Tuesday, April 15, 2008

Obama na H. Clinton wanasupport utoaji mimba

Jana nilikuwa nafuatilia mahojiano ya Faith Forum ya huko marekani.Nilisikitika sana kusikia kuwa wagombea wa Democratic Hilllary Clinton na Barak Obama wanasupport utoaji mimba (abortion).
Kwenye mdahalo huo wagombea hao walikuwa wakiulizwa kuhusu uhusiano wao na Mungu na mara ngapi wanasoma Biblia.Mgombea wa Repulblican McCain hakutokea kabisa na hatukuweza kuufahamu msimamo wake.Hata hivyo imezoeleka kwa miaka mingi kuwa Democratic mara nyingi wamekuwa wakiunga mkono vitendo vya ushoga na ndoa za jinsia moja pamoja na utoaji mimba na urutubishaji wa viini tete.
Itakumbukwa kuwa Rais George W. Bush amekuwa akipinga vikali uovu wote huo ambao Democratica wamekuwa wakiutetea.

Kwa mwelekeo huu naona ni heri Republican warudi tena madarakani japo ningependa Obama mwafirika mwenzangu awe Rais wa Marekani lakini kwa mtindo huu naona kama naanza kupunguza imani na hawa Democratic

No comments: