Thursday, May 1, 2008

HIVI KWA NINI WANAWAKE NI WEPESI KULIA?


Kijana mmoja mdogo alimuuliza mamaye, "Mama kwa nini mara nyingi unalia?" Akamjibu "...Kwa sababu mie ni mwanamke". "Sikuelewi" Akasema kijana." Mamaye akamkumbatia kisha akamwambia "Hutaweza lielewa jambo hili". Kitambo tena kijana akamuuliza swali hilo baba yake; "Baba, Kwa nini mama huonekana akilia wakati mwingine hata pasipo sababu"? Babaye akamjibu " Wanawake wako hivyo wakati mwingine hulia hata pasipo sababu"

Kijana akaendelea kukua hata mtu mzima akiwa na swali hilo maishani mwake, " Kwanini wanawake ni wepesi kulia"? Hatimaye aliamua kuwasiliana na Mungu kuhusu jambo hili. Na alimuuliza swali hilohilo " Mungu, kwanini wanawake ni wepesi kulia?

Mungu kwa upole akampa majibu yafuatayo akasema;

"Nalipomuumba mwanamke nalimuumba wa tofauti. Nalifanya mabega yake kuwa na nguvu ya kuweza kuutegemeza ulimwengu, sambamba na hiyo ni mororo kuweza kumpatia mtu faraja.

Nimempa uvumilivu na ustahimilivu wa ndani kuweza kuvumilia utungu wa kuzaa na kukataliwa kama si kubezwa kutoka kwa hao anaowazaa.


Nimempa moyo wa saburi hata kuto kata tamaa mapema kama wengine wachokapo na pia kuitunza familia hata katika vipindi vya mateso na magonjwa bila hata kulalalmika.

Nimempa kupenda watoto wake katika mazingira yeyote yale pasi kujali ni mara ngapi ameumizwa nao.

Nimempa nguvu ya kuchukuliana na mumewe kwenye mapungufu yake na kutoka mbavuni mwa mumewe nalimnadhifisha.

Nimempa hekima na busara za kutambua kwamba mume mwema si mwiba kwa mkewe, japo huweza kumpima/kumjaribu uwezo wake na namna ambavyo anaweza kuwa pamoja naye pasi kuchoka.

Na mwisho Mungu akasema; Nimempa machozi ili yatiririke. Haya ni muhimu kwake na huyatumia kwa wakati muafaka unaotakiwa.

Akaendelea kusema; Mwanangu umesikia? " Uzuri wa mwanamke hauko katika mavazi ayavaayo, umbo lake, au mtindo wake wa nywele. Uzuri wa mwanamke ni lazima uonekane machoni pake mwenyewe kwani huo ndo mlango kuelekea moyoni mwake mahali ambapo UPENDO wake unakaa.

Kijana hatimaye akasema, MUNGU INATOSHA!!!

Hebu na tujiulize leo wako wapi wale wanawake waombolezaji makanisani?? Hivi tunao kweli au wamesongwa na mawimbi ya maisha?

6 comments:

Anonymous said...

Hello friends,
I was happy to read this story and it is interesting.
But I am trying to imagine that one boy talking to God all that story !!!MMHHH do you believe it? is it anybody can talk to god? how and in which language? and that kijana ni mtanzania or from where in this world ilinikamuulize mwenyewe?

2. Do you remember the kibwetere story? http://www.culteducation.com/kibwetere.html soma hiyo Link.
he said he was able to hear jesus talking to marry and so he ended killing people.. What out who says I met jesus or mungu alinishukiaa sometimes they make stories and jesus warned you that --not all who say his name are his pple and not all who do miracles comes from him, some miracles comes from devil too.
Nasikia kuna manabii Arusha wanasaidia watu wakiwa utupu!!!

wow ! Just watch out these imaginary stories!

Mohamed Abdulrahman
United Kingdom

Anonymous said...

Kweli kabisa ndugu Abdularman Mohamed, hata mimi nakuunga mkono Imaginary story are not good but are existing, Yesu alitoa mifano mingi imaginary yenye reality ndani yake, hali kadhalika Mohamad alitoa hadithi nyingi imaginary akiwa na lengo la kuwafundisha waumini wake, THESE STORIES ARE EXISTING for good, for demonstration , for emphasizing, for alerting people. thats why tulipokuwa watoto tulihadithiwa hadithi na mababu but at the end of story, ulikuwa unatakiwa ueleze hadithi inakufundisha nini!

Nakukubalia tena upande wa manabii wa uongo na wanaowaombea watu uchi, dini hiz zimevamiwa, MIMI NI INJINIA, LAKINI WAKO MAINJINIA FEKI NA WAONGO, KUWEPO KWA MAINJINIA WA UONGO HAKUUONDOI UKWELI KUWA WALE WA KWELI HAWAPO!!!


Kuwepo kwa waislamu magaidi wanaoua binadamu wenzao kwa mabomu, mapanga N.k hakuifanyi dini yote ya waislamu ionekane ni magaidi au wauaji.WALA KUWWEPO KWA WAISLAMU WACHAWI WENGI, wanaokula watu vichwa na kutoa visingizio kuwa Mungu aliumba majini kwa hiyo wawe nayo na wanaweza kuyatuma kumuua mtua, HAKUIPELEKEI DINI YA WAISLAMU WOTE WAAMINI HIVYO NA YUAMINI KUWA WACHAWI.

Pia kitendo cha mtume Muhamad kuoa mtoto wa miaka tisa hatusemi kuwa waislamu wote wako hivyo sijaona muislamu Tanzania akioa msichana wa miaka Tisa.

Kw hiyo wako wasanii katika dini hizi kwa manufaa yao wakitumia kivili cha dini, kumbe matapeli, kama umegundua na utakubaliana na mimi basi ubarikiwe

Anonymous said...

Then what is your conclusion?

is this story real or among the fake one?

Mohamed abdulrahman

Anonymous said...

I think you were born by our lovely mom, it is simple just compare her with what written here!!!!

Anonymous said...

Hahahahahahahahaha WOW!
I do respect women too much and If only people and women would know their value this world would be as beautiful as ever. I was born among 10 children and 6 are ladies but suprisingly apart of showing that they are women , they almost as same to men. they perform to school, they are good business people, they are good managers, brave and everthing not as what this artical is trying to devalue them as if they can afford nothing more than crying.
Actually crying is a natural thing same as vomiting,sweating and culture is the one that makes men in africa not crying. If you come to europe and other part of the world both men and women cries with good propotion. Talk to psycologists.
That is why I am trying to tell you pple before you write something just use the brain. Anything that comes online is read by many people everywhere and so it is shame to hear unjustifiable stories. Especially from people who says they heard from GOD and I warned you before these people are just not to be trusted because now gospal is a business.

One day you will remember these words!

Mohamed Abdulrahman
United Kingdom

Anonymous said...

If you think this Article devalue women, then you are first muslim, respecting women!!! and you are against quran,Receiving Jesus is the best option for you now!!