Lengo na dhumuni la nakala hii ni kusupport mawazo ya ndugu Lema ambaye ameandika nakala ya iliyotangulia;
Unajua kwa nini viongozi wetu wa dini wako kimya? Wako kimya kwa sababu hawatoki tena mbinguni.Wanatoka duniani.Wanaitegemea serikali badala ya serikali kuwategemea wao ,
''tumepewa mamlaka'' inaishia madhabahuni
Nimefundishwa kanisani na nimeelewa uhusiano uliopo kati ya Kristo na Kanisa, achilia mbali kufundishwa kwenye mafundisho ya ndoa kwa undani zaidi, lakini kila mchungaji padri,maaskofu makadinali wanayajua haya, kuwa kanisa ni mfano halisi wa mwanamke!
Linatakiwa liwe na sifa zote za mwanamke, ambazo ni pamoja na utii,upendo,kujali,kukusanya kulinda n.k
Pamoja na kuwa tunaweza kuringa tuna roho mtakatifu hata na kuwa na nguvu za kuhamisha milima,kufufua wafu,katu bila upendo unaoendana na matendo halisi ya wakati na mahali husika karama zetu na kazi zetu ni bure,bila kuwa na moyo,hari na uwezo wa kutetea haki hatufai utumishi wetu tutaulizwa,wapentekoste wangapi wanalea yatima?,maskini?,wajane? n.k, ni aibu ya kuwa pengine wamataifa wametuzidi kwa mbali sana.
Kwa sababu tunajiona tumefika mbinguni,upako tulionano pengine umetupofusha? Nitakataa kumbe penye upako au nguvu za Mungu kuna haki kuna ukweli,kuna
ujasiri kama wa Stefano akifa bila kumkana Yesu, Kama tunasema Mungu habadiliki ni yule jana leo na hata Milele,tunaambiwa pia Eliya alikuwa mtu wa kawaida sawa na sisi aliamuru Mvua isinyeshe na ikawa,naam zaidi tunaishi pia katika kipindi ambacho Roho mtakatifu ni dhahiri kwa watu walioamini, wakati zamani nguvu hizo zilikuwa kwa wachache na ndio tunaowasoma hata leo. Wako wapi akina Daniel,Shadrack, Meshack na Abedinego,nimesikia kuna manabii wengi zama hizi ,
wako wapi akina Yohana mbatizaji ambaye alieleza uovu wa kiongozi serikalini!??????
Watu wanaishi kwa taabu nchi hii, maisha Magumu, rushwa kila mahali,ubadhirifu wa fedha za umma uko dhahiri, haki kupindishwa, uonevu mahali mahali, wakati kuwa Kuna baadhi ya viongozi wa dini wanadai waliomba wakajibiwa na kuwa ni majibu ya Mungu kuwa na viongozi tulionao sasa! Nikaamini zama za viongozi kupakwa mafuta kumbe hata sasa zipo japo si za moja kwa moja ‘indirectly’ .
Nikaamini basi watatokea akina Samweli na Nathani enzi za mfalme Sauli na Daudi ambao watakosoa utendaji kazi mbovu, baadhi ya mambo yasioyosahihi ya serikali,vyama,taasisi hata zisizo za kiserikali.Mmekaa kimya kama vile sio viongozi wa kanisa.Yesu ni Mfalme wa wafalme, yuko juu ya serikali na mamlaka zote, Yesu huyo mnae tena kila siku mnawaita watu waje kuombewa magonjwa mbalimbali yakiwemo ukimwi ambao nimeona kwa macho yangu watu wanapona hata kama serikali haitaki tuseme,
Kanisa likae kimya juu ya ununuzi wa rada, ndege ya raisi,matumizi mabaya ye serikali,kunyima haki watu, maisha ya taabu na dhiki wanayoishi watanzania,EPA,RICHMOND,? Kama tunaambiwa tuheshimu mamlaka ni pamoja na kuiambia ukweli, si mamlaka zote zinaheshimiwa kwani sidhani kama Mungu anaweza kuweka mamlaka kama za akina madikteta tunaowajua kama hatukutaka wenyewe!
Kanisa ni dhaifu kwa sababu tuna viongozi wa makanisa dhaifu katika kutambua na kuelewa wajibu wao katika jamii si kiroho tu bali hata kimwili.Yale yaliyo katika uwezo wetu kuyafanya mnatakiwa mfanye kwani ninyi ni miungu(Zaburi 82:6, Yohana 10:34) .
Waumini wenu au washirika wenu, wamesalitiwa vyama vinavyojiita vya upinzani vimewasaliti maana havina mpango wa kuungana pamoja kilammoja anataka chake,baadhi ya wasomi wakiwemo maprofesa wamewasaliti, wengine mmewaona juzi wakitoa maamuzi ya kisiasa wakati wao wasomi, Siasa imeingia kwenye elimu ambayo ni dira ya taifa,kodi wanazotoa waumini wenu na nyie maaskofu zinaharibiwa. Yesu alikasirika siku moja alipoingia hekaluni na kukuta minada inaendelea badala ya neno la Mungu,hekalu la sasa ni mtu.Tumaini la watanzania liwe viongozi wao wa kanisani.
Hawa wasomi, viongozi wa serikalini mafisadi ni waumini wenu na mnachukua sadaka zao! Mambo wanayopitia kizazi cha sasa ndio kinaelezea aina ya viongozi ambao tutakuwa nao baadae, aina ya wachungaji ambao tutakuwa nao baadae, hali ya maisha ya sasa inelezea jinsi ambavyo ni vigumu kwa viongozi wa kanisa kukataza rushwa hapo baadae,mmeona jinsi ambavyo mkuu wa mkoa wa DSM akipiga vita wasichana kujiuza mwili, wameacha au wamebadilisha maeneo?, jamani manabii,mitume,walimu,wainjilisti,wachungaji mko wapi? Au kwa sababu zaka na sadaka vinaletwa tu?
Lakini hao waumini wenu watafika mbinguni??? hizo sadaka na zaka zinapatikana kihalali
?(Fikiria wewe ni mchungaji wa Lowassa mpaka anapata aibu ile si ni aibu ya kanisa!! wewe mchungaji ulikuwa haujui kuwa ana tatizo, la hata inawezekana kweli ulikuwa haujui kwa jinsi ya kibinadamu, je Roho hakukuambia?? kama hakukuambia basi hauombi! na kama hauombi basi haufai kuwa mchungaji!!! na kama ulijua ukaka kimya dhambi hiyo pia ni yako.Timotheo aliambiwa ONYA, KARIPIA maana mchungaji wa kweli aliyejazwa Roho , hekima na mamlaka viongozi wa serikali wanatetemeka maana sio wewe unayeishi bali ni kristo) kuna mtu atasema mchungaji yule wa Lowassa hajaokoka , je ni wachungaji wangapi waliookoka wangeweza kuzuia kama yasimtokee Lowassa kamaLowassa angekuwa muumini wa kanisa lake??
Amkeni maaskofu kondoo wenu wanararuliwa kwani nyie ni viongozi wa mshahara?, Yesu alisema kiongozi mwema yuko tayari kuutoa uhai wake kwa ajili ya wengine.Mna Mungu anayetisha, anayeweza,wa haki muwazi mkweli,hashindwi,haogopi!.Jamani hata sasa tunahitaji kuwaona mashujaa wa Imani za kiroho na kimwili,hata kama hawataandikwa kwenye biblia mbinguni wataandikwa!
Ukiwa na viongozi wa kidini vipofu,wasiosema kitu wala kukaripia serikali kama akina Gamanywa,Kulola n.k ambao kwa nafasi zao walitakiwa wawe wakali na hakika Taifa lingewaogopa na kuwaheshimu si siri na si bure viongozi wa kilokole Tanzania hawaheshimiwi huwezi kufananisha heshima ya Pengo serikalini na Kulola?? Hiyo nguvu isiishie kuombea watu Yohana alimbatiza mpaka Yesu bado akaenda gerezani kwa kusema kuwa mkuu serikali ni mzinzi, je ni ngumu sana kwa mtu kama Gamanywa kukemea uovu nay eye ni mwenyekiti wa makanisa ya kipentecost!! Kalagabaho watu wanafanya biashara zao na wako tayari ku-compromise GOD’s standard by using money!! Sio kwamba simpendi nazungumza kwa nafasi yake na vita ya maisha bora tunayoyalilia.
Urafiki huu na uoga huu tutaletewa sheria ambazo watapitisha waumini wenu ili hali nyie mmekaa kimya.Wabunge wa Afrika kusini waliopitisha sheria ya kutambua
ndoa za jinsia moja, hivi hawa hamna wakristo?, si wana viongozi wao wa kanisa.Basi tunaweza kusema ndiyo wanayofundishwa kanisani? La! sasa wanatoa wapi.Kuchekea na kudharau mambo madogo huzaa makubwa,Kanisa lingekuwa na nguvu hata hiyo hoja ya mahakama ya kadhi wangejiuliza mara mbili kama waizue au wakae kimya , kutokana na udhaifu wa Kanisa linajadiliwa mpaka kuundiwa tume inayolipwa na kodi za waumini wa kanisa! Wameona sisi ni dhaifu tuko kimya kazi kuandaa matamasha na kuwaita viongozi wa serikali wazindue albamu na kugawa tuzo! Tumemwachia kazi hii Mtikila!!
Tusiangamie kwa kukosa maarifa yaliyo katika uwezo wetu kuyafanya tunayafanya,tuna mamlaka,tuna Mungu,tuna Roho tuna elimu,tuna mdomo tuna la kusema,hatujachelewa bado,
kumbe kweli mmomonyoko wa maadili,maisha ya taabu ya wananchi kanisa limechangia.Hivi ndio Nionavyo mimi INAWEZEKANA AMKENI!!
‘’Lakini nawasihi, ndugu,mchukuliane na neno hili lenye maonyo maana nimewaandikia kwa maneno machache’’ Waebrania 13:22
Nakala hii pia niliitoa gazeti la nyakati toleo la 335 May 2007, edited to suit now.
Kalenge-Canada
Imanimartini2222@gmail.com