Wednesday, September 4, 2013

Hatimaye Bishop Moses Kulola Amezikwa Kanisani EAGT Bugando Mwanza

Rais Wa Jamuhuri Ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete Awaongoza Maelfu Kuuzika Mwili wa Shujaa Wa Injili Tanzania Dr. Moses Kulola

Siku ya leo Mchana Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete amewaongoza maelfu ya Watanzania kuuzika mwili wa Shujaa wa Injili Tanzania Hayati Dr. Moses Kulola aliyezikwa katika Kanisa la Bugando, Mwanza.

Mhe. Kikwete waliongoza viongozi na waumini wa dini mbalimbali, viongozi wa vyama vya Siasa nchini katika Kutoa salamu za mwisho na kuulaza Mwili wa shujaa huyo aliyefariki mwishoni mwa wiki iliyopita. Shujaa wa Injili Dr. Kulola aliyezaliwa mwaka 1930 ameelezewa na Mhe. Rais kama ni mtu aliyejitoa kwa ajili ya kazi ya injili katika Tanzania na Nje ya Tanzania.

Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina la Bwana linarikiwe.
Mke wa Shujaa wa Injili akiweka Shada ya Maua

Mhe. Wenje akiweka udongo katika Kaburi
Mhe Rais JK akitoa salamu za Mwisho
Mama Josephine Slaa akiweka udongo
Mhe. Slaa akiweka Udongo kwenye Kaburi
Mhe. Mbunge wa Monduli Edward Lowassa akiweka Shada la maua
Mama Mjane akiweka udongo
Wachungaji wakisaidiana kushusha sanduku
Askofu Mwaisabila akiongoza ibada siku ya leo
 Mhe. Rais akiosha mikono baada ya kuweka udongo
Humu ndimo mwili ulivyolala
 Wachungaji wakisaidiana kushusha mwili
Mhe. Rais JK akiongea siku ya leo
Mhe Rais.
Mhe. Rais alipokuwa akiondoka
Mkandamizaji akienda sawa siku ya Leo
Mwalimu Mwakasege
Mhe. Peter Msigwa akisalimia siku ya leo
Mhe. Ngeleja
Bishop Kakobe
 
Source:http://samsasali.blogspot.com/2013/09/rais-wa-jamuhuri-ya-muungano-wa.html

No comments: