Tuesday, March 3, 2009

Smart Card ,Namba 666 na Mfumo wa Computer

Kama ilivyo ada , wataalamu wa kampuni inayokuwa kwa kasi hivi sasa hapa nchini Tanzania ya DigitalBrain jana walikuwa na mtumishi wa Mungu,mwalimu na mwinjilisti Isaya Mzolo ndani ya radio WAPO FM.Mwalimu Isaya Mzolo ambaye pia ni mtaalamu aliyebobea katika masuala ya computer aliyelezea kwa kina na kufafanua masuala hayo jinsi ambavyo mfumo wa computer na biochips mbali mbali zinavyoweza kupandikizwa kwenye mwili wa binadamu hasa kwenye paji la uso na kwenye mkono.



Soma hapa kwanza:



Ufunuo wa Yohana 13:16-18 "16Pia aliwalazimisha watu wote, wakubwa kwa wadogo, matajiri na mas kini, watu huru na watumwa, watiwe alama kwenye mikono yao ya kulia au kwenye vipaji vya nyuso zao. 17Hakuna mtu ye yote ambaye angeweza kununua au kuuza kitu kama hana alama ile, yaani jina la huyo mnyama au namba ya jina lake.
18Jambo hili linahitaji hekima. Mwenye akili ya kutambua apige hesabu ya mnyama huyo kwa sababu ni namba ya mtu. Namba yake ni mia sita sitini na sita. "



Ufunuo wa Yohana 14:9 "9Malaika wa tatu aliwafuata hao wawili akisema kwa sauti kuu, ``Kama mtu ye yote anamwabudu yule mnyama na sanamu yake na kukubali kutiwa alama yake kwenye kipaji cha uso wake au kwenye mkono wake, 10yeye naye atakunywa divai ya ghadhabu ya Mungu ambayo imemiminiwa katika kikombe cha ghadhabu yake bila kuchan ganywa na maji. Naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya mal aika watakatifu na mbele za Mwana-Kondoo. 11Moshi wa mateso yao hupanda juu milele na milele; wala hakuna nafuu, mchana au usiku, kwa wale wamwabuduo huyo mnyama na sanamu yake au kwa ye yote anayepokea alama ya jina lake.'' 12Jambo hili linahitaji watu wa Mungu, wale ambao wanazishika amri zake, wawe wavumilivu na kumwamini Yesu"

Waweza kusikiliza kwa undani mafundisho haya kutoka kwa mwalimu Isaya Mzolo kupitia hata http://www.digitalbraintz.com/

No comments: