huge amount of money.

His church headquarters is a magnificent glass building. Its blue and gold colours stand it out in the crowd of old buildings on Oregun Road, Ikeja, Lagos. The building which is a few poles away from the old Suzuki Motorcycle assembly plant glitters like the corporate headquarters of a progressive new generation bank.

Chris Oyakhilome, the Edo State-born pastor, runs the branches of the church and his other businesses from there. The church has provided for Oyakhilome a good platform for his other business interests which include banking, publishing, broadcasting, entertainment and the hospitality industries.

A normal Sunday service at the headquarters draws not less than 30,000 worshipers. Most of them come from distant parishes of the church and the attraction is Oyakhilome himself who they all want to see live on the pulpit.

Oyakhilome belongs to the growing clan of pastors who preach prosperity but he is better known for his mira. Even then, they have remained the source of his popularity and the huge fortunes that he has made.

The church operates like a conglomerate with no fewer than 10 subsidiaries that work with the common goal of oiling the purse of the ministry and its patron.

The major money spinning arms of the ministry includes LoveWorld Cyber Ministry, LoveWorld Television, Love World Christian Network, LoveWorld Multimedia Ministry and LoveWorld Publishing Ministry.

One business enterprise run by the church is the LoveWorld Records Limited located in Ikeja. It was incorporated in 2008 as a private limited liability company to carry on the business of music, entertainment and gospel merchandise. The Christ Embassy recording studio operates a distribution network that facilitates the selling and marketing of records within and outside Nigeria.

His group’s investments in the media include Minaj Broadcasting International, MBI; Superscreen television; National Standard, a monthly magazine; National Daily, a weekly newspaper; and a cable television network known as Loveworld Media.

The satellite television is based in South Africa and it is a free-to-air-no subscription channel. It was set up primarily for the purpose of the church evangelism.

Superscreen television station, owned by Oyakhilome, occupies the seventh floor of Lagemo House at Onipanu area of Lagos. The television which began operation in 2007, boasts of state of the art broadcast equipment. .

Majority of staff of the television station are members of Christ Embassy. The television station serves as the media arm of the church, especially because it routinely telecasts church programmes of Christ Embassy.

In pursuit of the church’s craze for publicity and in spite of huge investments in the broadcast media, Christ Embassy again set up its sole private television station called Loveworld News Media. The studio is located within the church headquarters and is said to operate a 12-hour daily service airing church programmes.

National Standard hit the news-stands in July 2004 as a monthly glossy magazine. Its first office was at Plot 2, Ajumobi Street, off ACME Road, Agidingbi, before relocating to 25 Ogunlowo Street, off Adeniyi Jones, where it is at the moment. Today, the publication has gone weekly. Its sister publication, National Daily, which is a weekly tabloid, is located on Emina Crescent, off Toyin Street, Ikeja. Paradigm Communications Limited oversees the publication of the papers for Oyakilome’s business empire. The church’s investments in these media enterprises alone is put at more than N5 billion.

Global Plus printing press is another investment of the pastor. The hi-tech ultra modern press is located along Ikosi Road, Oregun, Ikeja. Monthly financial yields of the printing press which is worth more than two billion Naira is about N10 million.

Christ Embassy also owns CFI Pictures, a company that produces Christian movies. Located within the headquarters premises is a digital media store that markets electronic books and a gift card shop. The two are also money spinning channels for the church.

The church also has investments in the event and entertainment sector. In 2008, it bought over a warehouse belonging to a shoe making factory along Oregun Road which was converted to an event centre called K and G Event Centre. The event and recreational centre which is located at 8a, Oregun Road, has relaxation spots and other entertainment conveniences for customers.

The church also has an eatery called Dicksons. The fast food joint is rapidly expanding its outlets. It is being developed to compete favourably with Mr Biggs and similar outfits in the country.

Oyakhilome has also spread his business tentacles to the financial sector. The church owns two microfinance banks one of which is Moneycom Microfinance Bank.

Pastor Matthew Ashimolowo

Matthew Ashimolowo of Kingsway International Christian Centre (KICC) has carved a niche for himself in the British Christian community. His church, which attracts 8,000 congregation, is considered one of the richest in Britain. According to Robert Booth of The Guardian (London) reports, Pastor Ashimolowo, with a £100,000 yearly pay, earns more than the Archbishop of Canterbury, the official head of the British church.

KICC is reported as one of the richest religious institutions in both Britain and Nigeria.

The Kingsway International Christian Centre, in Walthamstow, has filed company accounts which reveal it made a £4.9m profit over a period of 18 months. It also has assets of £22.9m, more than three times the amount held by the foundation which maintains St Paul’s Cathedral.

His church’s wealth, according to reports, stems largely from the donations it encourages from its 8,000-strong largely African and Caribbean congregation. They gave £9.5m in tithes and offerings in the 18 months to April 2008, dwarfing the £33,000 that the average Church of England congregation gave over the same period.

Rather than a more traditional plate collection, forms are handed out to worshippers so they can make bank transfers at some services.

KICC’s wealth is the clearest sign yet of the gathering popularity of evangelical Pentecostalism which is the only growing branch of Christianity in the UK with an estimated 300,000 weekly worshippers.

The church’s increasing wealth represents a transformation in its fortunes after the discovery in 2005 by Charity Commission investigators of financial irregularities. Ashimolowo was ordered to repay £200,000 after it emerged he used church assets to buy a £13,000 Florida timeshare and £120,000 on his birthday celebrations, including £80,000 on a car. New trustees were appointed and Ashimolowo was removed from his role as chief executive.

“The last 18 months have been a period of incredible journey in the life of KICC,” said Ashimolowo in a preface to the accounts. “It has been very exciting to see God move the ministry from one level to another as we witness the increased manifestation of His glory.”

Ashimolowo is understood to earn his salary from preaching as well as royalties from sermons published in books and on DVDs through his own company. Ashimolowo Media Ministries made a profit of close to £60,000 in 2003.

Four KICC directors earn between £60,000 and £80,000 each. By contrast, a typical Church of England vicar earns around £21,500 and even the Archbishop of Canterbury, who has responsibility for an active congregation of close to a million people, only earns £68,740 a year.

“This is a very well-financed business,” said a tax accountant who examined the accounts for the Guardian. “It holds more than £16m in short term investments. I am the honorary auditor of my local church and they have just £20,000 on deposit.”

“The teaching of the church is very much about self-development,” said James McGlashan, a former oil executive who is now KICC’s chief operating officer. “If that is preaching wealth then we are preaching wealth. Becoming financially independent, owning a house, getting a degree and a better job is good.”

According to the accounts filed with Companies House, KICC finances were boosted by the sale for £10.1m of its Waterden Road home in Hackney to the London Development Agency which needed the site for the 2012 Olympics. It is planning to spend between £50m and £80m on a five-year project to build a complex at a site in Rainham, Essex, with capacity for 8,000 worshippers, classrooms, a TV studio, bookstore and offices.

As in Britain, Ashimolowo is fast spreading his church in Nigeria, spending millions of naira to plant branches of his church in every part of the country. His expansive church auditorium in Mende area of Maryland, Lagos speaks volume of his financial muscles.

Tuesday, February 8, 2011

How great is our God!



The splendor of a King, clothed in majesty
Let all the earth rejoice
All the earth rejoice

He wraps himself in Light, and darkness tries to hide
And trembles at His voice
Trembles at His voice

How great is our God, sing with me
How great is our God, and all will see
How great, how great is our God

Age to age He stands
And time is in His hands
Beginning and the end
Beginning and the end

The Godhead Three in One
Father Spirit Son
The Lion and the Lamb
The Lion and the Lamb

Name above all names
Worthy of our praise
My heart will sing
How great is our God

How great is our God, sing with me
How great is our God, and all will see
How great, how great is our God

Tuesday, February 1, 2011

ANGALIZO

Blogu yenu ya mlima sayuni inapenda kuwataarifu wanasayuni wote na wale wasio wanasayuni kuwa HATUTOZI FEDHA YA AINA YOYOTE (MAPATO YA AIBU) KWA AJILI YA KUWAOMBEA WATU.
NI KWELI KABISA WATU WENGI WAMEKUWA WAKIPOKEA MAJIBU YA MAOMBI YAO HAPA MLIMANI SAYUNI (BLOGUNI) NA HILO NI JAMBO JEMA LA KUMPA MUNGU UTUKUFU.TUNAPENDA KUWAOMBA WALE WOTE WANAOPOKEA MAJIBU YA MAOMBI YAO WAENDE WAKAMTOLEE MUNGU KWENYE MAKANISA NA NYUMBA ZA IBADA KULE WANAKOABUDU.KAMA HUNA PA KUPELEKA SADAKA YAKO KWA AJILI YA KUMSHUKURU MUNGU TUNAKUOMBA UTAFUTE KITUO CHA WATOTO YATIMA AU MASKINI WALIO MABARABARANI UWAPATIE SADAKA YAKO NA MUNGU ATAKUBARIKI.
TUNAPENDA KUSISITIZA TENA HATUPOKEI FEDHA YA MTU YEYOTE KWA AJILI YA KUFANYA MAOMBI.MAOMBI HAPA MLIMANI NI BURE KABISA NA NI YA KUJITOLEA. FEDHA NA DHAHABU NI MALI YA BWANA.HATUCHUKUI MAPATO YA AIBU KWA AJILI YA KUKUFANYIA MAOMBI.YESU ALISEMA MMEPEWA BURE TOENI BURE.
PIA TUNAPENDA KUCHUKUA NAFASI HII KUWAOMBA WALE WANAOTAKA KUSHIRIKIKIANA NA SISI KATIKA HUDUMA YA KUWAOMBEA WATU WANAOHITAJI MSAADA KUPITIA HUDUMA HII MTUANDIKIE MAHALI KWA EMAIL: MIWLC@YAHOO.COM .
KUMBUKA SI KWA UWEZO WALA KWA NGUVU WALA BIDII ILA NI KWA ROHO MTAKATIFU WA MUNGU.
MUNGU AWABARIKI SANA.
MTADE,
SAYUNI

D-CHANGE FESTIVAL IN MWANZA

D-CHANGE FESTIVAL IN MWANZA


Askofu Ben Bahati toka kenya mmoja kati ya wahubiri wa mkutano
Umoja wa makanisa jijini mwanza jana jioni umefungua rasmi mkutano mkubwa wa injiri ujulikanao kama D-Change Festival katika viwanja vya Furahisha. kusanyioko hilo lililoanza jana linatarajia kumalizika tar 30mwezi huu na limehusisha wanamuziki wa injiri toka Kenya akiwemo Solomoni Mukubwa,Anastazia Mukabwa, kundi la The Fielder-Marshals pamoja na Mhubiri na Muimbaji mkongwe Askofu Ben Bahati .Umati wa watu ulijitokeza viwanjani hapo na wengi walimpokea kristo kama Bwana na Mwokozi wa maisha yao.

Zifuatazo ni Picha za matukio ya Mkutano huo.
Waimbaji toka kenya Solomon Mukubwa na Anastazia Mukabwa wakisikiliza mahubiri ya Askofu Ben Bahati
Mchungaji Irene Nzwalla kushoto na A. Mukabwa kulia wakimsifu MUNGU

Umati wa watu ulijitokeza kusikiliza habari njema za Kristo YESU

Kundi la The Field-marshals toka Kenya likimsifu MUNGU siku hiyo
Anastazia Mukabwa Akiwasalimia wakazi wa Mwanza kabla ya kuimba
Anastazia Mukabwa akiimba wimbo wa KIATU KIVUE mbele ya umati wa wakazi wa Mwanza,na kisha akaimba wimbo wake wa "Anayekudharau siku moja atakusalimia kwa Heshima" uliionekana kuwasisimua wengi uwanjani hapo.
Solomon Mukubwa kabla ya kuimba alisema Anaheshimu kila MADHABAHU ya MUNGU iliyo katika jiji la Mwanza
Solomon Mukubwa akiimba wimbo wake wa MUNGU Mwenye Enzi

Sehemu ya Umati uliojitokeza siku ya Ufunguzi wa Mkutano

Askofu Ben Bahati akiwaongoza watu sala ya toba kama ishara ya kumpokea YESU kama Bwana na mwokozi wa maisha yao