Thursday, December 23, 2010

What a coincidence..!

Mwaka mpya umeme bei juu


FURAHA ya Watanzania kusherehekea kuanza kwa mwaka mpya wa 2011 imetumbukia nyongo baada ya Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) kuruhusu Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kupandisha
bei umeme kwa asilimia 18.5.

Kwa uamuzi huo ulitolewa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa EWURA, Bw. Haruna Masebu, hapana shaka mwaka huo utaanza kwa bidhaa mbalimbali kupanda bei kutokana na gharama za uzalishaji kuwa juu kutokana na kupanda kwa kwa nishati hiyo.

Hata hivyo, kiwango hicho cha asilimia 18.5 kitakachoanza kutozwa Januari Mosi, mwakani ni karibu nusu ya ongezeko lililoombwa na TANESCO la asilimia 34.6.


++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++

Faini ya bil. 185/- yawashitua Watanzania

WAKATI wananchi wakishitushwa na hatua ya Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Biashara (ICC Court), kutoa uamuzi kuwa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) liilipe Kampuni ya Dowans Sh bilioni 185, shirika hilo linatafakari hukumu hiyo.

Meneja Uhusiano wa Tanesco, Badra Masoud akizungumza na gazeti hili jana kuhusu hukumu hiyo, alisema shirika hilo limepata uamuzi huo na linaufanyia kazi kabla ya kutoa taarifa kwa Watanzania.


No comments: