Thursday, February 28, 2008

FUNGUA BARUA YAKO HII

Kwako mwanangu .....................
Yawezekana ya kuwa hunijui lakini najua kila kitu juu yako. Zaburi 139:1
Najua kukaa kwako na kuondoka kwako. Zaburi 139:1
Nazifahamu njia zako zote. Zaburi 139:3
Hata nywele za kichwa chako najua hesabu yake. Mathayo 10:29-31
Kwa sababu uliumbwa kwa mfano wangu. Mwanzo 1:27
Ndani yangu unaishi na kutembea. Matendo 17:28
Kwa sababu wewe ni uzao wangu. Matendo 17:28-1
Nalikujua kabla sijakuumba. Yeremia 1:4-5
Nalikuchagua wewe nilipopanga kuumba ulimwengu. Waefeso 1:10-12
Hakuna makosa kwa sababu hata siku zako zimeandikwa katika kitabu changu. Zaburi 139:15-16
juu ya kuzaliwa kwako na mahali utakapokaa. Matendo 17:26
Wewe uliumbwa kwa jinsi ya ajabu ya kutisha. Zaburi 139:14
Nalikuunga pamoja katika tumbo la mamako. Zaburi 139:13
Nikakutoa tumboni mwa mama siku uliyozaliwa. Zaburi 71:6
Nimekosa kujulikana na kuwakilishwa nao wasionijua. Yohana 8:41-44 Sijakasirika lakini upendo wangu umekamilika. 1 Yohana 4:16
Na ni mapenzi yangu kukuonyesha upendo wangu kwako. 1 Yohana 3:1
Hii ni kwa sababu wewe ni mwanangu na mimi ni babako. 1 Yohana 3:1 Nimekupa mambo ambayo babako wa duniani hawezi kukupatia. Mathayo 7:11 Kwa sababu mimi ni baba mkamilifu. Mathayo 5:48
Kila kipawa kizuri hutoka mikononi mwangu. Yakobo 1:17
sababu mimi nakupa mahitaji yako yote. Mathayo 6:31-33
Mipango yangu kwa ajili yako ni kwa sababu nakupenda kwa upendo wa milele. Yeremia 31:3
Mawazo yangu kwako hayawezi kuhesabika ni kama mchanga wa baharini. Zaburi 139:17-18
Najifurahisha na vipaji vyako. Sefania 3:17
Sitaacha kukutendea mema. Yeremia 32:40
Kwa sababu wewe ni mali yangu ya thamani. Kutoka 19:5
Napenda kukupanda katika nchi kwa moyo wangu na nia yangu. Yeremia 32:41 Napenda kukuonyesha mambo makuu usiyoyajua. Yeremia 33:3
Ukinitafuta kwa moyo wako wote utanipata. Kumbukumbu 4:29
Nitegemee mimi nami nitakupa haja za moyo wako. Zaburi 37:4
Kwa sababu ni mimi ambaye huwapa watu haja za moyo wao. Zaburi 37:4 Maana ni mimi ninayekupa hayo mahitaji yako. Zaburi 2:13
Ninao uwezo wa kufanya makuu kuliko uyawazayo. Waefeso 3:20
Kwa sababu mimi ndiye niwezaye kukuimarisha. 2 Wathesalonike 2:16-17
Tena mimi ndiye ninayewapa wanaohitaji mahitaji yao. Zaburi 2:13
Ninao uwezo wa kukutendea makuu kuliko unayofikiria. Waefeso 3:20
Kwa sababu mimi ndiye ninayekupa nguvu. 2 Wathesalonike 2:16-17
Tena mimi ni baba anayekufariji wakati wa shida yako. 2 Wakorintho 1:3-4 Wakati moyo wako umevunjika niko karibu kukufariji. Zaburi 34:18
Kama mchungaji anavyomchukua mwanakondoo nimekuchukua ndani ya moyo wangu. Isaya 40:11
Nitayafuta machozi katika macho yako. Ufunuo 21:3-4
Na maumivu yako uliyoyapata hapa duniani nitayaondoa. Ufunuo 21:3-4
Mimi ni babako na ninakupenda kama nimpendavyo mwanangu Yesu Kristo. Yohana 17:23
Kwa sababu ndani ya Yesu upendo wangu huonekana. Yohana 17:26
Yeye huniwakilisha kuweko kwangu. Waebrania 1:3
Alikuja kuonyesha kuwa mimi niko upande wako si kinyume chako. Warumi 8:31
Na kukuambia ya kuwa sitakuhesabia makosa yako. 2 Wakorintho 5:18-19
Yesu alikufa ili mimi na wewe tuunganishwe pamoja. 2 Wakorintho 5:18-19 Kifo chake kilionyesha upendo wangu kwako. Yohana 4:10
Nilitoa yote ninayopenda ili nipate wewe na upendo wako. Warumi 8:32 Ukipokea zawadi ya mwana wangu ndipo unanipokea mimi.1 Yohana 2:23
Hakuna chochote kitakachoweza kukutenganisha na upendo wangu. Warumi 8:38-39
Karibu nyumbani na nitaandaa karamu ambayo haijaonekana huku mbinguni. Luka 15:7
Nimekuwa baba yako na nitaendelea kuwa baba yako milele. Waefeso 3:14-15 Swali langu kwako, je, utakubali kuwa mwanangu? Yohana 1:12-13
Nakungojea wewe. Luka 15:11-32
NAKUPENDA HUYU NI BABAKO WA MILELE-ISAYA 9:6

Muhuri(Roho mtakatifu)

NDIMI NIKO AMBAYE NIKO Kutoka 3:14

Imeletwa na Yesu-(neno la Mungu-Yohana 1:1)


Kalenge

1 comment:

Anonymous said...

Good art! Hii inapendeza sana, sikujua yawezekana kupata barua nzuri namna hii kutoka kwako Baba! Naam Baba yangu nashukuru na sitakuacha na natamani siku hiyo ifike upesi ntakayokuona uso kwa uso na kudumu katika pendo lako! Naja kwako Baba hivi nilivyo!!!!