Wednesday, January 30, 2013

MCHUNGAJI AACHANA NA MKEWE KWA KUMTUHUMU NI MCHAWI MBEYA

MCHUNGAJI AACHANA NA MKEWE KWA KUMTUHUMU NI MCHAWI MBEYA

Mchungaji wa kanisa linalojulikana kwa jina la Calnel Centre Mchungaji Elia Ambakisye Jongo alijikuta katika mzozo mkali na aliyedai kuwa ni mke wake baada ya kumtuhumu kuwa ni mchawi.
Sabina Lameck mke wa mchungaji anaedaiwa kuwachwa sababu ya uchawi 
Katikati mama mzazi wa mchungaji Elia Jongo wakiwa katika kikao hicho
Baadhi ya wazee wa kanisa wakiwa makini kusikiliza kisa hicho
“ Ninachotaka ni huyu mwanamke kurudisha nguo zangu kwa sababu alizichukua ili apeleke kwa mganga kwa nia ya kunisaidia mimi nirudiane na mchungaji lakini badala yake naona dawa hizo zimemsaidia mwenyewe hadi anataka kuolewa yeye,” alisema Mwanamke huyo. ambaye alikuwa mke wa mchungaji Elia
Huyu ndiye muumini wa kanisa hilo anayedaiwa kutaka kuolewa na mchungaji Elia pia muumini huyu ni mzee wa kanisa hilo
Mchungaji elia na dada yake wakiwa makini kumsikiliza mchawi wake
“ Huyu mwanamke ni mshirikina maana tangu tutengane alianza kunivurugia huduma ambapo waumini walianza kupungua kanisani nayeye kwenda kwa waganga wa kienyeji kwa lengo la kunivurugia huduma” alisema mchungaji huyo kwa hasira.
Askofu wa kanisha hilo aliyejulikana kwa jina moja la Pasta Lugito 
 Hili ndilo kanisa la Calnel Centre mbeya lipo katibu na kiwanja cha ndege mwanjelwa
 Mchungaji wa kanisa linalojulikana kwa jina la Calnel Centre Mchungaji Elia Ambakisye Jongo alijikuta katika mzozo mkali na aliyedai kuwa ni mke wake baada ya kumtuhumu kuwa ni mchawi.

Tukio hilo la aina yake lilitokea juzi katika kanisa hilo lililopo Airport Jijijini Mbeya baada ya Mchungaji huyo kupokea ujumbe mfupi katika simu yake ya mkononi kutoka kwa Mwanamke anayedai alikutwa mke wake ambaye waliachana miaka mine iliyopita.

Mchungaji huyo akiwa mbele ya wazee wa kanisa, Familia yake, waumini pamoja na wanahabari alisema sababu ya kuwakusanya watu hao kumetokana na mwanamke huyo aliyejulikana kwa jina la Sabina Lameck akitaka kutubu kwa mabaya aliyomtendea mumewe.

Hata hivyo baada ya mwanamke huyo kupewa nafasi ya kuanza kujieleza alianza kumtuhumu muumini wa kanisa hilo kuwa anauhusiano na mchungaji ambaye ni mumewe wa ndoa ambapo pia alidai kuwa mwanamke huyo alichukua nguo za mchngaji na mkewe kwa madai ya kupeleka kwa mganga ili kusudi awasaidie warudiane.

“ Ninachotaka ni huyu mwanamke kurudisha nguo zangu kwa sababu alizichukua ili apeleke kwa mganga kwa nia ya kunisaidia mimi nirudiane na mchungaji lakini badala yake naona dawa hizo zimemsaidia mwenyewe hadi anataka kuolewa yeye,” alisema Mwanamke huyo.

Kwa upande wake mchungaji Jongo alimtuhumu mwanamke huyo kuwa ni mshirikina na kwamba sababu ya kutengana naye ni kutokana na mwanamke huyo kuzaa na mwanaume mwingine nje ya ndoa hali aliyosema alidhalilishwa kama mchungaji.

“ Huyu mwanamke ni mshirikina maana tangu tutengane alianza kunivurugia huduma ambapo waumini walianza kupungua kanisani nayeye kwenda kwa waganga wa kienyeji kwa lengo la kunivurugia huduma” alisema mchungaji huyo na kuongeza.

“ amekuja leo hapa baada ya kusikia mimi nataka kuoa muumini wangu ambapo yeye ameanza kumzushia kuwa ni mshirikiana kitu ambacho si cha kweli lakini kama kuna ukweli wowote utajulikana kwa sababu Mungu yupo,” alisisitiza Mchungaji huyo.

Hata hivyo usuluhishi huo haukufika mwafaka baada ya kuibuka kwa malumbano hali iliyomlazimu msimamizi wa usuluhisho huo Askofu wa kanisha hilo laiyejulikana kwa jina moja la Pasta Lugito kuahilsha mazungumzo hayo huku wakimpiga marufuku mwanamke huyo kukanyaga katika makazi ya mchungaji.
Source:http://eddymoblaze.blogspot.com/2013/01/mchungaji-aachana-na-mkewe-kwa.html?zx=f963f3ff79b788d9

No comments: